Je, mbunge Luhaga Mpina ndiye aliyechukua nafasi ya kiongozi wa upinzani Bungeni?

Je, mbunge Luhaga Mpina ndiye aliyechukua nafasi ya kiongozi wa upinzani Bungeni?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kama mjuavyo, kutokana na namna ya uchaguzi mkuu ulivyofanyika hapa nchini mwaka 2020, hakuna Mbunge yeyote wa upinzani aliyechaguliwa, isipokuwa wawili tu ambao ni yule mama wa Chadema, aliyechaguliwa kutoka mkoani Rukwa na Mbunge mwingine wa upinzani kwa tiketi ya CUF toka mkoani Mtwara.

Kwa kifupi ni kuwa kutokana na mkakati alipokuwa ameuweka Mwendazake, ni kuwa alihakikikisha kuwa hakuna kitu kinachojulikana kama uchaguzi mkuu na badala yake kukawa na "uchafuzi" kwa lengo la kuirejesha nchi yetu kwenye mfumo wa chama kimoja cha siasa tuliokuwa nao hapo awali!🥺

Hata hivyo mbinu hizo za Mwendazake, zilikuwa za kutumia vyombo vya dola, kama vile kuwaengua wagombea wa upinzani, kutoruhusu mawakala wa vyama vya siasa vya upinzani vituoni na hata kuona maboksi ya kura yakiingizwa kinyemela na hao "manjagu" wetu kwenye vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo tumeshuhudia baada ya Bunge letu, tunaloweza kudiriki kuliita la mfumo wa chama kimoja, akiibuka Mbunge mmoja wa CCM, wa Jimbo la Kisesa akitema cheche Bungeni, utadhani kuwa yeye anatoka chama cha upinzani hadi amekuwa ni mwiba mkali Sana kwa Mawaziri wa CCM, hadi baadhi ya Mawaziri, wakijikuta wakiweweseka na kujikuta wakinena lugha, kama ambavyo yaliyomkuta Waziri wa chenji, Madeluu, wakati anajibu swali wa wapi zilipo trillion 360 za makinikia?

Ndipo Waziri huyo alipoonekana kama yupo kwenye maombi mazito huku ananena kwa lugha, akitumia lugha yayayayayayayaya.

Hata hivyo, siyo Madelu pekee aliyeonja chungu za Mbunge huyo Luhaga Mpina, bali Mawaziri wengine akina Bashe na Makamba nao "waliingiakwenye 18 zake" na kuonja chungu za Mbunge huyo machachari wa CCM.

Ndipo hapo ninauliza je Luhaga Mpina, ameziba pengo la kambi rasmi ya upinzani Bungeni, iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge Freeman Mbowe wa Chadema?

Hilo ni swali tu naomba majibu, msije mkanipopoa mawe😄
 
Kama mjuavyo, kutokana na namna ya uchaguzi mkuu ulivyofanyika hapa nchini mwaka 2020, hakuna Mbunge yeyote wa upinzani aliyechaguliwa, isipokuwa wawili tu ambao ni yule mama wa Chadema, aliyechaguliwa kutoka mkoani Rukwa na Mbunge mwingine wa upinzani kwa tiketi ya CUF toka mkoani Mtwara.

Kwa kifupi ni kuwa kutokana na mkakati alipokuwa ameuweka Mwendazake, ni kuwa alihakikikisha kuwa hakuna kitu kinachojulikana kama uchaguzi mkuu na badala yake kukawa na "uchafuzi" kwa lengo la kuirejesha nchi yetu kwenye mfumo wa chama kimoja cha siasa tuliokuwa nao hapo awali!🥺

Hata hivyo mbinu hizo za Mwendazake, zilikuwa za kutumia vyombo vya dola, kama vile kuwaengua wagombea wa upinzani, kutoruhusu mawakala wa vyama vya siasa vya upinzani vituoni na hata kuona maboksi ya kura yakiingizwa kinyemela na hao "manjagu" wetu kwenye vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo tumeshuhudia baada ya Bunge letu, tunaloweza kudiriki kuliita
la mfumo wa chama kimoja, akiibuka Mbunge mmoja wa CCM, wa Jimbo la Kisesa akitema cheche Bungeni, utadhani kuwa yeye anatoka chama cha upinzani hadi amekuwa ni mwiba mkali Sana kwa Mawaziri wa CCM, hadi baadhi ya Mawaziri, wakijikuta wakiweweseka na kujikuta wakinena lugha, kama ambavyo yaliyomkuta Waziri wa chenji, Madeluu, wakati anajibu swali wa wapi zilipo trillion 360 za makinikia?

