Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Mie siyo msomaji sana wa maandiko ya dini lakini nimewahi kusikia Yesu toka anatoka mbinguni ilikuwa ni lazima aje afe kama kafara ya utakaso wa dhambi za wanadamu, kwa hiyo swala la wayahudi kumuua sifikiri linafaa kuwahukumu kwalo kwa sababu kama alishushwa Israel tutegemeeje angetimiza hiyo kafara ya kifo kwa kuuliwa na walesotho? Bila Shaka hilo lisingekuwa rahisi.
 
Salamu wana jamvi,
Naomba nianze kuchangia mada hii nikionyesha msimamo wangu na imani yangu kuwa 'Israel hii ya leo bado ni taifa teule la Mungu. Pamoja na michango ya wanajamvi humuna mleta mada kujaribu kushawishi kwa maandiko kuwa Israel hii ya akina Netanyahu si lolote si chochote,na kuwa kanisa la leo ndio Israel mpya.Pamoja na dhumuni la YESU KRISTO kuja duniani kumkomboa mwanadamu hiyo bado haitoshi kulifanya kanisa kuwa Israel kamili hoja za kuunga mkono msimamo wangu ni nyingi na mojawapo ni hizi mbili.
1.Yako mambo yaliyotabiriwa tangu agano la kale hayajatimia na utimilifu wake utafanyika katika Israel hii hii ya akina Netanyahu na tena pale YESU atakaporudi mara ya pili.Hebu tutafakari hii kitu inyoitwa the GOLDEN GATE/EASTERN GATE OF JERUSALEM ambayo imendikwa ndani ya Biblia kwenye EZEKIEL 44.1-2 Nabii Ezekiel alioneshwa kwenye maono kuwa huo mlango/gate la mashariki halitafunguliwa mpaka atakaporudi YESU na sababu zake zikatolewa(Soma Ezekiel 44:1-2) na maandiko mengine nitawaletea na waarabu walishajaribu sana kubomoa huo mlango wa mashariki imeshindikana(Google ujisomee mwemyewe). Hivyo hoja yangu ni kuwa yapo maagano ambayo Mungu aliyaweka tangu enzi za akina Ibrahimu ambayo mpaka sasa yadumu kusubiri kutimia,wapi kama sio ISRAEL ya leo,na mengine mengi.

2.Dunia nzima inafahamu kuwa Israel ya leo ndio yenye wanasayansi bora kabisa waliotapakaa Ulaya na Amerika wakifanya mambo makubwa,kwa mfano inasemekana(sina uhakika) lakini haya yalitamkwa na Waziri mkuu wa Israel kuwa siku za karibuni kuwa katika makampuni makubwa 10 bora duniani ya IT,Telecom,Energy etc,yaliyoko Marekani matano yakiwemo(Yahoo,Whatsapp,Microsoft etc) yana research centres Tel Aviv hii ya leo,Kwa nini? Wazungu wa ulaya na Amerika wanaijua Israel hii ya leo mnayoipinga kuwa inazo zile baraka za Mungu kupitia Ibrahimu na uzao wake.Nani asiyejua kuwa modern agricultuere iko Israel,Jeshi lenye nguvu ni huko.Jamani habari za hili taifa la Isarel wanazijua waarabu wanaoizunguka Israel kama kweli hii Israel ya leo ndio ile ya ahadi ya Mungu?

Nimalize kwa kusema ahadi ya Mungu ni ya milele kanisa la leo kama Israel mpya limeandaliwa kwa ajili ya uzima wa milele baada ya maisha ya hapa duniani,

Nawasilisha, nitarudi
1.hoja yako ya kwanza inasema kuna nabii juu ya Israel hazijatimia na kwamba kuna agano la Ibrahim bado Mungu analisimamia. Hii ni hoja nzito sana mkuu lakini kwenye uzi wangu hakuna mahala nimekataa kuwa agano kati ya Mungu na Abraham limekufa ILA nilichosema na ndio mzizi wa mjadala ni NANI MRITHI WA BARAKA ZA ABRAHAM.... Je Israel ni ipi???

Hapo juu nimeweka mistari kadhaa inayoeleza warithi wa Baraka na ahadi zote za Ibrahim ni WAKRISTO sasa kwa namna yeyote ile iwe Israel ya kina netanyahu ni taifa la Mungu au lah lakini WAKRISTO pia wameshakuwa level moja na wayahudi kiasi wamekuwa warithi sawa wa baraka za Abraham sasa basi huo uteule unatoka wapi ilihali Biblia imeshasema warithi ni wakristo???

2.Kuhusu unabii nimeshaeleza hapo juu kuwa kuna namna wayahudi walikosea kwenye kutafsiri unabii hadi wakajikuta wanashindwa kumtambua kristo..... Next time ntakuja na uzi wa kutafsiri kwamba Biblia inaposema unabii wa hekalu,matetemeko,njaa,vita, haimaanishi ni vita au matetemeko ya kimwili hivyo huu mtego tusiingie.... Mwisho wa siku tutaumbuka kwa wayahudi waliodhani messiah atakuwa mwanajeshi kuwakomboa kam alexander the great, au atakuwa mfalme haswaa wa kimwili kumbe ikawa opposite ikala kwao.

3. Mkuu kibiblia Baraka za Ibrahim zipo kwa waaminio wote sio kwa waisrael tu so sikubali kwamba wakina Netanyahu wana akili kuliko sisi in fact kwenye kupima uwezo wa akili katika tafiti zote inaonyesha watu wa Asean yaani korea,singapore n.k wana IQ kubwa kuliko jamii zingine so sio kweli waisrael ndio wana akili kuliko wanadamu wengine labda ulete ushahidi wa tafiti gani imewahi sema hivyo.

4. Mnaosimamia hoja hii ya Israel kuwa bado taifa teule ningeomba tena mnisaidia kutafsiri mstari huu kwamba Yesu alimaanisha nini kusema ufalme wa Mungu umeondolewa kwao??

Mathayo 21:43
42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko,Jiwe walilolikataa waashi,Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni;Neno hili limetoka kwa Bwana,Nalo ni ajabu machoni petu?
43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.
 
Mie siyo msomaji sana wa maandiko ya dini lakini nimewahi kusikia Yesu toka anatoka mbinguni ilikuwa ni lazima aje afe kama kafara ya utakaso wa dhambi za wanadamu, kwa hiyo swala la wayahudi kumuua sifikiri linafaa kuwahukumu kwalo kwa sababu kama alishushwa Israel tutegemeeje angetimiza hiyo kafara ya kifo kwa kuuliwa na walesotho? Bila Shaka hilo lisingekuwa rahisi.
Hapana mkuu unabii kutimia sio justification ya ubaya unaofanyika.... Yesu angeweza kukubalika na waisrael wote ila angeuawa na hata warumi ila shida inaanza pale warumi waligoma kumuua walimuona hana kosa ila wayahudi wenyewe ndio wakamsaliti ukizingatia alitumwa kwao kuwakomboa!!! Hapo ndio shida ilipoanzia. Na ndio maana Yesu akasema haya baada ya kumkataa.

Mathayo 21:43
42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko,Jiwe walilolikataa waashi,Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni;Neno hili limetoka kwa Bwana,Nalo ni ajabu machoni petu?
43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.
 
Wakuu,
Mimi niseme tu kuwa pamoja na madhaifu yao yote ujeuri walionao,na hata kumkataa YESU KRISTO wakidai bado wanamsubiri mesiah wao,hiyo haiondoi kuwa wao ni taifa teule na baraka alizowatamkia Mungu na maagano aliyoyaweka toka enzi za agano la kale hayajaondoka wala kutenguliwa,ukitaka kuamini kuwa Israel hii ya sasa ndio ile ya kwenye agano la kale nenda kaanzishe vita na wao, au panga njama yeyote ya kulidhuru taifa lao hapo ndio utajua kama Mungu wa baba zao akina Ibrahimu ndio huyu wa akina Netanyahu.

Mungu ni yeye yule jana leo na hata milele,chokoza Israel kama hautauona mkono wa Mungu ukiwatetea, haya mataifa mengine Mungu alituhurumia tu akasema hawa nao ngoja tu warithi baraka za Ibrahimu ingawa hizo baraka mpaka leo huku Africa na kwingineko tunazisoma na pengine hatuziishi ipasavyo
Mkuu jikite kwenye Biblia hayo ya kushinda vita sio necessairily kwa kuwa ni taifa teule bali msaada wa marekani tu unawaweka mjini ukitaka kufahamu hilo jiulize kwanini kabla wapagani (SIO MUNGU) hawajawapa Israep ardhi ya palestina walikuwa wanatandikwa kila siku.

