Je, majukumu ya nafasi ya Waziri Mkuu yanapunguza nguvu ya nafasi ya Rais kiasi cha kusababisa msuguano baina ya nafasi hizo mbili?

Je, majukumu ya nafasi ya Waziri Mkuu yanapunguza nguvu ya nafasi ya Rais kiasi cha kusababisa msuguano baina ya nafasi hizo mbili?

Falsafa ya kwanza ya kuwepo kwa Waziri Mkuu ni Kumkinga Amiri Jeshi Mkuu na Mkuu wa nchi. Katika hali ya kawaida ikitakiwa Waziri Mkuu awe Mkuu wa Serikali ili aweze kuwa na nguvu ya kiuongozi ndani ya Serikali. Rais angebaki na Ukuu wa Nchi na Amiri Jeshi Mkuu. Mtu mwenye vyeo hivyo viwili vikubwa hapaswi kuwa mtu wa kulaumiwa laumiwa na wa kufanya teuzi hadi za Wakurugenzi wa Halmashauri za Serikali za Mitaa.
Kazi ya kuwa Mkuu wa Serikali, kuunda, kuiratibu na kusimamia ingebaki kwa Waziri Mkuu.
Falsafa ya pili ya kuwepo kwa nafasi ya WM Tanzania ni kuusharabu mfumo wetu wa Semi-Parliamentary System. Yaani sisi mawaziri wetu wanakuwa wabunge kabla ya kuwa mawaziri. Mawaziri wetu huwajibika kwa Bunge moja kwa moja ndani ya Bunge. Serikali yetu huwajibika kwa Bunge kupitia mawaziri na hivyo kuhitajika Mkuu wa Shughuli za Serikali.
Falsafa ya 3 ni kuusharabu na kuimarisha mfumo wetu wa Muungano. WM wa TZ ni kama leader of Tanganyika.
Kuhusu misuguano: haiepukiki. Hata bila PM, kungetokea mojawapo wa Mawaziri anakuwa machachari, anatishia nafasi ya Boss.
Haya mambo ya kutishiana kupitia vyeo ni ego zaidi ya waafrica...Vyeo kwetu siyo dhamana Bali kama vile Mali binafsi, kama Waziri ni machacharisi atakuwa ana chachafya sector yake? Rais anatishika Kwa lipi? Labda kama ana personal problems ama za inferiority complex or superiority complex ambazo ndizo zipo nyingi kwenye hii Dunia ya tatu.
 
Haya mambo ya kutishiana kupitia vyeo ni ego zaidi ya waafrica...Vyeo kwetu siyo dhamana Bali kama vile Mali binafsi, kama Waziri ni machacharisi atakuwa ana chachafya sector yake? Rais anatishika Kwa lipi? Labda kama ana personal problems ama za inferiority complex or superiority complex ambazo ndizo zipo nyingi kwenye hii Dunia ya tatu.
Umemaliza kila kitu
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom