Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Kwa tambuemi kuna Israel ya sas na Israel ya kale,ni tofauti.
Israel ya kale lilikuwa taifa la Mungu sababu alikua amelichagua kwa ajili ya mtumishi wake Ibrahim Mwanzo 12:7. Ahadi ya Mungu kwa Abrahamu ilitimizwa na wazal wa Yakobo/Israel pale walipotolewa Misri chini ya uongozi wa Musa na kuimiliki nchi ya Kanaani, baada ya kumiliki ikawa ya waisraeli. Taifa teule sababu Mungu alikua amelichagua na kulipa sheria na miongozo yake wazifuate. Lakini walianza kuasi agano la Mungu na kuanza kuabudu mabaali,wakaua manabii, mwishowe Yehova Mungu akawakataa Luka 13:34. Mwaka 70 ndio ulikua mwisho wa Israel ya kale pale jeshi la Roma lilipovamia na kuharibu kabisa hekalu,na wayahudi wote wakasambaa kama Yesu alivyosema Mathayo 24:2
Israel ya sasa ni kaa Tanzania tu haina uteule wowote wala uhusiano na Mungu kwani imeanza mwka 1948 ndani ya Palestina.
 
Habari za jioni wana JF mada ya leo ni sensitive kidogo maana inagusa moja ya topic zenye utata katika ulimwengu wa imani ila ningependa tusome kwa utulivu uzi wote alafu tujadiliane kwa hoja ili tuweze kusolve hili swali la karne nyingi sasa.
View attachment 929882
UTANGULIZI
Mwanzoni kulikuwa na agano kati ya wanadamu na Mungu kupitia Adam ila tunaona Adam analivunja agano hili

(Hosea 6:7)
Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu;

Hivyo Mungu alitaka kurudisha uhusiano tena na mwanadamu tunaona akapatikana Nuhu ambaye alimcha Mungu sana na akachaguliwa kuianza dunia upya baada ya gharika. Sasa baada ya gharika dhambi ilirudi tena kupitia Ham ambaye alipelekea Nuhu kumlaani mwana wake Ham yaani canaan kuwa atakuwa mtumwa wa kaka zake Ham yaani Shem na Yapheth (Hili la muhimu sana huko mbeleni) hivyo uzao wa Ham ukawa na watu waovu sana mfano Nimrod wa Babylon aliyeleta ibada za sanamu na dini za kipagani hadi kuleta machafuko kwenye ukoo wa Nuhu na kusababisha dunia nzima kumuacha Mungu wa Nuhu.

Katika sintofahamu hii aliyesimama imara alikuwa Shem/Melchizedek ndie aliendelea kushika wokovu na hata Abraham alipozaliwa aliendelea kumsimamia kiimani na hivyo hata alipokufa Abraham kati ya wanadamu wengi ndio aliendeleza imani ya kumuabudu Mungu wa babu zake (YAHWEH) hivyo baada ya Mungu kuona Abraham ana msimamo thabiti kwake akampa ahadi ya kuwa na uzao wa watu wengi kama nyota za angani lakini pia alimpa ahadi ya kumpa nchi hii ya canaan.

Mwanzo 15
18 Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,

Hivyo ni kupitia ahadi hii ndipo taifa la Israel lilipotabiriwa rasmi kuwepo. Na ahadi hiyo itakuja kutekelezwa na mjukuu wake yaani Yakobo ambaye aliiba urithi wa mtoto wa kwanza hivyo hii baraka ya Abraham akairithi yeye na tunaona uzao wake kupitia Joshua na Caleb ndio wanaingia kwenye nchi hii ya canaan rasmi na kuasisi taifa la Israel.

Je Mungu aliichagua Israel??

Kumb. La torati 7:6
6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.

Kupitia mstari huu tunaona Israel ilichaguliwa na Mungu lakini je kwanini aliichagua??

Kumb. Torati 7:7-8
7 BWANA hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote;
8 bali kwa sababu BWANA anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu.