Kasome historia ya wayahudi mkuu usisubiri propaganda za CNN mfano tokea mwaka 1096 kwenye crusade ya kwanza na ya pili wayahudi walipoamka walitandikwa sana na kutekezwa huko ulaya ya kati.... Hapo usisahau cruaade ya pili waliteketezwa kabisa huko ufaransa.... Bado miaka ya karibuni Hitler aliwachinja kama kuku wanadai million 6 !! Sasa kama tukienda kwa historia ya vita kuprove ni taifa la Mungu unaweza nieleza kwanini vita zote walitandikwa hadi pale walipopewa mgongo na wamarekani na kupewa nchi ya palestina kimabavu??? Utanisaidia hapa

2. Mkuu msichanganye hakuna mahala nimesema Israel sio taifa teule?? Wala hakuna mahala nimesema agano limevunjwa bali hoja yangu ni kwamba MRITHI wa hilo agano ni nani??? Je ni netanyahu au wakristo yaani waliomfuata Yesu na nimeweka hapo maandiko wewe unayesema Israel ya Netanyahu ndio taifa teule bado ningeomba unielezee mstari huu Biblia ilimaanisha nini kusema WAKRISTO na sio wayahudi ni warithi wa baraka za Abraham ??

Galatia 3
28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi
 
Wayahudi hawamtaTmbui Yesu kuwa masiah hivyo tunajisumbua bure. Wenyewe wanamsubiri masihya ambaye hajazaliwa.

Taifa teule ni lile ambalo liko kwenye biblia lakini siyo lile la agano jipya. Tembelea Jerusalem ndo utajua maana ya ukristo. Ukitaka kujua ukristo zaidi ongea na Orthodox ndo wanaoshikilia sehemu nyingi za Jerusalem. Nimefika na ninauhakika. Wakatoliki wana sehemu ndogo ya umiliki. Wakristo walipigana sana kurudisha Jerusalem kwa wayahudi/wakristo lakini walishindwa.
 
Nashukuru kwa hoja na ukaribisho wako.

Naomba ukumbuke agano la jipya ni marejeo ya agano la la kale kwa wale walioandika agano jipya.

Wakichofanya ni ku compare yale yaliosemwa zamani yawe katika wakati uliopo.

Paulo Alikua anawaambia warumi si kwamba Neno la Mungu limetenguka kwa sababu si wote waisraeli walio uzao wa israel (naiongeza mimi si wote walio wakristo watokanao na kristo)

Alichokua akiangalia Mungu ni Ahadi rejea sura 9-9 warumi.

Naomba niegemee agano la kale zaidi sura ya 31- 3 Yeremia Mungu anasena hivi "naam nimekupenda kwa upendo wa milele"

Mkuu nadhani unaelewa maana ya neno milele.
Na aliekua akiambiwa amependwa kwa upendo wa milele ni israeli alie mzao wa ibrahim kulingana na warumi 9:9 "maana ahadi ni yenyewe ni hii, wakati maalam nitarudi nae sara atapata mtoto".

Sura ya 31:20 yeremia anaandika "je efrahim si mwanangu mpendwa? Maana kila nisemapo neno ninamkumbuka sana, kwa sababu hio moyo wangu unataabika kwaajili yake BILA SHAKA NITAMREHEMU. Asema Bwana.

Mpaka hapo mkuu unaona nafasi ya Rehema ilivyo kubwa mpaka moyo wa Mungu unataabika kwaajili ya mzao wa israel.

Mungu alitoa ahadi ya Upendo wa milele kwa israeli na ujajua wazi kabisa Mungu hasemi kitu asicho kitekeleza.kwa hali kama hiyo mkuu atashindwaje kumsamehe israeli kwa kosa lolite?

