Je, Mungu kaumba baadhi ya wanadamu kwa upendeleo wa akili na maarifa?

Je, Mungu kaumba baadhi ya wanadamu kwa upendeleo wa akili na maarifa?

Kinachotuponza waafrika wengi ni uchoyo wa maarifa
Most of waafrika ni wabinafsi na wachoyo kupitiliza
Huwezi ukapata knowledge yoyote kutoka kwa muafrika kirahisi hivyo labda uwe mzungu
Yani iko hivi, mtu yuko tayari kufa na ujuzi wake kuliko kumpa muafrika mwenzie maana anajua akimpa atanufaika nao nayeye hataki mtu afanikiwe kupitia yeye.
Lakini muafrika huyohuyo jinsi alivyo bashite wa kiwango cha lami akitembelewa na mzungu atampatia siri zote za ujuzi wake huku akikenuakenua meno na kujiona amewin.
Yani wabongo safari yetu bado sana
Mpaka ikifika stage tumejitambua, tukajikubali na kujithamini kwa jinsi tulivyo bila kuwa na inferiority feeling hapo ndipo tutakapotoka kwenye hili dimbwi la kuwa mkia na kuamini kwamba nikimsaidia mwenzangu akafanikiwa kunizidi mimi its okay
Hili swala la uchoyo wa maarifa lipo sana maofisini na mashuleni hata mitaani pia .

Huwa napata maarifa mengi sana kupitia mitandao kama YouTube n.k na huko watu hujitoa kuelekeza vitu mbalimbali na bure compared na wabongo haupati somo lolote mitandaoni.
 
Uwezo wa kifikra inaendana na spirits/rituals za jamii husika.Mimi kwa kutazama tu na changamoto chache nilizopitia nilibaini kuwa jinsi tunavyoishi sisi watanzania hatuwezi fanya kitu kikubwa mfano angalia mtaani kwenu kuanzia wazazi wananaedesha maisha yao vipi? Shule ya msingi watoto wa mtaa wenu,vijana wa mtaa wenu? Je mawazo yao yapo vipi? Starehe Ulaya ndio kwao lakini bado watu wanafanya mambo makubwa sisi ata kilimo nenda kijijini ukutane na washirikina! na wazee wasio na Upeo wakiwaathiri vijana wao utasikitika!..
 
Hili swala la uchoyo wa maarifa lipo sana maofisini na mashuleni hata mitaani pia .

Huwa napata maarifa mengi sana kupitia mitandao kama YouTube n.k na huko watu hujitoa kuelekeza vitu mbalimbali na bure compared na wabongo haupati somo lolote mitandaoni.
Ndugu unafikiri ni uchoyo wa maarifa..hicho unachokisema mimi napenda kuanzia sasa watu wakifahamu kama kukosa Ufahamu!.. kuna kitu kukariri hicho kimeathiri sana jamii zetu!.. Mtu akikariri ana faida juu ya atachoulizwa tu!..kuhusu wabongo kutokuweka mambo mtandaoni ni ishara kuwa ata wale wabongo wanaotufundisha asilimia kubwa wamekariri..Mara ngapi wanashindwa kuja na ubunifu..hadi leo mtihani mgumu unaaminika kuwa ndio kipimo cha uelewa hivyo basi atakaekuwa amekariri kuliko mwenzake ndio atafaulu mtihani! pia kuna changamoto ya uvivu wa kujifunza vitu vipya!
 
Ngoja nikupe mfano! Kuna Siku nilienda kijijini nikakuta kuna magogo flani wanatengeneza kama pembe tatu kwa ajili ya kubebea plau(Jembe la kukokota na ngo'mbe) nikawauliza wazee kwa vijana inakuwaje wanatumia zana kama hiyo tangu enzi na enzi na inaleta mmomonyoko wa ardhi na kuleta makorongo, kwa nini hawafikirii kuweka matairi? majibu waliyonipa niliona yahitajika zaidi ya karne hicho kizazi kitoweke kabisa ndio maarifa yaje! hadi tunajadili hili ni watu wachache watajitokeza kuchangia!..wabongo hatutaki kuchoma kichwa,tunapenda mada za kelele kelele.. mtu akishapata sehemu ya mkate imetoka hiyo!
 
Mfano mwingine Mi nakaa karibu na Airport Jana umeme ulikatika mtaani na Uwanja wa Taifa kukiwa na mechi mchuanao wa CAF, wakati huko Airport umeme unawaka na ndege zinatua! Tujiulize tu! kwa nini Airport na sio kwingine utabaini udhaifu wetu! lakini watakuja watu kutetea ujinga badala ya kuomba radhi nakufanya mageuzi!
 
Hakuna haja ya kumlaumu Mwenyezi Mungu.Hakuna taifa lolote duniani lililoendelea bila ya kuwekeza KIKAMILIFU kwenye ELIMU.Ni kuwekeza KIKAMILIFU na si KIMZAHA na KUJARIBUJARIBU.Kosa kubwa mno kucheza na elimu.Kama nchi haitengenezi 'SKELETON' ya elimu iliyo madhubuti;yenye kuzalisha wataalamu wabunifu na si wasaka cheti, skeleton hiyo ikatekelezwa kiuadilifu na commitment ya hali ya juu na uzalendo usiotia shaka,nchi ikimbie kwa kasi ya kimbunga.Tusitafute mchawi kama tutacheza na elimu.
 
i think its just our thinking, mi naona wapo sawa tu na sisi hao wazungu maana kuna matajiri na maskini tu kama uku , na wanasoma sawa na sisi tu maana si kuna watu wanaendaga kusoma mambele akianza na raisi nyerere kabisa ila bado nchi ipo pale pale
 
Hii elimu tuliyonayo ni ya kishenzi sana.Ni elimu ya kutambia tu mtaani na si elimu ya kuleta mabadiliko.Na hata serikali inavyolipa watu wake,hailipi utendaji bali inalipa cheti,kwa hiyo hata vyuoni zinafanyika faulo za hatari ili mtu apate cheti na kinakuwa kama kibali cha kulipwa zaidi.

Niliona tofauti kidogo kwa wazungu,wao wanalipa uwezo wa kazi.Hata kama mtu ni darasa la saba kama anauwezo wa kuzalisha,wanalipa pesa nzuri sana.Nimeshuhudia mtu mmoja aliajiriwa kama meneja Australia mgodini akiwa darasa la saba tu tena la Tanzania. Alibahatika kufanya mgodini na akonesha uwezo mkubwa sana kiasi kwamba wazungu ilibidi wamkubali.

Kama serikali zetu zingekuwa zinamiliki timu,ungeshangaa wachezaji wangekuwa wanalipwa mishahara kwa vigezo vya elimu hata kama hawashindi ama hawafungi magoli. Hii ndiyo inaua sana uwezo wetu na kuturudisha nyuma.

Wako watu wanaonesha vipaji vikubwa kama kutengeneza silaha,dawa n.k wanakamatwa au kufungiwa kabisa.Huu ni ushenzi mkubwa.
mkuu kanywe soda ya ntalipa maana daa! una akil sana aisee umetoboa pale pale
 
Great poets ndo hao wazungu,
Great novel writers ndo hao wazungu,
Great fiction writers and actors ndo hao wazungu,
Great preachers ndo hao wazungu,
Great philosophers ndo hao wazungu,
Great lawyers & doctors ndo hao wazungu,
Great architect ndo hao wazungu,
Great painters ndo hao wazungu,
Great leaders ndo hao wazungu,
Great bloggers/freelancers ndo hao wazungu,
Great physician and phsycologists ndo hao wazungu,
Great teachers/lecturers/speakers/journalists ndo hao wazungu,

huku kwetu tumekalia majungu na roho mbaya, kwa mifano michache: mtu kasomea philosophy lakini hadi anakufa akiwa mzee hana hata falsafa mpya kuhusu chochote aliyoibaini.

Mtu kasomea literature lakini hadi anazeeka na kufa hajawahi kuandika great novel/poem ambayo mtu akisoma anapata cha kujifunza.

Wasomi wengi wanapambana kuwa malecturers lazimishi na siyo malecturers ongozaji. Watakulazimisha kuelewa walichokariri hawatakuongoza kuelewa.

UDSM na vyuo vingine vimejaa coward elites mtu kasomea economics halafu hadi anakufa hana CV yoyote ya kuanzisha economic venture yoyote, yaani mtu anakufa na CV ndefu ya utumishi wa umma lakini kwenye private life ana zero Cv.

