Je, ni kweli udhamini GSM ni wa kimkakati?

Kama TFF wameamua lifanyike Hilo wewe Nani UPINGE?
Hatimae umeonesha uwezo wako wa kufikilia ulipoishia, kumbe hoja ni kwakuwa TFF wamekubali Kwanini Simba ipinge sio? Okay kama TFF ndio waliandika kanuni juu ya rangi za mdhamini mkuu zilizopo kwenye nembo yake ziheshimiwe na hazitakiwi kubadirika Kwanini Yanga waga wanapinga? Kama TFF ndio final say? Acha uzwazwa tumia ata hizo akili zako ndogo kwa faida
 
Justification ya hili kikanuni ikoje?
 
Mimi nashauri hii nembo ya GSM iwekwe tu kwenye jezi za Marefarii,
Maana tumeshashuhudia Jitihada zao za uchezeshaji kwenye mechi ya Yanga vs Ruvu, Yanga vs Azam, Yanga vs Namungo na Yanga vs Mbeya Kwanza

Wanufaika wa fedha za GSM ni Yanga, TFF na waamuzi.
 
Kweli wewe Ni #mjingawewe#
 
Na ndo maana nikasema NYIE mna ushabiki maandazi.
Na mkiendelea hivi MPIRA wa Tanzania hauwezi kuendelea kamwe.
Mnapenda kurumbana kwa vitu vidogo Sana .kisa usimba na uyanga.
Na wao GSM wanafanya hivyo wanajua mtapanic.
Na Hilo ndo lengo lao.
TFF na mdhamini ndo wamekaa wakaamua iwe hivyo.
Kwanini Mara nyingi complain zinatokea kwa Simba na yanga?
mbona timu nyingine HAZILALAMIKI?
 
Justification ya hili kikanuni ikoje?
Kanuni inamtaka mdhamini mkuu peke yake ndio mwenye mamlaka ya kukaa mkono wa kulia wa jezi kwa team zote ambazo zinashiriki ligi kuu, na hazimuongelei mdhamini mwenza kabisa juu ya uwepo wake kwenye jersey, ila inajulikana mkono mwingine wa kushoto waga ni kwa ajili ya matumizi mengine ya club husika, wataamua wenyewe either wamuweke mdhamini wao au lahh, kwahiyo mamlaka ya TFF kwenye jersey na mdhamini mkuu kwa mujibu wa kanuni yanaishia katika bega la kulia

Lakini cha kuchekesha na kushangaza basi tuache mambo ya kanuni tuje kwenye amount ambayo ameitoa mdhamini mkuu ili akae kwenye jersey, NBC anatoa 2.5b kwa msimu ila GSM anatoa 1b kwa msimu, Sasa inaingia akilini kweli mtu alietoa 2.5b na alietoa 1b wote wakae kwenye jersey 1?

NBC watajonaje kwamba wao ni wajinga sana au washamba sana kupigwa mpunga mrefu kuliko mdhamini mwenza ambae ye katoa kidogo? NBC pia naamini walizisoma kanuni hadi kufikia kutoa pesa zao hivo wanajua yao na mipaka ya mdhamini mwenza sa itakuaje pale ambapo watakuja kuona kanuni zimevunjwa kwa ajili ya kumnufaisha GSM, je hapo hakutakuwa na mgongano wa kimaslahi kwa hao wadhamini wawili
 
Una haki yakujiita@mjingamimi
 
Una haki yakujiita@mjingamimi
kwa hyo unataka TFF waache kuchukua hela za udhamini sababu ya ushabiki wenu maandazi wa Simba na yanga?
LIGI Ina timu 16.
Ila wanaolalamika ni Simba tu?
Kama wao nfo watavaa hyo nembo Peke yao?
nje ya kanuni wanazo sema . kuna usimba na uyanga.yaani akiacha kulalamika yanga ,Basi Simba atalalamika.
Mimi ni shabiki wa Simba .
Ila siwezi kuendekeza ushabiki maandazi.mtu kaweka MZIGO .
Wakulalamika ni NBC sio Simba.
TFF wameshaamua.
Kanuni itabadilishwa na maisha yataendelea.
 
Unarudia yale yale ya kutokujibu hoja unabaki kuruka ruka tu, acha kuropoka kijana tumia akili zako basi mbona kwenye maswali na hoja ya msingi hujibu? Of course inaonekana huna unachokijua wewe unaropoka tu

aliekwambia ni Simba peke yake ndio wanagomea huo udhamini nani? Ulimskia almasi kasongo aliposema kuna vilabu 8 ambavyo vinataka ufafanuzi juu ya huo udhamini ila watakaotoa ufafanuzi sio bodi ya ligi ni TFF

Simba na Yanga zina nguvu kuliko hao wengine ndomana wanasikikaga wao tu na kuhusu hii case ya sasa Simba ndio kafungwa kengele na hivo vilabu vingine kwa sababu ana nguvu
 
Wewe umetoa shilling ngapi kwenye udhamini wa ligi?.
kanuni ikibadilishwa na mdhamini akaweka nembo yake na timu zikapata mgao
NYIE mnaumia nini?
unaleta complain wakati hauchangii hata 100.
 
Ulianza vizur ila mwishoni ndo ukaharibu.
 
Mkuu ni bora ungemquote jamaa nilemquote kuliko kuniquote mm. Ulichokiandika ndicho nilichokimaanisha ila in a very simple way.
Anaita wenzie mambumbumbu kumbe yeye ndo mkufunzi wao.
 
Wewe umetoa shilling ngapi kwenye udhamini wa ligi?.
kanuni ikibadilishwa na mdhamini akaweka nembo yake na timu zikapata mgao
NYIE mnaumia nini?
unaleta complain wakati hauchangii hata 100.
Kwahiyo wanaotakiwa kuhoji ni ambao wamechangia ata mia Sasa wewe unaendelea kujipitisha hapa unatafuta nini au mwenzangu umechangia?
 
Kwa miaka minne walivyoishi kama wafalme huwez amini kama leo hawa ndo wanalalamika.
 
Acha kukalili mambo, kwa taarifa yako ni kuwa hakuna kanuni inayozungumzia juu ya mdhamini mwenza nembo yake itakaa/haitakaa kwenye jezi ya timu, bali ni hao tff wanapomfuata huyo mdhamini kumuomba udhamini , na yeye ndiye anatoa masharti yake, mkiyakubali sawa anatoa pesa!!na tff ndio walimfuata GSM, na yeye akatoa masharti hayo.sasa kama hao wadhamini wenza wa nyuma hawakutoa sharti hilo ni wao!!kanuni zipi hizo ambazo zimekuwepo kwa miaka mingi?mbona hadi sasa timu hazifahamu hyo mdhamini mkuu washindi watapata kiasi gani?TFF, ndiye mwenye ligi na mikataba yote ya wadhamini ni yeye ndiye anaiingia, hata CAF, ni hivyo hivyo, nyie timu mtapewa tu utaratibu wa kuufuata basi, kuna timu hapa hapa ina udhamini wa ttcl na logo yake iko bega la kushoto , sasa watakapokuja kuambiwa waitoe/kuihamisha utasikia kelele tena!!wakati kanuni ziko wazi kuwa hata ukipata mdhamini wako huko lazima uijurishe tff kwanza!!Tatizo la kwetu u yanga na simba ndio kikwazo.
Ila ki kanuni ktk hili simba hoja zake hazina mashiko.mfano eti yanga hajatwaa kombe miaka 4, hivyo kuna kitu kinaandaliwa!!!si upuuzi huo, GSM, ndio atacheza?
 
Kwahiyo wanaotakiwa kuhoji ni ambao wamechangia ata mia Sasa wewe unaendelea kujipitisha hapa unatafuta nini au mwenzangu umechangia?
Acha hela ziingie huo Ushabiki wenu wa Simba na yanga.pelekeni huko.
TFF watakataa vipi bilioni 1 kisa kanuni?
ach kuota.
TFF wako sahihi.
 
Umetumia andiko refu sana kumpa elimu mtu ambae hawezi kuelewa,ila sio mbaya wenye kuelewa mambo watafaidika na elimu yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…