Je, Magic Mushrooms ni halali hapa Tanzania?

Je, Magic Mushrooms ni halali hapa Tanzania?

Status
Not open for further replies.
Kwa experience niliyonayo kwenye hiyo kitu sijui nianze kukuelezea wapi!

Kwanza kabisa: kama umesha toboa 25 na hujawahi tumia kilevi chochote, yani pombe, sigara na ganja, sikushauri uthibutu kuanza kutumia hivyo vitu kabisa wewe endelea kunywa juice za embe na machungwa na maji kwa wingi, hivyo vitu hapo juu usiviwaze kabisa.

Kwanini: mwili na akili yako hua havipokei effect zake kwa haraka, hua vinaenda vikijifunza taratibu hivyo ni ishu kuvi control mapema, hivyo mbali na kulewa baada ya kutumia wewe ndio unalewa kuzidi kutaka kuvitumia, utataka ujaribu kila linalowezekana ili uone matokeo yake na hapa ndipo watu tunapo poteana, wengine hua hawaridhiki na walivyotumia au walivyozoea tumia au walivyo kwisha tumia na kuendelea kujaribu vigeni zaidi kwao ndio hudondokea kwenye UNGA AKA NGADA na mpaka hapo biashara inakua imefika mwisho.

Hivyo mpaka kufikia kuvimudu hivyo vitu kwanza unatakiwa uwe na kichwa kizuri ( kwa neema ya Mungu na jinsi alivyo kuumba [emoji72] ) pia uweze kuhimili mihemko means uweze kuendesha akili zako sio kila amri inayotoka kichwani mwako uwe unaitekeleza, unapoona imetosha maana yake imetosha na sio " ngoja niongeze kidogo ", unapoona hiki hakiwezekani au ni hatari ukae kujiua ni hakiwezekani na ni hatari kweli sio " ngoja nijaribu nione "

Pia mwili na akili yako vikubaliane sio mwili hautaki alafu akili inakulazimisha au akili haitaki mwili unakulazimisha, ukisema unatumia maana yake unatumia na ukikataa maana yake usitumie kifupi vinahitaji nidhamu, ukiwa mfujaji navyo vitakufuja!

Bahati mbaya huwezi pata hiyo nidhamu mapema hua inachukua muda mpaka uvizoee ndio maana nikakwambia kama umetoboa 25 usivifikirie mf: ganja nimeitumia mfululizo ( matumizi ya kawaida ya kila siku asubuhi, sometimes mchana, na usiku na usiku ndio ilikua sherehe[emoji16]) kwa miaka kama 9 au kumi tangu gari limewaka form two[emoji2960]. Ndio nikaanza kubadili utaratibu wa matumizi na aina za matumizi lakini nilikua siwezi kufanya chochote kama sijapasha pia haikua rahisi ilini gharimu ila kwakua niliidhamiria akili na mwili vilikubali nika stop ghafla baada ya attempt kadhaa za kuacha kikawaida kushindikana ( kama kupunguza dose, kuruka siku moja moja na nyinginezo ), niliumwa hatari mpaka kulazwa hosp na hata nimetoka hosp hali haikua nzuri homa si homa, no kula no nini, ila shangaa dawa ikawa ni hiyo hiyo ganja tena, nimetoka hosp kufika home nikajichekecha nikaenda kuipuliza nilipona hapo hapo na ndio ikawa mwisho kuitumia mfululizo[emoji854] hivyo unapata picha ukiianza ulevi na 25 itakavyo kugharimu, huto pata muda wa ku turn_over

