Je! Mungu ni yule yule?

Je! Mungu ni yule yule?

Amri yangu kuu ni kumpenda jirani yangu kama nafsi yangu japo muda mwingine nashindwa kutokana na mapungufu ya kibinadamu japo najitahidi mara nyingi nisitoke kwenye huo msingi ,Mimi hata sisimizi nampenda japo hawajui kama Mungu yupo au hayupo
Kwa nini mungu wa upendo kaumba ulimwengu unaoruhusu watu wawe weupe na weusi na watu ambao hawajapata akili za kutosha kupitana migawanyiko ya rangi?
 
Kwa nini mungu wa upendo kaumba ulimwengu unaoruhusu watu wawe weupe na weusi na watu ambao hawajapata akili za kutosha kupitana migawanyiko ya rangi?
Kiranga kupenda sio lazima ujifunze kutoka kwa Mungu aliyeumba wabaya ama wema au weusi ama weupe ,nakuwa kwenye jovial mood ninapo penda kuliko mbadala wake
Na hiyo feeling kwangu ni natural
 
Kuna baadhi ya maswali yangu umeyakwepa page ya 14,ila sio case.!

Dhambi ni kama matumizi mabaya ya kitu.ili kuiondoa dhambi lazima uondoe hicho kitu.

Kwa mfano,kuna baadhi ya dawa zinafaa kwa matumizi ya nje tu/external uses

Ukizinywa ni sumu.

Dhambi ipo hivyo hivyo,ni kutokutii sheria zilizopo

Ili uondoe dhambi,lazima uondoe sheria na kiumbe kisichotii iyo sheria

Hivyo basi,ulimwengu usio na dhambi ni ulimwengu usio na sheria wala kiumbe chochote chenye maamuzi huru.

Ni ulimwengu usio na maana yoyote
Kwa hiyo mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna dhambi na una maamuzi huru ambayo yote si dhambi?

Maamuzi huru ni lazima yahusishe mazuri na mabaya? Hakuna maamuzi huru yanayohusu mazuri na mazuri tu?

Nikiwa na maamuzi kati ya kutoa sadaka na kusaidia yatima, hayo ni maamuzi mawili mazuri yote, Nina Uhuru wa kuchagua moja, kwa nini unataka kufanya kwamba maamuzi huru ni lazima yahusishe mazuri na mabaya?

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao maamuzi huru yapo, Ila ni mazuri tu?
 
Kiranga kupenda sio lazima ujifunze kutoka kwa Mungu aliyeumba wabaya ama wema au weusi ama weupe ,nakuwa kwenye jovial mood ninapo penda kuliko mbadala wake
Na hiyo feeling kwangu ni natural
Hujajibu swali uliloulizwa.

Na kama kuna swali umejibu, si nililouliza.
 
Hujajibu swali uliloulizwa.

Na kama kuna swali umejibu, si nililouliza.
Umeongelea kwanini Mungu wa upendo ,nikakujibu mimi kufanya upendo haina maana nam reflect Mungu aliye waumba weusi na weupe ama vinginevyo,
Hivyo kujibu swali la kwanini Mungu kafanya hivyo sina mamlaka hayo ,anajua mwenyewe kwanini kaamua kufanya hivyo na wala usiendelee kutafuta hayo majibu hapa duniani maana na hakika hutokaa kupata majibu yake
 
Umeongelea kwanini Mungu wa upendo ,nikakujibu mimi kufanya upendo haina maana nam reflect Mungu aliye waumba weusi na weupe ama vinginevyo,
Hivyo kujibu swali la kwanini Mungu kafanya hivyo sina mamlaka hayo ,anajua mwenyewe kwanini kaamua kufanya hivyo na wala usiendelee kutafuta hayo majibu hapa duniani maana na hakika hutokaa kupata majibu yake
Huwezi kujibu kwa sababu humuelewi Huyo mungu.

Humuelewi kwa sababu hayupo, katungwa tu shaghalabaghala na watu kibao wenye mawazo na elimu tofauti.

Biblia yenyewe imeungwaungwa na Mfalme Constantine at the Council of Nicea, aliwafungia maaskofu wakaamua kitabu gani kiingie kwenye biblia na kipi kisiingie.

Watu tu wamepanga.

Leo tunaambiwa kitabu cha mungu.

Quran ndo total hallucinations kama nilivyoonyesha hapo juu.
 
Huwezi kujibu kwa sababu humuelewi Huyo mungu.

Humuelewi kwa sababu hayupo, katungwa tu shaghalabaghala na watu kibao mwenye mawazo na elimu tofauti.

Biblia yenyewe imeungwaungwa na Mfalme Constantine at the Council of Nicea, aliwafungia maaskofu wakaamua kitabu gani kiingie kwenye biblia na kipi kisiingie.

Watu tu wamepanga.

Leo tunaambiwa kitabu cha mungu.
Kuna sehemu yeyote nimeongelea biblia kwenye majadiliano haya ? Wewe biblia ndio ushaidi pekee ulioa amua kuutumia kama reference ya Mungu kuwepo ??

Hilo swali lako la kwanini Mungu kaumba huyu mweusi ama mweupe au maskini nk hakuna mwanadamu atakayeweza kulijibu hapa duniani ,
Utakua unapoteza muda kwa maswali ambayo majibu yake anayajua Mwenyewe Mungu
 
Kuna sehemu yeyote nimeongelea biblia kwenye majadiliano haya ? Wewe biblia ndio ushaidi pekee ulioa amua kuutumia kama reference ya Mungu kuwepo ??

Hilo swali lako la kwanini Mungu kaumba huyu mweusi ama mweupe au maskini nk hakuna mwanadamu atakayeweza kulijibu hapa duniani ,
Utakua unapoteza muda kwa maswali ambayo majibu yake hayapo
Hakuna atakayeweza kulijibu kwa sababu mungu hayupo.

Ni kama kuuliza rangi ya wimbo wa Michael Jackson, au harufu ya duara.

Wimbo hauna rangi wala duara halina harufu.

Swali limepinda, haliwezi kuwa na jibu.
 
Hakuna atakayeweza kulijibu kwa sababu mungu hayupo.

Ni kama kuuliza rangi ya wimbo wa Michael Jackson, au harufu ya duara.

Wimbo hauna rangi wala duara halina harufu.

Swali limepinda, haliwezi kuwa na jibu.
Sio kwa sababu hayupo , kwa sababu huamini kama yupo.

huyo aliyekupa utashi wa kuelewa kwamba duara halina harufu ama wimbo hauna rangi ndiye pia aliye kunyima kujua kwanini kaumba weupe ama weusi ,ama vilema .
Angekunyima pua ama macho hapa leo usingekua unayaongelea haya
 
Sio kwa sababu hayupo , kwa sababu huamini kama yupo.

huyo aliyekupa utashi wa kuelewa kwamba duara halina harufu ama wimbo hauna rangi ndiye pia aliye kunyima kujua kwanini kaumba weupe ama weusi ,ama vilema .
Angekunyima pua ama macho hapa leo usingekua unayaongelea haya
There is such a thing as putting the cart before the horse.

And forwarding a circular argument.

Kabla ya kuniambia mungu kanipa nini na kaninyima nini, unaweza kuthibitishia kwamba yupo at all?
 
There is such a thing as putting the cart before the horse.

And forwarding a circular argument.

Kabla ya kuniambia mungu kanipa nini na kaninyima nini, unaweza kuthibitisha kwamba yupo at all?
Usingekua na pua ungejuaje kwamba duara halina harufu au usingekua na macho ungejuaje kwamba mziki hauna rangi ?? Pengine labda kuna kitu cha ziada unatakiwa uwe nacho ndio ujue siri za Mungu ambacho kitu hicho wewe huna

Wala sihitaji nguvu nyingi kuthibitisha Mungu yupo,
Sababu
1 Existence ya mwanadamu ,
Mimi kama mwanadamu nimetokana na nini ? Huwezi tu ukaja na nadharia za quantum physics kwamba sijui mwili unatokana na particles sijui molecules ,kirahisi tu hizo particles zikatengeneza mfumo wa mwili wa mwanadamu kuanzia kwenye brain mpaka kwenye unyayo ,
Particles au molecules hizo zikachagua kwamba sio lazima viumbe vyote viongee ni mwanadamu tu ila simba hapana ,
Hilo la kujiuliza mimi nimetokana na nini linatosha kabisa kujua kwamba kuna mwenye uwezo zaidi yangu aliyefanya mimi kuwa hapa
 
Usingekua na pua ungejuaje kwamba duara halina harufu au usingekua na macho ungejuaje kwamba mziki hauna rangi ?? Pengine labda kuna kitu cha ziada unatakiwa uwe nacho ndio ujue siri za Mungu ambacho kitu hicho wewe huna

Wala sihitaji nguvu nyingi kuthibitisha Mungu yupo,
Sababu
1 Existance ya mwanadamu ,
Mimi kama mwanadamu nimetokana na nini ? Huwezi tu ukaja na nadharia za quantum physics kwamba sijui mwili unatokana na particles sijui molecules ,kirahisi tu hizo particles zikatengeneza mfumo wa mwili wa mwanadamu kuanzia kwenye brain mpaka kwenye unyayo ,
Particles au molecules hizo zikachagua kwamba sio lazima viumbe vyote viongee ni mwanadamu tu ila simba hapana ,
Hilo la kujiuliza mimi nimetokana na nini linatosha kabisa kujua kwamba kuna mwenye uwezo zaidi yangu aliyefanya mimi kuwa hapa
Hujathibitisha kwamba mtu katokana na mungu, na mungu tu, si kitu kingine chochote.

