Je, kulikuwa na ulazima wa nchi kuingia vitani na Idd Amin?

Je, kulikuwa na ulazima wa nchi kuingia vitani na Idd Amin?

Somo tunalopata kwa vita ya Kagera, Ni kuwa kama ndani kwa ndani hamuelewani/hampo wamoja, Ni rahisi MTU Wa nje kushinda kirahisi.
 
Nawauliza wazee wangu mliokuwa na ufahamu wakati nchi inaingia kwenye vita vya Kagera. Je, kulikuwepo na ulazima wa kuingiza nchi kwenye vita ya Uganda ambayo tangu wakati huo mpaka sasa madhara yake bado yapo dhahiri?

Je, hatukuwa na diplomacy iliyokuwa matured kuepusha hasara ile?

Je hatukuwa na jeshi imara la kuwafurusha wavamizi wa mipaka yetu kimya kimya bila kutangaza vita?

Nisaidieni wazee wangu.
Nadhani hakukuwa na ulazima maana kilichomfanya Idd Amini avamie nchi yetu ni hofu ya Obote ambae baada ya kupinduliwa alikimbilia kwetu tz
Amini akakosa kujiamini akataka Obote aende kokote lakini sio Tanzania ambako ni karibu Sana na Uganda na ni rahisi kwake kujipanga na kumvamia ili kurudi madarakani, pia aliqmini kuwa mtawala wa Tanzania wa wakati huo alikuwa rafiki mkubwa wa hasimu wake
Hapo ndipo ngoma ilipokuwa ngumu.
Amini hajiamini kumwacha Obote aendelee kubaki tz na Mtawala weru hakubali Obote aondoke
Kama VIONGOZI hawa wangeyaweka haya Mambo katika namna nzuri tusingeingia vitani
 
Vita hiyo ni kumaliza hela tu. Kizazi cha zamani kilikuwa brainwashed na "uzalendo". Bora wangetuma radi ikamshughulikie amini.


Na huyo obote aliingia akafanya madudu kisha akaingia Museveni kwa bunduki ambaye mpaka leo yupo na hatoki. Afrika mtu/chama hawezi kutoka madarakani kwa karatasi mpaka bunduki.
 
Mwana kulitafuta mwana kulipata.
Tuliingia vitani kwa sababu tulitengeneza mazingira ya kukwaruzana na Field Marshall Iddi Amin Dadah
1.Amini Alimpindua Milton Obbote akiwa kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola.
2.Mwalimu Nyerere akamkaribisha Obbote aishi Tanzania.
3.Nyerere aliapa kutoitambua serikali ya Iddi Amin.
4.Wafuasi wa Obbote wakaanzisha Vita ya msituni wakitokea Tanzania.
5.Amin akashtukia mipango hiyo ndio mwanzo wa border crash za 1971 na 1972.
6.Iddi Amin alijaribu njia zote kumshawishi Mwl.Nyerere wafanye mahusiano mema lakini Mwl.Nyerere hakuwa na nia dhati ya kushirikiana na Amin.
7.Mauaji ya halaiki na ya kikatili ubakaji,kufukuza wahindi zaidi ya elfu 70 ulilaaniwa na mataifa mengi na kumpa Mwl.Nyerere sababu ya kumuodoa Amin kwa Nguvu.
8.Kilichofuata ni vita vya Kagera, Majeshi ya Amin yalivamia maeneo ya Mkoa wa Kagera na kuyatwaa.Mwl Nyerere alitangaza vita akayadunda na kuyasambaratisha Majeshi ya Amin yaliokuwa yanasaidiwa na Gaddafi.
9.Majeshi ya Amin yalisalim amri,Amin akatoroka kupitia mpaka wa Kenya.
10.Baada ya vita IMF,World Bank walitaka Mwl.Nyerere abadirishe sera za biashara, viwanda,Uchumi na Utawala bora Mwl.Nyerere aliyakataa mapendekezo hayo tukawekewa vikwazo vya kiuchumi .
11.Nchi iliyumba kiuchumi,hali ngumu ikakumba wananchi,kukosekana kwa vyakula,petrol, Sabuni,nguo,madawa, upatikanaji wa vipuli uilikuwa vya shida viwandani,njaa ilikuwa ni shida kweli kweli.
12.Ilifika muda vitendo vya kumuondoa Mwl.Nyerere madarakani vilipanda kasi kubwa.
13.Mwisho Mwl.Nyerere akasalim amri,akangatuka uraisi 1985.
 
Umeuliza maswali na majibu hutapata

Maswali mengine ni haya

Kwa nini tulikosa support ya OAU na UN???

Why Nyerere pia alituhumiwa kufadhili waasi wa Uganda??

Why Nyerere waziwazi aliwaunga mkono waasi wa Nigeria???
 
