Je, ni kweli kuna majini?

Sun is Sun

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2024
Posts
649
Reaction score
975
Habari zenu WanaJamiiForums?

Swali langu linauliza je, ni kweli majini wapo? Katika utafiti wangu kuhusu majini sijawahi kukumbana nao. Na nimefanya utafiti wa kina mpaka majaribio lakini mpaka sasa sijawahi kuwa-expirience.

Au hii pia tuweke kwenye story za ABUNUWASI? Kama kuna anayeweza kuweka muongozo wa namna ya kuwaita aje,. Nahitaji kumaliza huu utafiti.

Asanteni.
 
Majini Sio viumbe wa kawaida sasa huo utafiti ulifanyia wapi tueleze mkuu
 
Taja majina yako kamiri umri wako ragi ya nywele na rangi unao vutiwa nao sana , ni mtumie shkh majini pemba leo kabla asubuhi haijaingia utawapata hao wageni.........
 
Wewe chukua tu ubani kisha bakuli la chuma jaza mchanga au container yoyote ile jaza mchanga then weka mkaa wenye moto na ubani weka juu yake.
Ita "majini njoeni nawaita" rudia mara kadhaa kisha lala usingizi au Kaa tu macho utawaona kwa macho au utaona actions/impacts zao.
 
Na je vipi malaika wapo?ushawai kuwaona? oxgen nayo vipi ushawai kuiona kwa macho na una amini ipo?
 

Hakuna kitu kama hicho. Ni dhana ya kiarabu ya kuwatisha watu au kutumika kupigia fedha za mazwazwa wanaoamini ujinga huu. Majini, pepo, na roho mtakatifu ni dhana mfu na za kufikirika zisizoingia akilini kwa watu wenye vichwa vinavyochemka. Ukitaka kujua kuwa hivi vitu ni feki, vya kubuni, na havipo, waambie wanaodai vipo wavilete lau kimoja tuvione au kuvihisi.​

 
Waulize wasio penda kitimoto.
 
Kweli Mkuu, Maana formula zote nilifanya lakini sikuwahi kuwahisi wala kuwaona . Hizi ni story za kusadikika kama zingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…