Sura ya 31:27-28 Yeremia anaandika "Mwenyezi Mungu asema hivi, tazama siku zinakuja nitakapoijaza nchi ya israeli na yuda watu na wanyama. 28"kadiri nilivyokua mwangalifu kuwang'oa kuwaboma kuwaangsha kuwaharibu na kuwatesa ndivyo nitakavyokua mwangalifu kuwapanda na kuwajenga.

Sura ya 31:36 Yer. Mwenyezi Mungu asema hivi "mimi hulifanya jua liangaze mchana, mwezi na nyota vimulike usiku. Pia mimi huitikisa bahari nayo hutoa mawimbi: jina langu mimi ni Mwenyezi Mungu wa majeshi. Basi nami nasema KADIRI NINAVYOTEGEMEZA MIPANGO HIO YOTE YANGU, KADIRI HIO HIO ISRAEL WATAKAVYOBAKI KUWA WATU WANGU.

31:37 Yer kama mbingu zinawezekana kupimwa na misingi ya dunia kuchunguzwa basi nitawatupilia mbali wazawa wa israel kwa sababa ya mambo yote walionitenda. Mimi mwenyezi Mungu nimesema.

Ndugu yangu zitto junior na wadau wengine, kwenye Biblia inapotaja dunia ujue ina maana ya ulimwengu.
Mimi nawe tumeshuhudia zama zetu ukuwaji wa tecnologia lakini hijaweza kuupima au kuuchnguza msingi wa ulimwengu na wala anga halijajulikana kwao.
Mungu aliahidi kama utakujawezekana kuupima msingi wa mbingu ndipo atakapowatupa wana wa usrael.
Mstari ule wa 36 ametaja nmna anavyofanya kazi mf kuitisa bahari kuamrisha jua na mwezi na nyota kuwa sehemu yake kwa mpangilio ameahidi kwa namna hio hio anavyotenda ndivyo atakavyowahifadhi wana wa israel.

Mpaka hapo hakuna shaka juu ya israeli kwamba nafasi yake kwa Mungu sio ndogo.

Swali ambalo halina majibu ni kwa sasa hao wana wa israeli waliotajwa ndio hawa tulio nao sasa?

Rejea rumi 9:9 kwamba ahadi ilikua mahsiusi kwa mwana wa sara never otherwise.

Karibu mkuu.
Mkuu una hoja nzito sana lakini mimi ningejikita mstari huu wa hicho kifungu cha 9:9
Warumi 9
8 yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazao.

Ooh sasa tushajua kumbe sio kila muisrael wa kimwili anakuwa ISRAEL bali mtoto wa ile ahadi?? Irrespective ya kwamba ni ya Isaka je hapo mbele Biblia inasemaje kuhusu hii ahadi ya Isaka.

Galatia 3
7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu

Ooh kumbe mpaka wawe na Imani juu ya MUNGU wao ndio wanakuwa watoto wa Ibrahim?? Swali linakuja Je israel ya walimkubali Yesu?? Jibu hapana hivyo kama walimkataa wanakuwa na imani?? HAPANA.... Na kama hawana imani je kwa mstari huu ina maanisha sio watoto wa Ibrahim?? NDIO....

Sasa tujiulize kama waisrael hawana Imani ya kweli je sasa nani huyo mwenye imani ambaye ndio atarithi hizi ahadi

Galatia 3
29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi

Oooh sasa tunaona kuwa wakristo ndio walimuamini Yesu pale wayahudi walipomkataa ndipo ahadi hii inakumbushiwa kwamba inarithiwa na wote waliomfuata kristo either wawe wayahudi au mataifa mengineyo.

Hivyo kwa hapa tunaweza rejea mstari ule wa warumi 9:9 kuwa watoto wa ahadi ni wale wa Isaka.... Je isaka ana chochote common na hao wakristo ambao paulo anasema wana Imani ndio maana wakarithu ahadi ya Ibrahim

Waebrania 11
20 Kwa imani Isaka akawabariki Yakobo na Esau, hata katika habari ya mambo yatakayokuwa baadaye