Umeuliza maswali na majibu hutapata

Maswali mengine ni haya

Kwa nini tulikosa support ya OAU na UN???

Why Nyerere pia alituhumiwa kufadhili waasi wa Uganda??

Why Nyerere waziwazi aliwaunga mkono waasi wa Nigeria???
 
Ilikuwa lazima tuingie vitani kwa gharama yoyote ile kwa kuwa kipande cha ardhi kusini mwa mto Kagera, kilikuwa kimeishatekwa. Uhalali wa vita hiyo au haramu yake, hatuwezi kuijua kwa hakika bila kupata taarifa nyeti za kiinteligensia za wakati huo lakini zaidi sana siasa za wakati huo. Jambo lililo wazi na la uhakika ni kuwa Idd Amini alijipanga kumdhibiti hasimu wake Obbote kwa nguvu zake zote na alijiandaa kuanzia mwaka 1972 alipofanya jaribio la kwanza akashindwa, miaka sita baadae akiwa ameimarisha jeshi lake thabiti alifanikiwa kuingia ndani ya Tanzania kuteka maeneo ya nchi yetu na kufanya uharibifu mkubwa, kibaya zaidi kutangaza eneo liliotekwa kuwa mkoa mpya wa Uganda.

Ndio, nchi ikiwa imevamiwa na kutekwa, hakukuwa na namna yoyote ya kukwepa kuingia vitani. Kitendo cha kumpiga Idd Amini ndani ya Uganda hadi kuikimbia nchi, ilikuwa ni jukumu la waganda wenyewe na Jeshi letu lilikuwa kama walinzi wa amani na watoaji wa ushauri wa kijeshi tu.
 
Mwana kulitafuta mwana kulipata.
Tuliingia vitani kwa sababu tulitengeneza mazingira ya kukwaruzana na Field Marshall Iddi Amin Dadah
1.Amini Alimpindua Milton Obbote akiwa kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola.
2.Mwalimu Nyerere akamkaribisha Obbote aishi Tanzania.
3.Nyerere aliapa kutoitambua serikali ya Iddi Amin.
4.Wafuasi wa Obbote wakaanzisha Vita ya msituni wakiwa Tanzania.
5.Amin akashtukia mipango hiyo ndio mwanzo wa border crash za 1971 na 1972.
6.Iddi Amin alijaribu njia zote kumshawishi Mwl.Nyerere wafanye mahusiano mema lakini Mwl.Nyerere hakuwa na nia dhati ya kushirikiana na Amin.
7.Mauaji ya halaiki na ya kikatili ubakaji,kufukuza wahindi zaidi ya elfu 70 ulilaaniwa na mataifa mengi na kumpa Mwl.Nyerere sababu ya kumuodoa Amin kwa Nguvu.
8.Kilichofuata ni vita vya Kagera, Majeshi ya Amin yalivamia maeneo ya Mkoa wa Kagera na kuyatwaa.Mwl Nyerere alitangaza vita akayadunda na kuyasambaratisha Majeshi ya Amin yaliokuwa yanasaidiwa na Gaddafi.
9.Majeshi ya Amin yalisalim amri,Amin akatoroka kupitia mpaka wa Kenya.
10.Baada ya vita IMF,World Bank walitaka Mwl.Nyerere abadirishe sera za biashara, viwanda,Uchumi na Utawala bora Mwl.Nyerere aliyakataa mapendekezo hayo tukawekewa vikwazo vya kiuchumi .
11.Nchi iliyumba kiuchumi,hali ngumu ikakumba wananchi,ukosekana wa vyakula,petrol, Sabuni,nguo,madawa, upatikanaji wa vipuli uilikuwa vya shida viwandani,njaa ilikuwa shida kweli kweli.
12.Ilifika vitendo vya kumuondoa Mwl.Nyerere madarakani valipata kasi kubwa.
13.Mwisho Mwl.Nyerere akasalim amri,akangatuka uraisi 1985.


Rekebisha hapo
Hatujawahi wekewa vikwazo vya uchumi

Masharti ya IMF na world bank ni masharti Tu
Unapoenda kuomba mkopo na misaada
Haikuwa vikwazo vya uchumi
 
Ulazima ulikuwepo ndiyo maana yakatokea yaliyotokea,,,




Cc: mahondaw
Hatukuwa na ulazima wowote na wala Amin hakuwa na makosa yeyote bali ni Mwalimu kutaka tu kumrudisha rafikiye Obote. Vita ilikuwa na maslai ya kirafiki kati ya Nyerere na Obote. Na watawala wengi duniani wamezigharimu nchi zao kwa masilai yao binafisi. Ndo maana baada kumtoa Amin waliwekwa maraisi takribani 3 na baadaye Obote akarudishwa kutawala uganda. Sema tu walikosana tena na mwalimu wanadai eti alilipa visasi.
 
