Kweli na ndio maana Serikali ya Rais Samia Suluhu inatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana ili waweze kujiajiriVijana wapewe elimu, ujuzi na maarifa ya kazi za mikono. Wazazi tuwape mitaji watoto wetu waanze kujishughulisha na uwekezaji mdogo mdogo
Kweli kabisa kwa upande wa ajira Serikali ya Rais Samia Suluhu imejitahidi sana kutokomeza tatizo la ajira Tanzania kupitia miradi inayotekelezwa nchini wanaonufaika ni watanzania pia inatoa mikopo yenye mashart nafuu vilevile inawekeza katika kilimo na kuwapa vijana kipaumbele kupewa eneo mambo ni mengi sana aisee Rais Samia Suluhu tumpe hongera zakeSerikali lazima itengeneze Sera nzuri za kutengeneza ajira... tulishuhudia awamu ya Tano ikiiona sekta binafsi kama threat kwake, ikaimaliza - hili lilikuwa ni kosa kubwa mno.
Nafikiri Mama Kaliona hilo na walau sasa hivi kuna ka mzunguko ka hela mtaani, mama ntilie anapika, fundi ujenzi wana kazi, fundi chelehani anashona, maduka ya ujenzi wanauza bidhaa, Bar walau zinauza uza na wahudumu wao nao afadhali kidogo, makampuni binafsi nayo pamoja na NGO zimetema ajira.
Mnyonge mnyongeni jmn, kuna ka kupumua kidogo - maana ilifikia hali kubwa mbaya mbaya.
Hapana sio kweli Serikali inatakiwa kutengeneza mazingira ya kumuwezesha mwananchi kujiajiri maana haiwezekani Tanzania nzima tukaajiriwa na Serikali sio kweli kabisaNi kweli? Kazi yake ni kutengeneza
Issue ni kwamba kuna asilimia kubwa ya watanzania ambao hawajaariwa serikalini na sio kila mtu ataajiriwa kwaiyo ili kuondoa tatizo la ajira Serikali inatengeneza mazingira wezeshi ya kujiajiri kwa wale wasiokuwa na ajira serikalini ndio maana unaona mikopo yenye masharti nafuu..wakati wa kampeni huwa wanasema serikali ya Ccm itatengeneza ajira.
..pia ikitokea kukawa na ajira nyingi husema Raisi au Mwenyekiti wa Ccm ametengeneza ajira.
Umeomba maji unaskia wahudumu wanaambiana mletee yale maji ya Mavi.Kwanini mkuu, ni jina tu hilo. Halihusiani na kilichomo.
Na ndio maana Serikali ya Rais Samia Suluhu imekuja na mpango wa kujenga vyuo vya veta nchi nzima lengo ni vijana tupate elimu ya ufundi na tuweze kujiajiri au kuajiriwa na kama unafatilia Rais Samia Suluhu alisema mtaala wa elimu ubadilishwe uwe ule unaomtengeneza muhitimu katika mazingira yote ya kuajiriwa na kujiajiriAmekwepa jukumu!
Lini wameleta mtaala wa kujiajiri Ili vijana wawe na ujuzi wa kujiajiri!?
Vijana wanaandaliwa kuajiriwa halafu wanageuziwa kibao eti wajiajiri KWELI!???
Na ndio maana serikali ya Rais Samia Suluhu imeweka mazingira wezeshi kwa vijana kujiajiri na hakuna serikali kokote duniani inayoweza kuwaajiri wananchi wake wote watu inatakiwa waelewe hili sualaKazi ya serikali ni kutengeneza mazungira wezeshi ya watu wake kuajirika na kujiajiri. Sio lazima wala wajibu wa serikali kukuajiri.
Serikali au nchi yeyote ikiwa na nguvu kazi isiyotumika "untapped workforce" kama ilivyo sasa katika nchi nyingi ni hasara maana kunakuwa hakuna uzalishaji, lakini sio hasara inayoudhi au inayoleta sharti wala kukera. Ni juu ya serikali husika kujali hilo au kutojali.
Jitahidini vijana mtafute au mjitengezee ajira la sivyo mtazeeka na kufa huku mnailaumu serikali.
Exactly haya mambo ni bahati tu ya kuajiriwa na wala sio system na kitu kingine serikali haiwezi kuajiri nchi nzimaWengine tulifanikiwa tukiwa hakuna hata mzazi mmoja kwenye system. Kwa hiyo sio kesi
Mbona hata Hilo bado selikal yetu ime shindwa?HAKIKA HIYO SIYO KAZI YA SERIKALI.
