Je, ndio yamenikuta kwenye banda langu la mpira?

Je, ndio yamenikuta kwenye banda langu la mpira?

Yaani hadi banda umiza watu wanaroga...

Ndio maana kuna muda unajikuta ushafika banda umiza hata hujui umefikaje na umeacha TV maskani...
Naamini ulozi upo ila sijihusishi na ulozi ila kuna cenario imenisikitisha kuna mzee alilipa jero kwetu la mpira wa yanga ila kaenda kuangalia banda la pili. Nimecheka moyoni
 
Una ving'amuzi vipi na vipi? Game za EPL kuna mtu anaonesha hapo mtaani kwenu?

1. Tatizo mmeigana biashara. Kila mtu angefanya biashara kivyake bila kuibiana wateja.

Kama yeye amewekeza kwenye Azam wewe jikite EPL na La Liga za DSTV kua mbunifu.

2. Kua mbunifu zaidi, weka free Wi-fi.

View attachment 3103100
Nunua router ya Airtel Tsh 110,000/= weka wi-fi bure angalau wateja wa miezi ya mwazo.

3. Siku ya kufungua ilibidi ufanye grand opening, mfano unaweka mechi bure weekend nzima.

Sema ndio ushafungua lakini ulitakiwa uanze na offa kubwa sana.

4. Weka PS siku ambazo hakuna mechi chezesha game kwa bei sawa na bure especially game za soccer.
Kwa free WiFi hapa ni uongo labda hiyo ps ndio nina mpango wa mchakato huo.
 
Kumbuka mwenzio alijipa muda mpk amejipata. Mafanikio siyo kulala na kumka ni mipango. TULIZA KICHWA,USIACHE. ILA PIA USIWAAMINI SANA WANAOKUJAZA MANENO.
"dogo niliemuachia banda kaniambia tumefungua banda kitoto sana hatujazunguka kwa waganguzi."
Sure deal. Ila kwa taarifa za kunyapia nyapia jamaa upande wa pili kwanza alitafuta sana kwa watu ni nani anataka kufungua mpira pale kwenye lile banda. Hizo habar nimeletewa home .Oya ww anauliziwa huko ww kaa tu kizembe zembe nikawaambia huyo kuniroga mimi kama mimi hawezi labda aroge banda lile watu wasije.
 
Fuata ushauri huu mkuu mabanda mengi yanayofanya vizuri kwa sasa sehemu zenye ushindani yanaweka Free wifi kwa wateja. Wekeza upande wa Ligi nyingine ifanye ofisi yako iwe busy. Kuna banda moja liko pale geita meno ya mwatulole yule jamaa kawakamata watu haswa anaubunifu mno. Jamaa huwa anatoa hadi kombe kwa wa hudhuriaji bora.

Kwa kuwa ndo unaanza fanya kama vile maduka ya mangi ambayo mtaani yanaweza kuwa matano na kila mmoja anauza.. Toa vizawadi hovyo ili kutengeneza msingi mpya wa wateja wa kudumu. Zingatia Lugha nzuri kwa wateja na iweke kwa hadhi ya tofauti.

Na kwa maelezo yako uliwahi kuwa muhudhuriaji wa kile kibanda kingine kumbuka madhaifu yake na hakikisha unayatendea kazi kikweli kweli. USIKUBALI KUKATA TAMAA MAPEMA. Biashara hii inakutengenezea msingi wa Biashara nyingine mbeleni.

Na jambo la muhimu sana kwa kuwa wewe huamini katika mambo ya gizani(waganga). Hakikisha umewekeza sana upande wa nuruni fanya ibada kweli kwa maana maisha ya mwilini kwa ujumla wake yanaanzia rohoni..

Jambo jingine huyo dogo uliemuweka hapo sio mtu sahihi kabisa kwa kazi yako, kama ni ndugu yako mtafutie issue nyingine, na hapo uweke mtu mwingine(Ukiendelea kumuacha ipo siku utarudi kusoma hapa ukiwa una majonzi sana).

Ahsante
mwatulole 👍,
alafu pale mjini kati mitaa ya american chips
 
Katika harakati zangu za utafutaji nimejikuta nakodisha banda liliko lipo wazi msimu wa mwaka jana.

Mtaa ninao kaa kulikuwa na mabanda mawili ya mpira ila msimu huu jamaa mmoja hakufungua kabisa.Kupita kuuliza nikaambiwa jamaaa kashindwa kwahiyo anakodisha pale

Mimi huyo na kiranga changu nikalipia miezi kadhaa na nikanunua azam tv nikafunga nilikuwa na TV yangu inchi 43 home nikataka kuichukua wife akakataa akasema km unafungua mpira TV itakuwa huko muda mwingi tununulie hata TV ndogo

Nikamuona kama miyeyusho nikaenda kununua TV used inch 46 nikafunga fresh

Nikaeka vimatangazo vya uongo uongo basi siku ya mpira ikafika ambayo ilikuwa YANGA VS CBE .ila waliingia watu 7 tu nikarudi na 3500 ts.
Siku ikaisha hivyo na nikajipa moyo kuwa kesho ni SIMBA VS ALAHLY TRIPOL naweza nikatusua lakin pia haikuwa hivyo nikapata watu 8 tu

Nikasema hapa mbona km jau matarajio sio kabisa. Kivumbi hiki

Nikajipa moyo tena kwakuwa ni wiki ya kwanza ngoja tuangalie next game ya yanga vs cbe aman complex

La haula hii ndio ikatia fora kabisa mana walikuja watu wawili tu.

