Acha kulaumu mwanamke, hata akiwa ni mwanaume vita ni ile ile maana watapingana katika imani na makuzi ya watotoNi vita kati ya watu wawili au familia sana san mwanamke akiwa muislam ndio vita kubwa
Ndo juzi ilikuwa siku ya wanawake duniani, mama Abdul akahutubia jinsia yake, wakajiita super woman, unaiongeleaje?Sababu kubwa ni feminism tu, wala hakuna kingine. Msingi wa ndoa ulisukwa kwenda sambamba na mfumo dume, mwanaume atoke kutafuta mwanamke abaki nyumbani kuangalia familia.
Ukipenyeza hayo mambo ya 50/50 bila kufanya overhaul ya mfumo mzima wa ndoa basi lazima taasisi ya ndoa ianguke tu.
Acha kuwatetea ukweli ndio huo cha msingi uje na hoja ya kujengaAcha kulaumu mwanamke, hata akiwa ni mwanaume vita ni ile ile maana watapingana katika imani na makuzi ya watoto
Hii sasa ni moja ya sababu ambayo inafanya ndoa zinapungua, unajua asilimia kubwa ya wanaume hatuna muonekano mzuri wa kushtua wanawake, hivyo thamani pekee tunayobaki nayo wanaume wengi ni pesa, na pesa ya mwanaume inazidi kua worthless kwenye mahusiano, sababu wadada wengi sahivi wana make their own money, hivyo mdada akiwa na kipato cha million 2 kwa mwezi atataka aolewe na mwenye kipato cha million 5 kwa mwezi, hivyo options za huyo mdada kuolewa zinazidi kua limitedZamani wanawake walikuwa tegemezi kwa wanaume kwa sababu hawakuwa na njia nyingine, lakini sasa wanajitegemea.
Huenda tunasumbuliwa na Kiburi cha uzima? Huenda ndoa siyo mbaya ila viburi vyetu vinatupa upofu?Tùlishajichanganya tangu mwanzo..ndoa ni kitu cha kipuuzi kuwahi kutokea hapa duniani, kama ilivyo dini.
Nakubaliana na hoja yako kwamba wanawake wengi siku hizi wanajitegemea na wanapendelea wenza wenye kipato sawa au kikubwa zaidi. Hata hivyo, si wanawake wote wanapenda kuwa bila ndoa. Kuna wengi ambao bado wanathamini ndoa na mahusiano ya kudumu, si kwa sababu ya pesa tu, bali kwa ajili ya upendo, heshima, na familia. Kila mtu ana vipaumbele vyake, na si sahihi kusema kwamba wanawake wote wanachagua pesa badala ya ndoa au mahusiano ya kweli.Hii sasa ni moja ya sababu ambayo inafanya ndoa zinapungua, unajua asilimia kubwa ya wanaume hatuna muonekano mzuri wa kushtua wanawake, hivyo thamani pekee tunayobaki nayo wanaume wengi ni pesa, na pesa ya mwanaume inazidi kua worthless kwenye mahusiano, sababu wadada wengi sahivi wana make their own money, hivyo mdada akiwa na kipato cha million 2 kwa mwezi atataka aolewe na mwenye kipato cha million 5 kwa mwezi, hivyo options za huyo mdada kuolewa zinazidi kua limited
Au kwa maana ingine ni ngumu mwanamke kutongozwa na mwanaume handsome, kama akitongozwa na mwanaume handsome, basi huyo mwanaume ni dead beat dad, marioo, au mtu wa kupiga na kusepa. Hivyo mdada kama ana kazi yake nzuri anaona kuliko aolewe ni heri abaki single, sababu hana njaa ya kuolewa na mwanaume mwenye sura mbaya kisa hela Strong and Fearless
Eti akupikie, kwamba yeye hali anakupitia tu, eti akuzalie huyo mtoto anakuwa wa mwanaume peke yake, ukiingia kwenye ndoa mwenye uhitaji wa mtoto wa kwanza anakuwa mwanamke, sasa hizi kauli za akupikie, akuzalie, akutunze zinatoka wapi, kati ya mwanaume na mwanamke nani anatoa matunzo ndani ya nyumba?Ndio ndoa lazima iwe ngumu mtu unataka 50/50 Bado et akupikie akufulie akuzalie familia atunze Bado mammkwe amseme lazima msielewane ndani zaman ilikua unaacha buku ndani wala mke halalamik utarudi anakunyenyekea wtf 20th C itatuonyesha mengi!📌
Mbona wanifokea 😹😹😹Eti akupikie, kwamba yeye hali anakupitia tu, eti akuzalie huyo mtoto anakuwa wa mwanaume peke yake, ukiingia kwenye ndoa mwenye uhitaji wa mtoto wa kwanza anakuwa mwanamke, sasa hizi kauli za akupikie, akuzalie, akutunze zinatoka wapi, kati ya mwanaume na mwanamke nani anatoa matunzo ndani ya nyumba?
Ndoa ni taasisi inayohitaji utambuzi wa kina, utayari, na uwajibikaji wa pande zote mbili. Si kila mtu ameandaliwa kwa safari hii, na si kila mtu ana mtazamo sahihi wa kuishi ndani yake. Uzuri wake haupo kwa kila mtu, bali kwa wale wanaoelewa maana yake halisi na wanajituma kuiendesha kwa upendo, heshima, na uvumilivu. Kabla ya kuingia kwenye ndoa, ni muhimu mtu ajitambue na ajue kama yuko tayari kwa majukumu yake.Ndoa Ni Taasisi Nyeti Mnoo,Ambayo Ipo Mbali Mnoo Na Upeo Wa Fikra,,Mitazamo Na Maono Ya Wengi Kati Yetu Me na Ke Na Hii Taasisi Uzuri Wake Si Kwa Ajili Ya Kila Mtu,,Utambuzi Zaidi Unabaki Juu Yako.