Je Nadanganywa??? Pls nishaurini..

Je Nadanganywa??? Pls nishaurini..

Jitahidi katika maamuzi yako usije ukamharibia maisha mtoto wako. Kwani atakuja kukulaumu katika maisha yake. Kwani ukitaka kwenda usa kutembea kwa pesa yako kama umesevu huwezi? Fikiria kwa makini dada. Na huyo baba mtoto kuwa naye mbali ukitulia utapata mume wa maana.
 
Dada,fikiria kabla hujaamua kuja, maisha ya bongo nimazuri kuliko unvyofikiri! labda jamaa nimuumini ktk Financial Disciplin, kweli pesa ya hapa utaipata lakini kimatumizi itakwisha haraka tuu, pia ungelikuja umuone na maisha anayoishi maana unaweza fikiri utakapokuwa hapa utakuwa na muda wakuwa nae kama alivyokuwa bongo!!
Dada hapa kila mtu ni mtumwa wa muda!!
Mshukuru sana MUNGU kwa hiyo kazi uliyonayo!! ukizingatia na elimu yako.
 
Pole sana,usiamini kila usikiacho,uonacho na ufikiliavyo,ni heri ukawa katika mazingira magumu nyumbani kuliko ugenini,
 
mimi nashauri usikubali kuolewa na huyio jamaa wa bongo, kwanza kama ni stnd seven atakuwa na fujo mi nawajua hao kwa nin ukubali huyo wa 77777 bana mi napata hasira sana kwani wanaume hawakubali kuwa chini wana inferiorty complex bwana achana na stnd 7 sasa maisha gani ya stndrd 777 bwana, mimi love meter yangu inakataaa kabisa inasoma negative
 
Je huyo jamaa wa USA umeshahika kwao? ni mtu wa wapi hapa TZ?
 
Either or is not an option. Wkti mwingine you need to make a choice and think about your child, child's future and yourself. Jamani any man who plays with your mind and emotions is using emotional abuse na hamna kitu kibaya kama hicho.

The 2 are not worth it. Take it from someone who has seen the same scenario among many sisters. Good life na kuwin maishani ni wewe mwenyewe. Ningekushauri get furthur education...
 
Dada yangu kwanza hongera kwa huo mshahara, maana mimi mwenyewe nina digrii sipati huo mshahara. Kuhusu swala la yeye kushindwa kukusaidia vitu vidogo hapo dada kweli huyo atakuwa msanii kwasababu kama amedhamiria kukuoa lazima akujali na experience inaonyesha kwamba mwanaume anamsaidia zaidi mwanamke kabla ya kumuoa akishaoa anapunguza hata zawadi.

Pia swala la kwenda USA usidanganyike na maisha ya huko watu wanafanya kazi za hovyo sana maisha huko si lelemama. Mimi kusema kweli sijawahienda USA ila sasa hivi nipo BELGIUM nasoma hivyo kulingana na uzoefu wa kuishi huko pamoja na kuelezwa na mabest wangu ambao wanaishi huko. Swala la kusoma ni gharama sana ndio maana watu wengi wanaosoma huko wanakuwa wamepata Scholaship, huyo bwana wako anasema msomi lakini unaweza labda amesoma kozi za kuunga unga not complete kozi kama diploma na Digrii kwasababu ya gharama.Wewe hata kama akikusomesha labda unaweza soma english course.
Kuhusu mtoto kusoma sio gharama kubwa tatizo matibabu USA ni ghali mno kwa wenzetu kuna mambo ya bima ya afya ambayo lazima umlipie mtoto kwahiyo angalia usiende tesa damu ya watu. Lakini hebu mjaribu kwanza akulipie kwanza hapa TZ mwanao aende Babycare Peace of Heaven akiweza basi ujue kweli anakupenda na ataweza kumsomesha mwanao US.:nono:
 
dada 1m ni kubwa sana kwa elimu yako kuanza kupigia magoti mwanaume akusaidie.cha msingi mtembelee kwanza us na pili usiweke tamaa mbele kma alivyosema unalinganisha kwakua umepata wa kumlinganisha nae
 
Wana JF huyo Mdada anahitaji ushauri

Mimi ni msichana wa miaka 29 nina elimu ya form 4 na nikasoma Secretary VETA miaka 2 pamoja na Computer n.k…Nikabahatika kupata kazi kwenye kampuni binafsi mpaka sasa hivi nina miaka 9 katika hiyo kampuni nikapandisha vyeo mbalimbali ila nafanya kwa ujuzi tu hizo kazi na sio kwa vyeti na mshahara wangu sasa hivi ni 1.million pamoja na marupurupu yote (Nimeelezea haya ili niweze pata ushauri unaofaa kwa kulinganisha kipato na hali halisi ninayoishi.) nina uhusiano na kijana mmoja hapa na nikazaa nae mtoto mmoja wa kiume ana miaka 2 sasa..tatizo kijana mwenyewe ni jeuri/dharau/hana upendo kabsaa…na kikubwa zaidi yeye ana elimu ya darasa 7 na hata ufahamu wake ni mdogo yaani kazi anayofanay ni biashara za hapa na pale elimu kwangu sio issue muhimu ni Upendo n.k Japo anaonyesha nia ya kunioa lakin mmmh NIMESHINDWA.

Kwa bahati mbaya/nzuri nikakutana na kijana mwengine mtanzania ambae anaishi Marekani nae amezaa mtoto 1 wa kiume lakin bado hajaoa…..na ana passport ya Marekani (nimetoa hizo detailz ili mtakaponishauri mjue mnaanzia wapi) ..tulikuwa tunachat kwenye mitandao yaani tukawa tunapenda kama vile tumeonana..mpaka mwaka jana alipokuja tz tukaonana na kila mtu akaridhika na mwenzie….kwa kweli nina mpenda sana tu nay eye pia anaonyesha kunipenda…ILA TATIZO NI KWAMBA HATA NIKIWA NA SHIDA HUWA NAIELEZEA KWAKE KAMA STORY YA KAWAIDA TU ILI WALAU ASEME OK NITAKUTUMIA PESA..HASEMI WALA HAJAWAHI NISAIDIA NA NA HATA UKITAMKA PIA ANASEMA HANA…Ila hapa Dar es salaam amejenga nyumba nzuri tu amenipeleka pia kuiona n.k.

Kilichonifanya kuwauliza....ni hili Sasa hivi anataka kunioa ila yeye ni dini nyingine lakin nilipomwambia amesema yuko tayari kubadili kuja kwenye dini yangu…Na anataka anioe na kwenda kuishi marekani na amesema atanitafutia Shule na mtoto pia atasoma n.kk…na yeye pia ni msomi na ana kazi nzuri tu, na ni mpole sana, ana busara, ni mwepesi kuomba msamaha na hapendi nikasirike hicho ndicho nilichogundua kwa miaka 2 niliyomfahamu kwa kuongea na simu na miezi 3 alokuja tz tukawa pamoja.

1. SWALI LANGU NI HILI: JE KAMA HUYU MTU ANA UWEZO WA KUNIPELEKA U.S.A MIMI NA MTOTO NA AKATUSOMESHA SOTE IWEJE SHIDA NDOGO NDOGO TU ZA HAPA ANASHINDWA NITATULIA????? (Japo sehem kubwa ya maisha na mudu mwenyewe lakin kwasabab najenga huwa nakwama hapa na pale kibinadamu)…
2. JE KWA MTAZAMO WENU HASA AMBAO WANAISHI U.S.A KITU KAMA HICHO KINAWEZEKANA KUMUDU MAISHA YA KUMSOMESHA MTU NA MAMA YAKE??

3. NA KAMA HAKUFANYA AKANIDANGANYA JE NITAFANYAJE????? (Naogopa kufanya tamaa kisa nimesikia Nje baadae nikajuta).\

4. Na kama ni kweli…ATATUMIA UTARATIBU UPI WA MIMI NA MTOTO KUISHI PALE BAADA YA VISA HALALI KWISHA??

Niko njia panda naomba mnishauri Matusi na kejeli pia ntapokea…Ila nitashukuru kwa wale wote watakaonipa hali halisi ya maisha ya U.S.A kulingana na story yenyewe…NAKUWA NA WASIWASI SABAB KAMA NITACHEMSHA NA NIKAWA SIJAPATA CHANCE YA KUSOMA NIKIRUDI TZ NAJUA KAZI YANGU SITAIPATA TENA…NATAKA KUJUA KAMA NADANGANYWA AU HIVI VITU VINAFANANA NA UKWELI. NIKO NJIA PANDA....NAHITAJI USHAURI WA UKWELI NIFANYEJE?

unampima mpezi kwa kile anachoweza kukupa?!. Anashindwa kukusaidia shida ndogondogo (financialy) kwahiyo hudhani kama anaupendo wa dhati?, unadhani anazo nyingi kuliko wewe?. Unataka upendo au materials?!. Ukikua utaacha.
 
USA ipi ? usikute ile ya karibu na tengeru arusha .
 
Pole sana .............. dada zetu mnazidi kuwa tegemezi ............. sasa mtu hajakuoa unaaza kumlimbikizia majuku kivipi?
Nimesoma na kuishi Marekani kwa zaidi ya miaka nane. ............Gharama za shule na maisha ni ghali mno. Sisemi kwammba hawezi kukusomesha ila kaa ukitambua kwamba gharama za shule ni ghali. Pia utatakiwa kufanya mitihani ya kiingereza kabla hujapata admission kuingia chuo chochote, so sio hela tu ndio inayohitajika, kichwa pia ......... mshahara ulionao ni mkubwa sana tu ukilinganishwa na elimu yako, kaza buti na ujiendeleze hapohapo bongo masomo ya jioni n.k. ili hata siku ukisimamishwa kazi hapo uwe na vyeti vya kutafutia kazi sehemu zingine.
Shule ya awali na sekondari n i bure marekani, kuna vihela vidogovidogo vya hapa na pale kama stationary, field trips n.k lakini sio school fees. Kikubwa ni health care (bima ya afya, ni ghali na kama huna tiba ianweza kuwa mgogoro) kama jamaa anafanya kazi nzuri anaweza akalipiwa na mwajiri. Kupata kazi pia ni shida sana marekani, usitegemee kupata hiyo kazi yako huku kwa elimu yako ulinayo sasa hivi. Pia kuna ubaguzi sana hata kama una elimu nzuri unaweza usipate kazi kama kuna wazungu unashindana nao kwenye same job sio kama bongo mzungu akienda na wewe anakimbiliwa. Ukiwa mawanafunzi na visa ya uanafunzi hauruhusiwi kufanya kazi tambua hilo ........... sitaki kukukatisha tamaa lakini sio rahisi kama wengi wanavyofikiria.
Pia huku ukitoka na mdada sio lazima umlipie ............ yaani nikwambia twende lunch somewhere sio lazima nikulipie ......... labda kama nimekwambia I am giving you an offer, lakini ya twende lunch sio lazima nikulipie. So, labda jamaa anashangaa unavyoanza kumpangia the ........ to do list .......... any ngoja niachie hapo kwa sasa kama unahitaji ufafanuzi zaidi kuhusu shule nitafute .....
 
ACHA TAMAA YA PESA, eti shida ndogo ndogo nyie wanawake wa bongo ndo maana mnachezewa km tambala bovu, yaani ukipata mwanaume basi unajua shida zako zimekwisha, km jna kazi nzuri mama wewe jibidiishe hapa hapa bongo us hawachukuani km mnaelekea manyovu na reli ga kati.
 
Kwani huyo ex-wife wake yupo wapi?
 
Dah! FORM 4, unapata 1Million, mimi nina PhD sipati hiyo bado unajilengesha kwa wanaume tapeli in the name of USA (labda ya Tengeru). I do not advise. Fetch your own heart as you do it to your heart. Period!
 
mimi kwa ushauri wangu huyo dada aache tamaa za kijinga,kwanza atambue mume wa uhakika ni huo mshahara wake ambao hata mimi mwenye digiri na nipo serikalini silipwi huo mshahara,mwanaume kukutokea mara 1 na kuanza kupiga mizinga ya kijinga kamwe hatakaa na wewe na kama akikuchua ukaishi nae kama mume na mke utanyanyasika sana na mwishowe utamkumbuka huyo wako wa std 7 mara 100,na hapo kama huna kazi ndo imekula kwako. nachomshauri huyo dada aache kuhangaika na wanaume,atulie na huyo aliye nae japo ni mkorofi,ajaribu kutafuta watu wenye busara wamsaidie ktk ushauri jinsi ya kuishi nae kuliko kukimbilia usipokujua.Usa maisha ni magumu sana,kwa m2 wa kawaida matumizi kwa siku sio chini ya us$ 100-150,kwa hapa tz ni pesa nyingi ambayo wewe na family yako unaweza itumia kwa chakula kwa wk2 au zaidi.hapa tz ni ulaya tosha.
 
