Je, ni kweli kuwa Dodoma CBD inaipiku Mwanza CBD?

Kwani nimekosea nikisema ni moja kati ya mapanbo ya hapo jangwani Dodoma.
Bora mji unaopambwa na vitu icon vinavyopatikana katika majiji yote makubwa yanayoheshimika duniani kuliko jiji linalotegemea pambo la sanamu ya sato round about.
 
Nini kifanyike acha ujinga wakuongea bila kuleta suluhisho.
 
Hyo terminal haujajengwa Kwa pesa za mikopo acha uongo wako ...pesa zimejengwa Kwa force account...za halmashauri ya manispaa ya ilemela na mwanza CC ...kwanza magufuli alisema Ile ni temporary block ...

Sent using Jamii Forums mobile app
Bora umejibu wewe, na kama limekosewa je serikali ina mpango gani nalo?
 
Dodoma inachoizidi mwanza ni bunge, ukame, vumbi la trachoma na hiyo outer ring road
 
Na hiyo msalato ina umuhimu gani kwa sasa kama sio kujenga bila taaluma na kutokuangalia hali halisi ya mambo, hiyo airport itakuwa ni hasara kubwa kwa taifa, na litakuwa linachukua wasafiri wa kutoka nchi gani waje washukie hapo, uwanja wa ndege wa mwanza mnaufanyia figisu alafu tusiseme.
 
Miradi ya dodoma n dar huwa inafuata misingi gani? Huwa sisikii mbungeni lakini nakuta imeanza kutekelezwa huu ujinga nao unaitwaje?
 
Bora mji unaopambwa na vitu icon vinavyopatikana katika majiji yote makubwa yanayoheshimika duniani kuliko jiji linalotegemea pambo la sanamu ya sato round about.
Hiyo picha ya round about ya huyo sato anayetema maji, niliiona nilipokuwa Frankfurt, Germain.... Hilo sanamu ni maarufu kuliko jengo la bunge.
 
Hiyo picha ya round about ya huyo sato anayetema maji, niliiona nilipokuwa Frankfurt, Germain.... Hilo sanamu ni maarufu kuliko jengo la bunge.
Kwahiyo unajinasibisha kwa copy & paste[emoji23]
 
Miradi ya dodoma n dar huwa inafuata misingi gani? Huwa sisikii mbungeni lakini nakuta imeanza kutekelezwa huu ujinga nao unaitwaje?
Miradi ya Dodoma ni miradi ya kimkakati na bajeti yake utengwa na kuidhinishwa kila awamu na bunge, hivyo usianze kuleta mbishe za kiswahili
 
Kwanini unafikiri kiwanja cha ndege msalato ni project hewa?

Kwanini unafikiri Mwanza ndiyo inastahili kuwa na miundombinu bora ya usafiri wa anga na si Dodoma?
 
Kwanini unafikiri kiwanja cha ndege msalato ni project hewa?

Kwanini unafikiri Mwanza ndiyo inastahili kuwa na miundombinu bora ya usafiri wa anga na si Dodoma?
Dodoma ipo karibu na Dar, na tayari Dar kuna uwanja mkubwa wa kimataifa, je hao wageni wataacha kutumia JNIA na washukie msalato? Je msalato itapokea wageni wa aina gani? Jibu hayo nakuja kukupa facts kuwa hiyo msalato ni upotevu wa fedha kwenye nchi maskini kama hii
 
Dodoma inachoizidi mwanza ni bunge, ukame, vumbi la trachoma na hiyo outer ring road
Ungeendelea kutaja tunavyowazidi kuwa si bunge tu bali ikulu, jiji la kisasa la kiserikali, estates,majengo ya taasisi mbalimbali, vyuo vikuu, planned city, makazi bora, kilomita ndefu za mtandao wa barabara za lami mjini, bustani za kupumzikia,n.k

Bora unusu jangwa wenye trachoma kuliko kunywa maji yenye mchanganyiko wa vinyesi na mwisho wa siku ni kufa kwa kansa.
 
Hapo kwenye estate na makazi bora elezea vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…