Serikali kazi yake ni kutoa huduma na kuhakikisha kuna miundombinu wezeshi kwa ajili ya kufanyika uwekezaji utakao zalisha ajira
Copy that.
Binafsi mpaka leo sijawahi pata maana halisi ya serikali, siku zote naona serikali zote ulimwenguni zipo kwa ajili ya kutia ugumu ktk maisha ya mwanadamu. Na dunia nzima mfumo wa serikali ni mmoja. Na hakuna kitu kinachoitwa serikali bali ni Mamlaka.
Kwamba huyu mwenye mamlaka yeye ndio ataandaa sheria ambazo hazitamhusu yeye, ( hichi fanya, hichi usifanye-huku yeye akifanya, atajitengenezea ukuta wa kujilinda yeye( wao wenye hiyo mamlaka ) na agenda zake/zao.
*Ardhi ni mali ya serikali
*Wewe mwenyewe ni mali ya serikali
*Utatakiwa ulipe kodi zote stahiki kwa serikali ( waita chombo ) japo ni watu. Yaani unaambiwa pesa inaenda serikalini ( unknown place ) sababu serikali haipo. Serikali ni kitu ambacho ki ukweli hakipo na badala yake kuna Mamlaka.
Sasa hii serikali isiyokuwepo huku ikiwepo ktk kivuli cha Mamlaka hapa ndipo panaponichanganya.
*Serikali ili ikamilike inatakiwa iwe na vitu vingapi?
*Serikali kamili ina watu wangapi?
*serikalini ni wapi?
*Serikali inaongozwa na misingi ipi?
*Msimamizi wa Serikali ni serikali yenyewe?
Kodi zetu lakini Mali ni za Serikali, na Mwisho Serikali haiwezi kukutaftia ajira sababu ni hiyo kwamba Serikali ki uhalisia haipo.
Njaa tu hii pengine nikishiba ntarudi ku edit
Issue ni kwamba kuna asilimia kubwa ya watanzania ambao hawajaariwa serikalini na sio kila mtu ataajiriwa kwaiyo ili kuondoa tatizo la ajira Serikali inatengeneza mazingira wezeshi ya kujiajiri kwa wale wasiokuwa na ajira serikalini ndio maana unaona mikopo yenye masharti nafuu
Kijamii inagoma. Serikali Ina wajibu... Mbaya zaidi inalaumu wahanga kwamba wanapenda mteremko, wanashinda vijiweni, KUBETI na kukataa kazi zingine. Hili ni tatizo la jamii, maelezo ya siasa yanatoa kwenye jamii na kulipeleka ngazi ya mtu mmojammoja. Hiv unajua kama daktari akipata kazi lakini ya umeneja wa bar bado tatizo lipo?Hii hoja ni controversial kulingana na unavyoweza kutafsiri but ukiangalia kwa jicho la Uchumi Ni sahihi , Serikali haitengenezi ajira Bali Ni facilitors wa kutengeneza ajira.
Dah! Hiv unajua Kaka hoja hii ndo ilitumika 1986 na Serikali ikaweka private. Miaka ya 1990s Hali ya Ajira ikawa mbaya mnooNdio kazi ya serikali ni kutengeneza ajira (mazingira) , ila kutoa ajira sio kazi yake.
Bibi Kavurugwa,ni wajibu wa serikali kuhakikisha watu wake wanakuwa na kazi zenye staha.Kazi kuu za serikali Duniani ni KUWALINDA na KUWAENDELEZA watu wake!Rais Samia Suluhu kaika maadhimisho ya miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar maadhimisho hayo yamefanyika katika Kijiji cha Paje, Mkoa wa Kusini Unguja leo tarehe 10 Januari, 2023
Amezungumzia mambo mengi lakini pia amegusia suala la ajira kwa vijana na kusema
"Nataka kuwaambia, kazi ya serikali si kutengeneza ajira, kazi yake ni kuweka mazingira mazuri ili vijana muyatumie kutengeneza ajira na hiyo kazi tunaifanya vya kutosha, naomba mkatengeneze ajira kwa mazingira yaliyokuwepo,"- Rais Samia Suluhu Hassan
Kwa maoni yangu naona ni sahihi kwasababu kazi kubwa ya serikali ni kututengenezea mazira mazuri ya kufanya biashara au kuajiriwa na serikali imefanya juhudi hizo kupitia kufungua vyuo vya ufundi (VETA) nchi nzima kwaiyo kupitia elimu ya ufundi vijana wanaweza kujiari.