Unataka kusema JPM ndo kaijenga Mwanza? Unajua mwanza imekuwa jiji mwaka gani? Hayati W.B.Mkapa ndo kaitangaza Mwanza kuwa jiji mwaka 2000 inawezekana mlikuwa watoto bado mkiwa kijijini kwenu huko mlipo mda huu
Kipindi hicho JPM ndo anagombea ubunge for the 1st time tena jimbo ambalo lilikuwa ni la mkoa wa Kagera (Biharamulo) kwa lugha fupi ni kwamba JPM anakuwa Mbunge tayari Mwanza ni jiji
Harafu miradi yenyewe aliyoleta JPM Mwanza inahesabika na 70% ya hiyo miradi haijakamilika bado
Meli (Mv Mwanza)
Daraja Busisi-Kigongo
Ujenzi wa jengo la Mama na mtoto
Soko mjini kati
Standi za mabasi (Nyegezi na Nyamongoo)
SGR ni mradi wa kimkakati sio wa Mwanza pekeake
Zaidi ya hapo hakuna miradi mingine ya JPM
Aisee! Ngoja nikukumbushe fadhila kadhaa za ngosha kwa jiji la Mwanza:-
1. Kilomita za lami fupi za mijini Mwanza mlipewa nyingi tu kumaliza vumbi pale mjini na huko mitaani mfano sabasaba, nyasaka n.k.
2. Ujenzi wa terminal na jengo la mizigo, utanuzi wa run way katika airport ya mwanza
3. Ujenzi wa njia nne mjini to airport
4. Jengo jipya la taasisi ya kansa pale Bugando
5. Ujenzi wa bypass Kisesa to Usagara
6. Ujenzi wa nyumba za watumishi house
7. Ujenzi wa kiwanda kikubwa cha pharmaceutical
8. Uwekaji wa taa za barabarani na za wavukaji barabara ndani ya jiji zima
9. Ujenzi wa masoko ya dhahabu na kiwanda cha ukataji vito
10. Kipaumbele cha mikopo ya uhakika katika uwekezaji wa vituo vya mafuta kwa Mwanza ilitia fora (angalia sheli ngapi zilijengwa kwa fujo barabara ya kisesa to nyashishi)
11. Benki kuu ya Tanzania- Mwanza
12. Mradi wa kujenga tanki kubwa la maji kukamilisha ujazo unaokosekana sasa kuhudumia jiji zima (aliondoka kabla utekelezaji haujaanza) n.k