Je, Katiba yetu inamruhusu Rais Samia kukaa miaka 15 Ikulu?

Je, Katiba yetu inamruhusu Rais Samia kukaa miaka 15 Ikulu?

Mleta mada umetumia neno “kukaimu” vibaya na neno hilo linaweza kupotosha mada nzima. Kukaimu ni kushikilia madaraka kwa muda. Rais SSH alikaimu siku toka JPM alipokufa mpaka siku anaapishwa! Baada ya kuapa alishika madaraka ya uRais.

Katiba ya Tanzania inatambua muhula kuwa miaka mitano na hairuhusu kuongoza kwa zaidi ya mihula miwili, bila kujali mhula mmoja kati ya hiyo miwili ni miaka mitano kamili au pungufu. Ndio maana inaeleza kitakachotokea kama Rais aliye madarakani atakufa na atarithiwa na makamu wake. SSH angekuwa na nafasi ya kuongoza zaidi ya miaka 10 kama Rais JPM angekuwa amekuwa madarakani kwa zaid ya robo tatu ya muhula (JPM alitufa takribani miezi 6 baada ya kuapishwa) na hivo kipindi kilichobaki kitahesabiwa kwa Rais SSH (ndio maana inaitwa Serikali ya awamu ya sita)!! Na awamu ya Rais haizidi mihula miwili.

Namna pekee ya SSH kuwa mgombea wa 2030-35 ni kufanya kama wengine walivofanya - kutumia Bunge kubadilisha matakwa ya Katiba.

Hii ni awamu ya sita na kama anataka kuwa mgombea 2030 aanze kusema hii bado ni awamu ya tano na kwamba bado anakaimu madaraka ya Rais (jambo gumu kusema kwa sababu hawezi kuwa anakaimu wakati yeye sio Makamu wa Rais kama Katiba inavyotaka).
Nashukuru sana mkuu kwa kunirekebisha na pia kunielekeza kuhusu ufasaha wa utumiaji wa neno "kukaimu" basi ngoja kwa pamoja neno gani litafaa kutumika sawa pia ulivyoelezea kuhusu upande wa katiba ingawa mimi sina uzoefu sana na katiba nadhani kuna namna ambavyo wajuzi wa haya mambo wanapotumia maneno yaliyo katika katiba huyafanya nukuu kwa namna yao kama "kivifungu" vile unaweza ukanisaidia nukuu ili nipitie na mimi hiyo katiba au umeeleza vyema kwa namna unavyojua?
 
Heshima kwako Pascal
Ni kweli mleta mada amekosea kwa kutumia neno kukaimu Uraisi
Pamoja na hilo, ameleta hoja nzuri na fikirishi ( atleast kwa tusio na uelewa wa kutosha wa Katiba, japo najua kuna wengine ni wasomi wa sheria na hawana jibu la uhakika kwenye hili swali)
Mleta mada katoa mifano iliyoibua hoja yake ( maraisi wa Zambia, Burundi nk) hivyo ni swali lenye mashiko na lenye reasoning nyuma yake.
Ni kweli watanzania wengi ni viazi (na huo ndiyo mtaji wa CCM) Na watu ‘viazi’ wanazidi kuongezeka humu jukwaani, lakini swali lililoulizwa hapa lina mashiko maana sio kila mtu ana fursa ya kuijua katiba kama uijuavyo wewe.
Nikuombe sasa atleast utuambie katiba inasemaje kwenye hili au specifically kwanini Mh Rais Samia hawezi kugombea 2030.
Ok,Nashukuru sana kwa kutumia neno kukaimu inavyoonekana sijatumia neno tajika lakini wote hueleza sijatumia neno tajika lakini hawatoi neno mbadala linalofaa kutumika ngoja tuzidi kufikiria neno mbadala kwa pamoja.
Nashukuru kwa kukubali hoja kuwa ina mashiko kwa kuzingatia mifano niliyotoa.
Kweli huenda wapo hao "viazi" kati ya waTanzania lakini kwa mfano kama wewe ni mmiliki wa chombo cha moto fundi anaweza akakushangaa kuwa hujui "differential" inavyofanya kazi na kukuita "kiazi".
Na suala la ugeni humu jamvini nadhani nipo ni mwaka wa kumi+ toka nimejiunga.
Ila nashukuru kwa mawazo yasiyo na "quotation" yeyote kutoka kwenye hiyo katiba unayoijua.
 
oCeTF.jpg
 
SSH amemkaimu nani?

Na huyo aliyekaimiwa yupo wapi, na anatarajia kurudi lini kwenye kiti chake?!

Anyway, SSH hajakaimu bali ni Rais Kamili kwa mujibu wa katiba yetu!!
Sawa mkuu hapo niiweke vipi sentensi nitoe neno kukaimu niweke neno gani? Na pia katiba imekaaje maana sikuona karatasi la kupiga kura iliyoonyesha SSH akigombea nafasi ya uraisi au niweke neno mteule?
 
𝑴𝒌𝒖𝒖, 𝒖𝒏𝒂𝒊𝒌𝒆𝒋𝒆𝒍𝒊 𝑪.𝑪.𝑴, 𝒂𝒖 𝒏𝒂 𝒘𝒆𝒘𝒆 𝑼𝑵𝑨𝑨𝑴𝑰𝑵𝑰 𝒉𝒊𝒗𝒚𝒐?
P
 
Mkuu Thinker96, kwanza nikupe pole maana kiukweli kabisa, elimu ya katiba bado inahitajika sana kwa Watanzania walio wengi, maana Kiukweli wengi humu ni viazi mpaka basi!.

1. Rais Samia hakaimu urais wa JPM, urais wa JPM ilikoma ile March 17!. Sasa Samia ndiye rais wa JMT na sio kaimu.
4. Hii miaka 4 ya JPM, Samia
anayoimalizia, sio kumshikia JPM, bali ndio term yake ya kwanza. Term yake ya pili ya Samia ni 2025-2030!.

Kiukweli kadri siku zinavyokwenda, ndivyo viazi humu vinazidi kuongezeka!.
Pole!.

P
Umemjibu vizuri sana ,Watanzania wengi bado hatujui katiba yetu
 
P
𝑴𝒌𝒖𝒖,𝒏𝒊𝒎𝒆𝒌𝒖𝒆𝒍𝒆𝒘𝒂! 𝑵𝒊𝒎𝒆𝒆𝒏𝒅𝒂 𝒎𝒑𝒂𝒌𝒂 𝒉𝒊𝒚𝒐 𝒚𝒂 𝑲𝒂𝒚𝒂𝒏𝒛𝒂 𝑷𝒊𝒏𝒅𝒂! 𝑵𝒊𝒎𝒆𝒛𝒊𝒔𝒐𝒎𝒂 𝒕𝒉𝒓𝒆𝒂𝒅 𝒛𝒐𝒕𝒆 𝒌𝒘𝒂 𝒖𝒕𝒖𝒍𝒊𝒗𝒖!
 
Mkuu Thinker96, kwanza nikupe pole maana kiukweli kabisa, elimu ya katiba bado inahitajika sana kwa Watanzania walio wengi, maana Kiukweli wengi humu ni viazi mpaka basi!.

1. Rais Samia hakaimu urais wa JPM, urais wa JPM ilikoma ile March 17!. Sasa Samia ndiye rais wa JMT na sio kaimu.
4. Hii miaka 4 ya JPM, Samia
anayoimalizia, sio kumshikia JPM, bali ndio term yake ya kwanza. Term yake ya pili ya Samia ni 2025-2030!.

Kiukweli kadri siku zinavyokwenda, ndivyo viazi humu vinazidi kuongezeka!.
Pole!.

P
Mkuu P unatumia nguvu sana kuwaelimisha hili
Kama muhula mmoja kwa mujibu wa katiba ni miaka mitano basi ujue kuwe mama hawajaanza muhula hata mmoja
Tukae kwa kutulia mama anaweza ushangaza ulimwengu
 
Sawa mkuu hapo niiweke vipi sentensi nitoe neno kukaimu niweke neno gani? Na pia katiba imekaaje maana sikuona karatasi la kupiga kura iliyoonyesha SSH akigombea nafasi ya uraisi au niweke neno mteule?
Naona taabu kupekua katiba ili kujua ni ibara ipi hasa, isipokuwa ibara husika inasema (nukuu isiyo rasmi)--

Ikiwa rais aliye madarakani atashindwa kuendelea na nafasi yake kama rais, kutokana ama na kuumwa, kufariki, kujihudhuru, au kuondolewa madarakani (impeachment) basi makamu wa rais ataapishwa kushika kiti urais kwa kipindi kilichobaki.

Ikiwa kipindi kilichobaki ni pungufu ya mwaka mmoja (
sina uhakika sana hap), basi rais aliyeapishwa ataruhusiwa kugombea vipindi vingine viwili.

Lakini kama kipindi kilichobaki kinafika miaka 4, rais aliyeapishwa ataruhusiwa kugombea kwa awamu moja tu
!

Sasa basi, kwavile SSH aliapishwa na atakuwa rais kwa kipindi kisichopungua miaka 4, kwa mujibu wa katiba, ataruhusikwa kugombea tena awamu 1 tu, yaani 2025 na akishinda, ataweza kuwa rais hadi 2030.
 
Mkuu P unatumia nguvu sana kuwaelimisha hili
Kama muhula mmoja kwa mujibu wa katiba ni miaka mitano basi ujue kuwe mama hawajaanza muhula hata mmoja
Tukae kwa kutulia mama anaweza ushangaza ulimwengu
Kwa mujibu wa katiba, anaruhusiwa kugombea ONLY 2025 kwa sababu, alipishwa na kuwa rais, ikiwa imebaki miaka 4 na ushee!!!
 
Afadhali vilaza au watu wasio na msimamo, spineless?
Mkuu Thinker96, kwanza nikupe pole maana kiukweli kabisa, elimu ya katiba bado inahitajika sana kwa Watanzania walio wengi, maana Kiukweli wengi humu ni viazi mpaka basi!.

1. Rais Samia hakaimu urais wa JPM, urais wa JPM ilikoma ile March 17!. Sasa Samia ndiye rais wa JMT na sio kaimu.
4. Hii miaka 4 ya JPM, Samia
anayoimalizia, sio kumshikia JPM, bali ndio term yake ya kwanza. Term yake ya pili ya Samia ni 2025-2030!.

Kiukweli kadri siku zinavyokwenda, ndivyo viazi humu vinazidi kuongezeka!.
Pole!.

P
 
SSH amemkaimu nani?

Na huyo aliyekaimiwa yupo wapi, na anatarajia kurudi lini kwenye kiti chake?!

Anyway, SSH hajakaimu bali ni Rais Kamili kwa mujibu wa katiba yetu!!
Sawa mkuu hapo niiweke vipi sentensi nitoe neno kukaimu niweke neno gani? Na pia katiba imekaaje maana sikuona karatasi la kupiga kura iliyoonyesha SSH akigombea nafasi ya uraisi au niweke neno mteule?
 
Sawa mkuu hapo niiweke vipi sentensi nitoe neno kukaimu niweke neno gani? Na pia katiba imekaaje maana sikuona karatasi la kupiga kura iliyoonyesha SSH akigombea nafasi ya uraisi au niweke neno mteule?
Mbona unauliza swali ambalo nimeshakujibu hapo juu?!
 
Back
Top Bottom