Je, kulikuwa na ulazima wa nchi kuingia vitani na Idd Amin?

Je, kulikuwa na ulazima wa nchi kuingia vitani na Idd Amin?

Nawauliza wazee wangu mliokuwa na ufahamu wakati nchi inaingia kwenye vita vya Kagera. Je, kulikuwepo na ulazima wa kuingiza nchi kwenye vita ya Uganda ambayo tangu wakati huo mpaka sasa madhara yake bado yapo dhahiri?

Je, hatukuwa na diplomacy iliyokuwa matured kuepusha hasara ile?

Je hatukuwa na jeshi imara la kuwafurusha wavamizi wa mipaka yetu kimya kimya bila kutangaza vita?

Nisaidieni wazee wangu

Mjomba, ni ngumu sana kufanya Diplomasia na dikteta. Ukishakuwa Dikteta Maana yake chaguo lake ni USHINDI tu, hivyo diplomasia pekee ilikuwa ni kumuacha Amini afanye anavyotaka yeye.

Hiyo kitu hata mimi nisingeweza kukubali.

Sidhani kama ameshawahi kutokea Rais mwenye Diplomasia kama Mwalimu, Mwalimu was a good listener na alikuwa muelewa sana. Amin alikuwa stupid and ignorant feeding his little ego

Uamuzi wa Mwalimu ulikuwa ni sahihi kwa wakati wake hata kama kwa sasa unaonekana haukuwa sahihi.

Uamuzi wa Azimio la Arusha ulikuwa ni sahihi kwa wakati ule hata kama kwa sasa unaonekana haikuwa sahihi.

Leo Hii ukiangalia Utajiri wa JK na watoto zake, viongozi wakuu wa Serikali, utajiri wa Mkapa na Mke wake , Utajiri wa JPM na viongozi wake utaelewa umuhimu wa Arusha Declaration.
Mwalimu will remain the best ever
 
Baada ya vita tuliishi maisha magumu sana vitu madukani ilikuwa hamna pia dawa hospitalini zikawa hamna kabisa magonjwa ya kuambukiza tukawa tunapona tu kwa usugu wa miili yetu, ndo maana CORONA haijatusumbua maana hali hiyo inakuja ilikuta tuna corana teyari.

Vita vya kumtoa Idd Amin aliyevamia sehemu ya nchi yetu ilikuwa ni lazima , sema ya kumfukuza na kumnyang`anya Uganda yote ndo haikuwa ya lazima na ndiyo iliyotufirisi. Tuliwezeshwa tu kumshinda na Waganda wenyewe maana waliisha mchoka Idd Amin kabisa,
Urafiki was Nyerere na Obote ndio sababu,Nchi kama Nchi haikuwa na ulazima.hats IDD amino kuanza kuchukua kagera ni baada ya Nyerere kumpa Obote hifadhi ya kisiasa.

IDD amini alikuwa hana ugomvi na nyerere tatizo lilianza alipomkaribisha obote, Tanzania.
 
Urafiki was Nyerere na Obote ndio sababu,Nchi kama Nchi haikuwa na ulazima.hats IDD amino kuanza kuchukua kagera ni baada ya Nyerere kumpa Obote hifadhi ya kisiasa.

IDD amini alikuwa hana ugomvi na nyerere tatizo lilianza alipomkaribisha obote, Tanzania.

Kuna Tatizo kumpa Mtu hifadhi ya kisiasa? Sasa huoni kuwa Amin was immature ? Km aliamua kuingia vitani kwa context hiyo !

Mbona lema na wenzie walipewa hifadhi ya kisiasa kenya , je Magufuli ameenda kuikalia TAVETA na ku declare kuwa taveta is his ?

Amin was crazy na vita vilikuwa ni chaguo SAHIHI
 
Nawauliza wazee wangu mliokuwa na ufahamu wakati nchi inaingia kwenye vita vya Kagera. Je, kulikuwepo na ulazima wa kuingiza nchi kwenye vita ya Uganda ambayo tangu wakati huo mpaka sasa madhara yake bado yapo dhahiri?

Je, hatukuwa na diplomacy iliyokuwa matured kuepusha hasara ile?

Je hatukuwa na jeshi imara la kuwafurusha wavamizi wa mipaka yetu kimya kimya bila kutangaza vita?

