Je, ni adhabu gani uliyoifanya shuleni ambayo hutoisahau?

Je, ni adhabu gani uliyoifanya shuleni ambayo hutoisahau?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Nimesoma Uzi wa member mmoja humu kuhusu adhabu za matofali wapewazo wanafunzi nikakumbuka miaka nikiwa nasoma.

Shule bila adhabu inakuwa ya kiduwanzi kichizi. Yaani inakuwa ya kimama. Raha ya shule iwe na hekaheka bhana! Yaani shule Kama ipo na Kuku WA broiler.

Shule gani haina Wezi
Shule gani haina matukio ya Mapenzi,
Shule gani haina matukio ya ubabe,
Shule gani haina mabifu ya kimapenzi baina ya waalimu na wanafunzi 😀😀.
Shule gani haina wanafunzi wavuta bangi, hiyo ni shule au utopolo.
Shule gani haina Watoro waliobobea,
Shule gani ambayo muhula unaisha hakuna hata mwanafunzi aliyepewa Suspension. Hiyo sio shule.

Shule gani haina walozi au wapenda kwenda Kwa waganga,
Shule gani hiyo isiyo na manabii na walokole pamoja na Maostadhi wenye misimamo mikali. Hiyo sio shule.

Kila Mwanafunzi akiwa shuleni anakuwa na kitengo chake kulingana na nature yake.

Adhabu za kikulungwa ambazo zinabamba ambazo Taikon ninazielewa ni hizi;
1. Kupiga matofali
2. Kuchimba visiki
3. Kuchimba mawe kwenye Shamba la shule lililopo Mlimani. Hii adhabu ndio nyoko kuliko zote hapo juu ikifuatiwa na yakuchimba kisiki.
4. Kupasua vigogo/Juni
5. Kuchimba mashimo

Adhabu laini laini;
1. Kuchapwa
2. Kufagia au kudeki Darasa/ofisi/bweni
3. Kudeki chooni
4. Kumwagilia Bustani
5. Kuokota karatasi au kuzoa taka
6. Kumwagilia Bustani.

Adhabu ambazo niliwa kuzifanya na makosa yake.
1. Kupiga tofali 200 kutokana na kuiba chakula cha waalimu na kukila chote😀😀.
Tulikuwa wanafunzi watatu tuliokamilisha Jambo Hilo.
Alafu baada ya Kula tukawaandamanisha wanafunzi wasile Makande kwani wamepikiwa Wiki nzima. Muda huo Sisi tumeshashiba,
Tulimshawishi Headboy na kumchochea akafanya hivyo bila kujua Sisi tuna agenda yetu ya Siri. Hiyo ilikuwa Kidato cha nne.

Baadaye Sisi tulichapwa viboko sita mbele ya shule na adhabu ya kupiga tofali kila mmoja 200 na viongozi akiwepo kiranja wakapwa suspension na wakija waje na tofali 200.

2. Kuchimba visiki Kwa kosa la Kusababisha Fujo kwenye mchezo wa mpira baina shule yetu na shule ya jirani iloyokuja kucheza pale shuleni.
Tulipewa Visiki viwili viwili.
Hii adhabu sio nzuri😀😀 ni Kama Ile adhabu ya kuondoa mawe kwenye Shamba la shule.

3. Kutoa Mawe kwenye Shamba la shule Kwa kosa la kutokomea siku ya Outing Day. Shule yetu kila jumapili ya mwisho wa mwezi ilikuwa siku ya kutoka kwenda kuzurura bila haya ya kuomba ruhusa Kwa sharti la kuwahi Kurudi kabla ya saa 12jioni.

Tukaondoka kutoka Matema Beach Mpaka Mbeya Mjini. Tukakaa huko tukarudi kesho yake jioni😊😊. Bakora kisha adhabu ya kuchimba nawe.

Nilipewa jiwe Moja, ambalo Kwa juu nililiona dogo kumbe limeenda chini. Mbona nilimenyeka. Hapo ilikuwa chini ya Safu ya mlima Livingstone.

Adhabu zingine zilikuwa za kawaida Ila hizo hapo sio mchezo. Unamenyeka Haswa.

Je, ni adhabu gani uliyoifanya shuleni ambayo hautaisahau?

Wasalamu!