Pole sana dada yangu... Tumia akili yako na pia moyo wako kudadafua hayo mambo.
Siku hizi wakaka wanaoishi Marekani umekuwa ndo mtindo wa kuwapotezea wadada wa kibongo mda wao.
Unakuta akija likizo ndo anapata nafasi ya kumega kutokana na maisha ya US kuwa magumu sana alafu wengine wanadharauliwa sana na wadada walioko US hasa kutokana na tabia zao. Sasa akitokea kumpata wa kumdanganga ndo hujifanya yeye ndo muoaji kumbe huenda anapoteza muda tu.

Jaribu kujipanga ili uone ni jinsi gani utamwendeleza huyo mtoto wako kabla hujaingia mkenge mwingine na kupata mtoto wa pili.

Kuwa mvumilivu, jiendeleze kimasomo, nawe utampata tu wa ukweli.
 
Acha tamas.acha ndiyo za mchana na usihesabu hela isiyokuwa mfukoni. Ushauri wangu ni kuwa kwa vile una mshshara ambao ni mziri maana maafisa wengi mjini hawapati hivyo maliza taratibu nyumba yako na ujiendeleze kielimu. Usidanganyike maisha yako hapahapa. Nina mifano mingi ya watu wameenda marekani na uingereza na kuishi miaka mingi wamerudi bila kiti na kuanza kusoma ili kujenga au kuanza maisha
 
Nafkiri kwamba sasa inakubidi ,uangalie kwanza maisha ya mtoto wako, pili akuakishie kama kipato chake kinatosheleza mahitaji yenu watu 3 + kuwasomesha ww na mtoto ,na sio akuoe alafu ukawe maza house ,lazima ufanye kazi kama alivyo kukuta ,usije ukajikuta unaondoka peponi na kuelekea motoni,maisha ya ulaya ni magumu asikudanganye mtu,kama anakupenda kweli akuthibitishie
Hilo,asije kuwa drugs dealer kule akutie matatizoni.x
 
Nafkiri kwamba sasa inakubidi ,uangalie kwanza maisha ya mtoto wako, pili akuakishie kama kipato chake kinatosheleza mahitaji yenu watu 3 + kuwasomesha ww na mtoto ,na sio akuoe alafu ukawe maza house ,lazima ufanye kazi kama alivyo kukuta ,usije ukajikuta unaondoka peponi na kuelekea motoni,maisha ya ulaya ni magumu asikudanganye mtu,kama anakupenda kweli akuthibitishie
Hilo,asije kuwa drugs dealer kule akutie matatizoni.x
Ni kweli, if it were me, I would simply take atleast 2 months leave and not quit my job, maisha ya ughaibuni si sawa na bongo, lakini zaidi maisha ya kukaa wawili sio sawa na mlivyokuwa mbalimbali, japokuwa wanawake hatutakiwi kuwa tegemezi, there's no harm in she seeking or expecting some help...its expected of tht man to provide..naomba sana usiache kazi kabla hujatest zali
 
Form 4 ... Amefanya kazi miaka 9... Analipwa Net 1,000,000/= : You must be very lucky!

Achana na mapenzi, jiendelezi kelimu!

Point))) Dada angu nakushauri jiendeleze kielimu hapo hapo Bongo na mwambie msela kama anakupenda then akusaidie uendelee hapo bongo. Sio wote wenye maisha mazuri nje., we jiulize why anashindwa sometimes kukutumia pesa kidogo ukiomba wakati kajenga Bangaloo hapo Bongo? Mi nipo nje n maisha kwa wengine huku ni bora zaidi ya hapo home.
You ar Lucky., 4M4 wth a Salary of tht amount, THINK BIG:smile-big::smile-big:
 
Back
Top Bottom