Je, kuna fidia yoyote ya kulea mtoto wa kusingiziwa?

Je, kuna fidia yoyote ya kulea mtoto wa kusingiziwa?

Chaz Joe

Member
Joined
Jul 3, 2019
Posts
12
Reaction score
38
Habari zenu wadau!, nahitaji ufafanuzi kidogo hapa, nilikuwa na Girlfriend wangu ambaye alipata ujauzito na kuniambia kwamba ni ujauzito wangu. Tangu hapo niliamua kwa upendo tu kumhudumia katika kipindi chote cha ujauzito hadi alipojifungua. Japo sikuwa naishi nae lakini nilimpatia mahitaji yote aliyokuwa akiniambia. Baada ya mtoto kuzaliwa, niliendelea kumhudumia hadi akafikisha umri wa miaka 10.

Sasa naona mwanamke huyu amebadilika mno na anatumia hiyo kama fursa ya kunikandamiza, maana anadai matumizi ambayo ni makubwa kiasi cha kunifanya nione kabisa ananitumia kwa masilahi yake kwa kisingizio cha mtoto.

Basi baada ya hayo, nikaona suluhisho ni mimi kumchukua huyo mtoto nikae nae, nimhudumie mimi mwenyewe. Lakini mama yake aligoma, kilichofuata hapo ikawa ni migogoro daily.

Wakati migogoro hiyo ikiendelea, ndipo mama wa mtoto ananiambia kuwa huyu sio mtoto wangu, kitu ambacho kimeniuma sana na kunivunja moyo. Nikapatwa na hasira sana

Sasa nimeleta hili suala kwenu wadau mnisaidie, je kuna sheria yoyote ya kudai fidia kwa gharama zote nilizotoa kumlea huyu mtoto kwa kipindi chote hicho, hadi kufikia hapo ambapo mama yake anadai kuwa sio mtoto wangu?? Na kama ipo sheria ,je utaratibu upoje??
 
Habari zenu wadau!, nahitaji ufafanuzi kidogo hapa, nilikuwa na Girlfriend wangu ambaye alipata ujauzito na kuniambia kwamba ni ujauzito wangu. Tangu hapo niliamua kwa upendo tu kumhudumia katika kipindi chote cha ujauzito hadi alipojifungua. Japo sikuwa naishi nae lakini nilimpatia mahitaji yote aliyokuwa akiniambia. Baada ya mtoto kuzaliwa, niliendelea kumhudumia hadi akafikisha umri wa miaka 10.

Sasa naona mwanamke huyu amebadilika mno na anatumia hiyo kama fursa ya kunikandamiza, maana anadai matumizi ambayo ni makubwa kiasi cha kunifanya nione kabisa ananitumia kwa masilahi yake kwa kisingizio cha mtoto.

Basi baada ya hayo, nikaona suluhisho ni mimi kumchukua huyo mtoto nikae nae, nimhudumie mimi mwenyewe. Lakini mama yake aligoma, kilichofuata hapo ikawa ni migogoro daily.

Wakati migogoro hiyo ikiendelea, ndipo mama wa mtoto ananiambia kuwa huyu sio mtoto wangu, kitu ambacho kimeniuma sana na kunivunja moyo. Nikapatwa na hasira sana

Sasa nimeleta hili suala kwenu wadau mnisaidie, je kuna sheria yoyote ya kudai fidia kwa gharama zote nilizotoa kumlea huyu mtoto kwa kipindi chote hicho, hadi kufikia hapo ambapo mama yake anadai kuwa sio mtoto wangu?? Na kama ipo sheria ,je utaratibu upoje??
Kapime DNA kwanza.
 
Lea mtoto mkuu.Huyo mtu unayemuita "gerofrend" ana tabia za ukibaka tu.Ameshajua pa kukushika na wewe umeelekea kibla bila shuruti.Kubali kuwa Joseph baba mlishi.Hamna namna.
Mkuu hii kitu inatia hasira sana, usipojizuia unaweza jikuta hata umeua mtu. Imagine nimehudumia kwa kipindi chote hicho, alaf sasahivi anakuja kuniambia kuwa mtoto sio wangu, tena ananijibu kwa nyodo kabisa😡😡
 
Mkuu hii kitu inatia hasira sana, usipojizuia unaweza jikuta hata umeua mtu. Imagine nimehudumia kwa kipindi chote hicho, alaf sasahivi anakuja kuniambia kuwa mtoto sio wangu, tena ananijibu kwa nyodo kabisa😡😡
Ameshajua udhaifu wako na tabia yako.Mtoto ni wako.Lea tu usimsikilize huyo kibaka.
 
Kapime DNA kwanza.
Amekomaa kabisa anasema " mtoto sio wako ,kama unabisha kapime DNA"... yaan kiufupi alikuwa anafanya kusudi kuniingizia gharama huku akijua mtoto sio wangu. Pia japo mtoto hajafanana na mimi kwa sura, ilikuwa ngumu mimi kumtilia shaka, mana mtoto kafanana na mama yake copy kabisa,, so nikaona kawaida tu
 
Habari zenu wadau!, nahitaji ufafanuzi kidogo hapa, nilikuwa na Girlfriend wangu ambaye alipata ujauzito na kuniambia kwamba ni ujauzito wangu. Tangu hapo niliamua kwa upendo tu kumhudumia katika kipindi chote cha ujauzito hadi alipojifungua. Japo sikuwa naishi nae lakini nilimpatia mahitaji yote aliyokuwa akiniambia. Baada ya mtoto kuzaliwa, niliendelea kumhudumia hadi akafikisha umri wa miaka 10.

Sasa naona mwanamke huyu amebadilika mno na anatumia hiyo kama fursa ya kunikandamiza, maana anadai matumizi ambayo ni makubwa kiasi cha kunifanya nione kabisa ananitumia kwa masilahi yake kwa kisingizio cha mtoto.

Basi baada ya hayo, nikaona suluhisho ni mimi kumchukua huyo mtoto nikae nae, nimhudumie mimi mwenyewe. Lakini mama yake aligoma, kilichofuata hapo ikawa ni migogoro daily.

Wakati migogoro hiyo ikiendelea, ndipo mama wa mtoto ananiambia kuwa huyu sio mtoto wangu, kitu ambacho kimeniuma sana na kunivunja moyo. Nikapatwa na hasira sana

Sasa nimeleta hili suala kwenu wadau mnisaidie, je kuna sheria yoyote ya kudai fidia kwa gharama zote nilizotoa kumlea huyu mtoto kwa kipindi chote hicho, hadi kufikia hapo ambapo mama yake anadai kuwa sio mtoto wangu?? Na kama ipo sheria ,je utaratibu upoje??
ukweli umekuweka huru,
si kwamba wema wako umekuponza, bali umejiwekea hazina mbinguni,

umetekeleza wajibu wako ipasavyo kama baba mwema, bora sana muwajibikaji.

Hujapoteza kitu gentleman kwa malaika huyo japo ni kwa hadaa za Delilah, huo ni uwekezaji wa Neema, kwa ukarimu. Unayo hazina mbinguni.

Huna haja ya kubababika,
Umetenda wema, sasa nenda zako kwa amani.

Neema na Baraka za Mungu ziambatane na kuandamana nawe daima,
aimen🐒
 
ukweli umekuweka huru,
si kwamba wema wako umekuponza, bali umejiwekea hazina mbinguni,

umetekeleza wajibu wako ipasavyo kama baba mwema, bora sana muwajibikaji.

Hujapoteza kitu gentleman kwa malaika huyo japo ni kwa hadaa za Delilah, huo ni uwekezaji wa Neema, kwa ukarimu. Unayo hazina mbinguni.

Huna haja ya kubababika,
Umetenda wema, sasa nenda zako kwa amani.

Neema na Baraka za Mungu ziambatane na kuandamana nawe daima,
aimen🐒
Nashukuru sana ndugu🙏🙏
 
Hali hii ilinikuta nilihudumia kwa miaka nane, badae nikagundua mtoto anatumia jina tofauti na langu shuleni, (majina ya babu yake Mzaa mama yake) wakati cheti cha kuzaliwa kipo chenye jina langu.

Niliumia sana ila nikaamua kukaa mbali nao kwa kila kitu.

Endelea na maisha yako achana nao, ulichotoa ni sadaka
 
Sijui huwa mnatumia akili za wapi mimi mwanamke ajifanye kiburi aniambie hivyo ataona anavyoteseka!, chakufanya nikumchukulia ushahidi tu wa maneno yake halafu tulia usifanye chochote! akienda kwenye dawati la kijinsia kulalamika huko ni ataumbuka yeye!, halafu wewe shikilia msimamo tu.

Sidhani kama kuna fidia ya malezi labda ithibitike mtoto si wako ki DNA halafu apatikane baba halali ki DNA, huyu baba halali atatakiwa akulipe ila sidhani kama hiyo sheria ipo!.
vilevile anaweza kukukandia kama ukimpeleka mahakamani anaweza akakuomba risiti za matumizi yote uliyofanya ya mtoto!, maana huo ndo utakuwa kama kielelezo chakuwa ulitumia gharama so, unazo hizo risiti..?😂

by the way kwenye jamii linapokuja swala la familia wanaume huwa hatusikilizwi sana!, ni kama vile hatuna haki!, mwanaume unajitafutia haki mwenyewe na akili za kuishi vizuri ama vibaya ni zakwako mwenyewe!.

wewe ushaambiwa mtoto si wako, basi kusanya ushahidi wa maneno yake then kaa kimya, ukiitwa weka wazi huo ushahidi wausikie, najua anaweza akaomba msamaha wewe sema huna imani tena!.
Na hata kama pesa unayo usikimbilie kupima DNA, maana ipo sheria inawaruhusu madaktari wa DNA kukupa majibu batili pale atakapoona mtoto hana wa kumlea!, hivyo daktari hata akiongopa na ukaja ukagundua baadae kisheria huna chakumfanya!.

Sisi wanaume raha humu duniani tunajipa wenyewe, usitarajie maswala ya familia siku mambo yakigeuka yatakuwa upande wako never!, huwa tunaonekana ni mazumbukuku tu.
fanya vitu kwa utafakari mpana!.
 
Hali hii ilinikuta nilihudumia kwa miaka nane, badae nikagundua mtoto anatumia jina tofauti na langu shuleni, (majina ya babu yake Mzaa mama yake) wakati cheti cha kuzaliwa kipo chenye jina langu.

Niliumia sana ila nikaamua kukaa mbali nao kwa kila kitu.

Endelea na maisha yako achana nao, ulichotoa ni sadaka
Ahsante ndugu
 
Back
Top Bottom