Haya weka ushabiki pembeni, Kati ya mwanza na dodoma lipi ni eneo potential ambalo hata serikali inabidi iliwekee nguvu zaidi ili kujiingizia mapato? Ukiniuluza Mimi ntakwambia ni mwanza sababu
1.kuna ziwa kubwa ambalo shughulii za uvuvi na usafirishaji wa samaki hadi nje ya bara
2.iko karibu zaidi na nchi nyingi za Afrika mashariki
3.uwepo wa migodi na shughuli za uchenjuaji na usafishaji wa madini Kama almasi na dhahabu
4.idadi ya watu na muingiliano wa watu ni mkubwa ni kubwa hivyo hata upatikanaji wa mapato ni mkubwa
5. Ukubwa wa eneo
6. Hali ya hewa
7. Idadi ya viwanda ni kubwa kulinganisha na Hilo jiji lako
Haya na wewe utakae chagua dodoma tuletee potentiality yake na kwa nini serikali iwekeze sana
1. Dodoma haitaji sababu lukuki hili iwe potential kuwa center ya Tanzania pekee ni sababu kuu mojawapo. Dodoma lazima izingatiwe tu iwe icwe kwasababu ndiyo injini au ubongo wa nchi na tokea pale ndipo michirizi au neva za damu usambaza msosi kuelekea sehemu zingine za nchi, hivyo kiuchumi hili haliepukiki maana dodoma ikifubaa kama mwanza itaathiri uchumi wa nchi nzima.
2. Dodoma ni mzalishaji wa mazao makuu ya kibiashara kama zabibu, karanga na alizeti ambayo ni raw materials inayoitajika zaidi kwa uchumi wa viwanda.
3. Umbali wa Dodoma na Dar es salaam ni mfupi na efficient zaidi kuliko Dar to mwanza hii ni advantage nyingine kwa dodoma ku-reserve vitu vingi toka mikoa yote miwili lazima ipitie katika eneo lake. Mfano mdogo ukiwa dodoma bado waweza kunywa supu ya pweza na kachori ila ukiwa mwanza ni sato tu. Na vilevile bidhaa nyingi ufika Dom kwa wakati with measurable price mfano bei ya pombe na some stuff zingine toka bandarini kwa Dom ni nafuu kuliko mwanza.
4. Dodoma ni Las Vegas ya kibongo hivyo baadae kibiashara siku za usoni ni promising mno especially spending katika vitu luxury na starehe kutokana na nature ya wakazi wake kuwa ni vigogo wa serikali, watu wa makampuni na mashirika, wafanyabiashara na wananchi wengi wa kipato cha kati. Hivyo utakuwa ukishavuna mahindi yako ukauza huko mwanza una haja ya kusafiri mpaka Dar kusaka bata utadrop tu hapa Dom kutuachia hiyo hela.
5. Dodoma ina eneo kubwa zaidi na potential kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vingi na pia inavutia wawekezaji wengi kuwekeza kuliko mwanza. Hata mpaka sasa maeneo ya viwanda dodoma yako kwenye demand kubwa mno na isitoshe kuna huge investments zinaendelea matunda yake ni miaka mitano ijayo.
6. Dodoma ni eneo accessible na efficient linapokuja suala la kuingia kwa bidhaa na kutoka, hasa usambazaji wa bidhaa toka viwandani kwenda other parts za nchi na nje ya nchi wakati mwanza ni corridor iliyobanwa na ziwa hivyo hakuna budi pawezeshwe madaraja, bandari na airport ndo pafunguke.
7. Dodoma ni hub tech na logistics center kubwa kuliko mwanza, pili kupitia bandari kavu ya dodoma, jiji litapokea mizigo mingi zaidi kupitia SGR na barabara zake bora nakuzilisha sehemu nyingi zaidi kuliko mwanza. Ikiwemo mikoa ya kaskazini mpaka Nairobi, Mwanza na nchi jirani zinazoizunguka ikiwemo UG, Burundi, Rwanda na DRC. Hivyo kutokana na kuwa transit city kubwa na hub ya biashara, kimapato mwanza bado itaendelea kungoja.
8. Dodoma kwa future ya kibiashara ni potential zaidi ya mwanza kwa kuwa ina changamoto nyingi zinazohitaji uwekezaji rahisi wa watu binafsi dhidi ya soko lililopo tiyari ambazo zikitatuliwa na wawekezaji zitaleta impact kubwa kiuchumi.
Mfano kuanzisha viwanja vingi vya starehe, kuanzisha biashara ya vyakula freshi na viwandani, kufungua showrooms za magari luxury na vito mbalimbali, kutengeneza theme parks na maeneo ya michezo, kujenga shule na taasisi mbalimbali za elimu zenye hadhi ya kimataifa, kuwekeza kwenye kujenga apartments, display na mapambo ya mji.
Viwanda, usafirishaji wa bidhaa na watu, kuwekeza kwenye miundombinu ya maji, usanifu majenzi na makampuni ya ujenzi, teknolojia n.k
kuliko mwanza ambayo potential yake kubwa siku za usoni ni sekta ya Afya tu kutokana na kuzidi kuenea kwa magonjwa ya matumbo, sumu ya mercury na zebaki mwilini na saratani.