Kwa story hiyo fupi kulingana na swali lako, sio ganja pekee! Kilevi cha aina yoyote mpaka ukijue na kukidhibiti kinakuhutaji muda na lazima kikugharimu kwanza ndio uweze kuki control. Sijui nitakua nimekujibu!!?
Janii ni nyokoooo.....nnadhani watu wengi wanaokosea kwenye jani ni wake wanaotafuta ile stimu ya ukungu...kwa uvutaji ule unaweza ukawa unapiga hata sita mpaka 10 per day....ukisikiliza mziki unausikia kwenye angle nzuri...kula sana na mambo kadha wa kadha...mtu wa aina hii anauwezo wa kuvuta bangi kila siku mpaka siku atakayoamua kuigeukia heroin.....wengine wanakuwaga mateja kabisa...
Kuna hii bangi inayokupeleka kwenye hallucination na mara nyingi huchangiwa na namna unavyotaka kujitafuta na kujielewa wewe mwenyewe...ukiipeleka kujiaminisha maisha ambayo hayapo kwenye jamii trust me utaishia huko....ukiipeleka vizuri itakufundisha namna ya kuishi na watu vizuri....Kuelewa uwepo wa Mungu maana kuna hali utakuwa unaipitia ya kuhisi kabisa uwepo wake na ukimueleza kuhusu ni kwa namna gani ungependa akusaidie kwenye maisha yako.....utafanya mema mengi...Ego itashuka...hutakuwa judgemental kwenye maisha yanamhusu mtu zaidi utapenda kuelewa zaidi kilichompelekea yeye kuingia kwenye hio hali....Lakini kipindi unakutana na hii hallucination broooo ni nyoko kuna muda nilikuwa ninahisi nnakuwa kichaa.....maisha yako unayoyaishi unakuwa unayaangalia kama movie...kuna kipindi utahisi unakufa ile hali ikikukuta utaandika mpaka wosia utapiga simu kuaga....nnakumbuka .hali mbaya zaidi niliyowahi kuipitia ni ya kuhisi nnaingia kwenye version mpya ya maisha... akili inatengeneza segment utoto ujana uzazi uzee kwa hiyo kama ulikuwa unajihisi wewe ni kijana kwenye sober life utaona kama ndio unaingia kwenye kuwa mzazi....unajuta kwa yale mabaya yote uliyoyafanya na kile kitu kinakufanya unakuwa weak sana.by that time..jamii ilikuwa inaelekeza hivi wewe unaenda hivi...kuna mtu ulimkosea maybe......so siwezi kusema bangi ni nzuri kwasababu sio kila mtu huwa anafaulu kwenye kujitafuta....
 
Kuelezea hivi vitu i mean experience wanayokutana nayo watu kipindi wanakutana hallucination ni ngumu its like unakuwa na mind nyingine ambayo ni intelligent na advanced kuzidi ile unayoitumia kila siku kwenye maisha...na ni kama vile huwa ina take over na kuanza kukufundisha how to live....hivi sio sawa, pita hapa, fanya hivi, usifanye hivi, ambayo sijawahi kuielewa ni pale nnapopitiaga ile hali ya kuhisi kama vile kuna mazungumzo unafanya na Mungu ukisha notice tuu ile hali...utaongea kwa muda pale tuu utakapoanza kufikiria cha kuongea, ile connection huwa inakatika....huwa nnahisi nimetumia hata lisaa...kumbe ukiurudisha ule muda kwenye dunia yetu sidhani kama hata dakika mbili huwa ninamaliza.haitokei unapokuwa na mtu huwa ni jeshi la mtu mmoja
 
Mkuu hii mada iko very interesting,natamani watu wajijue how they operate within..watu wengi wanajiambia kuwa mimi ndivyo nilivyo..mtu akiwa na mahasira anajiambia nmezaliwa hvyo.

Simply because they don't know their true nature ni ipi..hayo mengine yote unayaaccumulate wewe mwenyewe.

Bahati nzuri tunacho jadili ni njia sahihi ya kuachia takataka zote na kurudi kwenye uhalisia wetu kama being.. automatic unakuwa na Consciousness ya hali ya juu pamoja na compation kubwa
Hauwez kufanya kila mtu ajue mkuu , kama soul ya mtu sio wakati wake wa kuamka atabaki tu hivyo hivyo.
 
Hapana. Ntakupa jibu refu ambalo nataman ningempa huyo father

Mie ni Taoist lkn bado ni mkatoliki.

Taoism ni way of life lkn sio religion na haipo kwenye dimension moja na dini, ipo juu sana ya hapo sababu inaweza kukufanya u-tap directly into spirituality bila kuwa na gateway zilizozoeleka ambazo ndio hizi dini.

Why bado ni mkatoliki? Sababu religion by one way or another is just a culture, na nmezaliwa kwenye hio culture na kama haiko negative to Tao basi naendelea nayo hadi labda siku iwe negative to Tao.

Kwenye Taoism tunaamini kwenye cultivation, lazima kucultivate virtues na kufuata the Tao, lakini hayo yote huwezi kufanya bila kuwa na CALM MIND. Mind ikiwa calm ndipo utaweza toa vitu vibaya na kuingiza vitu vzr, ndipo utaweza kuona vitu in a very clear way. Chukulia maji yenye matope (muddy water) yale maji yakisettle ndipo utaona clearly matope yako wapi na maji yako wapi, same as human mind too.

Sasa huko kucalm mind na kujialign na nature kuna practice inabidi ufanye ndipo ufikie hizo states, na hapo ndipo tunafikia kwenye MEDITATION na YOGA.

Kuna affirmations pia nazo hufanyika sambamba na meditation.

Haya hadi hapo nielekeze huo uchawi unatokana na nini?

Hao hao wanaoita meditation uchawi nao wanafanya meditation bila kujijua.

Na pia ukisoma Tao Te Ching utakuja kuona dini zote za kweli zimechukua summary mule.

Kuna mtu aliwahi kusema kwamba ukianza kupractise sheria au virtues unazofundishwa na dini yako mfano ukarimu etc.... ndipo utakuja kuona All roads lead to taoism.

Ni kwamba tu hawa ma-father hawataki kuwa challenged na ukweli na wanataka waendelee kutegemewa. Sasa kwa kuwa wanajua mtu ambae ni anaweza cultivate virtues mwenyewe na kuharness nguvu ya nature hatowahitaji tena service yao ndipo wanaipinga kwa nguvu zote wakiogopa kupoteza waumini, lkn haya mambo the more una-advance ndipo unajua ukweli wa mambo, you just taste the vinegar, smile, and let it go.
Mkuu huu ni ukwel 200%
 
Kabisa mkuu,ukielewa hili jambo na ukaliishi na na uka empty takataka zote za kwenye SUBCONSCIOUS MIND..unakuwa mwenye huruma na matendo mema kwa wengine Automatically..means unarud kule kule kwenye Dini..ambako wao wanalazimisha tu watu watende matendo mema bila kujua wana garbage nyingi kwenye mind zao ambazo wanatakiwa wazi release kwanza
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Kuelezea hivi vitu i mean experience wanayokutana nayo watu kipindi wanakutana hallucination ni ngumu its like unakuwa na mind nyingine ambayo ni intelligent na advanced kuzidi ile unayoitumia kila siku kwenye maisha...na ni kama vile huwa ina take over na kuanza kukufundisha how to live....hivi sio sawa, pita hapa, fanya hivi, usifanye hivi, ambayo sijawahi kuielewa ni pale nnapopitiaga ile hali ya kuhisi kama vile kuna mazungumzo unafanya na Mungu ukisha notice tuu ile hali...utaongea kwa muda pale tuu utakapoanza kufikiria cha kuongea, ile connection huwa inakatika....huwa nnahisi nimetumia hata lisaa...kumbe ukiurudisha ule muda kwenye dunia yetu sidhani kama hata dakika mbili huwa ninamaliza.haitokei unapokuwa na mtu huwa ni jeshi la mtu mmoja
Yaani! Kwa bahati mbaya " kutoa hawa wanaopitia humu kupata experience kabla hawajatumia " wengi tumetumia tukia hatujui maana halisi ya meditation, hivyo tulikua tuna enda enda tu, Mungu muweza kuna tulio mudu kui control na kuna walio feli na wengine kuangukia kwenye Heroin nadhani hiyo heroin ndio janga halisi
 
Dawa sio meditation hizo, dawa ni kumpokea Yesu moyoni mwako, ukiokoka utajazwa Roho Mtakatifu, utapata maono na mafunuo kutoka kwa Mungu wa kweli, utapata uzima wa milele.
Yesu mwenyewe alikua anafanya meditation unafikir alikua anajitenga milimani kufanyaje? Sala za wakatholic za rozali ni aina ya mantra meditation , hakuna din isiyo na kipengele cha meditation japo kwa uchache.
 
Dah Hii Kitu Jamani sitaki kukumbuka Maana kila nikikumbuka naona kama ni Jana imenitokea kumbe ni kama miaka 10 ilopita...

Sasa nisikilize nikupe Experience yangu kuhusu Hii Magic mushroom ambayo sijawahi kuisema popote kwa sababu zangu binafsi..

Ilikuwa mwezi wa 12 Mwaka 2011 Nikitoka kwenye mishe mishe Nikapoteza Baadhi ya pesa ambazo sikujua nimeziweka wapi na zilikuwa pesa za Muhimu sana Kuna watu niliwahisi wamechukua Ila wakagoma sasa kwa wakti huo siku na uwezo wa kupata hizo pesa...Kila nikijaribu kuwaza mwezi wa kwanza 2012 zinatakiwa hizo pesa na kwa muda huo nisingeweza kuzpata kwa wik8 mbili zilizobaki...

Sasa nikamshirikisha Rafiki yangu Mmoja akaniambia mbona hilo jambo Dogo Twende Maramba (Tanga) kwa fulani tukaangalie...

Sasa me nikajua tukifika Atafanya mambo yake na atasema anazo nani na atafanya dawa Ya kuzileta (Maana mimi sikiwahi kabla kwenda kwa mganga)..

Bhna jamaa si akaja na maji kwenye Chupa ya Kilimanjaro Ndani yana kama vitu vyeupe vimechangnywa akaniuliza "umekula"

Nikamwambia sijala akasema vizuri akamimina kwenye kikombe yale maji mchanganyiko na vitu vyeupe akaniambia kunywa bila kufikiria radha nikanywa yote..

Akaniambia nikae juani ili dawa ifanye kazi Guyz "Mushroom halucination we zisikie tu"

Hakuna matukio niliacha kuyaona mengine sikuwahinhata kuyajua na nilipowauliza wahusika niliowaona kwenye matukio hayo walikuabli kweli yalitokea...