Ooh very good kumbe Isaka alikuwa na imani pia... Sasa basi jibu linakuwa hili

Watoto wa Isaka = Imani
Watoto wa Abraham= Imani

Je nani ana imani kwa kristo = Wakristo

So mpaka hapa tunajua nani mrithi wa ahadi equation inakuwa hivi

Ahadi ya Abraham + Ahadi ya Isaka = Wakristo

Wagalatia 3
29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

Hivyo mstari unaosema Mungu kawapenda Israel milele ni kweli kabisa ila definition ya ISRAEL ndio imebadilika..... Na pia hao Israel bado wanapendwa na Mungu kama anavyopenda mataifa mengine ila condition ni lazima wawe WAKRISTO yaani wakubali kuwa Yesu ni masiah wao ili nawe wawe watoto wa Ibrahim na warithi hizo ahadi otherwise bila kufanya hivyo wanakuwa ni watoto wa shetani tu ambao watahukumiwa kama wapagani mwingine siku ya mwisho at least kwa mujibu wa Biblia

Karibu kwa mjadala mkuu
Ubarikiwe
 
Ni vema kutofautisha kati ya taifa la Mungu na taifa teule. Wayahudi ni taifa teule. Hilo haliwezi kubadilika. Baadhi yao wapo kwenye taifa la Mungu.

Mungu alitwaa mwili kama Myahudi na akakaa nasi. Aliliteua taifa la Wayahudi kwa tukio hilo. Ni kitu kisichobadilika. Kwa maana hiyo, Israel ni taifa teule milele.

Taifa la Mungu ni wote wale waliopo katika Kanisa lake. Wapo Wayahudi wachache na watu wengi wa mataifa.

There is a non-empty intersection between taifa teule na taifa la Mungu but neither set contains the other.
 
Ni vema kutofautisha kati ya taifa la Mungu na taifa teule. Wayahudi ni taifa teule. Hilo haliwezi kubadilika. Baadhi yao wapo kwenye taifa la Mungu.

Mungu alitwaa mwili kama Myahudi na akakaa nasi. Aliliteua taifa la Wayahudi kwa tukio hilo. Ni kitu kisichobadilika. Kwa maana hiyo, Israel ni taifa teule milele.

Taifa la Mungu ni wote wale waliopo katika Kanisa lake. Wapo Wayahudi wachache na watu wengi wa mataifa.

There is a non-empty intersection between taifa teule na taifa la Mungu but neither set contains the other.
Naona wakuu bado sieleweki narudia tena ISRAEL NI TAIFA TEULE na AGANO LA MUNGU NA ISRAEL HALITOISHA KAMWE ila mzizi wa hoja yangu ni ISRAEL NI NANI???

Nimeshaeleza hapo Juu kuwa Israel ilichaguliwa sababu ya ABRAHAM sio Kingine sasa basi Biblia iko wazi kuwa WATOTO wa Abraham (sijasema watoto wa Mungu) ni wakristo na ndio warithi wa ahadi.

Sasa basi kama watoto wa Abraham ni wakristo (including waisrael wanaomfuata Yesu) na sio wayahudi tena (at least kwa macho ya MUNGU ) je Israel ya kina netanyahu ambao hawamfuati Yesu wanapata wapi uhalali wa kuitwa taifa teule???

Na kama hukubaliani na hoja yangu basi nisaidie Biblia inaposema wakristo ndio watoto wa Abraham na warithi wa ahadi ilikuwa na maana gani??

Ni hayo tu
 
Mkuu Mnabuduhe nimeona hoja yako nzito na natamani wana JF hada kwenye mada za kiimani waige mfano wako kwamba licha ya kuwa mara nyingi tuna misimamo tofauti ila unaapproach mada kwa utulivu na hoja sio jazba na mahaba ya kidini kwa hilo nikupongeze sana

Back to mada nimeona mengi ila ntajikita kwenye swali lako kwamba hakuna mahali kokote Biblia inasema wakristo ni taifa teule

Tuanze kwa ahadi ya Mungu kwa Israel

Kutoka 19:5
5 Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu,
6 nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu


Sasa basi tuangalie ahadi hii amepewa nani ya kuwa taifa takatifu baada ya Yesu kukataliwa na wayahudi.

1 Peter 2:7-10
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
......................
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.Ishini kama Watumishi wa Mungu


Sasa swali hapa ili twende sawa je kama agano jipya kupitia petro anasema kuwa waaminio ndio taifa teule yaani wakristo Wa makanisa 5 waliokuwepo Asia ya magharibi ambao hawakuwa wayahudi je ina maana alikuwa anawapotosha mkuu??

Na kama amesema waaminio ndio taifa teule je ni lini wayahudi hawa wa kimwili wamekuwa waaminio wa kristo?? Na kama hawajawahi je wanapataje uhalali wakuitwa taifa teule??

Labda tuanzie hapa kwanza ili twende pamoja.... Natanguliza shukrani
 
Mkuu Mnabuduhe nimeona hoja yako nzito na natamani wana JF hada kwenye mada za kiimani waige mfano wako kwamba licha ya kuwa mara nyingi tuna misimamo tofauti ila unaapproach mada kwa utulivu na hoja sio jazba na mahaba ya kidini kwa hilo nikupongeze sana

Back to mada nimeona mengi ila ntajikita kwenye swali lako kwamba hakuna mahali kokote Biblia inasema wakristo ni taifa teule

Tuanze kwa ahadi ya Mungu kwa Israel

Kutoka 19:5
5 Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu,
6 nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu


Sasa basi tuangalie ahadi hii amepewa nani ya kuwa taifa takatifu baada ya Yesu kukataliwa na wayahudi.

1 Peter 2:7-10
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
......................
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.Ishini kama Watumishi wa Mungu


Sasa swali hapa ili twende sawa je kama agano jipya kupitia petro anasema kuwa waaminio ndio taifa teule yaani wakristo Wa makanisa 5 waliokuwepo Asia ya magharibi ambao hawakuwa wayahudi je ina maana alikuwa anawapotosha mkuu??

Na kama amesema waaminio ndio taifa teule je ni lini wayahudi hawa wa kimwili wamekuwa waaminio wa kristo?? Na kama hawajawahi je wanapataje uhalali wakuitwa taifa teule??

Labda tuanzie hapa kwanza ili twende pamoja.... Natanguliza shukrani
Wayahudi sio kwamba watakua na upendeleo wakwenda mbinguni Kama hata wakifa katika Dhambi.....Kama hawatotubu na kumkiri kristo nao wataangamizwa katika Moto wa milele....ila hata kwa uasi wao walionao hivi Sasa bado ile Hali ya kuitwa taifa teule bado ipo ila haiwafanyi kuwa Bora zaidi ya wengine katika maswala ya kiimani Kama hawatotubu
 
Taifa teule ni nchi yetu Tanzania walahi
 
Mkuu Zitto, asante kwa kuchuja hoja yako na kusema swali lako hitimisho lake ni jibu la swali hili: "Israeli ni nani?"

Kwenye historia ya wokovu, Israeli ni Yakobo, mtoto wa Isaac, mtoto wa Abraham. Bila shaka umesoma simulizi la jinsi Mungu alivyofanya agano na Yakobo na kumwambia tangu sasa utaitwa Israel. (Genesis 32:22-32)

Kwa hivyo basi, kihistoria ni kwamba Waisraeli ni kizazi chote cha Yakobo. Kiimani, kuna mnyambuko wa neno Israeli. Ni mnyambuko wa Kitheolojia ambao unahitimishwa kwa kusema Kanisa ni Israeli mpya.

Wayahudi wote ni kizazi cha Yakobo. Kwa hivyo kihistoria ni Waisraeli, hata kama wengi wao hawakubali kwamba Yesu ndiye Masia waliyemsubiri.
 
Wayahudi sio kwamba watakua na upendeleo wakwenda mbinguni Kama hata wakifa katika Dhambi.....Kama hawatotubu na kumkiri kristo nao wataangamizwa katika Moto wa milele....ila hata kwa uasi wao walionao hivi Sasa bado ile Hali ya kuitwa taifa teule bado ipo ila haiwafanyi kuwa Bora zaidi ya wengine katika maswala ya kiimani Kama hawatotubu
Mkuu Zitto, asante kwa kuchuja hoja yako na kusema swali lako hitimisho lake ni jibu la swali hili: "Israeli ni nani?"

