Je, Mpunga umeibiwa Kimazingara: Ukweli au Tamaa?

Je, Mpunga umeibiwa Kimazingara: Ukweli au Tamaa?

Joined
Aug 1, 2024
Posts
30
Reaction score
53
Habari wana JF,

Nimeleta uzi huu kwenu ili nipate msaada wa mawazo.

Kuna rafiki yangu wa muda mrefu zaidi ya miaka 15 ambaye alinishirikisha kuhusu kilimo cha mpunga huko Tabora. Nilipokea wazo hilo na tukakubaliana kushirikiana. Tulikodi ekari 8 na kufanikiwa kupanda mpunga. Japo muda mwingi yeye ndiye alikuwa akiangalia maendeleo ya shamba kutokana na mimi kuwa na majukumu mengi kazini, nilichangia gharama kwa asilimia kubwa sana.

Muda wa mavuno ulipowadia, nilipanga kwenda kushiriki lakini sikuweza kupata ruhusa kazini. Hivyo, ilibidi rafiki yangu aende peke yake. Alipofika shambani, alikuta mpunga umekomaa vizuri, na makadirio yalionyesha tungepata gunia 120 au zaidi. Hata hivyo, baada ya mavuno, alinipa taarifa kwamba magunia yaliyopatikana ni saba (7) tu kutoka ekari zote 8.

Nilipouliza sababu, aliniambia kwamba mpunga umeibiwa kimazingara (uchawi). Sasa naomba kuuliza:

  • Je, hili jambo la mpunga kuibiwa kimazingara linawezekana kweli?
  • Au rafiki yangu aliingiwa na tamaa?
Nawakaribisha mawazo yenu.
 
😄😄 uko serious brother?? N vigum sana kuibiwa kichawi kutoka makadilio ya gunia 120 hadi 7. Jamaa kakupiga sana. Ushauri:- usifanye kilimo kupitia phone ama mitandao.
Ni kweli bro, m pia nimejua kuwa kanipiga na sio kwamba nimefany kilimo online bali ni muingiliano tu wa majukumu ika nimejifunza kitu maan ndo ilkuw mara ya kwanz kujaribu kilimo
 
Mtafute mteke,. Mkae sehemu wawili tu, unamuhoji huku unanoa panga, akileta ujinga, unamnyoa nywele na panga, kisha unarudia kumuhoji tena, asipotoa majibu yanayoeleweka, unampga nalo kichwani kule kusiko na makali, Atapasuka kidogo ila hatojua kama umempigia pasipo na makali, unachukua uzi unamshona alipopasuka, unamuhoji tena, asipoleta ushirikiano, fyeka sikio kisha mshone. Mwenyewe atanyoosha maelezo
 
Habari wana jf, nimeleta kwenu huu uzi nipate msaada.
Kuna rafiki yangu wa muda mrefu sana zaid ya miaka 15 alinishirikisha kuhusu kilimo cha mpunga huko tabora nikakubali kushirikiana nae kwenye kilimo eneo tulikodi ekari 8 na tukadanikiwa kupanda mpunga japo muda mwingi alienda yeye kuangalia maendeleo ya mpunga shambani hii kutokana na mim kuwa na majukum mengi zaid kazini lakin gharama zilizokuwa zinahitajika nilichangia kwa asilimia kubwa sana .Ulipofika muda wa mavuno nilitamani kwenda kushiriki nikakosa ruhusa kazini ikabidi aende peke yake, alipofika akakuta mpunga umekomaa vizuri sana na makadirio yalikuwa tupate gunia 120+ akafanikiwa kuvuna,ulipofika muda wa kupakia kwenye magunia akanipa taarifa kuwa yamepatikana magunia saba(7) tu kwa ekari 8 nikauliza sababu ni nini akajibu kuwa mpunga umeibiwa kimazingara(uchawi).sasa naomba kuuliza hiki kitu kipo kweli ? Au aliingiwa na tamaa?
Heka 8 unapata gunia 7?Yaani kwa wastani heka haikufikisha hata gunia1 ? hapa kuna kuja maajabu.asingeweza kukuibia kwa kiwango hiki.ila pia unaweza kufanya upelezi utapata jibu.Hasa wale walioshiriki kazi za shambani.Watu ni wema sana watakunyima fedha ila siyo neno
 
Heka 8 unapata gunia 7?Yaani kwa wastani heka haikufikisha hata gunia1 ? hapa kuna kuja maajabu.asingeweza kukuibia kwa kiwango hiki.ila pia unaweza kufanya upelezi utapata jibu.Hasa wale walioshiriki kazi za shambani.Watu ni wema sana watakunyima fedha ila siyo neno
Kiukweli inafikirisha sana, nimejaribu kufanya reseach ndogo watu wanadai kuwa wizi wa kishirikina huwa upo maeneo hayo lakin pia kuna baadhi ya mabadiliko nimeyaona kwa mwenzangu huenda alikuwa anatafuta hela ya mtaji kupitia mimi kwa sababu kabla ya hapo hakuwa na chochote.
 
Wizi wa mazao kichawi upo. Wenyew wanasem mazO yakisha stawi yanahamishwa kwenda kwenye shamba lao.
Ila hpo uyo jamaa kakupiga parefu. Mvimbishe tumbo atasema magunia yalipo
Watu wana mbinu nying san za kupata hela
 
Habari wana JF,

Nimeleta uzi huu kwenu ili nipate msaada wa mawazo.

Kuna rafiki yangu wa muda mrefu zaidi ya miaka 15 ambaye alinishirikisha kuhusu kilimo cha mpunga huko Tabora. Nilipokea wazo hilo na tukakubaliana kushirikiana. Tulikodi ekari 8 na kufanikiwa kupanda mpunga. Japo muda mwingi yeye ndiye alikuwa akiangalia maendeleo ya shamba kutokana na mimi kuwa na majukumu mengi kazini, nilichangia gharama kwa asilimia kubwa sana.

Muda wa mavuno ulipowadia, nilipanga kwenda kushiriki lakini sikuweza kupata ruhusa kazini. Hivyo, ilibidi rafiki yangu aende peke yake. Alipofika shambani, alikuta mpunga umekomaa vizuri, na makadirio yalionyesha tungepata gunia 120 au zaidi. Hata hivyo, baada ya mavuno, alinipa taarifa kwamba magunia yaliyopatikana ni saba (7) tu kutoka ekari zote 8.

Nilipouliza sababu, aliniambia kwamba mpunga umeibiwa kimazingara (uchawi). Sasa naomba kuuliza:

  • Je, hili jambo la mpunga kuibiwa kimazingara linawezekana kweli?
  • Au rafiki yangu aliingiwa na tamaa?
Nawakaribisha mawazo yenu.
Nililima ufuta hekari 3 nikapata kilo 89 mpaka leo sijaelewa what happened! Maisha Safar ndefu
 
Mkuu ni changie kidogo kwa uzoefu wangu.

Kwanza kubali dawa zipo na hii mimi sibishi. unaweza lima na usitoe hata gunia kwa heka yaani
mazao yako yanaenda mazima mazima {kuhamishwa}

wasuku na hao wanyamwezi wanaroga hadi viazi yaani shina la kiazi unaliona limenawili bala
ukichimba unakutana na mizizi tu bila kiazi ili hali jirani yako wa ng'ambo yeye ana[ata vya kutosha.
sio viazi tu na mazao ni mazao yote.

Nenda hadi kule mliko limia jifanye unakodi kisha uliza wenyeji kuwa kwa wastani heka inatoa magunia mangapi?
baada ya hapo akikuambia muulize aliyekuwepo mwaka jana hapa mbona alipata magunia 7 kwa heka zote saba?

Hapo atakuambia ukweli wote kama kuna uchawi { hakutengeneza shamba} atakuambia ama kama alipata zaidi utaambiwa pia. usiishie huyo tu uliza zaidi ya watu4 hasa vibarua walio husika kuvuna lazima utawapata tu
 
Mkuu ni changie kidogo kwa uzoefu wangu.

Kwanza kubali dawa zipo na hii mimi sibishi. unaweza lima na usitoe hata gunia kwa heka yaani
mazao yako yanaenda mazima mazima {kuhamishwa}

wasuku na hao wanyamwezi wanaroga hadi viazi yaani shina la kiazi unaliona limenawili bala
ukichimba unakutana na mizizi tu bila kiazi ili hali jirani yako wa ng'ambo yeye ana[ata vya kutosha.
sio viazi tu na mazao ni mazao yote.

Nenda hadi kule mliko limia jifanye unakodi kisha uliza wenyeji kuwa kwa wastani heka inatoa magunia mangapi?
baada ya hapo akikuambia muulize aliyekuwepo mwaka jana hapa mbona alipata magunia 7 kwa heka zote saba?

Hapo atakuambia ukweli wote kama kuna uchawi { hakutengeneza shamba} atakuambia ama kama alipata zaidi utaambiwa pia. usiishie huyo tu uliza zaidi ya watu4 hasa vibarua walio husika kuvuna lazima utawapata tu
Hatari sana aisee kika sehem ina changamoto zake
 
Back
Top Bottom