Je, kanuni na sheria za Uchaguzi kwa taifa letu zinaruhusu mtu mwenye uraia pacha kugombea nafasi nyeti ya urais?

Je, kanuni na sheria za Uchaguzi kwa taifa letu zinaruhusu mtu mwenye uraia pacha kugombea nafasi nyeti ya urais?

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
Wakuu leo katika press conference ya Ndugu Humphrey PolePole nimemsikia akisema kwamba ana taarifa kwamba kuna mgombea wa Urais ameshapata uraia wa nchi nyingine, ndio maana anachochea watu kufanya vurugu baada ya uchaguzi.

Je, sheria na kanuni za uchaguzi mkuu wa nchi yetu zinaruhusu mtu aliye na uraia pacha kugombea nafasi nyeti kama ya urais?

Kama taarifa hizi ni za ukweli, je Tume ya Uchaguzi inaweza kuingilia kati jambo hili? Kama taarifa hizi ni za uongo, je ndugu Humphrey Polepole kama msemaji kwa niaba ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi atasababisha chama chake kuwajibishwa kwa kutoa taarifa za uongo na upotoshaji?

Sheria ni msumeno na haina budi kukata pande zote.
 
Raia wa Ubelgiji anagombea urais Tanzania.

Ubaya ni kutosema ukweli kuwa una uraia wa nchi mbili
 
Achana na huyo Pole Pole.
Ni mtu wa kupuuzwa tu.
Anaropoka kila upumbavu unaotokea kichwani mwake.
Kwa sasa hata wanaCCM wanamuona ndio anawaharibia chama chao.
 
Hivi nyie ni wajinga kiasi gani mpaka mufikirie ni rahisi kupata uraia wa Belgium kiasi hicho?
Acheni upuuzi wenu
 
Rabda kuna raia wa Burundi anayegombea Urais.... Maana kuna maneno mengi yashasemwa huko nyuma. Na pia kuna Akina Rungwa nasikia jwao Kigoma. Anaweza kuwa na utata kama Akina Kakobe.
 
Kuishiwa sera huko. Nyerere alisema watu wakiishiwa sera wanajipambanua kwa ukabila, udini... CCM wameishiwa sera.
 
Lissu hizo sifa za kuwa raia atazitoa wapi?

If you are an adult, you can acquire the Belgian nationality.
...
1.being registered in the population register.
2. staying legally in Belgium for at least 5 years.
3. showing knowledge of one of the national languages.
4. showing social integration and participation in economic life.
 
Achana na siasa mfu za Chakubanga. Unauliza kuruhusu kugombea hali ya kuwa taifa haliruhusu raia wake kuwa na uraia wa nchi mbili. Kwa namna alivyobanwa Magufuli saa hizi angekuwa ameshapata uchochoro wa kupita bila kupingwa.
 
Mpaka sasa kuna mgombea na ameshashika madaraka makubwa nchi hii ni raia wa nchi jirani
 
Hakika mwaka huu Lissu anayachezesha maccm ngoma kadiri apendavyo. Kiukweli wamepoteana!

Yaani nguvu ya wasanii 100, nguvu ya kufanya siasa peke yao kwa miaka yote mitano, nguvu ya kujimilikisha vyombo vyote vya habari, nguvu ya kuwahonga wabunge na madiwani njaa, nguvu ya kubandika mabango ya mgombea wao nchi nzima, vyote hivi vimegonga mwamba!

Lissu ni noma aisee!
Wamekata moto kitambo.
Alafu wakijaribu kuvuruga uchaguzi tutawazalisha kabla ya siku zao!
 
Hayo ni matapolo ya ccm usiwe na wasiwasi, ccm inajifia hivyo.
 
Back
Top Bottom