Wazungu wanawaambia wanao: Mwanangu soma ili ujielewe na kuelewe mazingira yako.

Waafrika wanawaambia wanao: mwanangu soma uje uajiriwe na kutajirika.

Hivi kweli Maprof wa hapa Tz watakufundishia mtoto apate akili ya kujiongeza nje ya elimu? Maana wao wenyewe wanaishi kwa huruma za serikali, hapa Tz karibia maprof wote wako controlled in minds.

Controlled minds can't think to discover new things.
 
Kabla ya wazungu kuja Africa tulikuwa na wahandisi wetu walifua vyuma tukapata majembe, visu, mapanga n.k walipotuvamia wazungu waliwaua wote waliokuwa na ujuzi huo tukakwama kuendelea kuhusu madawa na vifaa tiba tulikuwa na dawa zetu nzuri za miti tulitibiwa nazo kuongezeka kwa magonjwa kunatokana na maendeleo ya kisayansi usione kama wao ni wabunifu kwani hata hayo magonjwa wanatengeneza wawo ili wafanye biashara ya dawa magonjwa mengi ni mapya tumeyasikia miaka ya 1980 na kuendelea wazungu na waafrika wote tupo sawa kiakili
Hii ni hoja dhaifu mno ya kujifariji. Mpaka unahisi wao wanatengeneza mashua/meli zinazoweza kutoka ulaya mpaka Africa sisi tulikuwa tumetengeneza nn cha ajabu walichoiga? Mpaka wao wanagundua kuwa madini ni mali na kutusainisha mikataba ya kilaghai sisi tulikuwa wapi kugundua hayo yote?
 
Great poets ndo hao wazungu,
Great novel writers ndo hao wazungu,
Great fiction writers and actors ndo hao wazungu,
Great preachers ndo hao wazungu,
Great philosophers ndo hao wazungu,
Great lawyers & doctors ndo hao wazungu,
Great architect ndo hao wazungu,
Great painters ndo hao wazungu,
Great leaders ndo hao wazungu,
Great bloggers/freelancers ndo hao wazungu,
Great physician and phsycologists ndo hao wazungu,
Great teachers/lecturers/speakers/journalists ndo hao wazungu,

huku kwetu tumekalia majungu na roho mbaya, kwa mifano michache: mtu kasomea philosophy lakini hadi anakufa akiwa mzee hana hata falsafa mpya kuhusu chochote aliyoibaini.

Mtu kasomea literature lakini hadi anazeeka na kufa hajawahi kuandika great novel/poem ambayo mtu akisoma anapata cha kujifunza.

Wasomi wengi wanapambana kuwa malecturers lazimishi na siyo malecturers ongozaji. Watakulazimisha kuelewa walichokariri hawatakuongoza kuelewa.

UDSM na vyuo vingine vimejaa coward elites mtu kasomea economics halafu hadi anakufa hana CV yoyote ya kuanzisha economic venture yoyote, yaani mtu anakufa na CV ndefu ya utumishi wa umma lakini kwenye private life ana zero Cv.

Wazungu wanawaambia wanao: Mwanangu soma ili ujielewe na kuelewe mazingira yako.

Waafrika wanawaambia wanao: mwanangu soma uje uajiriwe na kutajirika.

Hivi kweli Maprof wa hapa Tz watakufundishia mtoto apate akili ya kujiongeza nje ya elimu? Maana wao wenyewe wanaishi kwa huruma za serikali, hapa Tz karibia maprof wote wako controlled in minds.

Controlled minds can't think to discover new things.
Good comment
 
Aliyechangia kwamba kabla ya kuja wazungu tulikua na tekinologia yetu lakini wakatudanganya na kuiharibu, sasa mtu kuja nyumbani na kukudanganya ni akili ya hali ya juu. Ni kwa nini wewe usitumie akili uende kwake?? Wamejaliwa akili na maarifa ya kutosha. Umeshaona formula ya kisayansi ya mwafrika? Tunaishia kukariri za kwao eg Archimedes principle, Newtons law of motion nk Basi tuseme hakuna Mungu kwani hakuna Mungu mwenye upendeleo kiasi hicho. Check the concept of time in Africa
 