Kwa sasa Dar es salaam
 
Kupigwa fimbo zisizo na Idadi mbele ya darasa huku nimelazwa kwenye dawati wanafunzi wengine wakinishika miguu wengine wakizuia movement upande wa kichwa nikawa siwezi kujitikisa baada ya hapo nikaambiwa nipitie mtu mmoja baada ya mwengine nikiamkia darasa zima.

Nilitokwa na malengelenge kwenye makalio kama nimebabuka na moto na sikuweza kukaa vizuri kwa muda wa wiki Moja.
 
Wakati tunamaliza kufanya mock ya mkoa form 4 tulianza kupiga mayowe tukifurahi kuwa tumebakiza shuhuli mbili nazo ni Graduation na Necta ambayo ni final

Sasa zile kelele ziliwaboa sana maticha maana zilikuwa zimeambatana na vurugu wengine wakiangusha mabenchi nk.

Maticha wakashuka Class kuja kututuliza darasa letu likuwa jirani na ofisi ya walimu, tulivyowaona wameshika bakora wanakuja tukawa tunawazomea

Walipolikaribia darasa letu wanaume wote back benchers na mademu kadhaa wale watukutu tuliruka madirisha tukasepa.

Tukawa tunarudi home, njiani kuna mwana akatoa wazo kuwa tuzibe njia, wazo lake likaungwa mkono.

Tukaenda kukata miti ya miba tukaziba njia zote afu si tukaamsha ma home.

Hiyo ilikuwa ni ijumaa, juma tatu wote hatukutokea skonga, kunaye mchizi wetu mmoja ye faza yake alikuwa ni diwani so alikuwa mkali kwa mtoto wake.

Ikawa inamlazimu jamaa kila siku asubuhi anavaa uniform za shule halafu anaibukia gheto tunalala mpaka saa 4, ikifika saa 5 tubaibukia kwa mwanetu mmoja aliachiwa nyumba na Kaka yake ambaye alikuwa mwalimu, kaka yake alienda kusoma

Huyo jamaa aliachiwa yale makuku ma broiler ayafuge maana walikuwa wanauza mayai so walitaka aendeleze kufuga ili pesa imsaidie kwenye shida ndogo ndogo.

Kufupisha stori

Ni kwamba kile kitendo cha sisi kuziba njia kiliwaumiza sana maticha, wakafikiri tutawapataje hawa na kwa saizi hata shuleni hawaji kwasabbu wanasubiria Graduation na Necta ambapo ni ngumu kutuadhibu

Wakatangaza kuwa kutakuwa na mtihani wa Pre Necta kwa lengo la kutukamata wakijua kivyovyote tu lazima tuje.

Pre necta ikaanza lakini sisi hatukuingia darasani tulikaa chimbo flani tunakula matoo, tukiwa huko tukawa tunaangalia barabarani nikashangaa kumuona mzazi wa rafiki yangu anaelekea shuleni

Jamaa alimkataa akasema yule sio baba yangu kwanza hawezi vaa kishamba vile, yule faza kafika mpaka shuleni walimu wanamuambia ingia humo darasani mtafute mwanao, mzazi haamini macho yake mtoto hayupo na asubuhi amemuona akija shuleni.

Baada ya wanafunzi kutoka kwenye mtihani ikawa kila tunayekutana naye anasema Daah wanetu mnabonge la msala, kwanza dingi yako kaingia mpaka class kakusachi kila pembe hajakuona"

Mwana alivyosikia hivyo ikabidi home asitokee, akaja kwangu nikamuambia hili jambo tulimaliza kiume we tulia.

Kesho yake nikasema twende tuibuke skonga, tulivyofika wakatupa adhabu ya kujaza kifusi kwenye msingi, ilikuwa ni maabara ya kisasa ndio inajengwa basi ule msingi ulikuwa mrefu.

Watu waliokuwa wanakutukubali walikuja kutupa kampani tukajaza lakini hatukumaliza tukaacha na maticha hawakufatilia ikaisha ikiw hivyo.
 