Nisaidieni wazee wangu
Kwa hakika ukweli utabaki ukweli nyerere alituingiza ktk vita iliyogharimu maisha na mali za watanzania bila sababu zenye maslahi mapana ya taifa
 
Nadhani hakukuwa na ulazima maana kilichomfanya Idd Amini avamie nchi yetu ni hofu ya Obote ambae baada ya kupinduliwa alikimbilia kwetu tz
Amini akakosa kujiamini akataka Obote aende kokote lakini sio Tanzania ambako ni karibu Sana na Uganda na ni rahisi kwake kujipanga na kumvamia ili kurudi madarakani, pia aliqmini kuwa mtawala wa Tanzania wa wakati huo alikuwa rafiki mkubwa wa hasimu wake
Hapo ndipo ngoma ilipokuwa ngumu.
Amini hajiamini kumwacha Obote aendelee kubaki tz na Mtawala weru hakubali Obote aondoke
Kama VIONGOZI hawa wangeyaweka haya Mambo katika namna nzuri tusingeingia vitani
Hapana Tanzania tuliwahifadhi na kuwapa mafunzo waasi wa Uganda ma hao waasi mashambulizi yao dhidi ya amin yalianzia hapa tanzania huo ndo ukweli ulikua na kambi za waasi wa uganda tabora na arusha msiwe vipofu na viziwi nyerere alituingiza vitani na sisi watanzania tulikuwa wachokozi kwa kuhifadhi waasi na kiongozi wao dk milton obote na waliishambulia uganda kutokea bukoba ardhi Tanzania
 
Ilikuwa lazima tuingie vitani kwa gharama yoyote ile kwa kuwa kipande cha ardhi kusini mwa mto Kagera, kilikuwa kimeishatekwa. Uhalali wa vita hiyo au haramu yake, hatuwezi kuijua kwa hakika bila kupata taarifa nyeti za kiinteligensia za wakati huo lakini zaidi sana siasa za wakati huo. Jambo lililo wazi na la uhakika ni kuwa Idd Amini alijipanga kumdhibiti hasimu wake Obbote kwa nguvu zake zote na alijiandaa kuanzia mwaka 1972 alipofanya jaribio la kwanza akashindwa, miaka sita baadae akiwa ameimarisha jeshi lake thabiti alifanikiwa kuingia ndani ya Tanzania kuteka maeneo ya nchi yetu na kufanya uharibifu mkubwa, kibaya zaidi kutangaza eneo liliotekwa kuwa mkoa mpya wa Uganda.

Ndio, nchi ikiwa imevamiwa na kutekwa, hakukuwa na namna yoyote ya kukwepa kuingia vitani. Kitendo cha kumpiga Idd Amini ndani ya Uganda hadi kuikimbia nchi, ilikuwa ni jukumu la waganda wenyewe na Jeshi letu lilikuwa kama walinzi wa amani na watoaji wa ushauri wa kijeshi tu.
Wewe hujui lolote unafuata mkumbo tu jiulize kwa nn nyerere alimpa hifadhi obote? Kwa nn mwl aliwapa kambi za mafunzo waasi wanaomuunga mkono obote kwa nn mwl alikubali waasi waishambulie uganda kutokea ktk ardhi ya tanzania bukoba halafu pia nyerere huyo huyo kamsadia obote kumg'oa amin lkn nyerere huyo huyo akamsadia museveni kumng'oa obote kwa nn? Mwl alituingiza ktk vita isiyo tuhusu wala lazima mwisho wa siku uchumi ukaporomoka tukaumia sisi wananchi kupanga foleni kununua sabuni 'unga' sukari mpk mchele baki wale walio achwa wajane 'yatima nk hapo mwl aliyumba
 
Ulazima haukuwepo tatizo kale kazee ka Ccm kalikuwa hakashauriki kalijifanya kujua kila kitu.Kaliingiza nchi kwenye vita kakaangusha uchumi wa nchi.
 
Mtu anachukua sehemu ya ardhi yetu na kutaka kuitawala Kijeshi halafu wewe huchukui hatuna yeyote? Fashisti na Dikteta Idd Amin Dada alipata alichokitafuta. Kwa hili sisi Wahenga hatukua na simile. Tulimfuata hadi ndani ya nchi yake na kumfurusha hadi akatokomea na kufia huko Uarabuni.
Wewe hujafiwa na ndg yako ndio maana unapayuka tu hakukuwa na sababu ya msingi kuingia vitani kiasi kuporomosha uchumi namna ile' amini hakuvamia zile ni propaganda za kisiasa za mwl ili aweze kutekeleza azma yake amini alipompindua obote mwl alikataa katakata kutambua utawala wake pia ailimhifadhi obote pia waasi wanaomuunga mkono obote walipewa mafunzo na jeshi la tz na wakawa wanaishambulia uganda kutokea bukoba sasa hapo nani mchokozi? Mwl huyu kamsadia obote kuingia madarakani lkn mwl huyohuyo akamsadia museveni kumng'oa obote ambaye alimsadia kumng'oa amini. Usipayuke payuke eti ilikua lazima tuingie vitani ungeenda wewe ukapata kilema au kumpoteza ndg au jamaa yako usingepayuka hivo kama mlevi wa mataptap
 
Kuna Tatizo kumpa Mtu hifadhi ya kisiasa? Sasa huoni kuwa Amin was immature ? Km aliamua kuingia vitani kwa context hiyo !

