Je, kwenye Biashara hizi uendeshaji na faida vinapatikanaje?

Je, kwenye Biashara hizi uendeshaji na faida vinapatikanaje?

Kuna vituo vya mafuta hutoa 'Bonus' ya fedha kwa Mwezi kutokana na manunuzi yako. Mfano kuna wakati nilikuwa napata hadi Sh ef 50 kwa Mwezi kituo cha Petrol Africa. Wanakokotoa vipi hii hesabu? Au unajiibia mwenyewe mteja kwenye kiwango cha mafuta unachonunua?
Hiyo ni loyalty card wanaita, mteja anapo jaza Mafuta Kila siku mfano hiace, coaster, tipper, Malori Wana record kwenye kitabu Kila siku then mwisho wa Mwezi Wana jumlisha total Ltrs ulizojaza Kwa mwezi wanazidisha mara hiyo 50 ama 30 kupata hiyo bonus.
 
Gharama kubwa ni kupata eneo/ kiwanja Cha kujenga. Eneo liwe tambarare kupunguza gharama za kuujaza kufusi. Vibali vya ujenzi Unaanzia NEMC Hadi EWURA. Hapo lazima uwe na 10M to 20Million.

Gharama za ujenzi zimegawanyika kulingana na ukubwa wa eneo Eg. Kujaza zege inaweza eneo la pump,
Inaweza fika 10- 15 millioni, inategemea ukubwa wa kituo.

Gharama za Canopy / paa la kisasa linaanzia 30-60millioni, ila yapo ya kawaida unaweza Jenga Kwa 10-18 millioni.

Gharama za kutengeneza matanki ya kuhifadhia Mafuta, Tanki mbili zenye ujazo wa Ltrs 35elfu ukinunua material mwenyewe na kumleta fundi site kwako ni 20millioni.

Pump mbili za Mafuta zenye mikonga miwili / midomo miwili Kila upande mdomo, moja ni 34 millioni Kwa zote.
Generator nzuri ya kuendesha kituo 5-8millioni.

Gharama za kujenga office, vyoo, vyumba vya kubadilishia nguo wafanyakazi ni 15millioni. Gharama za kuchimba mashimo ya Tanki mawili, kutengeneza mfumo wa kutenganisha Maji na Mafuta, pamoja na kuchimba mfereji wa kupitisha Mafuta 3 millioni.

Gharama za pipe za kutoka kwenye matanki Hadi kwenye pump ni 1.5 millioni. Gharama za kufunga. Mfumo wa umeme ni 3-6millioni.

NB: Hizi ni gharama Kwa kituo standard, ila kama ukiamua kubana kwa maeneo ya vijijini unaweza punguza gharama kidogo.
Nimejifunza kitu hapo. Kumbe wastani ili kituo kikamilike kabisa ni 200,000,000.
 
Anatoa kwenye faida yake au anakuminya kwenye lita unazonunua. Mfano badala ya Sh ef 2700 kupata lita 1, yeye anakupa lita 0.9?
Yeye anapo enda kununua Kwa wauzaji wa jumla huwa Wanapewa. Bonus / discount then na wao huwa wanairudiaha Kwa wateja wao , hiyo piya wanapunguza kwenye sehemu ya profit.
 
Kuna mtu aliniambia wauza mafuta wanalipwa laki 2 nilibisha.kumbe kweli.
Na wale wanaobetisha pale caunta mshahara bei gani?
 
Yeye anapo enda kununua Kwa wauzaji wa jumla huwa Wanapewa. Bonus / discount then na wao huwa wanairudiaha Kwa wateja wao , hiyo piya wanapunguza kwenye sehemu ya profit.
Nimekupata. Security wise ikoje?. Siku hizi sisikii habari za vituo kuvamiwa kama zamani. I don't believe kuwa kila baada ya saa 1 wana bank mzigo.
 
Nimekupata. Security wise ikoje?. Siku hizi sisikii habari za vituo kuvamiwa kama zamani. I don't believe kuwa kila baada ya saa 1 wana bank mzigo.
Issue za kuvamiwa zinatengenezwa na wafanyakazi wa ndani wanauza ramani ya Kwa majambazi mfano pump attendant anavyopekea Hela na kuuza Mafuta wanaona wameuza kiasi Gani Wana kadiria mauzo then wanawatafuta watu wa kazi wamaluze mchezo.
Solution;-
Kusisitiza malipo through Lipa Number, Kuwa na POS mashine mtu akija anatumia kulipia na fedha zote kwenda Bank direct .
Kuwa na sheria Kali kuhusu Hela anazoruhusiwa pump attendant kuwa nazo nje. Inatakiwa mauzo Kila yakizidi laki mbili waende kwenye chombo Cha kutumbukiza fedha ( huwa kunakuwa na shimo / tunduukutani linakwenda direct kwenye sefu ndani ya strong room) Hilo Shimo/Tundu linatengenezwa Kwa pipe inakuwa na Kona nyingi na slopi Kali za kuterezesha hela
 
Tumechangia vya kutosha Hii thread, Sasa naomba tufike hitimisho, Kwa mwenye location eneo la kijijini ama makao makuu ya Wilaya,
Kifupi mwenye eneo ambalo anaweza kujenga Kituo Cha Mafuta.
Kama mwana JF yoyote yule mwenye Capital ya kuanzia 70/90millioni akiwa na eneo tayari , nipo tayari kumuonyesha njia nyepesi ya kujenga Kituo Cha Mafuta Kwa huo mtaji.
Nitamsadia Kila kitu Bure bila malipo, Kila siku tunajadili mada nyingi bila mrejesho.
NB ;- Kwa maeneo ya wilayani na vijijini Nina uwezo wa kumsadia mtu mwenye mtaji wa kyanzia 70/90Millioni kujenga Kituo Cha Mafuta.
 
Tumechangia vya kutosha Hii thread, Sasa naomba tufike hitimisho, Kwa mwenye location eneo la kijijini ama makao makuu ya Wilaya,
Kifupi mwenye eneo ambalo anaweza kujenga Kituo Cha Mafuta.
Kama mwana JF yoyote yule mwenye Capital ya kuanzia 70/90millioni akiwa na eneo tayari , nipo tayari kumuonyesha njia nyepesi ya kujenga Kituo Cha Mafuta Kwa huo mtaji.
Nitamsadia Kila kitu Bure bila malipo, Kila siku tunajadili mada nyingi bila mrejesho.
NB ;- Kwa maeneo ya wilayani na vijijini Nina uwezo wa kumsadia mtu mwenye mtaji wa kyanzia 70/90Millioni kujenga Kituo Cha Mafuta.
Thanks a lot brother, nitakutafuta I promise you .
 
Back
Top Bottom