Je, ndio yamenikuta kwenye banda langu la mpira?

Je, ndio yamenikuta kwenye banda langu la mpira?

chala41

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2024
Posts
300
Reaction score
606
Katika harakati zangu za utafutaji nimejikuta nakodisha banda liliko lipo wazi msimu wa mwaka jana.

Mtaa ninao kaa kulikuwa na mabanda mawili ya mpira ila msimu huu jamaa mmoja hakufungua kabisa.Kupita kuuliza nikaambiwa jamaaa kashindwa kwahiyo anakodisha pale

Mimi huyo na kiranga changu nikalipia miezi kadhaa na nikanunua azam tv nikafunga nilikuwa na TV yangu inchi 43 home nikataka kuichukua wife akakataa akasema km unafungua mpira TV itakuwa huko muda mwingi tununulie hata TV ndogo

Nikamuona kama miyeyusho nikaenda kununua TV used inch 46 nikafunga fresh

Nikaeka vimatangazo vya uongo uongo basi siku ya mpira ikafika ambayo ilikuwa YANGA VS CBE .ila waliingia watu 7 tu nikarudi na 3500 ts.

Siku ikaisha hivyo na nikajipa moyo kuwa kesho ni SIMBA VS ALAHLY TRIPOL naweza nikatusua lakin pia haikuwa hivyo nikapata watu 8 tu

Nikasema hapa mbona km jau matarajio sio kabisa. Kivumbi hiki

Nikajipa moyo tena kwakuwa ni wiki ya kwanza ngoja tuangalie next game ya yanga vs cbe aman complex

La haula hii ndio ikatia fora kabisa mana walikuja watu wawili tu.

Sasa najiuliza ni kuwa ya mabango haikutosha ?? Au TV inchi 46 bado ni ndogo ?? Mana banda la pili ana inchi 43 tu na kule nyomi ila siwez laumu kwa kuwa ana experience ya muda na yule alienikodisha mimi mwanzo alikuwa na TV ndogo ndio maana nikaona kama Alikuwa anafeli

NACHOOMBA WAZOEFU NA HIZI MAMBO MNISHAURI CHA KUFANYA

dogo niliemuachia banda kaniambia tumefungua banda kitoto sana hatujazunguka kwa waganguzi.

Majirani wengine wakasema mwenzenu kashawai kwa wazee porini kwa hiyo nyie msipoangaika mtakuwa mnalipa kodi na kingamuzi hakuna hela mtapata hapo. Hii kauli imetolewa na watu watatu tofauti hapa mtaani

Chakushangaza kabisa ndugu wa mpinzani wetu kutuambia nyie yule hamumjui kama ni mchawi?

Mimi nilichomwambia dogo ni kuwa game ya simba tunaweka promotion watu 5 wa mwanzo wanaingia bure ili kuhuisha brand mana tunapoelekea ntakata tamaa mapema mno.

Wadau mna maoni gani kwenye mabanda ya mpira je kuna nginjanginja hizi za kurogana mwengine asipate wateja.

Mama mimi sijawai kwenda kwa mganga tangia nizaliwe na sina mpango huo nimeamua kama watu hawatakuja hata kwa bure Bora nifunge banda au nikatafute sehemu ambayo haina kurogana lakini sio kwenda kusema TAWIRE mana mganga anapatiaga kwa kupita mule mule na Ramli zao chonganishi.

Ni hayo wadau
 
Usiweke watu watano wa mwanzo,
Weka baadhi ya match bure kabisa,
Tena ikiwezekana hata ya simba au yanga tangaza bure, watu waje waone maboresho uliyofanya, mana mpaka sasa wanajua humo ndani kuna Tv ndogo,

Kuhusu uchawi ni mapema sana kuamini
 
Una ving'amuzi vipi na vipi? Game za EPL kuna mtu anaonesha hapo mtaani kwenu?

1. Tatizo mmeigana biashara. Kila mtu angefanya biashara kivyake bila kuibiana wateja.

Kama yeye amewekeza kwenye Azam wewe jikite EPL na La Liga za DSTV kua mbunifu.

2. Kua mbunifu zaidi, weka free Wi-fi.

PXL_20240922_094129816.jpg

Nunua router ya Airtel Tsh 110,000/= weka wi-fi bure angalau wateja wa miezi ya mwazo.

3. Siku ya kufungua ilibidi ufanye grand opening, mfano unaweka mechi bure weekend nzima.

Sema ndio ushafungua lakini ulitakiwa uanze na offa kubwa sana.