Mbona lema na wenzie walipewa hifadhi ya kisiasa kenya , je Magufuli ameenda kuikalia TAVETA na ku declare kuwa taveta is his ?

Amin was crazy na vita vilikuwa ni chaguo SAHIHI
Kwani Lema ni Rais ninyi uvccm mtakuwa lini?
 
Wewe hujafiwa na ndg yako ndio maana unapayuka tu hakukuwa na sababu ya msingi kuingia vitani kiasi kuporomosha uchumi namna ile' amini hakuvamia zile ni propaganda za kisiasa za mwl ili aweze kutekeleza azma yake amini alipompindua obote mwl alikataa katakata kutambua utawala wake pia ailimhifadhi obote pia waasi wanaomuunga mkono obote walipewa mafunzo na jeshi la tz na wakawa wanaishambulia uganda kutokea bukoba sasa hapo nani mchokozi? Mwl huyu kamsadia obote kuingia madarakani lkn mwl huyohuyo akamsadia museveni kumng'oa obote ambaye alimsadia kumng'oa amini. Usipayuke payuke eti ilikua lazima tuingie vitani ungeenda wewe ukapata kilema au kumpoteza ndg au jamaa yako usingepayuka hivo kama mlevi wa mataptap
Umemjibu vyema japo umepandisha morali.
 
Mjomba, ni ngumu sana kufanya Diplomasia na dikteta. Ukishakuwa Dikteta Maana yake chaguo lake ni USHINDI tu, hivyo diplomasia pekee ilikuwa ni kumuacha Amini afanye anavyotaka yeye.

Hiyo kitu hata mimi nisingeweza kukubali.

Sidhani kama ameshawahi kutokea Rais mwenye Diplomasia kama Mwalimu, Mwalimu was a good listener na alikuwa muelewa sana. Amin alikuwa stupid and ignorant feeding his little ego

Uamuzi wa Mwalimu ulikuwa ni sahihi kwa wakati wake hata kama kwa sasa unaonekana haukuwa sahihi.

Uamuzi wa Azimio la Arusha ulikuwa ni sahihi kwa wakati ule hata kama kwa sasa unaonekana haikuwa sahihi.

Leo Hii ukiangalia Utajiri wa JK na watoto zake, viongozi wakuu wa Serikali, utajiri wa Mkapa na Mke wake , Utajiri wa JPM na viongozi wake utaelewa umuhimu wa Arusha Declaration.
Mwalimu will remain the best ever
Mwl ni dikteta kuliko idi amini amini usiamini mwl ni snitch mwl huyo huyo kamsadia obote kuingia madarakani lkn mwl huyo huyo akamsadia museveni kumng'oa obote mobutu seseko unaujua usnitch wa mwl labda best ever kwa malofa wasio na uelewa kama wewe
 
Kwani Lema ni Rais ninyi uvccm mtakuwa lini?
Usimfananishe lema na obote' lema kapewa hifadhi yeye kama yeye kwa mujibu wa sheria za kimataifa pia lema hana wanamgambo wanaopewa mafunzo nchini kenya 'kama ilivokuwa kwa obote ambaye wanamgambo waliokuwa wanamuunga mkono walikuwa na kambi ktk ardhi ya tz na mafunzo walipewa. na jeshi letu pia walikuwa wanashambulia uganda kutokea ardhi ya tz
 
Kwa kweli mwl aliingiza nchi ktk vita na mateso ya mporomoko wa uchumi wetu bila sababu ya msingi na kuacha makovu makubwa kina mama kuwa wajane watoto kuwa yatima na wafanyabiashara kufilisika kwa hilo na mengine mengi tusioyajua atajibu kwa mungu
 
Usimfananishe lema na obote' lema kapewa hifadhi yeye kama yeye kwa mujibu wa sheria za kimataifa pia lema hana wanamgambo wanaopewa mafunzo nchini kenya 'kama ilivokuwa kwa obote ambaye wanamgambo waliokuwa wanamuunga mkono walikuwa na kambi ktk ardhi ya tz na mafunzo walipewa. na jeshi letu pia walikuwa wanashambulia uganda kutokea ardhi ya tz
Mkuu hukunielewa nilimjibu uvccm aliyemfananisha Lema na Rais Obotte.
 