Hivyo Mungu aliwachagua Israel sababu hiyo ya kutimiza uapo kwa mababu ikiwemo Nuhu + Abraham. Na hili ndio lilisababisha Israel wapewe nchi ya Canaan sababu ilikuwa inahitimisha unabii wa Nuhu kuwa Canaan atakuwa mtumwa wa shem (Babu wa Abraham) na sio kwa sababu nyingine yeyote.

Mwanzo 9
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake

View attachment 929883
Ramani ya canaan


Hivyo baada ya Agano hili na Israel ambalo kupitia wao ndio Mungu alipanga kuwaletea Messiah yaani Yesu ili aweze kurejesha uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu kama wa kipindi cha Adamu lakini wayahudi walimkataa Yesu kwa sababu hawakujua kutafsiri unabii ulioandikwa kuhusu maisha ya Yesu kwenye agano la kale. Kwa kifupi maisha yote ya Yesu kuanzia kuzaliwa mpaka kufa yalikuwa yanaendana na unabii wa agano la kale 1 korinto 15:1-4 Mfano wa nabii zilizotimizwa kupitia maisha ya Yesu ni hizi. Kuanza mahubiri yake galilaya ulitabiriwa na Isaya 9:1-2 na ukatimia Mathayo 4:13, Pia Yesu kupanda Punda kuingia jerusalem ulitabiriwa na Zakaria 9:9 na kutimia Mathayo 21:1-9 n.k yaani kuna mistari zaidi ya 100 iliyotabiriwa kuonyesha Huyo Messiah ataishije.

Lakini wao wayahudi hawakuliona hili sababu walidhani Yesu atakuwa handsome boy, Damu ya kifalme,Mwanajeshi kama alexander the great n.k hivyo kwa jinsi alivyokuja "kimasikini" wakaona kama anakufuru mwisho wa siku wakamuua na yote ni kutokana na kushindwa kutafsiri maandiko ya unabii.

Matendo 13:26-27
27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.
First thing first wahayudi hawapendi wakristo wala waislamu.
 
Wewe ndio wa hovyo kweli, ndani ya Palestina kuna Wayahudi Wakristo na Waislam.
Judaism sio dini tengua kauli yako, wanatumia biblia kuabudu.
.
Alafu huko Palestine kati ya wakristo na waislam dini ipi inazaidi ya 80% ya washirika? Jibu kama ni waislam nyamaza na kama ni wakristo mjadala uendelee
 
Judaism sio dini tengua kauli yako, wanatumia biblia kuabudu.
.
Alafu huko Palestine kati ya wakristo na waislam dini ipi inazaidi ya 80% ya washirika? Jibu kama ni waislam nyamaza na kama ni wakristo mjadala uendelee
1 JUDAISM NI NINI KAMA SIO DINI?
2.MAJORITY RULE MINORITY RIGHT UNAELEWA MAANA YAKE?
Judaism - Wikipedia
 
1 JUDAISM NI NINI KAMA SIO DINI?
2.MAJORITY RULE MINORITY RIGHT UNAELEWA MAANA YAKE?
Judaism - Wikipedia
Haya endelea kuwa na misimamo yako isiyo natija wala uhalisia.
.
Nimebahatika kufika kfar saba ni mji waki_Hebrew ni kazi sana kumpata mzungumzaji wa kiingereza kule kila baada ya hatua tatu unakutana na muyahudi (ambayo wewe unaiita dini) wao wanamisingi yao ambayo pia inatumiwa na kufuatwa na wa_Orthodox wa ukraine 100%.
.
Wanatumia biblia kama tunayoitumia sisi biblia yao ya Early Christianity yenye torati za mussa haitumiki tena kwa wayahudi walio wengi ila misingi yao haijafa.
.
Ni kama wakristo wasasa hutumia zaidi agano jipya na kuachana na lakale kwa mafundisho yaliyomengi (lakini misingi ya ukristo iko palepale.)
.
NB;JUDAISM IS AN EARLY CHRISTIANITY sasa wewe fuata unachokiamini.
.
Kwa kumalizia nenda mkoani dodoma kuna wayahudi wakitanzania na wayahudi wa israel wanafundisha vyema kabisa bila propanganda unazozisikia au kadhuru israel kama unahela.
 
Haya endelea kuwa na misimamo yako isiyo natija wala uhalisia.
.
Nimebahatika kufika kfar saba ni mji waki_Hebrew ni kazi sana kumpata mzungumzaji wa kiingereza kule kila baada ya hatua tatu unakutana na muyahudi (ambayo wewe unaiita dini) wao wanamisingi yao ambayo pia inatumiwa na kufuatwa na wa_Orthodox wa ukraine 100%.
.
Wanatumia biblia kama tunayoitumia sisi biblia yao ya Early Christianity yenye torati za mussa haitumiki tena kwa wayahudi walio wengi ila misingi yao haijafa.
.
Ni kama wakristo wasasa hutumia zaidi agano jipya na kuachana na lakale kwa mafundisho yaliyomengi (lakini misingi ya ukristo iko palepale.)
.
NB;JUDAISM IS AN EARLY CHRISTIANITY sasa wewe fuata unachokiamini.
.
Kwa kumalizia nenda mkoani dodoma kuna wayahudi wakitanzania na wayahudi wa israel wanafundisha vyema kabisa bila propanganda unazozisikia au kadhuru israel kama unahela.
Hivyo umehitimisha uyahudi nini?
 
Uko sahihi, ila kwenye kipengele cha *Angalizo* naona kama hauko sawa.
Njaa, matetemeko, vita n.k vimetabiriwa kuwa vitatokea physically na kuna baadhi yalishatokea.

Mfano WWI, WWII n.k
Sidhani kama waandishi wa Biblia walilenga kuyatabiri haya matukio kwa code!
 
Uko sahihi, ila kwenye kipengele cha *Angalizo* naona kama hauko sawa.
Njaa, matetemeko, vita n.k vimetabiriwa kuwa vitatokea physically na kuna baadhi yalishatokea.

Mfano WWI, WWII n.k
Sidhani kama waandishi wa Biblia walilenga kuyatabiri haya matukio kwa code!
Mkuu biblia imeandikwa figurative sio lateral... Yaani 80% ya maneno yana maana ya kiroho sio kimwili wanatheolojia watanielewa kwa mfano hio njaa Biblia imeeleza vzuri kabisa njaa ni ipi

Amos 8:11
11 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya BWANA.

Kwenye Biblia ARDHI sio hii ya kimwili bali Ardhi kiroho ina maana Kanisa au wakristo soma wakorintho 3:9 hata vita inayoongelewa sio ya kimwili bali vita za kiroho kati ya wakristo dhidi ya shetani kama

Waefeso 6:10-20
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama


And a lot nikipata wasaa ntaleta mada humu maana naona watu wengi sana mnafikiri Biblia inaongelea vita za kimwili mnapotoka mtashangaa Yesu wenu anarudi huku nyie mnasubiri eti vita sijui matetemeko..... World war 1 ma 2 zimeua watu zaidi ya million 50 je Yesu alirudi?? Matetemeko makubwa yamekuwepo toka karne ya 1 je Yesu alirudi??

Waisrael ndio walipotoka pia walidhani Yesu atakuja kama mfalme fulani wa kimwili ndio maana alipokuja kama mchonga mbao wakamdharau wakamuua

Amkeni wakuu
 
Haya endelea kuwa na misimamo yako isiyo natija wala uhalisia.
.
Nimebahatika kufika kfar saba ni mji waki_Hebrew ni kazi sana kumpata mzungumzaji wa kiingereza kule kila baada ya hatua tatu unakutana na muyahudi (ambayo wewe unaiita dini) wao wanamisingi yao ambayo pia inatumiwa na kufuatwa na wa_Orthodox wa ukraine 100%.
.
Wanatumia biblia kama tunayoitumia sisi biblia yao ya Early Christianity yenye torati za mussa haitumiki tena kwa wayahudi walio wengi ila misingi yao haijafa.
.
Ni kama wakristo wasasa hutumia zaidi agano jipya na kuachana na lakale kwa mafundisho yaliyomengi (lakini misingi ya ukristo iko palepale.)
.
NB;JUDAISM IS AN EARLY CHRISTIANITY sasa wewe fuata unachokiamini.
.
Kwa kumalizia nenda mkoani dodoma kuna wayahudi wakitanzania na wayahudi wa israel wanafundisha vyema kabisa bila propanganda unazozisikia au kadhuru israel kama unahela.
Uyahudi ni nini?
 