Sasa najiuliza ni kuwa ya mabango haikutosha ?? Au TV inchi 46 bado ni ndogo ?? Mana banda la pili ana inchi 43 tu na kule nyomi ila siwez laumu kwa kuwa ana experience ya muda na yule alienikodisha mimi mwanzo alikuwa na TV ndogo ndio maana nikaona kama Alikuwa anafeli

NACHOOMBA WAZOEFU NA HIZI MAMBO MNISHAURI CHA KUFANYA

dogo niliemuachia banda kaniambia tumefungua banda kitoto sana hatujazunguka kwa waganguzi.

Majirani wengine wakasema mwenzenu kashawai kwa wazee porini kwa hiyo nyie msipoangaika mtakuwa mnalipa kodi na kingamuzi hakuna hela mtapata hapo. Hii kauli imetolewa na watu watatu tofauti hapa mtaani

Chakushangaza kabisa ndugu wa mpinzani wetu kutuambia nyie yule hamumjui kama ni mchawi?

Mimi nilichomwambia dogo ni kuwa game ya simba tunaweka promotion watu 5 wa mwanzo wanaingia bure ili kuhuisha brand mana tunapoelekea ntakata tamaa mapema mno.

Wadau mna maoni gani kwenye mabanda ya mpira je kuna nginjanginja hizi za kurogana mwengine asipate wateja.

Mama mimi sijawai kwenda kwa mganga tangia nizaliwe na sina mpango huo nimeamua kama watu hawatakuja hata kwa bure Bora nifunge banda au nikatafute sehemu ambayo haina kurogana lakini sio kwenda kusema TAWIRE mana mganga anapatiaga kwa kupita mule mule na Ramli zao chonganishi.
Kufupi hapo hakuna biashara ndg yangu, utazidi kujipa hasara tu ndo maana wenzio walifunga

Biashara hii naijua vizuri changamoto yake
 
Hahah...

Kuna banda umiza moja hilo tulikuwa tuna majina a.k.a, kuna mtu anaitwa Ferguson, Wenger, Scholes, Viera...

Ukiwa mgeni pale ukamuuliza mtu kwa jina lake halisi unaweza usimpate kabisa...

Banda lina vibe hatari halafu limejengwa kwa mabati tu, chuma kikipigwa yale mabati yanabamizwa mamaeee kama vile parapanda ya kumpokea bwana mawinguni...
hatar sana,, 🤣🤣
 
Kwani hujawahi kuona bar mbili ziko karibu moja inajaa nyingine haijai?
Huyo mwenzio ana wateja wake. Sasa na wewe tafuta wateja wako au mnyang'anye wateja kwa kuwa na kitu bora zaidi sio utopolo ule ule.
🙏🙏
 
Yani mtu unafungua BIASHARA leo kesho unataka umkute mtu mwenye miaka mi-tano kwenye game
 
Katika harakati zangu za utafutaji nimejikuta nakodisha banda liliko lipo wazi msimu wa mwaka jana.

Mtaa ninao kaa kulikuwa na mabanda mawili ya mpira ila msimu huu jamaa mmoja hakufungua kabisa.Kupita kuuliza nikaambiwa jamaaa kashindwa kwahiyo anakodisha pale

Mimi huyo na kiranga changu nikalipia miezi kadhaa na nikanunua azam tv nikafunga nilikuwa na TV yangu inchi 43 home nikataka kuichukua wife akakataa akasema km unafungua mpira TV itakuwa huko muda mwingi tununulie hata TV ndogo

Nikamuona kama miyeyusho nikaenda kununua TV used inch 46 nikafunga fresh

Nikaeka vimatangazo vya uongo uongo basi siku ya mpira ikafika ambayo ilikuwa YANGA VS CBE .ila waliingia watu 7 tu nikarudi na 3500 ts.
Siku ikaisha hivyo na nikajipa moyo kuwa kesho ni SIMBA VS ALAHLY TRIPOL naweza nikatusua lakin pia haikuwa hivyo nikapata watu 8 tu

Nikasema hapa mbona km jau matarajio sio kabisa. Kivumbi hiki

Nikajipa moyo tena kwakuwa ni wiki ya kwanza ngoja tuangalie next game ya yanga vs cbe aman complex

La haula hii ndio ikatia fora kabisa mana walikuja watu wawili tu.

