Ndio Hugo kwenye avatar pia etii..Hapana mm n ke
Kukwesa??Kikwetu ngambo ngali ni sigara kali ni njia ya kistaarabu ya neno bangi.Njia pekee ya kuinua ari ya wanyonge, wadhulumiwa na wenye viraka kuwafanya wawe na sauti.
Mo mumo, linga utikukwesa ulindemaKukwesa??
Nyani mkindu tumkindulepamoja na jingalao na nyani mkindu
Dah..mimi niko nyuma sana kwa kweli!Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?
Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.
Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.
Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.
Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.
Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukumbi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.
Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.
Pole sanaMtoto wa baba- kwa sababu nimelelewa na baba tangu nikiwa mdogo sana.
Jina langu linaashiria kwamba mimi ni kijana kweli tena alozaliwa mhula wa mwisho wa Rais Mwinyi ila tu nilianza ujasiriamali nikiwa mdogo maana mama yangu alitangulia mbele za haki kipindi cha mkapa.Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?
Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.
Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.
Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.
Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.
Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukumbi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.
Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.
[emoji839]Kisoda,ni kifuniko/mfuniko/kizibo wa chupa ya soda.
Nalitumia hili kutokana na kumbu kumbu za shule za awali enzi zile za mwalimu,unatunga viiingi kwenye kijiifito na kamba mfano wa upinde ili upate jifunxa kuhesabu(macalculee flan nyakati hizo).
Pia kama ilivyo matumizi yake ni kuziba/kuzuia kitu kisitoke/mwagika.Kwa maana hiyo kwangu ikitokea nimekereka/kerwa hua na amua kukaa kimya kwa muda nikitafakari kulikoni iwe hivyo,kuepusha kutoa kauli ambayo inaweza kuwa mbaya zaidi upande wa pili ama kwangu pia.
Natumia Kisoda2 ikiwa ni mfuniko tu hata uniudhi vipi nitanyamaza kwanza kisha nikutafutie jibu/neno sahihi la kukupa.
Post ya octoba...
Kama ni hamu mm nishakufa
Njopino ni jina la muhusika mkuu kwenye riwaya yangu niliyoianza kuitunga na kuiandika kwenye pc yangu mwaka 2014 na ilipofika 2017 ilibaki sura moja ya mwisho nikamilishe kitabu kizima pc ikazima gafra nilivyopeleka kwa fundi akafuta kila kitu pc ikawa empt Hadi ile riwaya, niliumia sana, sikuwa hata na hard copy ya ile riwaya nikavunjika moyo sikuiandika tena, nikabaki na jina tu humu jf.
Sent using Jamii Forums mobile app
hahahahahahahKama ni hamu mm nishakufa
Siku nykngine usinfanyie Ivo napata tabu sanaMtoto wa Baba postt: 30262595 said: