Je, ni kweli kuwa hadi Rais Magufuli anafariki mfuko wa UREA Kg 50 ulikuwa Tsh. 50,000/- leo umefika Tsh. 147,000/-

Afya Elimu Na Kilimo Sio Kipaumbele cha serikali ya ccm
 
Jiwe alikuwa ni jembe ila jembe la ovyo , aliacha kuweka misingi imara ila akaendekeza ukabila, umimi na kutengeneza legacy yake, Jiwe hastahili sifa , alikosa maona ya kuacha mfumo imara, ila akatengeneza mazingira ya kutawala milele.
 
JIWE alikuwa muuaji na mtesaji wa watu wote waliokuwa wanaibia Serikali na kuharibu uchumi wa nchi na wa mtu mmoja mmoja. Aliyeko madarakani anakumbatia kundi dogo linaloibia Serikali na kutesa walio wengi. UKWELI NDIO HUO
Inaonekana alikufanya vibaya sana kiroboto naona kwa sasa unaenjoy maisha baada ya mtesi wa familia yenu kutoweka juu ya uso wa dunia
 
Vita vya Ukrain,kama vimeanza alivyofariki na bado wapo kwenye Royal tour hawajali chochote .tukiongea tunaambia tukazikwe naye Chato.Hovyo kabisa.
 
Mtaimba nyimbo zote. Jiwe aliitwa shetani na wahuni!
 
Jiwe alikuwa ni jembe ila jembe la ovyo , aliacha kuweka misingi imara ila akaendekeza ukabila, umimi na kutengeneza legacy yake, Jiwe hastahili sifa , alikosa maona ya kuacha mfumo imara, ila akatengeneza mazingira ya kutawala milele.
Umesema vizuri. Yeye mwenyewe akawa kilakitu. Hata katiba/sheria akawa yeye.
 
Waliorudishwa kwenye System ni wale MAJIZI makubwa yasiyo na huruma hata kidogo kwa Watanzania.

Yana uwezo wa kuiba hata zaidi ya 80% ya mali za umma bila kujali kuna Watanzania watapata madhara kwa kukosa huduma kutokana na wizi huo.
Unadhani kwa hayo MAJIZI yaliyorudishwa kwenye mfumo kuna chochote kitaendelea Nchini. La hasha.
Hapa ni mwendo wa shida mpaka maamuzi magumu yatakapokuja kufanyika mwaka 2025.
 
Twafwa wakulima mweeh!
Na wao watakufa tu ! Kwanza kama mazao yasipopatikana ya kutosha itabidi waagize chakula kutoka nje ! Na mambo yao ya siasa hayatakuwa rahisi huko 2025 !! Kila Mara tunashauri bei ya bidhaa muhimu ni lazima zidhibitiwe na Serikali maana ukiwaachia wafanyabiashara wapange bei wanavyotaka ni lazima hali itakuwa mbaya kama ilivyo sasa !! Wafanyabiashara hawana huruma na watu! Wao wanafukuzia faida kubwa tu kila siku ! Nchi zote duniani hutoa bei elekezi katika bidhaa muhimu zinazogusa maslahi ya watu wengi !! Nimemsikia Waziri Kijaji akisema IPO sheria ya kudhibiti bei za bidhaa !! Sasa kwanini isitumike sasa ambapo wafanyabiashara wanajipangia bei kiholela eti sababu ni vita vya Ukraine ???!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…