Je, mliomaliza shule pamoja miaka ya nyuma bado mnaendelea kuwasiliana?

mlinzi mlalafofofo

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2008
Posts
725
Reaction score
1,282
Kama jibu ni ndio funguka hapa huwa mnasaidiana kwa vipi au kwenye mambo gani?

Pia kama mmeishia kusababishiana presha na vichomi tu, funguka ilikuwaje?

Funguka upone
 
Hatuwasiliani kabisa, ila tukikutana inakuwa surprise na kuitana classmate tu no matter tumezidiana elimu na vipato, wengine wana hadhi za kisiasa, wengine hadhi za wanadini, wafanyabiashara, wanataaluma, wajasiriamali na wengine raia wa mitaani wasio na shughuli rasmi huku kukiwa na walioharibika akili japo wana ufahamu na utambuzi kuwa tulisoma pamoja.

Ila kuna changamoto kama utataka offer kwa aliyekuzidi kipato hutapata katika wengi, ni wachache sana wanaweza kukujali akakupa japo soda au chochote cha ghafla kuonesha ku approciate u schoolmate wenu. Wengine mkishatofautiana hadhi ni ngumu hata kusalimiana kwa kuwa anaona wewe si hadhi yake.
 
Mawasiliano yamekatika ila tukikutana huwa tunachangamkiana, baada ya hapo kama hatutakutana tena, mawasiliano yanakatika ndani ya siku 2 tu.

Kwa sasa tupo na watu tunaoshinda nao zaidi sehemu zetu za utafutaji makazini na kwenye biashara, nao si ajabu mawasiliano yatakatika hapo baadae tusipoonana muda mrefu.

Tunazidi kujifunza watu pekee ambao tutakuwa nao maishani ni watoto wetu, mwenza wako kama mnaishi kwa amani, familia tulizotokea na baadhi ya ndugu. Hao wengine nao ni muhimu pia lakini huwa ni wa muda tu, wanakuja na kupotea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…