Je! Mungu ni yule yule?

Je! Mungu ni yule yule?

Hivi Kiranga amewahi kuthibitisha kwamba Mungu hayupo? Kuna ushahidi aliokuja nao kuthibitisha kwamba Mungu hayupo? Au ni dhana ile ile iliyozoeleka ya kuzunguka mbuyu!
Kama kitu hakipo. Unaanzia wapi kuthibitisha kwamba hakipo?

Uthibitisho wa aina gani utakufaa kuonesha kwamba kitu hakipo?

Nikikwambia pembetatu yenye pembe sita ipo, ila wewe huijui na huna akili za kuiona tu (wakati kwa kweli haipo), utanithibitishiaje kwamba haipo?

Aliyeua kwa kisu unaweza kutoa ushahidi wa alama za vidole zake ukasema huyu kaua kwa kisu, kisu kimepatikana eneo la mauaji kina damu, kina alama zake za vidole, jeraha lililoua limetokana na kisu hiki, huyu ambaye alama zake za vidole zipo kwenye kisu hana alibi.Zaidi kuna video imemrekodi akiua. Zaidi, nyumba ina alarm na ikajifunga milango, polisi wakaja wakamkuta muuaji ndani. Jirani walimuona dirishani akiua.

Overwhelming evidence. Huyu kaua.

Sasa kama hakuna aliyeua kwa kisu, utathibitishaje kwamba hakuna aliyeua kwa kisu wakati hakuna maiti, hakuna kisu, hakuna alama za vidole?

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kama alivyoandikwa katika vitabu vya Biblia na Quran, hayupo.

Hayupo kwa sababu, dhana nzima ya kuwepo kwake, inajipinga yenyewe.Contradiction.

Dhana ya kuwepo kwake inajipinga yenyewe, kwa sababu, kwa upande mmoja, Mungu huyu ni mtakatifu sana kiasi kwamba kibaya chochote hakiwezi kutoka kwake. Kwa maana hiyo, angekuwepo, dunia isingewezekana kuwa na mabaya. Ukisema aliumba dunia isiwe na mabaya ila Shetani ndiye akaleta mabaya, nitakuambia hata huo uwezo wa Shetani kuweza kuleta mabaya ni ubaya ambao Mungu mwenye utakatifu unaosemwa hatakiwi kuwa nao.

Kwa hiyo, utaona kwamba, kuwepo kwa mabaya, na zaidi, kuwezekana kuwepo kwa mabaya katika dunia hii, ni uthibitisho kwamba Mungu huyu hayupo.

Wengine wamejaribu kujibu kwa kusema Mungu kaachia mabaya ila katupa uwezo wa kuchagua mabaya na mazuri. Hili ni jibu lisilo na mantiki. Ukiwa na mtoto wako mchanga ambaye uelewa wake ni mdogo sana, na wewe una uelewa mkubwa sana kujilinganisha naye, unampenda, utampa chupa ya maziwa na pembeni umuwekee chupa ya sumu ili tu aweze kuchagua anachotaka? Hapana. Utahakikisha nyumba nzima haina sumu anayoweza kuifikia. Utampa maziwa tu.

Sasa kama binadamu mwenye uwezo mdogo, upendo mdogo na ujuzi mdogo anakataa kumpa mtoto wake mchanga maziwa na sumu ili mtoto awe na uhuru wa kuchagua, imekuwaje Mungu huyu mnayemsema mwenye uwezo usio na mwisho, ujuzi usio na mwisho na upendo usio na mwisho ameruhusu ulimwengu uwe na mazuri na mabaya ili watu wawe na uhuru wa kuchagua tu?

Watu kama wangeumbwa katika dunia ambayo haiwezekani kuwa na mabaya na mabaya hata hayajulikani, in fact hayapo kabisa hata kidhana, wangekosaje uhuru wa kitu ambacho hakijulikani wala kufikirika wala kuwepo kidhana tu?

Huyu Mungu yupo kweli au hadithi tu?

Kaachia dunia yenye magonjwa, vita, matetemeko, mafuriko, njaa, umasikini, kuteseka etc, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hivyo vyote haviwezekani watu wakaishi raha mustarehe.

Kwa nini?

Sijajibiwa jibu la kueleweka kwenye swali hili.
 
the world of spirit v/s the world of flesh,,,
hapo lugha tofauti ,,elimu tofauti,,kila kitu tofauti hoja ipi a person from spirit world can explain to convince a person from the world of flesh lugha gongana hapo
 
Kama kitu hakipo. Unaanzia wapi kuthibitisha kwamba hakipo?