Kwenye historia ya wokovu, Israeli ni Yakobo, mtoto wa Isaac, mtoto wa Abraham. Bila shaka umesoma simulizi la jinsi Mungu alivyofanya agano na Yakobo na kumwambia tangu sasa utaitwa Israel. (Genesis 32:22-32)

Kwa hivyo basi, kihistoria ni kwamba Waisraeli ni kizazi chote cha Yakobo. Kiimani, kuna mnyambuko wa neno Israeli. Ni mnyambuko wa Kitheolojia ambao unahitimishwa kwa kusema Kanisa ni Israeli mpya.

Wayahudi wote ni kizazi cha Yakobo. Kwa hivyo kihistoria ni Waisraeli, hata kama wengi wao hawakubali kwamba Yesu ndiye Masia waliyemsubiri.
Okay kama Israel ya kina Netanyahu ndio taifa teule na sio kanisa ina maana hapa Petro alipotosha aliposema wakristo wa makanisa matano kulea Asia nao ni TAIFA TEULE na TAIFA TAKATIFU ilihali alijua sio watoto wa Yakobo?? Na kama hakupotosha je tuchukue lipi kati yao kuwa ndio taifa teule

1 Peter 2:7-10
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
8 Tena,Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.Ishini kama Watumishi wa Mungu
 
Okay kama Israel ya kina Netanyahu ndio taifa teule na sio kanisa ina maana hapa Petro alipotosha aliposema wakristo wa makanisa matano kulea Asia nao ni TAIFA TEULE na TAIFA TAKATIFU ilihali alijua sio watoto wa Yakobo?? Na kama hakupotosha je tuchukue lipi kati yao kuwa ndio taifa teule

1 Peter 2:7-10
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
8 Tena,Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.Ishini kama Watumishi wa Mungu
Kwanza inabidi tukubaliane kwamba sisi wakristo wakovu tumeupata kwa neema ,kwani waliokusudiwa kumpokea Masihi walikua waisraeli....sisi wakristo pia ni taifa teule kiroho maana sisi ndio tuliopokea ufalme wa Mungu toka kwa waisraeli...ukisoma Mathayo 21 :33-46 hoja yako inakua Ina nguvu kabisa kwamba Kuna kuhama kwa utaifa katika ulimwengu wa Roho hapo naunga mkono hoja yako, Sasa tuje kwenye hii Israeli yakina Netanyau.

Hii Israeli yakina netanyau inaendeleza andiko lilivyosema kwamba Mungu aliwapa Roho ya usingizi,macho Wala wasione na masikio hata wasisikie hata siku hi ya Leo Rumi 11:8

Kwa maana,ndugu zangu sipendi msijue Siri hii ili msijione kuwa wenye akili ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata israeli mpaka utimilifu wa Matifa uwasili. Rumi 25

Kwaio kuasi kwao sisi ndo tumepata Neema na wasingehasi story ingekua nyingine na hawa watu wamepewa Roho ya usingizi ndomana wao hawamwamini Yesu na wanaona story za kizushi.

Basi kwa habari ya Injili wamekuawa adui kwa ajili yenu;Bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu Rumi 11:28.

Basi kimwili wao ni taifa teule kwani mababu ni wao,Bali sio taifa takatifu na ufalme wa Mungu kwao ushahama.
 
Kuna taifa la Israel lenye wayahudi na kuna wakristo waliomwamini Yesu na kuwa kanisa.Mtu anapokuwa amemwamini Yesu hawi mwananchi wa Israel ila anakuwa kanisa.ile kuwa mwana wa Ibrahim hakuondoi haki ya waliokuwa na hio hadhi kiasili ila ni kuiongeza tu idadi ya wana wa Ibrahim..Kwa hio kama Mungu alifanya agano na Ibrahim la milele kwa nchi aliompa ile hadhi haijachukuliwa na kanisa.Bado ile nchi ipo na bado wayahudi wapo.Hao kina Netanyahu ni wayahudi wa asili kabisa na ile ni nchi yao.Na wameachwa wachache kwa mpango ulio rasmi kabisa.
Mkuu labda sijaeleweka hakuna mahali nimesema Mungu kavunja AGANO na Abraham na Israel

Pia nimekubali Israel ni nchi ya ahadi

Pia nimekubali Israel ilichaguliwa na Mungu

Pia nimekubali Israel inahusika na unabii wa siku za mwisho

LAKINI nachohoji Israel ni nani kwa muktadha wa agano jipya.... Je ni lile taifa la kina Netanyahu lililopo pale mashariki ya kati au ni wakristo yaani waliomfuata Yesu.

