Je, ni kweli kuna Waziri anaugua Corona inafanywa Siri? Tunaficha nini? Hala hala kisa cha mficha maradhi! Truth & Transparency the only way out!

Na hata siku ikifika ya kumrudia mola, kama ni Waziri, lazima kwanza aombwe aliyemteua kwanza kuwa Mh. Waziri inatakiwa arudi mavumbini. Waziri ni mtu mkubwa hawezi kuondoka tu wakati yawezekana akawa hajamaliza kuwahudumia wanyonge.
Usishangae mochwari akalindwa na askari aliye hai! Akizikwa familia inakabidhiwa jukumu baada ya kuweka zege juu ya kaburi.
 
Sasa alienda Italy kutafuta nini ? Huu si upuuzi

Sent using Jamii Forums mobile app

Huyu bila ya shaka alitumwa kwenda Italy KUCHUKUA Covid-19 na kuileta Tanzania for a purpose...!!
Naanza kuwa na mashaka kuwa hii Corona umeletwa au kuachiliwa maksudi iingie Tanzania kwa maslahi ya Kisiasa ya chama FULANI!!!...jina kapuni...!
 
Waziri kiongozi wa kwanza wa SMZ amefariki jijini Darisalama alikokuwa amelazwa hospitali na mwili wake kuahirishwa kupelekwa Zanzibar.
Source: Mwananchi
 
Sijui ni nini definition ya siri kwa kiswahili, but toka pale tu waziri alipofika hospitali ya mnazimoja akilalamika kusumbuliwa na mafua na homa wazanzibari tulianza kutumiana taarifa hii. Zanzibar ni ndogo sana na kabla hata daktari mkuu wa mnazimoja hajamwambia mgonjwa "sema aagghhhh" watu walishajulizana kuwa huyu waziri amerudi safarini england na italy sio zamani sana kwa hivyo watu wakafanya 1 + 1 = 3 !!

Tatizo ambalo liliwakera wazanzibari wengi ni kule kwa waziri huyu kukataa kwenda katika hopspitali ambayo serikali anayoitumikia imeitega kwa wagonjwa wa corona. Pia kule kwa waziri wa afya kushindwa kuwalinda wafanyakazi wake kuanzia wafagizi mpaka madaktari kwa kushindwa kumshawishi waziri mwenzake kufuata utaratibu ulioweka na kwenda hospitali ya kidimni. Kubwa zaidi lilowakera wazanzibari wengi ni kule Rais wa nchi kuchukuwa muda mrefu kuingilia kati suali hili.

Huyu waziri anaonyesha ana kiburi sana, yaani kusema yeye hawezi kupelekwa kidimni kwa sababu ya status yake ni dharau kubwa kwa wananchi wote wa zanzibar. Amesahau ule msemo mpanda ngazi hushuka. Kuna siku atashushwa madaraka na ataona cha moto.
 
Wazanzibari washaanza kampeni ya kuhakikisha akipona anashushwa madaraka. Watu wanataka ajieleze alikwenda uk na italy kwa kazi gani, maana muda mkubwa alipokuwepo uk alikuwa katika mji wa Northampton ambao uko mbali sana kutoka londo. London ndiko ambako ulipo ubalozi wa Tanzania na ndiko ambapo serikali ya UK ina inapoendesha shuhuli zake zote ikiwa pamoja na mikutano yote na mawaziri kutoka nchi za kigeni. Isitoshe wakati akiwa Northampto alikuwa akikaa kwa jamaa yake badala ya hoteli, watu wanataka kujua amezifanya nini pesa alilolipiwa kwa ajili ya malazi yake. Inaaminika kuwa alifanya vivo hivyo alipokwenda Italy. Tunangoja tuone serikali itafanya nini hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…