Asante kwa bandiko zuri na hoja fikirishi. Kwa kiasi fulani nimekuelewa hiyo dhana ya Israel kiroho.

Halafu huyu Yakobo (Dotto) aliiba Baraka za pacha wake Essau (Kurwa) akaachwa hivi hivi tu.. Lengo lilikuwa nini? Mungu alibariki wizi? Yaani ina maana taifa la Israeli ambalo limetokana na Yakobo lilianzishwa kwa misingi ya wizi na utapeli?
Taifa teule ni taifa la kitapeli? Haki ya Essau iko wapi?
Suala la Esau na Yakobo ni tata tangu tumboni. Kimsingi mpango wa Mungu ulikuwa kwa Yakobo ambae ndio Israeli. Esau ni gugu lililopandwa kuuvuruga mpango huo. Ndio maana tunaona mapigano kati yao tangu tumboni mwa nama yao. Yaani yule mpinzani alijaribu kuzuia kusudi la Mungu kwa kuingiza roho ya utasa kwa Rebeka. Ile roho ilipong'olewa akapanda gugu.
Habari za jioni wana JF mada ya leo ni sensitive kidogo maana inagusa moja ya topic zenye utata katika ulimwengu wa imani ila ningependa tusome kwa utulivu uzi wote alafu tujadiliane kwa hoja ili tuweze kusolve hili swali la karne nyingi sasa.
View attachment 929882
UTANGULIZI
Mwanzoni kulikuwa na agano kati ya wanadamu na Mungu kupitia Adam ila tunaona Adam analivunja agano hili

(Hosea 6:7)
Lakini wao wamelivunja hilo agano kama Adamu;

Hivyo Mungu alitaka kurudisha uhusiano tena na mwanadamu tunaona akapatikana Nuhu ambaye alimcha Mungu sana na akachaguliwa kuianza dunia upya baada ya gharika. Sasa baada ya gharika dhambi ilirudi tena kupitia Ham ambaye alipelekea Nuhu kumlaani mwana wake Ham yaani canaan kuwa atakuwa mtumwa wa kaka zake Ham yaani Shem na Yapheth (Hili la muhimu sana huko mbeleni) hivyo uzao wa Ham ukawa na watu waovu sana mfano Nimrod wa Babylon aliyeleta ibada za sanamu na dini za kipagani hadi kuleta machafuko kwenye ukoo wa Nuhu na kusababisha dunia nzima kumuacha Mungu wa Nuhu.

Katika sintofahamu hii aliyesimama imara alikuwa Shem/Melchizedek ndie aliendelea kushika wokovu na hata Abraham alipozaliwa aliendelea kumsimamia kiimani na hivyo hata alipokufa Abraham kati ya wanadamu wengi ndio aliendeleza imani ya kumuabudu Mungu wa babu zake (YAHWEH) hivyo baada ya Mungu kuona Abraham ana msimamo thabiti kwake akampa ahadi ya kuwa na uzao wa watu wengi kama nyota za angani lakini pia alimpa ahadi ya kumpa nchi hii ya canaan.

Mwanzo 15
18 Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,

Hivyo ni kupitia ahadi hii ndipo taifa la Israel lilipotabiriwa rasmi kuwepo. Na ahadi hiyo itakuja kutekelezwa na mjukuu wake yaani Yakobo ambaye aliiba urithi wa mtoto wa kwanza hivyo hii baraka ya Abraham akairithi yeye na tunaona uzao wake kupitia Joshua na Caleb ndio wanaingia kwenye nchi hii ya canaan rasmi na kuasisi taifa la Israel.

Je Mungu aliichagua Israel??

Kumb. La torati 7:6
6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi.

Kupitia mstari huu tunaona Israel ilichaguliwa na Mungu lakini je kwanini aliichagua??

Kumb. Torati 7:7-8
7 BWANA hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote;
8 bali kwa sababu BWANA anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu.

Hivyo Mungu aliwachagua Israel sababu hiyo ya kutimiza uapo kwa mababu ikiwemo Nuhu + Abraham. Na hili ndio lilisababisha Israel wapewe nchi ya Canaan sababu ilikuwa inahitimisha unabii wa Nuhu kuwa Canaan atakuwa mtumwa wa shem (Babu wa Abraham) na sio kwa sababu nyingine yeyote.

Mwanzo 9
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake

View attachment 929883
Ramani ya canaan


Hivyo baada ya Agano hili na Israel ambalo kupitia wao ndio Mungu alipanga kuwaletea Messiah yaani Yesu ili aweze kurejesha uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu kama wa kipindi cha Adamu lakini wayahudi walimkataa Yesu kwa sababu hawakujua kutafsiri unabii ulioandikwa kuhusu maisha ya Yesu kwenye agano la kale. Kwa kifupi maisha yote ya Yesu kuanzia kuzaliwa mpaka kufa yalikuwa yanaendana na unabii wa agano la kale 1 korinto 15:1-4 Mfano wa nabii zilizotimizwa kupitia maisha ya Yesu ni hizi. Kuanza mahubiri yake galilaya ulitabiriwa na Isaya 9:1-2 na ukatimia Mathayo 4:13, Pia Yesu kupanda Punda kuingia jerusalem ulitabiriwa na Zakaria 9:9 na kutimia Mathayo 21:1-9 n.k yaani kuna mistari zaidi ya 100 iliyotabiriwa kuonyesha Huyo Messiah ataishije.

Lakini wao wayahudi hawakuliona hili sababu walidhani Yesu atakuwa handsome boy, Damu ya kifalme,Mwanajeshi kama alexander the great n.k hivyo kwa jinsi alivyokuja "kimasikini" wakaona kama anakufuru mwisho wa siku wakamuua na yote ni kutokana na kushindwa kutafsiri maandiko ya unabii.

Matendo 13:26-27
27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.
Hongera sana mleta mada. Umejitahidi sana kuielezea kwa mapana. Uko sahihi ila usitake kulifuta taifa LA Israeli la kimwili kwani bado lina nafasi take katika mpango mzima wa Mungu. Katika Kitabu cha ufunuo wametajwa kwa kutenganishwa na watu wa mataifa na mabila na lugha mbalimbali. Pia usisahau mambo yote yaliyo katika join went I was roho hudhihirishwa katika ulimwengu wa mwili hadi pale mbingu mpya na nchi mpya zitakapochukua nafasi ya mbingu na nchi ya sasa. Hiyo ni baada ya shetani na walio wake kutupwa jehanamu. Nikipata muda nitachangia baadhi ya vipengele ili tupate kuelimishana kwa mapana zaidi. Ubarikiwe sana.
 
Sio Wayahudi hawa , hawa ni Ma ashkenazi Watu wanitoka KHAZAR KARIBU NA URUDI HAWANA DAMU YA KIYAHUDI KABISA ila walijiigiza kujifanya wayahudi wakati wa vita vya kwanza ili wasiwe chini ya utawala wa KIKRISTO WALA KIISLAM WAKACHAGUA UYAHUDI BUT ki ukweli sio uzao wa YAKOBO na wanafahamu hivyo ASHKANAZI JEWS SIO TAIFA TEULE LA MUNGU
 
Sio Wayahudi hawa , hawa ni Ma ashkenazi Watu wanitoka KHAZAR KARIBU NA URUDI HAWANA DAMU YA KIYAHUDI KABISA ila walijiigiza kujifanya wayahudi wakati wa vita vya kwanza ili wasiwe chini ya utawala wa KIKRISTO WALA KIISLAM WAKACHAGUA UYAHUDI BUT ki ukweli sio uzao wa YAKOBO na wanafahamu hivyo ASHKANAZI JEWS SIO TAIFA TEULE LA MUNGU
Huu ni ukweli mchungu ambao wafia dini hawataki kuusikia..... Kitabu cha 13th tribe kimechambua vizuri sana hii hoja yako.

Shukrani
 
Je,Wayahudi wa UKWELI Ni Wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haijulikani walipo maana walipotea utumwani zaidi ya makabila 10 na walichanganyika na mataifa mengine hivyo bado hawajulikani wako wapi leo labda iko siku watapatikana ila hawa waliopo Tel Aviv ni wahuni tu waliojivika uyahudi wakati walitokea kwenye milima ya Khazaria na sio Judeah.
 
Huyo Esau baada ya kutoka kwenye "mishe" zake alirudi amechoka sana hivyo akaahidi kutoa chochote ilimradi Yakobo amuandalie chakula. sasa akaamua kutoa haki yake kma mzaliwa wa kwanza kwenda kwa Yakobo hivyo automatically ikawa Yakobo ndio mzaliwa wa kwanza.

Sasa wakati Isaka anakaribia kufa alimuita mzaliwa wa kwanza ila kwa kuwa Yakobo alishakuwa ameuziwa hiyo haki akatumia fursa kumrubuni Esau hadi yeye ndio akawekewa mikono ya baraka na kwakuwa Isaka alikuwa haoni vizuri basi akabariki tu bila kujua.

Hivyo kimaandiko ile baraka ya Abraham ambayo iliritihiwa na isaka sasa ikarithiwa na Yakobo ndio maana Mungu alipotaka kutimiza agano lake na Abraham akaenda kwa familia ya Yakobo na Sio Esau au ukoo mwingine yeyote.

I hope nimeeleweka kidogo
Mkuu Isaka alikuwa specific alimuita ESSAU kwa jina wala sio kwa TITLE(mzaliwa wa kwanza) , hivyo Yakobo anabaki kuwa mdanganyifu kwa gharama ya mama yake, swali vip Mungu aruhusu aliedanganya apate baraka ?
 
Asante kwa bandiko zuri na hoja fikirishi. Kwa kiasi fulani nimekuelewa hiyo dhana ya Israel kiroho.

Halafu huyu Yakobo (Dotto) aliiba Baraka za pacha wake Essau (Kurwa) akaachwa hivi hivi tu.. Lengo lilikuwa nini? Mungu alibariki wizi? Yaani ina maana taifa la Israeli ambalo limetokana na Yakobo lilianzishwa kwa misingi ya wizi na utapeli?
Taifa teule ni taifa la kitapeli? Haki ya Essau iko wapi?
Nimekuelewa vizuri mkuu ila ujue Yacob siyo mwizi, but kulikuwa na utapeli fulani wa kishetani wa kutaka ku-Divert urithi wa Mungu kwa taifa lake pendwa Israel kupeleka upande wa shetani. kila mpango wa Mungu unapofanyika shetani ana plan b, ndo maana alitamka wazi kuwa alimchukia Esau japo yacob babae alimpenda, hata hivo Esau alioa kwa wa- edomites, ambao walikuwa hawa-comply na Mungu na hao hao wa-edom ndiyo walimuua Yesu wakishirikiana na utawala wa Warumi mfano mzuri ni Herode the Great Caipha nk. watu kama, Er na ndugu yake Onan wana wa Judah, na wengine wengi Mungu hakuwapenda sababu hawakufuata misingi ya imani ya Mungu,na pia walikuwa ni plan b ya shetani.always shetani alikuwa ana plant his own seeds katika uzao wa israel kupitia Mwanamke huyu huyu mama wa viumbe vyote [yaani vinavyoonekana na visivyoonekana).


Kwa akili ya kawaida ya kibinadamu tunaoana wizi mwingi na uasherati vilifanyika pale, lakini ilikuwa ni mipango ya Mungu kutunza pure generation of Israel. mfano Judah alimtia mkwewe Tamar na akazaa mapacha Perez na Meziah. kupitia Perez ikawa ni blood line ya King solomon son of David na kuendelea.
 
Nimekuelewa vizuri mkuu ila ujue Yacob siyo mwizi, but kulikuwa na utapeli fulani wa kishetani wa kutaka ku-Divert urithi wa Mungu kwa taifa lake pendwa Israel kupeleka upande wa shetani. kila mpango wa Mungu unapofanyika shetani ana plan b, ndo maana alitamka wazi kuwa alimchukia Esau japo yacob babae alimpenda, hata hivo Esau alioa kwa wa- edomites, ambao walikuwa hawa-comply na Mungu na hao hao wa-edom ndiyo walimuua Yesu wakishirikiana na utawala wa Warumi mfano mzuri ni Herode the Great Caipha nk. watu kama, Er na ndugu yake Onan wana wa Judah, na wengine wengi Mungu hakuwapenda sababu hawakufuata misingi ya imani ya Mungu,na pia walikuwa ni plan b ya shetani.always shetani alikuwa ana plant his own seeds katika uzao wa israel kupitia Mwanamke huyu huyu mama wa viumbe vyote [yaani vinavyoonekana na visivyoonekana).


Kwa akili ya kawaida ya kibinadamu tunaoana wizi mwingi na uasherati vilifanyika pale, lakini ilikuwa ni mipango ya Mungu kutunza pure generation of Israel. mfano Judah alimtia mkwewe Tamar na akazaa mapacha Perez na Meziah. kupitia Perez ikawa ni blood line ya King solomon son of David na kuendelea.
Mkuu unatuthibitishia kuwa Mungu anaweza kucheza rafu ili mradi tu Mipango yake itimie ?
 
AFTERMATH
Hivyo basi kwa kuwa Mungu alikwisha dhamiria kurudisha uhusiano na mwanadamu ikabidi ageukie mataifa mengine ambayo ndio yangeendeleza agano lile na hapo ndipo likapatikana agano jipya ambapo neema ya wokovu haukuwa wa Wayahudi pekee sababu walimkataa bali ukawa wa mataifa yote as long as watamfuata Yesu (Yohana 1:11-12) pia Mathayo 21:42-43 ambapo tunaona ufalme wa Mungu umehamishwa kutola Israel kwenda kwa mataifa mengine.

42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko,Jiwe walilolikataa waashi,Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni;Neno hili limetoka kwa Bwana,Nalo ni ajabu machoni petu?
43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.

View attachment 929907


Swali linaibuka je Israel inabakia taifa la Mungu??

NDIO ni kweli Mungu aliendelea na agano na taifa la Israel ila tafsiri ya taifa la israel ni lipi limebadilika kupitia agano jipya.

Warumi 9
6 Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. Maana hawawi wote Waisraeli walio wa uzao wa Israeli.
7 Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa;
8 yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazao.


Na pia hapa ndipo tunaona kunazaliwa waisraeli wa kimwili (mashariki ya kati) na Israel ya Kiroho (wakristo)

Warumi 2:28-29
28 Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili;
29 bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu.


Hivyo kufikia hapa tunaona kuna wayahudi/waisrael aina mbili sasa je ahadi za ISRAEL ya agano la kale anarithi nani za kuwa taifa teule,chaguo la Mungu n.k

Galatia 3
6 Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.
7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu
.
.......................................
13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.Ahadi kwa Abrahamu
..............................
28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.


Kupitia mistari hii tunaona sasa ahadi zote walizopewa Abraham na Israel zinarithiwa rasmi na wale wote wamfuatao Yesu yaani wakristo ambao ndio wale paulo kawaita waisrael wa Kiroho sio kimwili. Hivyo ningependa nichukue fursa hii kutoa msimamo wangu kwamba Israel hii ya kimwili sio taifa la Mungu na halitokaa liwe unless na wao wamfuate Yesu hapo ndipo watakuwa NCHI YA AHADI na taifa la Mungu. Kwa kuhitimisha kupitia agano jipya ambapo sasa wanaomfuata wote Yesu bila kujali ni muisrael au lah ndio wanakuwa TAIFA TEULE ama ISRAEL hivyo baraka zote ahadi zote na unabii wote wa TAIFA LA ISRAEL sio tena wa hii Israel ya yakobo bali ni wote wamfuatao Yesu kristo na hii ni kwa mujibu wa Biblia.

However upande kinzani unasema Israel ya mashariki ya kati bado ni taifa teule kama zamani na hakuna kilichobadilika na wanatumia mstari huu.

Warumi 3:3-4
3 Ni nini, basi, ikiwa baadhi yao hawakuamini? Je! Kutokuamini kwao kutaubatili uaminifu wa Mungu?
4 Hasha! Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo; kama ilivyoandikwa,Ili ujulike kuwa una haki katika maneno yako,Ukashinde uingiapo katika hukumu.