Na nimeweka hapo mistari juu hivyo jikite hapo je Israel ni nani??

Natanguliza shukrani
 
Kuna taifa la Israel lenye wayahudi na kuna wakristo waliomwamini Yesu na kuwa kanisa.Mtu anapokuwa amemwamini Yesu hawi mwananchi wa Israel ila anakuwa kanisa.ile kuwa mwana wa Ibrahim hakuondoi haki ya waliokuwa na hio hadhi kiasili ila ni kuiongeza tu idadi ya wana wa Ibrahim..Kwa hio kama Mungu alifanya agano na Ibrahim la milele kwa nchi aliompa ile hadhi haijachukuliwa na kanisa.Bado ile nchi ipo na bado wayahudi wapo.Hao kina Netanyahu ni wayahudi wa asili kabisa na ile ni nchi yao.Na wameachwa wachache kwa mpango ulio rasmi kabisa.
Mkuu mi natofautiana nawewe kidogo ukisoma injili ya Mathayo 21 :33-46 unaona Yesu anawaambia mafarisayo kwa mifano ,mifano ambayo ilikua inawahusu kwani yote walifanya na Mfano wa Mwisho unaona mwenye shamba anamtuma Mwana nadhani unajua ule Mfano unamaanisha nini ila pia huyo Mwana wanamuua. Mistari iliyoendelea unaona kabisa Yesu anawaambia ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.

Kwa mistari hii ukiitafakari unaona kabisa taifa jengine ndio wakristo na wayahudi walinyang'anywa kutokana na makosa yao.

Naweza nikasahahihishwa
 
Kuna taifa la Israel lenye wayahudi na kuna wakristo waliomwamini Yesu na kuwa kanisa.Mtu anapokuwa amemwamini Yesu hawi mwananchi wa Israel ila anakuwa kanisa.ile kuwa mwana wa Ibrahim hakuondoi haki ya waliokuwa na hio hadhi kiasili ila ni kuiongeza tu idadi ya wana wa Ibrahim..Kwa hio kama Mungu alifanya agano na Ibrahim la milele kwa nchi aliompa ile hadhi haijachukuliwa na kanisa.Bado ile nchi ipo na bado wayahudi wapo.Hao kina Netanyahu ni wayahudi wa asili kabisa na ile ni nchi yao.Na wameachwa wachache kwa mpango ulio rasmi kabisa.
Hapana mkuu imewekwa condition ya kuwa mtoto wa Abraham sio tu mpaka akuzae maana unasema wameongeza namba ya watoto wa Abraham.... Sasa baso tujiulize watoto wa Abraham ni nani??

Galatia 3:7
7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu

Sasa naomba unisaidie ni lini wayahudi walimuamini Yesu?? Kama hawana Imani kwa Mungu wao kivp wanaqualify kuwa watoto wa Abraham??

Pia nimeeleza kupitia Kitabu cha petro nanukuu

1 Peter 2:7-10
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
8 Tena,Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.Ishini kama Watumishi wa Mungu


Biblia ipo very clear kuwa waaminio katika kristo ndio TAIFA teule.... Je waisrael kina Netanyahu wanaamini?? Kama hawaamini je kivipi huu uteule uwahusu na wao?? Na kama hauwahusu ina maana petro alipotosha kusema wateule ni WAKRISTO??
 
Wayahudi hawamtaTmbui Yesu kuwa masiah hivyo tunajisumbua bure. Wenyewe wanamsubiri masihya ambaye hajazaliwa.

Taifa teule ni lile ambalo liko kwenye biblia lakini siyo lile la agano jipya. Tembelea Jerusalem ndo utajua maana ya ukristo. Ukitaka kujua ukristo zaidi ongea na Orthodox ndo wanaoshikilia sehemu nyingi za Jerusalem. Nimefika na ninauhakika. Wakatoliki wana sehemu ndogo ya umiliki. Wakristo walipigana sana kurudisha Jerusalem kwa wayahudi/wakristo lakini walishindwa.
Wakatoliki na Orthodoxy wana tofauti gani?
 
Back
Top Bottom