Hii sikupewa shule manake ningetimuliwa

Baada ya kutoroka shule na kwenda kununua Malaya wakati tunarud na mskaji wangu tukadakwa na sungusungu wa hapo kijijini wakidhani ni wezi baada ya kuibiwa nguruwe wa mwananchi kijijini hapo Jana yake Aloooo sungu sungu na mgambo sio watu wale wallai.....walitaka kututoa roho kilichotuokoa ni ID zetu za shule
 
Nakumbuka nilikamatwa na series ya makosa sasa bana yule headmaster akantangazaga assembly makosa yangu na kila kosa lilkua kama linakifungu chake cha adhabu[emoji23][emoji23].

Mwisho wa siku nikakutwa na bandle la kama fimbo 250 ivi, daah yule hmaster kuona vile akanpanga kwamba kwa fimbo hizi dogo hutotoboa nkikuchapa kwa mda mmoja, kwaio kila siku utakua unakuja ofisini kama dozi unapokea kiasi cha fimbo au ataniasign kwa mwalimu yeyote anchape kama yeye atakua katingwa na majukumu mengine[emoji23].

Kwaio kila nkipokea kipondo natia sign kwa leo nmepokea dozi fimbo ngapi.. dah ule mwezi haukua mzuri kwangu aisee.

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
 
Nakumbuka nilikamatwa na series ya makosa sasa bana yule headmaster akantangazaga assembly makosa yangu na kila kosa lilkua kama linakifungu chake cha adhabu[emoji23][emoji23].

Mwisho wa siku nikakutwa na bandle la kama fimbo 250 ivi, daah yule hmaster kuona vile akanpanga kwamba kwa fimbo hizi dogo hutotoboa nkikuchapa kwa mda mmoja, kwaio kila siku utakua unakuja ofisini kama dozi unapokea kiasi cha fimbo au ataniasign kwa mwalimu yeyote anchape kama yeye atakua katingwa na majukumu mengine[emoji23].

Kwaio kila nkipokea kipondo natia sign kwa leo nmepokea dozi fimbo ngapi.. dah ule mwezi haukua mzuri kwangu aisee.

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app


😂😂😂😂
 
Mie nilikuwa mtoro sugu.... nilikuwa siendi shule hata mwezi mzima lakini walimu na wanafunzi wenzangu wananiona Kariakoo kwenye mishe zangu. Na bado baadhi ya walimu nilikuwa nawakopesha pesa sasa wakakosa la kunifanya.

Sasa kuna siku nimeenda zangu shule baada ya utoro wa karibia miezi miwili, nimefika class kama kawaida mara anaingia mwalimu mpya wa Physics(Mpya sababu sikuwahi kumuona).

Anadai aliacha notes na anakagua ambao hawajaandika. Kufika kwangu anaona sura ngeni. Ikabidi aniulize wewe umehamia hapa?

Darasa zima likaangua kicheko.[emoji23][emoji23][emoji23] ikabidi awaulize mbona mnacheka, wakamjibu huyo sio mgeni. Yule ticha kwa unoko akaenda kuchukua attendance ili atizame mahudhurio yangu.[emoji23][emoji23][emoji23]

Bwana wee si akaona nina muda mrefu sijafika shule. Akasema nimfate mpaka ofisini, na bahat nzuri nikamkuta yeye na mwalimu mwingne mgeni wakawa wananiuliza maswali ya kejeli. Na mie nikawa nawajibu kwa dharau.

Si waka-panick wakaamua wafunge mlango kwa ndani ili wanipige. [emoji23][emoji23][emoji23]
Asee niliwagezia kibano niliwabonda hadi wakaanza kupiga kelele za kuomba msaada.

Yani hadi kuja kufunguliwa na ufunguo wa akiba huko nje walimkuta mmoja ameshavimba manundu na mwingne yupo chini ana bleed puani. [emoji23][emoji23][emoji23]

Ila daaah... baadae yake ilipigwa kengele ya emergency na kupelekewa assemble then kupigwa fimbo 6 na kupewa suspension ya mwezi mzima. Na mzazi wangu akaitwa.