Mwl ni dikteta kuliko idi amini amini usiamini mwl ni snitch mwl huyo huyo kamsadia obote kuingia madarakani lkn mwl huyo huyo akamsadia museveni kumng'oa obote mobutu seseko unaujua usnitch wa mwl labda best ever kwa malofa wasio na uelewa kama wewe

..Mwalimu hakumrudisha Obote madarakani.

..baada ya Iddi Amini kufukuzwa Waganda waliunda serikali ya mpito.

..Maraisi walioongoza serikali ya mpito walikuwa ni Prof.Yussuf Kironde Lule, Godfrey Lukongwa Binaisi, na Paul Muwanga.

..serikali ya mpito iliandaa uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1980 ambapo chama cha UPC kilichokuwa kikiongozwa na Obote kilishinda.

..Milton Obote hakupinduliwa na Museveni, bali alipinduliwa kutokana na maasi ya askari wa kabila la Acholi walioongozwa na Brigadier Basilio Olara-Okello.

..Basilio Olara-Okello aliongoza baraza la mapinduzi kwa muda mfupi na kumuachia madaraka General Tito Okello Lutwa, ambaye alikuja kupinduliwa na Yoweri Museveni mwaka 1986.
 
..Mwalimu hakumrudisha Obote madarakani.

..baada ya Iddi Amini kufukuzwa Waganda waliunda serikali ya mpito.

..Maraisi walioongoza serikali ya mpito walikuwa ni Prof.Yussuf Kironde Lule, Godfrey Lukongwa Binaisi, na Paul Muwanga.

..serikali ya mpito iliandaa uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1980 ambapo chama cha UPC kilichokuwa kikiongozwa na Obote kilishinda.

..Milton Obote hakupinduliwa na Museveni, bali alipinduliwa kutokana na maasi ya askari wa kabila la Acholi walioongozwa na Brigadier Basilio Olara-Okello.

..Basilio Olara-Okello aliongoza baraza la mapinduzi kwa muda mfupi na kumuachia madaraka General Tito Okello Lutwa, ambaye alikuja kupinduliwa na Yoweri Museveni mwaka 1986.

Tuongee ukweli pia
Kwanini hatukupata baraka za UN wala OAU
Kumtoa Amin??

Je wanamgambo waasi wa Iddi Amin hatukuwapa mafunzo na support??
 
..Mwalimu hakumrudisha Obote madarakani.

..baada ya Iddi Amini kufukuzwa Waganda waliunda serikali ya mpito.

..Maraisi walioongoza serikali ya mpito walikuwa ni Prof.Yussuf Kironde Lule, Godfrey Lukongwa Binaisi, na Paul Muwanga.

..serikali ya mpito iliandaa uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1980 ambapo chama cha UPC kilichokuwa kikiongozwa na Obote kilishinda.

..Milton Obote hakupinduliwa na Museveni, bali alipinduliwa kutokana na maasi ya askari wa kabila la Acholi walioongozwa na Brigadier Basilio Olara-Okello.

..Basilio Olara-Okello aliongoza baraza la mapinduzi kwa muda mfupi na kumuachia madaraka General Tito Okello Lutwa, ambaye alikuja kupinduliwa na Yoweri Museveni mwaka 1986.

Na kwanini Mwalimu Nyerere aliunga mkono
Waasi wa Biafra kinyume na misimamo ya OAU wala ma Rais wengine Afrika?
 
..Mwalimu hakumrudisha Obote madarakani.

..baada ya Iddi Amini kufukuzwa Waganda waliunda serikali ya mpito.

..Maraisi walioongoza serikali ya mpito walikuwa ni Prof.Yussuf Kironde Lule, Godfrey Lukongwa Binaisi, na Paul Muwanga.

..serikali ya mpito iliandaa uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1980 ambapo chama cha UPC kilichokuwa kikiongozwa na Obote kilishinda.

..Milton Obote hakupinduliwa na Museveni, bali alipinduliwa kutokana na maasi ya askari wa kabila la Acholi walioongozwa na Brigadier Basilio Olara-Okello.

..Basilio Olara-Okello aliongoza baraza la mapinduzi kwa muda mfupi na kumuachia madaraka General Tito Okello Lutwa, ambaye alikuja kupinduliwa na Yoweri Museveni mwaka 1986.
Ukweli ushajulikana ndugu kaa pembeni.Umewahijiuliza kwanini Nyerere aliamua kuhifadhi waasi wa IddiAmnin Kagera na Taboro?
 
Back
Top Bottom