Elections 2010 Je, Mtanzania gani anafaa kuwa Rais wetu 2010?

Elections 2010 Je, Mtanzania gani anafaa kuwa Rais wetu 2010?

Nani anafaa kuwa Rais wa Tanzania 2010-2015?

  • Jakaya Mrisho Kikwete (CCM)

    Votes: 591 23.9%
  • Willibrod Slaa (CHADEMA)

    Votes: 1,785 72.1%
  • Ibrahim Lipumba (CUF)

    Votes: 89 3.6%
  • Hashim Rungwe (NCCR-Mageuzi)

    Votes: 7 0.3%
  • Mutamwega Mugahywa (TLP)

    Votes: 7 0.3%

  • Total voters
    2,475
  • Poll closed .
nionavyo mimi, Rais as an individual pekee haitoshi kumfanya mtu afae, nionanvyo mimi. Tunahitaji powerful, effective governing structures kama bunge ambazo zinaweza kumfanya hata rais wa kawaida sana aendeshe nchi kwa namna inavyotakiwa...wabunge wasio watumishi wa serikali, wanaoweza kumdindishia rais na kumwambia kama atafanya hicho au kile, wanaweza kummwaga kwa kura za kutokuwa na imani naye...


Mbalamwezi, basi kama ni hivyo mimi naona wananchi wasiji-involve moja kwa moja kumchagua rais tuwe kama Marekani, wananchi wachague wabunge kama wawakilishi wao bungeni, bunge kama mwakilishi wa wananchi lipendekeze majina matatu na kuyapigia kura angalau moja kutoka chama tawala na jingine toka upinzani, atakayepata kura nyingi ndiye awe rais mshindi wa pili awe makamu wa rais, hii si tu itasaidia kupunguza gharama za uchaguzi pia italifanya bunge kuwa na nguvu kwenye utendaji wa rais.

Kazi itakatakiwa kwa vyama vyote kuhakikisha kinapata wabunge wengi ili kiweze kutoa rais na hata makamu wake.
 
Naona kuna tatiz la wishful thinking na kutoangalia reality ya nchi yetu kwa sasa. Being in JF na kujua mengi mabaya ya CCM hayapelekei CCM kukosa kura!

CCM na JK wao watashika nchi tena hii haina ubishi, unless watanzania hawa hawa ninaowajua watabadilika, na hii lazima external force should be applied,

bado jamani

Kweli mkuu?
 
Wanajamii,

Uchaguzi mkuu wa Tanzania ndo umekaribia.

Hebu tupeane changamoto kidogo hapa.

Ni nani
- unadhani,
- au ungependelea,
- au unatabiri,
- au una uhakika

atakuwa RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA?

Huna ulazima wa kutoa sababu kwanini umemtaja fulani.
Atatoka CHADEMA.
 
[...............atakuwa RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA!

Bado demokrasia iko chini haswa katika mlongo hu wa karne ya 21, nasema hivi ikiwa na maana ifuatayo!

-Wanasiasa wengi ni waoga haswa wale wa chama kilichoko madarakani kwani hawezi kumpinga aliyeko madarakani.

-Ukweli ni huu hata kama wanavyama vya upinzani watajiunga pamoja bado ni vigumu kuingia madarakini kwani wote hao hawalengi maslahi ya wananchi bali tu maslahi yao.

-Kwa changamoto tunayoiona ya Raisi Kikwete bado atakuwa madarakani kwa miaka minginne mitano kama ilivyo ada kwa watanzania na si mwingine.

-Hivyo kwa hali iliyoka mwanajamii wa Forum, KIKWETE ndo Raisi wa 2010. Ningalionelea ni bora Uchaguzi usifanyike wa Raisi ila wabunge tupige kura kwani si wote watakaorudi tena Dodoma kutokana na Ufisadi ulioko ndani ya Bunge na nje.

-Itakuwa ni bora karatasi za kura za uraisii zisichapishwe kwa maana hakutakuwa na mabadiliko katika nafasi hiyo, pia kupunguza gharama za uchapishaji.

Wako

Owoya-Jamii Forum
Ehe,
Mawazo makubwa haya.
 
jakaya mrisho kikwete. If history and status quo is anything to go by then he will be president for a second term.

Irrespectve of his first term poor rating as a President and compromised health status?Wadanganyika tuamke ama sivyo iko siku tutatawaliwa na misukule!!
 
Profesa Mwesiga Baregu. Huyu hayuko ktk chama cha mafisadi na ndiye atakayeshughulikia ufisadi na unyonge wa Wananchi kwa vile chama chake kina sera zinazoeleweka na zinazolenga kutekeleza hayo.

MWESIGA BAREGU FOR PRESIDENT 2010!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
JK ataendelea lakini naomba a pull up his socks, awe serious na kwendesha nchi sio kurukaruka hapa na pale na kuchekacheka tu.Asahau urafiki ashugulikie wahalifu,achaguwe viongozi wenye uwezo wa kuongoza siyo marafiki tu.
 
sina mengi ila watanzania mnamfahamu vizuri rais wa zanzibar mh. karume
jinsi alivyoleta amani zanzibar je tujiulize anafaa kuwa rais wa tz mwaka 2010?
 
sina mengi ila watanzania mnamfahamu vizuri rais wa zanzibar mh. karume
jinsi alivyoleta amani zanzibar je tujiulize anafaa kuwa rais wa tz mwaka 2010?

Una mengi sana wewe acha uongo....breaking news?

Unafaa uingizwe kule kwenye ignore list
 
Watu wengine bwana kwa kutafuta umaarufu wa ghafla? Acha ujinga
 
This aint breaking news ni hoja mchanganyiko/jukwaa la siasa. change title yako fasta
 
Godwine Jamhuri ya tanzania ndio ipi hiyo??au kuna Nchi mpya inaitwa Jamhuri ya Tanzania.Tupe ufafanuzi
 
Back
Top Bottom