Na kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba mtu ambaye ana udhaifu mwingi, anahitaji kula na kunya, anaumwa etc wakati alikuwa na uwezo wa kuumba mtu asiyeumwa wala kuhitaji kula na kunya?
 
Hujathibitisha is kwamba mtu katokana na mungu, na mungu tu, si kitu kingine chochote?

Na kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba mtu ambaye ana udhaifu msingi, anahitaji Kula na kujua, anaumba etc wakati alikuwa na uwezo wa kuumba mtu asiyeumwa wala kuhitaji kula na kunya?
Kiranga unarudia maswali ambayo majibu yake nimekuambia huwezi kuyapata popote duniani hilo la Mungu wa upendo kuumba mtu anayehitaji kula na ama asiye umwa hakuna mwanadamu atakaye weza kulijibu ,sawa sijathibitisha ila hilo la existence ya mwanadamu peke yake linatosha kabisa kunifanya niamini kuna aliye juu ya uumbaji wangu na usiniambie nithibitishe imani kwa sababu ni mambo yasiyo onekana ,

Kwa wewe ambaye Mungu hayupo ,mwanadamu ametoka wapi ??
 
Kiranga unarudia maswali ambayo majibu yake nimekuambia huwezi kuyapata popote duniani hilo la Mungu wa upendo kuumba mtu anayehitaji kula na ama asiye umwa hakuna mwanadamu atakaye weza kulijibu ,sawa sijathibitisha ila hilo la existance ya mwanadamu peke yake linatosha kabisa kunifanya niamini kuna aliye juu ya uumbaji wangu na usiniambie nithibitishe imani kwa sababu ni mambo yasiyo onekana ,

Kwa wewe ambaye Mungu hayupo ,mwanadamu ametoka wapi ??

Ukiniambia hujui majibu ya maswali haya, unaniambia humjui huyo mungu.

Unamuamini mungu ambaye humjui.

Na kwa sababu unaamini kitu ambacho hukijui, kuna nafasi kubwa sana unaamini kitu ambacho hakipo. Mungu ambaye hayupo, katungwa tu na watu kama hadithi.

Mimi sijajua mwanadamu katoka wapi, bado nachunguza.Lakini hawezi kuwa kaumbwa na mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote. Maana ana mapungufu mengi sana ambayo kama kweli angekuwa kaumbwa na mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, asingekuwa nayo.

Njia moja ya kutafuta jibu ni "elimination process". Unapewa theory, unaipima, inapita au kutopita mitihani Fulani.

Mathalani, naweza kuwa sijui square root ya 2 ni nini. Lakini najua square root ta 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2.

Mtu akiniambia kwamba square root ya 2 ni 10, nitamwambia kakosea, hilo jibu si sahihi. Hata kama sijui square root ya mbili ni nini. Najua ni lazima itakuwa ndogo kuliko mbili, si kubwa zaidi.

Wewe unachoniambia hapa, logically, ni kama uansema square root ya mbili ni 10. Mimi nakwambia si 10, ni lazima iwe ndogo kuliko 2.

Wewe unaniuliza square root ya mbili ni ipi.

Hata kama siijui, jibu lake haliwezi kuwa 10.

Hata kama sijui mtu katokea vipi, jibu lake si kwamba kaumbwa na mungu wako mjua yote, mwenye upendo wote na muweza yote.
 
Hakuna mungu, huyo unayemsoma ni hadithi tu zimetungwa na watu.

Ukijua hili swali lako halitakutatiza.
Nani mwenye jina mungu?
Kama kuna jina lake basi yupo hatakama ni upepo.
Ningekuelewa kama ungesema huyi mwenye jina hana sifa anazo pewa ila uwepo wake upo na ndomana ww unasema hakuna mungu bila kujua unapotaja jina mungu unatambua uwepo wake.
 
Nani mwenye jina mungu?
Kama kuna jina lake basi yupo hatakama ni upepo.
Ningekuelewa kama ungesema huyi mwenye jina hana sifa anazo pewa ila uwepo wake upo na ndomana ww unasema hakuna mungu bila kujua unapotaja jina mungu unatambua uwepo wake.
Nikiitaja "pembetatu duara" , hilo linamaanisha kuna pembetatu duara?
 
Back
Top Bottom