Nakubaliana na Mstari huu unaosema Mungu hajawaacha wayahudi licha ya kumkataa lakini bado msimamo uko pale pale kwamba ni lazima wamkiri massiah ndio wawe teule till then hawana tena hadhi ya kuitwa taifa teule kulingana na vifungu nilivyoweka.
View attachment 929908

ANGALIZO
Kumekuwa na interpretation nyingi sana za unabii kuhusu Israel ya kimwili yaani hii ya mashariki ya kati na nina hofu kuwa na wakristo pia wameingia mkenge kama wa wayahudi wa kale kwa kutoelewa unabii na wakatafsiri kwa akili zao kiasi kwamba Yesu alipokuja hawakujua na wakamkataa. kuna wakristo wengi leo wanaamini vita na matetemeko yaliyotabiriwa kwenye ufunuo ni ya kimwili au hekalu litajengwa kimwili hivyo watashituka Yesu amekuja kivingine wao bado wanasubiri vita ya amragedon sijui kujengwa hekalu ilihali hizo mambo zina maana tofauti kabisa ingawa hii ni mada ya siku ingine ila nachoweza hitimisha ni kwamba Biblia imeandikwa kwa codes nyingi hivyo kuitafsiri inahitaji umakini na utulivu sana sio kwenda kichwakichwa mfano inapotabiri kuwepo kwa njaa na kiu haimaanishi njaa ya kimwili ila ukisoma Amos 8:11 utajua njaa inaongelewa ni ya kusikiliza neno la Mungu such phrases mtu akisoma kwenye ufunuo ana conclude kuwa kutakuwa na njaa,vita matetemeko,ukame huu wa kimwili kumbe zina maana nyingine kabisa hivyo nilitaka kuliweka hilo sawa. Kwa kusema hayo naomba kuwasilisha mada kwa ajili ya michango na maoni ya wanajukwaa letu pendwa.

Cc cc Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Najaribu kwenda nawe kidogo kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mun
Hahaa...Taifa Teule, sasa iweje Mungu ambaye hana upendeleo awe na taifa teule tena? Ina maana kuna watu wengine wanakuwa na maana zaidi kwake kisa wamezaliwa sehemu fulani ya Dunia tu na sio matendo yao?
Mungu hana ubaguzi, yeyote anayekubalika nae ni wake.... (nimesahau andiko)
Kwa sasa Mungu Israeli haina agano lolote na Mungu, mana waliwakataa manabii wote waliotumwa kwake. Ukitaka uhusiano wako na Mungu ww mkaribiee tu nae atakukaribia (Yak 4:8)
 
Hapana mkuu unabii kutimia sio justification ya ubaya unaofanyika.... Yesu angeweza kukubalika na waisrael wote ila angeuawa na hata warumi ila shida inaanza pale warumi waligoma kumuua walimuona hana kosa ila wayahudi wenyewe ndio wakamsaliti ukizingatia alitumwa kwao kuwakomboa!!! Hapo ndio shida ilipoanzia. Na ndio maana Yesu akasema haya baada ya kumkataa.

Mathayo 21:43
42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko,Jiwe walilolikataa waashi,Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni;Neno hili limetoka kwa Bwana,Nalo ni ajabu machoni petu?
43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.

Bro yani sina shida kabisa na mtizamo wako, hongera kwako. Ninapopapenda mimi ni mafunuo ya kifikra na sio kimwili kama wengi wanyoamini au kuelewa. Kwamba hata hadithi ya kuanguka kwa kuta za Yeriko kwa kupuliza tu tarumbeta na sauti ni swala la kifikra na sio kimwili.Kila mtu anatakiwa aifikie kanaani yake na kuna kuta za kifikra zinatuzuia bila kujua. Yani ufalme wa mbinguni utanyakuliwa na wenye nguvu, sio nguvu za gym bali za kifikra/kiroho. Kuna namna ya kufikiri sawa sawa. Ukianzisha Uzi juu ya mada hii nitag
 
Back
Top Bottom