Je, ni kweli Hayati Magufuli alihusika katika kuandaa kesi ya ugaidi ya Mbowe? Ilikuwa kwa lengo lipi?

Je, ni kweli Hayati Magufuli alihusika katika kuandaa kesi ya ugaidi ya Mbowe? Ilikuwa kwa lengo lipi?

Baada ya uchaguzi wa 2020, Mwendazake alidhamiria kuiangamiza CDM kabisa. Baada ya mbinu ya kununua wapinzani kuto kuleta matunda yaliyotarajiwa...na ugumu alioupata kwenye campaign za 2020 na kwa jinsi Lissu alivyo mkalia kooni na kumpelekesha kwenye campaign dhamira yake ilikuwa kumaliza game kwa kuua yeyote ambaye alionekana hatari au kuwafungilia kesi za ugaidi ili waozee gerezani.

Utakumbuka pia Mwendazake alitaka kubadili katiba ili agombee tena 2025...hivyo alikuwa hataki kabisa kelele wakati wa mchakato wa mabadiliko ya katiba.
Unaweza kutoa udhibitisho hata wa kimazingira juu ya hicho unachokisema?, au na wewe ni wale wale tu maroboti?
 
Embu mwacheni mzee wa watu hapumzike
Huyo mzee wako hata pumzika hadi kizazi hiki cha waliomshuhudia akiwa kiongozi kiishe.
Alijisahau sana yule jamaa, na ni ujinga ambao mtu mwingine hapaswi kurudia kuufanya.
Cheo ni dhamana ambayo unapewa na watu, badala ya kuwashukuru na kutenda yakupasayo kwa moyo wako wote hasa ukizingatia kuwa cheo hicho kitakufanya wewe na familia yako muishi kwa raha wewe unawageuzia kibao watu hao na kuwapa mateso na vifo?
Ashukuru sana corona ilimchukua hapo ndio pona yake, lakini watu kama yeye wengi wanaishia kama Samwel Doe.
 
Sijui wale police walioshirikiana na jamaa kumtesa Mbowe wanajisikiaje SAsa hivi Mbowe alivyo juu.
Unamtesa mtu ambae hata ustaafu pensheni YAKO hata ukiuuzwa na wewe ufikii hata robo ya mapato yake.
Acheni ujinga hii Dunia ikanyage polepole.
Leo wanaona aibu.
Pana siku Kova kova baada ya kustaafu alimkimbia Gwajima supermarket akikumbuka alipokuwa akimsotesha kabla ajastaafu.
Mbona walipandishwa vyeo ndugu?
 
Habari JF ,binafsi huwa nakuwa na Shaka sana na upinzani wa Mwenyekiti wangu mbowe

Kuna muda huwa napata mawazo ni mtu aliyewekwa kimkakati kuhakikisha CCM haitoki madarakan...
Kesi ile ya Mbowe iliandaliwa na mwendazake kwa madhumuni ya kukifutilia mbali CHADEMA,kwamba kama Mbowe ni gaidi basi na wafuasi wake wote ni magaidi hivyo chadema kimekosa uhalali wa kuwa chama cha siasa na kuwa chama cha kigaidi zaidi.
 
Waliotaka Lowasa, Mbowe wafe wametangulia wao.

Rip komba, Sitta, kombani, mwendazake, mtikila, Mshana
 
Habari JF ,binafsi huwa nakuwa na Shaka sana na upinzani wa Mwenyekiti wangu mbowe

Kuna muda huwa napata mawazo ni mtu aliyewekwa kimkakati kuhakikisha CCM haitoki madarakani...
Sema tu unataka tu unataka kumnaga hayati. Lakini kila kitu kinajulkana. JAJI liganga alishamaliza kazi kesi ilikuwa ya Mchongo ndio Maan Mama aliitema.
 
Modus operand za serikali za kidikiteta,huwa zinafanana,
Zuia mawazo binafsi, bana vyombo vya habari ua wapinzani, funga wapinzani, wazungu wanaita attach on descent...
Mpaka wakepeleka pesa za umma China😅😅😅
 
Habari JF ,binafsi huwa nakuwa na Shaka sana na upinzani wa Mwenyekiti wangu mbowe

Kuna muda huwa napata mawazo ni mtu aliyewekwa kimkakati kuhakikisha CCM haitoki madarakani...
Day light dreams
 
Habari JF ,binafsi huwa nakuwa na Shaka sana na upinzani wa Mwenyekiti wangu mbowe

Kuna muda huwa napata mawazo ni mtu aliyewekwa kimkakati kuhakikisha CCM haitoki madarakani.

Nimekaa nimejiuliza sana je Kesi ya Mbowe ilianza kusikilizwa kwa BENEFITS au FAIDA kwa awamu ya TANO au SITA au WANANCHI ?

Ilifunguliwa kwe lengo gani? Maana kwa Awamu ya Tano Mbowe alinyamazishwa na akanyamaza tofauti na Tundu Lissu.

Ushahidi ulikuwepo hata kabla uchaguzi 2020 ni Kesi yenye shutuma nzito vile, kwanini haikufunguliwa mapema ikichukuliwa ingeidhohofisha CHADEMA uchaguzi 2020?

Kwa haya mazingira ni kweli serikali ya awamu ya TANO ilihusika na ilikuwa kwa lengo lipi? Au ndio ulikuwa mwanzo wa kinachoitwa sasa ni MARIDHIANO?
Magufuli alishirikiana na Samia kuandaa kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe, ndio maana aliithibitishia BBC kuwa ni gaidi na alikimbia kujificha Kenya
 
Kama hujuma, udhalimu na ufedhuli mkubwa ulifanyika katika vitega uchumi vyake, katika akaunti zake binafsi, kwa wafuasi, wanachama na viongozi wa chama chake, nini ambacho kilishindikana katika kufanya maandalizi ya kesi ile ya mchongo?

Moderators, tunaomba nyuzi zote zenye kumuhusu hayati huyu ziunganishwe katika uzi mmoja tu, pengine ambao upewe kichwa kinachosemeka kama;

"Mazuri na mabaya yaliyofanyika katika utawala wa awamu ya tano"

Ili kama mtu atajisikia kuupitia, aende humo kwa wakati wake, na siyo kama ilivyokuwa hivi sasa nyuzi nyingi zinakuja kwa vichwa vya habari tofauti lakini "the bottomline" ni kwamba kuna mazuri na mabaya yaliyoambatana na utawala wake.

Hayati kafa na matendo yake mengi ya jinai yaliyoambatana na utawala wake, lakini pia anawiwa na madeni kupitia madai mengi dhidi yake. Ukweli ni lazima usemwe, na kama ambavyo yeye mwenyewe alipenda kusisitiza, msema kweli ni mpenzi wa Mungu, hii kwa kuwa ukweli utatuacha huru, utawala wake ulikuwa ni wa kibabe, kidikteta, na ulitamalaki kila aina ya uovu.
Pamoja na kwamba udikteta mkubwa ni mbaya lakini kwa Nchi zetu hizi za Africa bila kuwepo na kaudikteta dikteta mambo mengi hayaendi kama inavyopaswa kwenda !! Nitajie Nchi za Africa zinazoitwa Zimeendelea !! Developed Countries !!
 
Magufuli alishirikiana na Samia kuandaa kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe, ndio maana aliithibitishia BBC kuwa ni gaidi na alikimbia kujificha Kenya
Kwa katiba hii iliyopo hakuna kiumbe chochote kinachoweza kumkatalia Mkuu wa Nchi kitu chochote akitaka kifanyike !!
 
Back
Top Bottom