Mkuu umeibua hoja nzuri sana. Nataka nikufahamishe tu kuwa kama tukitazama kwa hoja yako hiyo ya Upendeleo basi Mungu alitupendelea maarifa sisi waafrika ila tu hatuna juhudi hasa kizazo hiki cha sasahivi.
Mwandishi Walter Roodney aliwahi kuandika kitabu cha HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA. Katika kitabu hiko ameelezea namna gani Afrika ilikua na maendeleo zaidi ya wazungu.
Ukisema kwamba waafrika hatuna maarifa ya kugundua kitu unakua unakosea sana. Kwanza tambua kwamba uhusiano wa Mzungu na mwafrika ulianza mnamo karne ya 15. Hapo tunazungumzia miaka ya 1400.
Wazungu walipokuja Afrika kwa mara ya kwanza, walikuta tayari tumeendelea kuzidi wao wenyewe kiasi kwamba wakaiga sehemu kubwa ya teknolojia yetu na kwenda kuziendeleza kwao. Najua utabisha katika hili, lakini nitakudhibitishia kwa nadharia za kihistoria na kisayansi kupitia nyanja zifuatazo.

ELIMU
(Hesabu na maandishi)
Hesabu nyingi unazoziona hivi leo zilianzia MISRI (Egypt). Njia hii tunayotumia leo kuhesabu ilianza zaidi ya miaka 35000 iliyopita kutoka Africa. Wamisri walianza kuandika vitabu kuhusu hesabu za kugawanya kuzidisha, hesabu za sehemu na Geometry.
Mfumo wa kuandika herufi tunazozitumia leo, ulianza Misri pia mnamo miaka ya 3100 KB (Kabla ya kristo).
Kalenda inayoipa dunia siku 365 na robo , ilitengenezwa na wamisri. Kugwanywa kwa masaa 24 kwa siku kulianza misri zamani sana na enzi hizo walitumia misimu hasa ya maji kutambua masaa.

DAWA

Katika hoja yako umesema kwamba wazungu wamegundua dawa. Sio kweli!! kuna tofauti kati ya kugundua na kuendeleza. (invent and develop)
Dawa zinazotumiwa leo ziligunduliwa Africa zamani sana huko Misri, Nigeria na Afrika kusini enzi hizo kabla nchi hizo hazijapewa hayo majina. Walitumia mizizi na mimea kutibu magonjwa mbalimbali. kwamfano Salicylic acid kwaajili ya kupunguza maumivu ambayo leo hii wazungu wameindeleza tunaitambua kama Aspirin. Kaolin Acid kwaajili ya ugonjwa wa kuhara ambayo leo hii dawa inaitwa Kaopectate. Utafiti umeendelea kueleza kua, waafrika walikua na uwezo wa kufanya upasuaji (under antiseptic conditions) wakati huo ujuzi huo ndo ulikua unaanza kuibuka barani ulaya.

ENGINEERING
Moja ya kidhibiti hai cha utafiti kwamba Africa ilikua na maengineer na maachitecture wake hata kabla ya wazungu ni Pyramid of Giza (Cairo) ambayo ipo kwenye maajabu saba ya dunia. Utafiti unaonyesha Pyramid hyo ilijegwa mnamo Miaka ya 2580 KB (Kabla ya kristo) kipindi ambacho hta mzungu hakuwa na jengo lolote la ajabu kama hilo. Kinachofanya pyramid hii iwe ya ajabu ni ufundi uliotumika.
Waliosimamisha pyramid ile walibeba tani milioni sita na nusu za mawe ambapo kila jiwe lilikuwa na tani zisizopungua 9. Kwa kipindi hiko ambapo hakukua na mawinch wala minyororo wala cement waliwezaje kupandisha haya mawe? Ni wazi kabisa mwafrika alikua na teknolojia ya kipekee kabla ya mzungu.

Nina mifano mingi natamani kukushirikisha ila kwa leo naishia hapo. Waafrika tuna akili na kama ni upendeleo basi Mungu alitupendelea sisi. Ila tu waafrika sisi ni wavivu kujituma na kufikiri. Mzungu hana akili kama tunavyodhani, ila tu kapewa juhudi na kiu ya kujifunza. Sisi tumelala sana na kwa mantiki hiyo Mzungu anaokana ana akili kuliko sisi.
ASANTENI!!
Hatari sana
 
Back
Top Bottom