Uthibitisho wa aina gani utakufaa kuonesha kwamba kitu hakipo?

Nikikwambia pembetatu yenye pembe sita ipo, ila wewe huijui na huna akili za kuiona tu (wakati kwa kweli haipo), utanithibitishiaje kwamba haipo?

Aliyeua kwa kisu unaweza kutoa ushahidi wa alama za vidole zake ukasema huyu kaua kwa kisu, kisu kimepatikana eneo la mauaji kina damu, kina alama zake za vidole, jeraha lililoua limetokana na kisu hiki, huyu ambaye alama zake za vidole zipo kwenye kisu hana alibi.Zaidi kuna video imemrekodi akiua. Zaidi, nyumba ina alarm na ikajifunga milango, polisi wakaja wakamkuta muuahi ndani. Jirani walimuona dirishani akiua.

Overwhelming evidence. Huyu kaua.

Sasa kama hakuna aliyeua kwa kisu, utathibitishaje kwamba hakuna aliyeua kwa kisu wakati hakuna maiti, hakuna kisu, hakuna alama za vidole?

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kama alivyoandikwa katika vitabu vya Biblia na Quran, hayupo.

Hayupo kwa sababu, dhana nzima ya kuwepo kwake, inajipinga yenyewe.Contradiction.

Dhana ya kuwepo kwake inajipinga yenyewe, kwa sababu, kwa upande mmoja, Mungu huyu ni mtakatifu sana kiasi kwamba kibaya chochote hakiwezi kutoka kwake. Kwa maana hiyo, angekuwepo, dunia isingewezekana kuwa na mabaya. Ukisema aliumba dunia isiwe na mabaya ila Shetani ndiye akaleta mabaya, nitakuambia hata huo uwezo wa Shetani kuweza kuleta mabaya ni ubaya ambao Mungu mwenye utakatifu unaosemwa hatakiwi kuwa nao.

Kwa hiyo, utaona kwamba, kuwepo kwa mabaya, na zaidi, kuwezekana kuwepo kwa mabaya katika dunia hii, ni uthibitisho kwamba Mungu huyu hayupo.

Wengine wamejaribu kujibu kwa kusema Mungu kaachia mabaya ila katupa uwezo wa kuchagua mabaya na mazuri. Hili ni jibu lisilo na mantiki. Ukiwa na mtoto wako mchanga ambaye uelewa wake ni mdogo sana, na wewe una helewa mkubwa sana kujilinganisha naye, unampenda, utampa chupa ya maziwa na pembeni umuwekee chupa ya sumu ili tu aweze kuchagua anachotaka? Hapana. Utahakikisha nyumba nzima haina sumu anayoweza kuifikia. Utampa maziwa tu.

Sasa kama binadamu mwenye uwezo mdogo, upendo mdogo na ujuzi mdogo anakataa kumpa mtoto wake mchanga maziwa na sumu ili mtoto awe na uhuru wa kuchagua, imekuwaje Mungu huyu mnayemsema mwenye uwezo usio na mwisho, ujuzi usio na mwisho na upendo usio na mwisho ameruhusu ulimwengu uwe na mazuri na mabaya ili watu wawe na uhuru wa kuchagua tu?

Watu kama wangeumbwa katika dunia ambayo haiwezekani kuwa na mabaya na mabaya hata hayajulikani, in fact hayapo kabisa hata kidhana, wangekosaje uhuru wa kitu ambacho hakijulikani wala kufikirika wala kuwepo kidhana tu?

Huyu Mungu yupo kweli au hadithi tu?

Kaachia dunia yenye magonjwa, vita, matetemeko, mafuriko, njaa, umasikini, kuteseka etc, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hivyo vyote haviwezekani watu wakaishibraha mustarehe.

Kwa nini?

Sijajibiwa jibu la kueleweka kwenye swali hili.
democrasia ndo ilipoanzia huko uhuru wa kuchagua
 
HAKUNA ANAYEWEZA KUMJIBU KIRANGA HOJA ZAKE ....WOTE WANAOJARIBU KUZIJIBU WAMEKUWA WANAISHIA KUONGEA BLAAA BLAA TU "''Jamaa ana maswali mazito mtu ambayo mtu mwenye upeo mdogo hawezi kung'amua kitu
Anapatikana wapi huyu kiranga?
 
hahaa kumbe upo online ..kwakweli mimi ni muislam lakini ukifuatilia deep kuhusu haya maswala ya dini yanatia kichefu chefu aiseee ..Mara cjui malaika ana mabawa " Mara cjui tukifa tutakwenda mbinguni ..ilahli mbingu mpka leo haijulikani ilipo
Ni kujifariji tu.

