Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Mimi hii ID yangu ni jina langu halisi, "I am Bless" tafsiri yake mimi ni Bless, "Bless" ni jina langu la kuzaliwa nililopewa na mama, na nimeamua kutumia jina hili pia kama ID yangu humu Jf,
verified User...! Moderator nendeni mitamboni.
 
Pole sana kaka
Njopino ni jina la muhusika mkuu kwenye riwaya yangu niliyoianza kuitunga na kuiandika kwenye pc yangu mwaka 2014 na ilipofika 2017 ilibaki sura moja ya mwisho nikamilishe kitabu kizima pc ikazima gafra nilivyopeleka kwa fundi akafuta kila kitu pc ikawa empt Hadi ile riwaya, niliumia sana, sikuwa hata na hard copy ya ile riwaya nikavunjika moyo sikuiandika tena, nikabaki na jina tu humu jf.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
DE ni kifupi cha jina la babu yanguu alafu MISS nimetoa herufi moja ya mwanzo kwenye jina la baba angu hii ilitokea kipindi nipo form one tukiwa tunatengeneza a.k.a hivyo nikatengeneza hiyo ya kwangu na ni jina nililolitumia nikiwa o level
@Demiss tafadhali njoo utuambie asili ya Jina lako mrembo wa DOM

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Asili ya jina langu ni wakati nafikiria kujiunga rasmi jamii forum 2017 niliugua, nikaenda hosipitali nikapewa dawa, kilichotokea baada ya kutumia dawa ile dawa ikaniletea madhara makubwa sana kuliko tatizo lililokuwa linanisumbua, daktari akaniambia ni adverse effect ya dawa, na hapo ndipo nilipoacha kutumia dawa na nikatumia adverse effect kama ID wakati naendelea kutaabika na madhara yaliyosababishwa na dawa niliyotumis.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asili ya jina langu ni wakati nafikiria kujiunga rasmi jamii forum 2017 niliugua, nikaenda hosipitali nikapewa dawa, kilichotokea baada ya kutumia dawa ile dawa ikaniletea madhara makubwa sana kuliko tatizo lililokuwa linanisumbua, daktari akaniambia ni adverse effect ya dawa, na hapo ndipo nilipoacha kutumia dawa na nikatumia adverse effect kama ID wakati naendelea kutaabika na madhara yaliyosababishwa na dawa niliyotumis.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole Sana mkuu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini huenda kila mmoja wetu hapa Jamii Forums ana chanzo/sababu mahsusi ya kuja na ID yake aidha kuna jambo/tukio lilimvutia/huzunisha hivyo kuja na Id fulani.Binafsi Id yangu ilitokana na kipindi fulani kufanya kazi kwenye 'Camp' moja ya wakimbizi hivyo wakati huo ndo nimeanza kuingia Jf kama Guest kabla ya kujiunga rasmi.Neno 'cmp' nimefupisha neno camp.
 
Back
Top Bottom