Je, Ndugai ataenda Msibani kwa Malecela?

East African

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2013
Posts
704
Reaction score
993
Ndg poleni na Msiba mkubwa wa Mwele ambaye ni mtoto wa Mzee Malecela.

Yapata mwezi mmoja sasa Ndugai hajajitokeza hadharani tangu ajiuzulu Uspika. Hata vikao vya binge hajaonekana.

Sasa swali la msingi ni Je atakuja kwenye Msiba wa ndg yake Malecela ambaye wote ni wenyeji wa Dodoma?

Acha tuone.
 
Nadhani ataenda kwa sababu yeye na malecela wamekuwa viongozi wa juu katika taifa letu na ni watu wanaofahamiana na si lazima wawe marafiki, hili la kwenda sababu wote wanatoka mkoa wa Dodoma hapa unaongelea ukabila Sasa. Na kama sababu ni ukabila Basi mwenyeji yeyote wa Dodoma ambaye hataenda mtaje ajadiliwe humu.
 
Kwani LAZIMA kwenda msibani ???!
 
Hivi kwa nini watu wa Dodoma wakipewa nafasi kubwa za uongozi huwa wanaboronga? Rejea ya Malechela na Ndugai.
 
Hakuna watu wanapitia wakati mgumu ktk nchi hii kama Ndugai, Bashiru, Makonda na Polepole.
Wala usiwahurumie wala kuwasikitikia kwani wamejitafutia wenyewe.

Uwasikitikie wale wote wenye Madaraka Kwa sasa kisha wakayatenda Sawa Sawa na walivyotenda kina Ndugai na kundi lake. Hawa watu ndiyo chimbuko la kina Kingai na wenzie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…