Je, kuna umuhimu kama taifa kufanya usaili kwa kada ya Afya na Ualimu ndo Uajiri?

Labda wanaogopa kugundulika kuwa hawana sifa.

Mtu uliyesomea kwa msuli wako, ukafaulu kihalali, cheti ukapata bila makando kando, na elimu bado ipo kichwani, kwanini uogope usaili?
Hakika.
Kama ulisoma kwa uhakika, una ufahamu mzuri wa fani yako, huwezi kuogopa usaili.
 
Lengo sio usaili lengo ni kuendelea kuwaibia hela hawa wajinga wanajiita wasomi tumewapiga ada sasaiv tunataka watuhonge siku za usail na hapa tutapata mahela mengi sana,,,tutahongwa sana dogo pesa ngumu lazima tutengeneze money game plan ili tupate pesa
 
Sawa tukirudi kwenye mada wewe binafsi unataka usaili uwepo au usiwepo na kama uwepo lete sababu kwanini uwepo na kama usiwepo lete sababu kwanini usiwepo

Ukijibu hilo swali nadhani utaelewa hoja zetu
 
umeongea ukweli unaouma sana
 
Kwahiyo hamtaki interview? Serikali haiwezi kuwaajiri wote, nendeni mkapigwe intavyuu watakao pita ndio wapate hiyo ni mizania moja hamna wa kulaumiwa ukikosa
 
Kwahiyo hamtaki interview? Serikali haiwezi kuwaajiri wote, nendeni mkapigwe intavyuu watakao pita ndio wapate hiyo ni mizania moja hamna wa kulaumiwa ukikosa
Kwaiyo mkuu una maana siku ajira zikiwa nyingi na waajiriwa wakiwa wachache kutakuwa hakuna umuhimu wa interview?
 
lete hoja sio dharau kaka
Hoja gani? mjibu swali kwanini hamtaki kufanya interview wakat kada zingine wanafanya interview what is so special with you, au wengine hawajasom vyuo mlivyosoma nyie mtuambie
 
Kwaiyo mkuu una maana siku ajira zikiwa nyingi na waajiriwa wakiwa wachache kutakuwa hakuna umuhimu wa interview?
ndivyo ilivyokuwa kwa kada ya ualimu na afya, kwani hukumbuki walimu wa upe, walimu wa Voda Fasta? ni kwa sababu kulikuwa na upungufu mkubwa, na serikali iliweka favour ulikuwa ukienda kusoma kozi ya ualimu na kozi ya sayansi mkopo ulikuwa wa lazima na ukimaliza unaenda kazini moja kwa moja tofauti na Kozi zingine ambazo uhitaji haukuwa mkubwa sana, tofauti na sasa hivi walimu ni wengi na watu wa kada ya afya ni wengi, ndio maana serikal imerudi kwenye utaratibu ili kuweka fairness kwa kada zote, yaani haiwezekani Mhasibu afanyiwe usaili halafu mwalimu asifanyiwe usaili wakati wote wako level moja
 
Bado hujajibu swali umeleta historia

Swali: Kwahiyo siku walimu wakiwa wachache na ajira zikawa nyingi hakutakuwa na umuhimu wa interview?

Jibu:....kwanini....
 
Hakuna haja ya usaili ""Ualimu ni content"" mfano mtu kamaliza almost 10years
Leo hii uanze kumpa mitiani ya Nini je hakuna faida yeyote ni upuuzi..
 
Bado hujajibu swali umeleta historia

Swali: Kwahiyo siku walimu wakiwa wachache na ajira zikawa nyingi hakutakuwa na umuhimu wa interview?

Jibu:....kwanini....
kwani unazijua sababu za kwanini serikal ilitumia walimu wa UPE au haujawah wasikia?
 
Sawa tukirudi kwenye mada wewe binafsi unataka usaili uwepo au usiwepo na kama uwepo lete sababu kwanini uwepo na kama usiwepo lete sababu kwanini usiwepo

Ukijibu hilo swali nadhani utaelewa hoja zetu
Nilishaandika tangu mwanzo, hakuna mwajiri anaweza kuajiri watu bila kufanya USAILI. Huwezi kutenganisha mchakato wa kupata ajira na zoezi la usaili. Kitendo tu cha muajiri kutangaza ajira na kuelekeza watu wenye sifa wapeleke vyeti na yeye kupitia vyeti vyao kabla ya kuwaajiri huo tayari ni mchakato wa Usaili.

Upande wa pili, anayeamua mchakato wa usaili uweje ni muajiri na sio muajiriwa. Haijarishi mchakato huo utakuwa mfupi au mrefu, wenye busara au upumbavu, kamwe muajiriwa hawezi kuuhukumu kwa haki kwa sababu hapaswi kuupanga yeye bali anayemuajiri kumpangia.
 
Sasa mtu kama amesahau mambo ya taaluma yake kwa sababu ya kukaa muda mrefu sana tangu ahitimu, sasa serikali imuajiri ili akafanye kazi gani? Yaani mtu hana ufahamu wowote, ana vyeti tu, apewe ajira ya nini?
Kama umepita pita shule kidgo huwez kuuliza haya maswali, Kuna tofauti kubwa sana kati ya Yale unayosoma na unayoyafanyia kazi tunasoma mambo mengi sana it ila sio yote tunaenda kuya appy kazini na hii sio afya Wala ualimu tu Bali professional zote, kama kweli unahitaji Dr mzuri mpime akiwa na mgonjwa na sio kumuuliza tuswali viwili vitatu akishindwa kufikisha marks unazozihitaji ww unamwambia hafai hi sio sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…