Mtaniwia radhi kwa uandishi wangu mbaya.
 
kuchimba kisiki baada ya kufeli mtihaninwa Mock form 4. Sikuchimba hadi ninamaliza

Kupalilia migomba ya shule kisa kuna simu iliita darasani sehemu niliyokaa nikagoma kumtaja mwenye simu. Simu ikarushwa kwa mtu upasnde mwingine mwalimu akapiga msako pale tulipokaa akaikosa. Akatupa adhabu ya kupalilia migomba

Adhabu ya tofali mia mbili kidato cha 5. Chanzo kuingia na chakula bwenini. Ilikuwa ni karibu na likizo ya December. Sikuifanya hiyo adhabu nilivyoenda likizo nikahama shule
 
Kwenye shamba la shule walimu wakawa wanatafuta namna ya kuwapata walimaji, ikawa kila ticha anatoa test ngumu na watao feli wanaenda kulima.

Kweli vichwa vibovu hizo adhabu zikatuandama mpaka tukazizoea, ikafika muda wa kupanda mazao

Wakatupa mahindi yaliyosindikwa tulivyofika shambani tukayapika bisi tukala.

Tukarudi shuleni walimu wakauliza tayari mmepanda tukasema ndio afu tupeni na karanga maana ile ardhi inaonekana ina rutuba sana kwa zao la karanga

Walimu wakagoma kutupa karanga, baada ya wiki kadhaa wakawa wanajiukiza mbona hatuoni hata tuta moja lenye kuchomoza kimwindi.

Wakaitwa scout kufanya upelelezi, walipofuka mwisho wa shamba upande wa pori wakakuta kuna masalia ya maindi yaliyopikwa bisi kule tunaita "kandunya"

Haraka haraka ikabidi zoezi la upandaji liamze upya likiwa linasimamiwa na Scout wenyewe na walipomaliza kupanda wakapiga marufuku kupitabile njia ambayo ipo jirani na shamba.

Baada ya muda wa mazao kukomaa kufika, tukasema haiwezekani tulime halafu kula tusile.

Tukapanga ratiba ya kwenda shambani kwanza tukafika huko tukaanza kucheza na "migagi" kuna mwana ye alikuwa amepanga tukawa tunamuona akikomaa na mboga za maboga

Tukafika chimbo tukachoma yale mahindi tukala kesho yake assemble wakatangaza kuwa walioiba mazao shambani tumewaona ila tunataka wajilete wenyewe kabla ya sisi kuwafata, hatukutokea na hakuna aliyaletufata
 
Wakuu kama kuna mtu anaifaham KIZUKA Atanishuhudia...
KOSA..NILIKUTWA NA PULI LA GANGA KWENYE SOCKS ASSMBLE.(zilikua kama stick 72)
1.NILILIMA NUSU HEKA KWA MKONO.
2.NILICHIMBA SHIMO FT 8.
3.WAKANIBUZA FIMBO 82-96.
Then nichague Suspnsn ya miezi 6 AU kusafisha mabanda ya nguruwe na kuziogesha miez 6...
NB:NLICHAGUA KUOGESHA NGURUWE.
 
Nilipalilia mistari 15 ya mahindi usawa wa ekari. Mahindi yalipokomaa nikageuza kama shamba langu nilikuwa naenda kuchuma mchana kweupe mahindi ya kande na ya kuchoma.

Adhabu nyingine ya kung'oa kisiki ambacho labda greda lije. Nilipiga siku nne nikaona kisiki hakina dalili ya kutoka. Na ukizingatia usipomaliza huingii darasani.
 
Stress za walimu wa zamani ziliongeza ukali wa adhabu acha waendelee kuminywa na mama tozo,
 
Dah! Kipigo kama hicho nilikipataga nikiwa Form One Kantalamba sema mimi ilikua Smart Area,nilichezea bakora zisizo na idadi kutoka kwa Headmaster huku mabroo wa advance wakiwa wamenishikilia chini kama wanachinja Ng'ombe mpaka fimbo ikachakaaa
Jina la shule 'Kantalamba' limenikumbusha mbali headmaster wetu shule moja Advance dar alikuwa anapenda kutumia kudhihaki wageni wanaohamia ambao wengi ndio walikuwa watu wa matukio mara nyingi ilikuwa utamsikia "mtu ametoka Kantalamba ameshindikana anakuja kumalizia uhuni wake huku" ukawa ndio msamiati wa wageni wanaitwa wakantalamba.
 
Kuchimba shimo ***** ardhi semi desert ni ngumu balaa ilibidi nimwagie maji ya kutosha hilo eneo
 
Back
Top Bottom