Japo sikuafanikiwa kumuona mwizi wangu wlaa aliyechukua wala tukio la hela ila kuna baadhi ya matukio ya mbele niliyaona (Ambayo baadae nilikuja kuyashuhudia in reality ila niliyaona kwenye ile hallucinative )...
Baadaye nilipokuja kuchunguza nilijua kuwa walinipa Mushroom..

Guyz msijaribu kabisa maana ukiangalia ukutani utaona hallucinatiom ukifba macho utaona vild vile ni hatari sana msijatibu hii kitu....
Naungana na wale wanaosema unaweza ukachizi kwa sababu unaona Vitu in reality na sio kuwaza unaona kitu kama unaangalia Movie....

Namalizia kwa Kusema KAMA WEWE NI MFANYAJI WA MEDITATION NA TAYARI UOGA KWAKO UMEONDOKA UNAWEZA UKAJARIBU HII KITU...

LAKINI KAMA WWE SI MFANYAJI WA MEDITATION NA UNA UOGA WA ASILI USIJARIBU KABISA HII KITU WALA HATA KUISOGELEA NI HATARI SANA
 
Kuelezea hivi vitu i mean experience wanayokutana nayo watu kipindi wanakutana hallucination ni ngumu its like unakuwa na mind nyingine ambayo ni intelligent na advanced kuzidi ile unayoitumia kila siku kwenye maisha...na ni kama vile huwa ina take over na kuanza kukufundisha how to live....hivi sio sawa, pita hapa, fanya hivi, usifanye hivi, ambayo sijawahi kuielewa ni pale nnapopitiaga ile hali ya kuhisi kama vile kuna mazungumzo unafanya na Mungu ukisha notice tuu ile hali...utaongea kwa muda pale tuu utakapoanza kufikiria cha kuongea, ile connection huwa inakatika....huwa nnahisi nimetumia hata lisaa...kumbe ukiurudisha ule muda kwenye dunia yetu sidhani kama hata dakika mbili huwa ninamaliza.haitokei unapokuwa na mtu huwa ni jeshi la mtu mmoja
Huu ni ukweli kwa 100%
 
Huitwa Psychedelic Drugs..
Hutumika kuua Ego (Our false Identity) ambayo umeitengeneza kupitia mind since ukiwa mdogo mpaka hapo ulipo...na inakuonyesha the real you..

Jukumu lako ni ku handle hyo path ambayo ni ngumu mnoo huitwa THE DARK NIGHT OF THE SOUL. ukimaliza hyo safari unakuwa mpya kabisa mwenye Consciousness ya hali ya juu mnoo..
Au Nabii daudi anaita "Bonde la uvuli wa mauti" kwenye Zaburi 23
 
Huu uongo kabisaa,huyu samaki namla sana Tena mtamu balaa ila sipati hizo hallucinations. Tena wapo aina mbili wanaofanana wanaitwa kibua mbono
😅😅😅🤣🤣 Mzee huyo sio kibua wala mbono wala hata Sio Samaki changu 🤣🤣🤣
 
1000002456.jpg

Golden teacher strain. I took 2grams of it and the trip was nice and I discovered myself more. The visuals were amazing.
 
Watu tumepewa uwezo wa kuona bila hata hayo madude...

Hichi nilichoona juzi ndicho kinaniwazisha...

Mungu wangu nisaidie..

Naona kama maono...

Mwendazake akiwa kaja kuchukua majina ya waliomdedisha...

Jamani, ni kama nimemuona sehemu ya watu wengi ni kama sokoni, ila ghafla nikamuona akitoka nje ya mlango wa soko akawa anaondoka, ila nikaona amerudi na alipofikia mlango, pembeni kulikuwa na msalaba upo nje juu ya kitu, ndani yake kuna majina ya waliomdedisha nikaona anauchukua msalaba..

NB: Si mara moja naona yanayohusu Mwendazake...
Rabbon
 
Watu tumepewa uwezo wa kuona bila hata hayo madude...

Hichi nilichoona juzi ndicho kinaniwazisha...

Mungu wangu nisaidie..

Naona kama maono...

Mwendazake akiwa kaja kuchukua majina ya waliomdedisha...

Jamani, ni kama nimemuona sehemu ya watu wengi ni kama sokoni, ila ghafla nikamuona akitoka nje ya mlango wa soko akawa anaondoka, ila nikaona amerudi na alipofikia mlango, pembeni kulikuwa na msalaba upo nje juu ya kitu, ndani yake kuna majina ya waliomdedisha nikaona anauchukua msalaba..

NB: Si mara moja naona yanayohusu Mwendazake...
Rabbon
Si pekeako, wengi wanaona.

Zipo Roho ambazo hutangatanga, ni zile Hasa ambazo maisha yalikatiliwa kabla ya muda wake. Ni zipo kudai kisasi.

Tusubiri.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom