Mkuu angalia usije kuwa wewe ndio Mtanzania usie na Akili na sio wengine, GSM ni kit supplier wa Yanga na mfadhiri mkuu kwa sasa ambae muda wowote ataenda kupata umiliki wa hisa za umiliki wa club
Team zingine ikiwemo Simba ina mikataba na kit supplier wa makampuni mengine, let's say Vunjabei anadhamini Simba na polisi kama sikosei, Leo hii akakae kwenye jersey moja na kit supplier wa team ingine we huoni kama kuna mgongano wa kimaslahi? Umewahi kuwaona Adidas na Nike kwenye jersey 1?
Kingine katiba ya TFF imeelezea vizuri kabisa juu ya mdhamini Mkuu wa ligi anatakiwa kukaa wapi kwenye jersey za team zote zinazoshiriki ligi kuu bara, na hakuna sehemu inamtaka mdhamini mwenza akae kwenye jersey, hii ya safari hii imetokea wapi?
GSM sio wadhamini wenza wa kwanza kupatikana katika ligi ya Tanzania na hao hawajawahi kukaa kwenye jersey zaidi ya kwenye mabango na kutambulika tu kama wadhamini wenza imekuaje kwa GSM ikae kwenye jersey na katiba inatumika ile ile ya miaka yote?
Kinachoonekana kuna harufu ya rushwa imetumika ili kukiuka baadhi ya kanuni zao wao wenyewe na ndomana wakati watu wanaanza kuhoji uhalali wa udhamini huu TFF ilitoa tamko kuwa watu hawaruhusiwi kuhoji Kwani huo mkataba ni kati ya TFF na GSM
Ni kama vile GSM wamefanya kuikomoa Simba na kufurahisha mashabiki wao kwamba Simba amevaa nembo yetu na sioni kama kulikuwa na dhamira ya kweli ya kudhamini ligi na kama ingekuepo basi kanuni zingefatwa
Hakuna mahusiano ya moja kwa moja yaliyopo kati ya GSM kudhamini ligi na kuchukua ubingwa wa ligi kuu ila tatizo taratibu zinavunjwa ili tu GSM akae kwenye jersey ili iweje? Lengo hasa ni nini? Ukinijibu hayo maswali niliyouliza ndio nitaweza kujiweka namie kama ni miongoni mwa watanzania ambao hatuna Akili, ila ukishindwa basi utakuwa wewe ndio Mtanzania usie kuwa na Akili