Ndipo Waziri huyo alipoonekana kama yupo kwenye maombi mazito huku ananena kwa lugha, akitumia lugha yayayayayayayaya........

Hata hivyo, siyo Madelu pekee aliyeonja chungu za Mbunge huyo Luhaga Mpina, bali Mawaziri wengine akina Bashe na Makamba nao "waliingiakwenye 18 zake" na kuonja chungu za Mbunge huyo machachari wa CCM.

Ndipo hapo ninauliza je Luhaga Mpina, ameziba pengo la kambi rasmi ya upinzani Bungeni, iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge Freeman Mbowe wa Chadema?

Hilo ni swali tu naomba majibu, msije mkanipopoa mawe😄
Kwani trat na trab anasemaje?
 
Lazima mawazo kinzani yawepo whatever the stuation
 
Kama mjuavyo, kutokana na namna ya uchaguzi mkuu ulivyofanyika hapa nchini mwaka 2020, hakuna Mbunge yeyote wa upinzani aliyechaguliwa, isipokuwa wawili tu ambao ni yule mama wa Chadema, aliyechaguliwa kutoka mkoani Rukwa na Mbunge mwingine wa upinzani kwa tiketi ya CUF toka mkoani Mtwara.

Kwa kifupi ni kuwa kutokana na mkakati alipokuwa ameuweka Mwendazake, ni kuwa alihakikikisha kuwa hakuna kitu kinachojulikana kama uchaguzi mkuu na badala yake kukawa na "uchafuzi" kwa lengo la kuirejesha nchi yetu kwenye mfumo wa chama kimoja cha siasa tuliokuwa nao hapo awali!🥺

Hata hivyo mbinu hizo za Mwendazake, zilikuwa za kutumia vyombo vya dola, kama vile kuwaengua wagombea wa upinzani, kutoruhusu mawakala wa vyama vya siasa vya upinzani vituoni na hata kuona maboksi ya kura yakiingizwa kinyemela na hao "manjagu" wetu kwenye vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo tumeshuhudia baada ya Bunge letu, tunaloweza kudiriki kuliita
la mfumo wa chama kimoja, akiibuka Mbunge mmoja wa CCM, wa Jimbo la Kisesa akitema cheche Bungeni, utadhani kuwa yeye anatoka chama cha upinzani hadi amekuwa ni mwiba mkali Sana kwa Mawaziri wa CCM, hadi baadhi ya Mawaziri, wakijikuta wakiweweseka na kujikuta wakinena lugha, kama ambavyo yaliyomkuta Waziri wa chenji, Madeluu, wakati anajibu swali wa wapi zilipo trillion 360 za makinikia?

Ndipo Waziri huyo alipoonekana kama yupo kwenye maombi mazito huku ananena kwa lugha, akitumia lugha yayayayayayayaya........

Hata hivyo, siyo Madelu pekee aliyeonja chungu za Mbunge huyo Luhaga Mpina, bali Mawaziri wengine akina Bashe na Makamba nao "waliingiakwenye 18 zake" na kuonja chungu za Mbunge huyo machachari wa CCM.

Ndipo hapo ninauliza je Luhaga Mpina, ameziba pengo la kambi rasmi ya upinzani Bungeni, iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge Freeman Mbowe wa Chadema?

Hilo ni swali tu naomba majibu, msije mkanipopoa mawe😄
Huyo anahasira na wanakijani wenzie,kwani walimpora tonge mdomoni🏃
 
Hana lolote unafiki tu, mtetezi wa Jiwe huyo

Nimemsikia akiuliza eti inakuaje serikali imefuta zile trilioni 360 za makinikia na kukubali bilioni 700, wakati hilo lilifanyika kipindi cha Jiwe
 
Hana lolote unafiki tu, mtetezi wa Jiwe huyo

Nimemsikia akiuliza eti inakuaje serikali imefuta zile trilioni 360 za makinikia na kukubali bilioni 700, wakati hilo lilifanyika kipindi cha Jiwe
Siyo alikuwepo mserikalini, waziri, wakati ule? Ameshasahau??
 
Ndipo hapo ninauliza je Luhaga Mpina, ameziba pengo la kambi rasmi ya upinzani Bungeni, iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge Freeman Mbowe wa Chadema?

Hilo ni swali tu naomba majibu, msije mkanipopoa mawe😄
Mkuu 'Mystery', mada zako hapa JF zimetokea kuwa tofauti kidogo na hizi nyingine nyingi tunazokumbana nazo mara kwa mara hapa ukumbini siku hizi.

Napenda kukupongeza na kukutia moyo kwa kuendelea kutufikirisha zaidi kama unavyofanya.

Nianze na Luhaga Mpina na dhana ya Chama Kimoja kilichoshika hatamu. Historia inaonyesha kwamba hata kule kwenye enzi zile za chama kimoja, ndani ya Bunge kulijitokeza wabunge wachache, au kikundi cha wabunge kilichojitambulisha kuwa tofauti na kondoo wengine wote ndani ya Bunge la Chama Kimoja.
Kwa vile hapa ninatiririka tu, sina nafasi ya kutoa mifano mingi ya wabunge wa aina hiyo, lakini sikosi kumkumbuka Mbunge Njeru Kasaka. Najuwa wapo wengi zaidi ya huyo mmoja.

Lakini inabidi pia nikiri hapa hapa, kwamba kwenye Bunge la siku hizi, chini ya CCM hii ya siku hizi, ni vigumu sana kulinganisha hawa wabunge maslahi na wabunge wale wa CCM, Chama kilichojitambulisha kuwa ni cha Wafanya Kazi na wakulima. Hii CCM ni CCM Maslahi, kwa hiyo wabunge wote wanatokana na mfumo huo huo wa kimaslahi, huwezi kutegemea wawe tofauti na kinachosiimamiwa na chama chao.

Inawezekana sana Mbunge mmoja mmoja kama uyo Luhaga Mpina akajikuta amejisahau na kudhani maslahi ya Nchi ndilo lengo la chama na serikali.

Nirudi kule juu kuhusu mafanikio yaliyotokana na "Uchafuzi" aliofanya Magufuli, na jinsi alivyomnufaisha Samia bila kutegemea ingekuwa hivyo.

Aliyofanya Magufuli, pamoja na kuonekana kama alishindwa kukiuwa chama cha CHADEMA, lakini ni wazi kwamba aliyofanya Magufuli matokeo yake ndiyo haya anayofaidi Samia kwa kutumia njia tofauti na zile za Magufuli kukilegeza kabisa chama kikuu cha Upinzani CHADEMA.

Nasubiri tu, kuona yatakayotokea baada ya Novemba nihitimishe hofu yangu ya kuwaaga CHADEMA.
 
Ndipo hapo ninauliza je Luhaga Mpina, ameziba pengo la kambi rasmi ya upinzani Bungeni, iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge Freeman Mbowe wa Chadema?
Hili swali linahitaji jibu makini kuliko ninavyosoma hapa juu yake.
Luhaga Mpina kazungumzia yapi yanayoweza kutafsiriwa kuwa ni yaleyale ambayo CHADEMA wangeyasimamia Bungeni, hadi aonekane kuwa anafanya kazi ambayo ingetekelezwa na wabunge wa CHADEMA!

Nadhani inafaa tuwe watu wa kudadisi kwa kina yanayozungumzwa na kusimamiwa na vionozi. Tukifanya hivyo ndipo tutakapoanza kuwatambua viongozi wenye 'conviction' ya kweli, badala ya kusikia tu wayasemayo juu juu.

Luhaga Mpina anayo rekodi yake ya utendaji, na bila shaka inajulikana msimamo wake ni upi juu ya nchi na watu anaowaongoza jimboni kwake.
Kama tunataka kumjua Luhaga Mpina, basi inalazimu tuangalie kazi zake alizofanya na malengo anayoweka katika uongozi wake.

Binafsi naendelea kusikiliza ili nimfahamu vizuri kiongozi huyu.
 
Hawezi kuchukua hiyo nafasi kwani sharti lake lazima itoke upande wa upinzani, Mpinza ni mbunge aliueamua kutumia vizuri akili zake kwa maslahi ya taifa letu.
 
Back
Top Bottom