Ni ngumu sana kufikiria kufanya diplomasia na dikteta, diplomasia pekee ilikuwa kuichukua uganda mazima
Mtu anachukua sehemu ya ardhi yetu na kutaka kuitawala Kijeshi halafu wewe huchukui hatuna yeyote? Fashisti na Dikteta Idd Amin Dada alipata alichokitafuta. Kwa hili sisi Wahenga hatukua na simile. Tulimfuata hadi ndani ya nchi yake na kumfurusha hadi akatokomea na kufia huko Uarabuni.
 
Chanzo cha vita hii ilikua ni ugomvi wa binafsi wa walinzi wa mpaka wa pande zote mbili, aliyesababisha ni Mwanamke malaya. Chanzo cha kutupiana risasi ni hicho. Kama kungekua na diplomasia nzuri tusingefika huko vitani. Pamoja na kuwepo na ugomvi wa siku nyingi kati ya nchi hizi mbili wote walikurupuka au kuchuka advantage ya false kick off.
Full Stop
 
Walikosea strategy, uganda ilitakiwa kufanywa jimbo chini ya Tanzania kwa miaka angalau 30 kabla ya kupewa uhuru.
 
Nawauliza wazee wangu mliokuwa na ufahamu wakati nchi inaingia kwenye vita vya Kagera. Je, kulikuwepo na ulazima wa kuingiza nchi kwenye vita ya Uganda ambayo tangu wakati huo mpaka sasa madhara yake bado yapo dhahiri?

Je, hatukuwa na diplomacy iliyokuwa matured kuepusha hasara ile?

Je hatukuwa na jeshi imara la kuwafurusha wavamizi wa mipaka yetu kimya kimya bila kutangaza vita?

Nisaidieni wazee wangu.
Mtu anaingia ndani ya nyumba yako anaua watoto wako na ku baka mkeo, halafu wataka diplomasia?
Uanaume wako utakuwa wa kusingiziwa!
 
Nawauliza wazee wangu mliokuwa na ufahamu wakati nchi inaingia kwenye vita vya Kagera. Je, kulikuwepo na ulazima wa kuingiza nchi kwenye vita ya Uganda ambayo tangu wakati huo mpaka sasa madhara yake bado yapo dhahiri?

Je, hatukuwa na diplomacy iliyokuwa matured kuepusha hasara ile?

Je hatukuwa na jeshi imara la kuwafurusha wavamizi wa mipaka yetu kimya kimya bila kutangaza vita?

Nisaidieni wazee wangu.
Hiyo Diplomasia itatokea wapi wakati tayari Idi Amin Dada kwa Kusaidiwa na Libya walishaelekeza 'Makombora' yao katika Hospitali ya Bugando Mwanza huku wakiwa wameshawauwa baadhi ya Watanzania wenzetu hasa Mkoa wa Kagera ( Bukoba ) kwa Watani zangu Wahaya?

Jeshi la Tanzania ( JWTZ ) hakuna hata Siku moja limeacha kuwa 'Imara' pamoja na Idara ya Usalama na ndiyo maana Tanzania imesimama vyema. Ulazima wa Vita ulikuwepo kwani Kipimo chetu cha Uvumilivu Kwake Idi Amin Dada na 'Uchokozi' wake ulikuwa umefikia Kikomo.
 
Unajua Idd Amin alikuwa ni mwanaharakati kama Tundu Lisu na aliingizwa jeshini kwa nguvu na siyo kwa hiyari yake.

Sasa watu wa aina ya Amin hawakomagi uchokozi na dawa yao ni kichapo tu hakuna namna bwana mdogo!
Bwashee, Idd Amin aliingia jeshi la mkoloni kwa hiari yake Kama mpishi.
Taratibu akapanda vyeo na kuwa koplo na kuwa mwafrika mwenye cheo cha juu kwenye jeshi hilo na alishiriki upande wa Waingereza kwenye vita ya Mau Mau .Kenya
 
Hata waislam sababu tu peke ya kutangazwa jihadi ni kuvamiwa kwa ardhi yao, hiyo itoshe kuwa sababu ya vita vya Tanzania na uganda kwani amani aliitangazia dunia juu ya kuhodhi baadhi ya maeneo ya Tanzania.
 
Walikosea strategy, uganda ilitakiwa kufanywa jimbo chini ya Tanzania kwa miaka angalau 30 kabla ya kupewa uhuru.
Aise hiyo isingekubalika na OAU/UN kwa sababu tayari Uganda ilikuwa ni nchi huru, hivyo ingepelekea kuwekewa vikwazo vya kiuchumi.
 
Back
Top Bottom