Je, kama kila ukijaribu myamalize ila mpenzi wako haoneshi kutaka yaishe je kuachana hapo ni uamuzi mzuri?

Asante sana kwa

Asante sana kwa Mchango wako nimekuelewa vizuri
 
kusikia kwa kenge mpaka atoke damu, toka jana unaambiwa kuwa mwanamke huyo achana naye lakini hutaki kuelewa sasa naanza kuelewa tatizo linalokusumbua ni wewe kuwa GIGOLO.
🤣😅 kabla ya maamuzi sijaona vibaya kuja kuchukua busara zenu
 
Songa mbele ndugu ukimuona mwanamke wako hataki suluhu jua kuna mwamba anamtia kibri.Nikupe stori kuna rafiki yangu alikuwa anamtaka kabinti yuko twenty years halafu mshikaji wangu ni mkubwa akawa anamcheki yule kisichana sasa kuna siku tukakipanga kile kisichana tukakipeleka out maeneo executive plus kausafiri juu.Tulivyokuwa out kale kasichana kakawa kanapigiwa simu na mchizi wake ikawa hapokei basi mshikaji akamaindi,yule msichana hakumtafuta tena mshikaji ila mshikaji ikawa anamcheki demu halafu demu anamzingua mwamba kwa kuwa alishakuwa na mshikaji wangu plus outing ..kiufupi demu akimpata anayekuzidi huwa anakupotezea mazima.
 
Mkuu pole sana Mahusiano yanakutesa sana inaonekana. Formula ni hii kama mwanaume mapenzi kwako yawe last option usiyaforce kabisa.

Hawa wanawake wanatabia hii pale ambapo unaonesha kumpenda sana, kumjali ataanza kukuona boya. Hapo ambapo unamlazisha muyamalize unazidi kumweka mbali na wewe. Hapo anaona bila yeye wewe ni punda atakutesa sana.

Hapa inatakiwa uendelee na maisha yako kama ni kutafuta hela tafuta kwa hasira. Kula kwa bidii fanya mazoezi, toka out na marafiki zako have funny. Taratibu utazoea na utaenjoy maisha, fanya mambo yako sahau kama ulishawai kuwa naye.

Akikutext usimjibu haraka wewe endelea na mambo yako ikiwezekana mjibu badae sana. Usimpigie simu wala kutuma msg, kama anakupenda atakutafuta mwenyewe myajenge. Hicho kitendo unachofanya unakosea hapo ndo unafanya upendo juu yako uendelee kufa.

Usiumize kichwa kama wako ni wako tu. Ukianza huo ujinga wa kumpigia simu na kumlazimisha utampoteza.
 
Asante sana mkuu nimekuelewa vizuri
 
Ni yile single mother wako mwenye watoto wanne mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…