Tunajipa majibu rahisi kwa maswali magumu ambayo hatuyajui.
 
Tunaporuhusu bongo zetu zitawaliwe na kutaka majibu na ithibati za kidunia kwenye ulimwengu wa roho ndio hapo mkanganyiko unapoanza....
Jambo lolote la kiroho halina ithibati za kisayansi hivyo mtu anapokukazania umthibitishie uwepo wa Mungu nawe ukaanza kubabaika jua umekwisha... Atacheza nawe atakavyo kwakuwa tayari ameshakutega nawe ukategeka
[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Kiranga Ana hatari na siku hizi naona amepunguza kidogo kuzungumza ilo swala. Mwanzoni alizua mtafaruku Jf nzima kwa hoja zake
Huyo jamaa sijawai kukutana nae humu JF, ila kuna kijana fulani nimepata kukutana nae mara nyingi Dar city center asee yule jamaa ana hoja zenye nguvu sio mchezo,

Yani akianza kukupa hoja zake wether awe kwenye upande wa MUNGU yupo au upande wa MUNGU hayupo asee huchomokii....kile kichwa sijui ni cha wapi na aliwezaje kuijua biblia vile, mm mpaka nikahisi yule alikua na mapepo/majini [emoji23][emoji28][emoji23]

Kama ni huyo yupo humu kwa ID ya kiranga basi namsalimia tu [emoji125][emoji125][emoji125]
 
kila kitu kina chanzo chake bro,, we human being ,we exist sababu kuna jambo lilifanya sisi tuexist ,,creation ,,and who created us is the most high GOD
Hapo katika logic umefanya kosa linaitwa non sequitur.

www.dictionary.com

non se·qui·tur

ˌnän ˈsekwədər/

noun

a conclusion or statement that does not logically follow from the previous argument or statement.




Umeunganisha premise na conclusion wakati hazina uhusiano.

Ni kama vile umesema.

1.Kila mwanamke ni mtu.

2.John Magufuli ni mtu.

3.Hivyo, John Magufuli ni mwanamke.

Tukikubali kwamba kila kitu kina mwanzo wake (nitarudi hapa kama ukiweka kwenda nami), hujathibitisha chanzo chetu ni Mungu. Umelazimisha bila kuonesha kimantiki umetokaje kwenye "kila kitu kina chanzo chake" ukafika kwenye "chanzo chetu ni Mungu".

Umeruka step na kufikia conclusion uliyoitoa hewani kama yuke aliyefikia conclusion ya "John Magufuli ni mwanamke".

Hujajibu suala la "the problem of evil".

Kama Mungu yupo, ana uwezo wote, ujuzi wote na uoendo wote, kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kutokea?

Je, alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, lakini hakutaka tu?

Kama ni hivyo, je, ni kweli ana upendo wote?

Au, alitaka kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani kuwepo, lakini hakiweza tu?

Kama ni hivyo, je, ni kweli ana uwezo wote?

Mungu huyu yupo kweli au ni hadithi za mapokeo tu?
 
najua kunavuta ambavyo vimefanya ukamilifu mpak sisi kuitwa human bein,,,
tumepewa utashi...
kila binadamu na utashi wake,, hata malaika nao waliumbwa vivyo hivyo kila malaik alipewa utashi wake.
Ndomana hata kuna malaika walitaka kufanya mambo makubwa kumzid mungu sababu waliamin TASHI zao.
Maovu mengi na matatizo mengi yanayotokea sasa si mungu ameleta ila UTASHI wa kila mwanadamu ukikinzana na mwengine lazima ulete contradictions na with the name of God yeye ni kama a centre of UNITING those differences who else than GOD??
 
najua kunavuta ambavyo vimefanya ukamilifu mpak sisi kuitwa human bein,,,
tumepewa utashi...
kila binadamu na utashi wake,, hata malaika nao waliumbwa vivyo hivyo kila malaik alipewa utashi wake.
Ndomana hata kuna malaika walitaka kufanya mambo makubwa kumzid mungu sababu waliamin TASHI zao.
Maovu mengi na matatizo mengi yanayotokea sasa si mungu ameleta ila UTASHI wa kila mwanadamu ukikinzana na mwengine lazima ulete contradictions na with the name of God yeye ni kama a centre of UNITING those differences who else than GOD??
Mpaka sasa.

1. Hujathibitisha Mungu yupo.

2. Unazidi kutaja vitu vingine ambavyo hujathibitisha vipo, kama malaika.

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?

Kwa nini Mungu aumbe ulimwengu unaoruhusu maovu?

Mungu huyo ni muovu?
 
Back
Top Bottom