Sasa najiuliza ni kuwa ya mabango haikutosha ?? Au TV inchi 46 bado ni ndogo ?? Mana banda la pili ana inchi 43 tu na kule nyomi ila siwez laumu kwa kuwa ana experience ya muda na yule alienikodisha mimi mwanzo alikuwa na TV ndogo ndio maana nikaona kama Alikuwa anafeli

NACHOOMBA WAZOEFU NA HIZI MAMBO MNISHAURI CHA KUFANYA

dogo niliemuachia banda kaniambia tumefungua banda kitoto sana hatujazunguka kwa waganguzi.

Majirani wengine wakasema mwenzenu kashawai kwa wazee porini kwa hiyo nyie msipoangaika mtakuwa mnalipa kodi na kingamuzi hakuna hela mtapata hapo. Hii kauli imetolewa na watu watatu tofauti hapa mtaani

Chakushangaza kabisa ndugu wa mpinzani wetu kutuambia nyie yule hamumjui kama ni mchawi?

Mimi nilichomwambia dogo ni kuwa game ya simba tunaweka promotion watu 5 wa mwanzo wanaingia bure ili kuhuisha brand mana tunapoelekea ntakata tamaa mapema mno.

Wadau mna maoni gani kwenye mabanda ya mpira je kuna nginjanginja hizi za kurogana mwengine asipate wateja.

Mama mimi sijawai kwenda kwa mganga tangia nizaliwe na sina mpango huo nimeamua kama watu hawatakuja hata kwa bure Bora nifunge banda au nikatafute sehemu ambayo haina kurogana lakini sio kwenda kusema TAWIRE mana mganga anapatiaga kwa kupita mule mule na Ramli zao chonganishi.

Ni hayo wadau
Wenzako wanafanya hivi, mwanzoni wanakuwa wanatoa ofa, kama ilivyo wabongo wanaingia kwa wingi halafu anachota mchanga anaenda kupiga pini, akianza kutoza hela tayari wale waliopigwa pini hawahami zaidi wataongezeka wapya!
 
Ushauri mzuri wengi wamekupatia, mie naongezea kidogo hapa usiwe serious sana mkuu kiasi kwamba unachojua wewe ni kuchezesha mkono wenye ela kuomba kiingilio, wakati mwingine unakuwa ni mtu wa story za soka za hapa na pale. Ikiwezekana ujulikane unashabikia timu gani ili watani wako wawe wanakuja kukuzongazonga kama utafungwa. Unajifanya kutoa offa hata krate la soda siku moja Kwa moja (unapiga mkwara yenu ikishinda Leo natoa soda)
 
Sure deal. Ila kwa taarifa za kunyapia nyapia jamaa upande wa pili kwanza alitafuta sana kwa watu ni nani anataka kufungua mpira pale kwenye lile banda. Hizo habar nimeletewa home .Oya ww anauliziwa huko ww kaa tu kizembe zembe nikawaambia huyo kuniroga mimi kama mimi hawezi labda aroge banda lile watu wasije.
nikawaambia huyo kuniroga mimi kama mimi hawezi labda aroge banda lile watu wasije.
Nakufungulia codes unazo-fail. Biashara na ww ni kit ki1...vita ya kiuchumi hii boss wangu. AMKA....
 
Hakuna cha uchawi wala Uganga,biashara za aina hiyo zina wateja wa kudumu,mteja siyo tu anaangalia mpira banda moja pia huwa anakaa kiti kile kile eneo lile lile.Huyo mwenzako amewahi wateja wake na wewe tafuta wa kwako.

Nenda kwenye banda la jirani yako angalia mashabiki wachache wenye ushawishi/ maneno mengi washawishi kwa kuwapa posho kidogo na wawe wanaangalia bure.Hao watavuta wateja kutoka banda la jirani,angalia udhaifu wa banda la jirani kama feni,nafasi nk.
Haujawahi kufanya biashara yeyote ile ndio maana umetoa ushauri wa kipuuzi
 
Yani mtu unafungua BIASHARA leo kesho unataka umkute mtu mwenye miaka mi-tano kwenye game
Hiyo ipo sana sema ndio hivyo vitoto vya humu kila kitu munakijua sijui ni nani kakudanganya eti mteja anakuwa wa kudumu....mteja anapenda sehemu mpya
 
Una ving'amuzi vipi na vipi? Game za EPL kuna mtu anaonesha hapo mtaani kwenu?

1. Tatizo mmeigana biashara. Kila mtu angefanya biashara kivyake bila kuibiana wateja.

Kama yeye amewekeza kwenye Azam wewe jikite EPL na La Liga za DSTV kua mbunifu.

2. Kua mbunifu zaidi, weka free Wi-fi.

View attachment 3103100
Nunua router ya Airtel Tsh 110,000/= weka wi-fi bure angalau wateja wa miezi ya mwazo.

3. Siku ya kufungua ilibidi ufanye grand opening, mfano unaweka mechi bure weekend nzima.

Sema ndio ushafungua lakini ulitakiwa uanze na offa kubwa sana.

4. Weka PS siku ambazo hakuna mechi chezesha game kwa bei sawa na bure especially game za soccer.
Mganga huyu hapa kamaliza Kila kitu bila hata tunguli
 
Bro kwa kifupi bongo hakuna mfanyabiashara ambae harogi..jiongeze
 
Back
Top Bottom