Je, na Wagombea wengine wa 'Urais' nchini Tanzania nao watakuwa na 'Confidence' kubwa ya Kuongea Kiingereza na Balozi wa US kama alivyoweza Lissu?

GENTAMYCINE mtaalamu wa lugha ya picha.

Mbavu zangu 😂😂🤣🤣🤣
 
Balozi wa marekani wa sasa hivi, ujana wake aliumalizia Zanzibar ambako alijifunza kiswahili fasaha!
Kwa hiyo hawa waswahili (wagombea urais) aongee nao kwa lugha wanayo feel comfortable nayo. Hawa wakina Putin, Rais wa Ufaransa, Chancellor wa Ujerumani, waziri mkuu wa Japan, Rais wa China, wa Korea zote mbili, waziri mkuu wa India, waziri mkuu wa Ethiopia, Rais wa Egypt n. k - wote hao wanajua kiingereza kuliko Lissu, lakini wanapoongea na vyombo vya habari au viongozi wa nje wanatumia lugha zao za taifa.

Ni utumwa na kujiingiza kwenye mitego isiyo kuwa na tija kwako kuongea kwa lugha ya mwenzio. Mfano Lissu aliingia mkenge mahojiano ya HardTalk kwa sababu ya lugha. Kama angekuwa anaulizwa kwa kiswahili asinge vurunda kama ilivyo tokea - nikienda mbali zaidi, na kama angeulizwa kwa Kinyaturu, Lissu ange perform wonders!

Nchi zinazo jielewa wamepiga marufuku kuongea lugha za wenzao kwenye mambo nyeti yahusuyo taifa lao. Elewa hivyo.
 
Law healer, heri ya mjinga kuliko mpumbavu wewe. Do you know the official language of Tanzania?
Yes.I know!
1. Kiswahili.
2. English.

Hata katiba imesemea Mgombea wa Urais Lazima ajue Kiswahili AU kiingereza.

Tatizo ni hili..Kuona Mtu anaezungumza kiingereza ni kiongozi katikati ya waswahili bora kuliko yule anaezungumza kiswahili kwa waswahili.

Uhalisia ni Huu..Watanzania Wengi hawajui kiingereza ndio maaana asilimia kubwa ya shughuli za kila siku zinafanyika kwa Lugha ya kiswahili.

Hii superiority ya ya Lugha ya kiingereza imetoka wapi??
 
English ni lugha ya kibiashara, wajapan, urusi, china, ujerumani, wafaransa wamefanya mambo makubwa bila kutumia kiingereza ila sisi tunadanganywa kuwa kujua kiingereza ni kila kitu
 
kumbe ndio.maana unalipenda hilo.jina kisa ni la kiingereza ,huu sasa utumwa wa kujitolea achana na ule wa kina kinjekitile ,ila hongera
 
Hivi kwa nini tuchukulie kuongea Kiingereza kuwa kigezo muhimu sana kwa rais mtarajiwa wa Tanzania? Yaani unatuambia Watanzania tuchague rais anayeweza kumfurahisha Balozi wa Marekani kwa kuongea Kimombo? Mbona mawazo duni sana haya. Yaani tushushe hadhi ya Mtanzania kiasi hicho? Balozi yuko hapa nchini na ndiye anayepaswa kuongea Kiswahili.
 
Mbona wewe unakuwa mshamba sana na lugha ya kiingereza au hujui kwamba kiingereza ni lugha tu kama kiswahili, kingoni na kindengereko? Umenikumbusha marehemu karume akiwa seaman alifika Liverpool akawaona watoto wadogo wanaongea kiingereza sasa aliporudi Zanzibar akawaambia wazanzibari ninyi wakubwa wazima mnashindwa kuongea kiingereza nilipokuwa Liverpool niliwakuta watoto wadoogo wanaongea kiingereza tena kwa ufasaha
 
Kiongozi kujua kujua kiingereza itatusaidia nini!?
Itatusaidia Kuondoa Upumbavu ( Upopoma ) wako ulionao na wa wale wengi wao ambao 'Wanatetea' hili tatizo lake la Kimsingi linalomgharimu pia.
 
CCM hatutaki mamluki kama ww....
Jijue kama uko upinzani tujue... Nyambafu ww.... Ww umeona ni mgombea gani wa urais hajui kiingereza.... Kuanzia ripumba hadi Magufuli?
Kinachonishangaza tu hapa ni kwamba huu 'Uzi' ninayemlenga hasa ni Mgombea Hashim Spunda Rungwe nashangaa Watu 'wanaweweseka' sana.
 
Tunachohitaji Sasa Ni uwanja sawa wa kampeni na siyo kiingereza
 
Kama lugha zinajenga barabara sasa tuambie, Kiswahili kimeweza kukujengea kilometa ngapi za lami ????
Kuna Watu ( Members ) hapa Jamvini ( JamiiForums ) mna 'Akili / Uwerevu' mkubwa wa Kuchambua na Kujibu 'Hoja' hadi ninawapendeni. Heko!!!!
 
Wewe 'Pimbi' kumbe kuna muda huwa unakuwa na 'Akili' kubwa kweli kweli hadi Kunifanya nikukubali japo kuna nyakati huwa 'tunakwazana' sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…