Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

mtuwatu katika maisha mtu lazima akutane na mtu mwingne na hapo ndpo uzuka watu, na kingne mtu ni watu, hakuna mafanikio ya mtu pasipo watu kuhusishwa nao.. mtuwatu ni bonge la jina tena lenye maana zaidi ya1000
 
Mimi hii ID yangu ni jina langu halisi, "I am Bless" tafsiri yake mimi ni Bless, "Bless" ni jina langu la kuzaliwa nililopewa na mama, na nimeamua kutumia jina hili pia kama ID yangu humu Jf,
 
Asee nkiw mgambo jkt 2014 mafunzo ya mujibu,hii ilikuwa kombania yangu ....vituko Sana kipindi hicho
 
King ni jina langu halisi na Y ni jina la pili yaani Yen
 
Mkuu mbona huyu dada wa kwny avatar yako umemnyima ziwa, kakukosea nn dada wawatu bhas at least ungempa hata chura..
Real person na yuko hivyo huyo msela wangu huyo tungekuwa tunafahamiana ningeonesha potrait za kufa mtu z huyo mdada hakuna imagination hapo
 
GENTAMYCINE ni Mghani ( Waswahili mnaita Rapa sijui Repa ) ila Wakongo ( Wazairwa ) wanaita ' Atalaku ' na Wafaransa wanaita ' Animateur '. Kama kuna Repa / Rapa ambaye Bendi ya Wenge Musica BCBG huwa ikienda Kupiga mahala popote pale iwe Afrika au Ulaya au Marekani halafu GENTAMYCINE majina yake halisi yakiwa ni Pitshou Lisimo hayupo basi kuna uwezekano mkubwa sana hiyo ' Show ' ama ikaboa au hata isijaze Watu kihivyo.

Baada ya Kuondoka kwa Marepa / Marapa wa mwanzoni wa Bendi ya Wenge Musica BCBG akina Roberto Wunda Enkokota ( ambaye sasa anaumwa Saratani ya Koo na yupo zake huko nchini Ufaransa ) na baadae Mwalimu wa Marepa / Marapa wengi Congo DR Tutu Caludgi majina yake kamili akiitwa Yombo Lumbu aliibuka huyu Rapa / Repa GENTAMYCINE au wengine humuita ANTIBIOUTIQUE ambaye ameweza kuiweka Bendi nzima ya Wenge Musica BCBG chini yake Rais mwenyewe Jean Bedele Tshituka Mpiana ( JB Mpiana ) hapo juu ilipo.

Rapa / Repa huyu GENTAMYCINE ni Mchangamfu, Mbunifu na ni Mjanja Mjanja mno bila kusahau pia kuwa ana Kiwango Kikubwa sana cha Elimu tena ya Chuo Kikuu ila hakupenda Kuitumia Elimu yake kwa kile alichosomea na badala yake akaamua aendeleze Kipaji chake cha Kuimba na hasa hasa Kughani huko na kwakweli amekuwa ni ' Kivutio ' kikubwa sana wa Wapenzi wa Muziki wengi wa Congo DR na ndiyo roho nzima ya Bendi kwani asipokuwepo Yeye basi hakuna starehe wala raha tena kutokana na kwamba ana Vitu ' adimu ' sana ambavyo huwezi Kuvikuta kwa Marepa wengine wa Kizazi chake kama Kerozene ( jina kamili ni Eyale Kalondji ) aliyekuwa Rapa / Repa wa Bendi ya Quarter Latin ya Koffi Olomide, Brigade Sabateur ( jina kamili Rwinga Keps ) aliyekuwa Rapa / Repa mahiri wa Wenge Musica Maison Mere yake ' Mtaalam ' wa Kung Fu na Mmiliki wa Black Belt Ngiama Makanda Werrason na Kila Mbongo ( jina kamili Mazikou Ghislain ) aliyekuwa Rapa / Repa wa Bendi ya Extra Musica Zangul chini yake Mpiga Solo hatari sana wa Kizazi cha Pili Roga Roga ( jina kamili ni Ibambi Ikombi )

Na huu ndiyo ' Uzao ' kamili wa hii ID yangu hapa Jamvini JamiiForums nikiamini ya kwamba matendo yangu mengi hapa na uwasiliwashi wangu wa mambo mbalimbali basi navivaa vizuri mno Viatu vya Rapa / Repa wangu Kipenzi kabisa wa Bendi ya Wenge Musica BCBG Pitshou Lisimo a.k.a GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE.

Kila la kheri,
Umetisha
 
Mwanzoni nilikuwa natumia ID moja, ikikuwa maarufu sanaa humu hasa kipindi cha uchaguzi, baada ya sekeseke la lowassa na vijana wa IT, nikabadili ID nikajiita Id nyingine ile nayo nikaona miyeyusho,

Hii sasa ni baada ya Bibi yangu kuniambia utakuja kuwa Mangi kweli,
Kama si juwa na mapesa mingimingi basi hata Rais.

Kwasasa naona pesa ndo zinakuja taratibu na wosia kutimiaa.
Nikifika 35s nitakuwa tajiri mkubwa tz.
Sasa chief hizo connection naomba unishirikishe. Hata kua follower wako
 
Nilikuwa na Id moja longtime ikihusisha jina la ukoo wangu,jina maarufu kidogo na kote nilikopita mtaani,skuli,chuo na hata job natumia hilo jina.
Kisa kilichonifanya niibadili hii Id ni siku moja nilipodondosha uzi,akatokea mdau mmoja na kuleta za kujuana,tokea hapo nikaona ni kheri kuwa na Id tatanishi kidogo.
Id niliyonayo sasa imetokana na kusimamia kweli/haki/kutoyumba kwenye maamuzi na ukizingatia na dini yangu, wadau huwa wananiita kwa Id hiyo.
23 ni tarehe yangu ya kuzaliwa..
 
Jina la babu wa babu.Juzi nilithimuliwa story na mzee kuhusu family tree yetu naona hili jina sikupaswa kulitumia n ndg ila sio wa karibu kama nilivyokuwa nadhan.
 
Back
Top Bottom