4. Weka PS siku ambazo hakuna mechi chezesha game kwa bei sawa na bure especially game za soccer.
 
Umeshapewa ushauri wa kitaalamu lakini unaupuuza. Biashara siyo lelemama!
Tafuta fundi apaweke sawa hapo ili upate riziki kwa kadiri Mungu alivyokubarikia.
Usitafute fundi aroge wengine ama akuzindike, bali tafuta ambaye atazuia wenzako kukuzunguka.
SIMPLE!
 
Katika harakati zangu za utafutaji nimejikuta nakodisha banda liliko lipo wazi msimu wa mwaka jana.

Mtaa ninao kaa kulikuwa na mabanda mawili ya mpira ila msimu huu jamaa mmoja hakufungua kabisa.Kupita kuuliza nikaambiwa jamaaa kashindwa kwahiyo anakodisha pale

Mimi huyo na kiranga changu nikalipia miezi kadhaa na nikanunua azam tv nikafunga nilikuwa na TV yangu inchi 43 home nikataka kuichukua wife akakataa akasema km unafungua mpira TV itakuwa huko muda mwingi tununulie hata TV ndogo

Nikamuona kama miyeyusho nikaenda kununua TV used inch 46 nikafunga fresh

Nikaeka vimatangazo vya uongo uongo basi siku ya mpira ikafika ambayo ilikuwa YANGA VS CBE .ila waliingia watu 7 tu nikarudi na 3500 ts.
Siku ikaisha hivyo na nikajipa moyo kuwa kesho ni SIMBA VS ALAHLY TRIPOL naweza nikatusua lakin pia haikuwa hivyo nikapata watu 8 tu

Nikasema hapa mbona km jau matarajio sio kabisa. Kivumbi hiki

Nikajipa moyo tena kwakuwa ni wiki ya kwanza ngoja tuangalie next game ya yanga vs cbe aman complex

La haula hii ndio ikatia fora kabisa mana walikuja watu wawili tu.

Sasa najiuliza ni kuwa ya mabango haikutosha ?? Au TV inchi 46 bado ni ndogo ?? Mana banda la pili ana inchi 43 tu na kule nyomi ila siwez laumu kwa kuwa ana experience ya muda na yule alienikodisha mimi mwanzo alikuwa na TV ndogo ndio maana nikaona kama Alikuwa anafeli

NACHOOMBA WAZOEFU NA HIZI MAMBO MNISHAURI CHA KUFANYA

dogo niliemuachia banda kaniambia tumefungua banda kitoto sana hatujazunguka kwa waganguzi.

Majirani wengine wakasema mwenzenu kashawai kwa wazee porini kwa hiyo nyie msipoangaika mtakuwa mnalipa kodi na kingamuzi hakuna hela mtapata hapo. Hii kauli imetolewa na watu watatu tofauti hapa mtaani

Chakushangaza kabisa ndugu wa mpinzani wetu kutuambia nyie yule hamumjui kama ni mchawi?

Mimi nilichomwambia dogo ni kuwa game ya simba tunaweka promotion watu 5 wa mwanzo wanaingia bure ili kuhuisha brand mana tunapoelekea ntakata tamaa mapema mno.

Wadau mna maoni gani kwenye mabanda ya mpira je kuna nginjanginja hizi za kurogana mwengine asipate wateja.

Mama mimi sijawai kwenda kwa mganga tangia nizaliwe na sina mpango huo nimeamua kama watu hawatakuja hata kwa bure Bora nifunge banda au nikatafute sehemu ambayo haina kurogana lakini sio kwenda kusema TAWIRE mana mganga anapatiaga kwa kupita mule mule na Ramli zao chonganishi.

Ni hayo wadau
Ongeza ma dstv uoneshe EPL na viywaji,fen vyote iwepo
 
Hakuna cha uchawi wala Uganga,biashara za aina hiyo zina wateja wa kudumu,mteja siyo tu anaangalia mpira banda moja pia huwa anakaa kiti kile kile eneo lile lile.Huyo mwenzako amewahi wateja wake na wewe tafuta wa kwako.

Nenda kwenye banda la jirani yako angalia mashabiki wachache wenye ushawishi/ maneno mengi washawishi kwa kuwapa posho kidogo na wawe wanaangalia bure.Hao watavuta wateja kutoka banda la jirani,angalia udhaifu wa banda la jirani kama feni,nafasi nk.
 
Una ving'amuzi vipi na vipi? Game za EPL kuna mtu anaonesha hapo mtaani kwenu?

1. Tatizo mmeigana biashara. Kila mtu angefanya biashara kivyake bila kuibiana wateja.

Kama yeye amewekeza kwenye Azam wewe jikite EPL na La Liga za DSTV kua mbunifu.

2. Kua mbunifu zaidi, weka free Wi-fi.

View attachment 3103100
Nunua router ya Airtel Tsh 110,000/= weka wi-fi bure angalau wateja wa miezi ya mwazo.

3. Siku ya kufungua ilibidi ufanye grand opening, mfano unaweka mechi bure weekend nzima.

Sema ndio ushafungua lakini ulitakiwa uanze na offa kubwa sana.

4. Weka PS siku ambazo hakuna mechi chezesha game kwa bei sawa na bure especially game za soccer.
Fuata ushauri huu mkuu mabanda mengi yanayofanya vizuri kwa sasa sehemu zenye ushindani yanaweka Free wifi kwa wateja. Wekeza upande wa Ligi nyingine ifanye ofisi yako iwe busy. Kuna banda moja liko pale geita meno ya mwatulole yule jamaa kawakamata watu haswa anaubunifu mno. Jamaa huwa anatoa hadi kombe kwa wa hudhuriaji bora.

Kwa kuwa ndo unaanza fanya kama vile maduka ya mangi ambayo mtaani yanaweza kuwa matano na kila mmoja anauza.. Toa vizawadi hovyo ili kutengeneza msingi mpya wa wateja wa kudumu. Zingatia Lugha nzuri kwa wateja na iweke kwa hadhi ya tofauti.

Na kwa maelezo yako uliwahi kuwa muhudhuriaji wa kile kibanda kingine kumbuka madhaifu yake na hakikisha unayatendea kazi kikweli kweli. USIKUBALI KUKATA TAMAA MAPEMA. Biashara hii inakutengenezea msingi wa Biashara nyingine mbeleni.

Na jambo la muhimu sana kwa kuwa wewe huamini katika mambo ya gizani(waganga). Hakikisha umewekeza sana upande wa nuruni fanya ibada kweli kwa maana maisha ya mwilini kwa ujumla wake yanaanzia rohoni..

Jambo jingine huyo dogo uliemuweka hapo sio mtu sahihi kabisa kwa kazi yako, kama ni ndugu yako mtafutie issue nyingine, na hapo uweke mtu mwingine(Ukiendelea kumuacha ipo siku utarudi kusoma hapa ukiwa una majonzi sana).

Ahsante
 
Yaani hadi banda umiza watu wanaroga...

Ndio maana kuna muda unajikuta ushafika banda umiza hata hujui umefikaje na umeacha TV maskani...
kule tunafata vibe 🤣,
hakuna uchawi bwa shee,, sema kule ubishi mwingi,, kule kusikia "kmmake" ni kawaida sana,, hapa nnampango mchana niwakimbie family nikachek mnyama😅 + man cty na asenali,,
 
kule tunafata vibe 🤣,
hakuna uchawi bwa shee,, sema kule ubishi mwingi,, kule kusikia "kmmake" ni kawaida sana,, hapa nnampango mchana niwakimbie family nikachek mnyama😅 + man cty na asenali,,

Hahah...

Kuna banda umiza moja hilo tulikuwa tuna majina a.k.a, kuna mtu anaitwa Ferguson, Wenger, Scholes, Viera...

Ukiwa mgeni pale ukamuuliza mtu kwa jina lake halisi unaweza usimpate kabisa...

Banda lina vibe hatari halafu limejengwa kwa mabati tu, chuma kikipigwa yale mabati yanabamizwa mamaeee kama vile parapanda ya kumpokea bwana mawinguni...
 
Hahah...

Kuna banda umiza moja hilo tulikuwa tuna majina a.k.a, kuna mtu anaitwa Ferguson, Wenger, Scholes, Viera...

Ukiwa mgeni pale ukamuuliza mtu kwa jina lake halisi unaweza usimpate kabisa...

Banda lina vibe hatari halafu limejengwa kwa mabati tu, chuma kikipigwa yale mabati yanabamizwa mamaeee kama vile parapanda ya kumpokea bwana mawinguni...
Hii Sasa ndio akili ya mtu mweusi
 
kule tunafata vibe 🤣,
hakuna uchawi bwa shee,, sema kule ubishi mwingi,, kule kusikia "kmmake" ni kawaida sana,, hapa nnampango mchana niwakimbie family nikachek mnyama😅 + man cty na asenali,,
Unatoka nyumbani unaenda kusikiliza matusi na harufu ya ushuzi maana mtu akijamba na mlivyowengi aisee na joto la dar dunia unaiona chungu siji kufanya huo ujinga
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Back
Top Bottom