Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Mimi ndio naiona hii leo ila kitu ambacho unatakiwa kujua kuhusu UTT ni mutual funds au tukisema a collective investment scheme ambapo ni kama unachangia pesa katika utekelezaji wa jambo fulani alafu pesa inarudi na faida kutokana na kile kilichowekezwa. Na wewe kama mwekezaji unatakiwa kujua lengo lako la uwekezaji, muda unaotaka na ukwasi(liquidity). Na uwekezaji unawakilishwa na kipande ambao ni uwiano wa umiliki wako kwenye mfuko. Alafu wakati wa gawio mwenye ana vipande vya juu basi na gawio linakua uko juu. Sasa UTT ina mifuko 6 nadhani na mfuko ulioambiwa unaitwa liquid na ni mfuko wa wazi wa muda mfupi/kati na unaweza kupewa riba nzuri kabisaaaa na kianzio chake ni 100,000
 
Mimi ndio naiona hii leo ila kitu ambacho unatakiwa kujua kuhusu UTT ni mutual funds au tukisema a collective investment scheme ambapo ni kama unachangia pesa katika utekelezaji wa jambo fulani alafu pesa inarudi na faida kutokana na kile kilichowekezwa. Na wewe kama mwekezaji unatakiwa kujua lengo lako la uwekezaji, muda unaotaka na ukwasi(liquidity). Na uwekezaji unawakilishwa na kipande ambao ni uwiano wa umiliki wako kwenye mfuko. Alafu wakati wa gawio mwenye ana vipande vya juu basi na gawio linakua uko juu. Sasa UTT ina mifuko 6 nadhani na mfuko ulioambiwa unaitwa liquid na ni mfuko wa wazi wa muda mfupi/kati na unaweza kupewa riba nzuri kabisaaaa na kianzio chake ni 100,000
Shukran mkuu, nilishafungua huu kwakwel sio sawa na kuweka pesa bank ambapo inakaa tu.
 
Asante kwa huu uzi mkuu, I hope ulipata enough knowledge kwasababu na mimi nimejifunza kitu.

Je kiasi cha chini kabisa kuweka ni kiasi gani? And naweza ku deposit kila mwezi?
Kwa kuanzia ni laki moja, unaweza kudeposit kuanzia tsh 10000 wakati wowote ata ukiamua kila siku. Mm nilijiunga na liquid.
 
Asante kwa huu uzi mkuu, I hope ulipata enough knowledge kwasababu na mimi nimejifunza kitu.

Je kiasi cha chini kabisa kuweka ni kiasi gani? And naweza ku deposit kila mwezi?
Kwakweli ni sehem nzr na sahihi sana kuliko kuweka hela bank, huku unaona trend ya ongezeko la hela yako each day, the more the deposit, the more the profit.
 
Uza tu mkuu wala hautajutia.
Unajua ndio maana wahindi wengi hawajengi. Sio kwamba wanaogopa ila wanajua hasara ya kuweka pesa chini isiyozalisha, Imagine mtu ana nyumba ya 200m lakini napata shida na ada ya mtoto ya sh 4m wakati pesa aliyoweka chini anaweza kupata 20m kwa mwaka. Usishangae wahindi kwa biashara ndogo tu watoto wanasoma shule za maana, hata nje ya nchi.
Mkuu hizi vitu huwa naona ndio vya kufanya kwa wale ambao hatuna maarifa ya biashara ama karama. Kama risk appetite ndogo bora uweke hela huko ambapo kama una nyingi unaweza kukuta hela unayopokea kwa mwaka tu inaweza kuendesha maisha vyema tu ukalipa ada na kila kitu ukafanya huku pengine una kazi yako maisha yanaenda tu!

Uwekezaji wa Real Estate ufanye ule wa kikweli kweli yani! Upangishe makampuni au staff wa makampuni ndio utainjoy uwekezaji wa nyumba ila ile style ya kukabana kila mwezi na wapangaji ni ngumu na inaboa.
 
Kwa wastani hii mifuko y UTT ina faida zinazolingana, tofauti ni ndogo sana. Utachagua mfuko ambao unakidhi mahitaji/malengo yako.
Nitakupa stori yangu.
Mimi nilipata kama 60m mahali fulani. Nikaamua niihifadhi mahali ili niongezee itoshe kununua kiwanja na kujenga. Baada ya ushauri na utafiti nikafungua Jikimu fund (re investment) Hii wanatoa gawio mara 3 kwa mwaka na faida hupewi ila inaongeza mtaji.
Baada ya miaka miwili wazo la kujenga nikalifuta maana nilikua na mtaji wa karibu 100m na faida yake kwa mwaka ni zaidi ya 10m. Nachukua 6m nalipia kodi ya nyumba iliyobaki naiacha ikuze mtaji wangu, kuliko kuwa na nyumba isiyoingiza chochote.
Hii ni faida ndogo sana kulinganisha na unachoweza kupata kwenye biashara. Lakini kumbuka si kila mtu anaweza kufanya biashara. Wengine kazi tunazofanya inakua ngumu kusimamia biashara nyingine. Wengine utaalam wa biashara ni mdogo. Wengine wanatafuta mahali pa kuweka hela zao kwa muda tu ili waweze kuzitumia hapo baadaye.
Kwa hiyo kuwekeza huku sio kubaya.
Mkuu hii 60m ulikuwa unapewa gawio la kiasi gani kwa mwaka? What was the rate?
 
Nahisi hii kitu ni kizuri, kina faida zifuatazo.
1. Kinalindwa akiba yako.
2. Kinatengeneza faida ya baadaye.
3. Kinachangamsha hari ya kuongeza mapato yako.
4. Kinakupa nidhamu na uvumilivu wa kipato.

Binafsi ningemshauri mfanyakazi yoyote aliyeajiriwa na kutegemea mshahara wake, ni bora kuwekeza kwenye UTT sasa kuliko kukaa kungojea mafao ya uzeeni ili kuja kutoboa kimaisha.

Small profit but stress free and very minimal risk of loss.
 
Mkuu hizi vitu huwa naona ndio vya kufanya kwa wale ambao hatuna maarifa ya biashara ama karama. Kama risk appetite ndogo bora uweke hela huko ambapo kama una nyingi unaweza kukuta hela unayopokea kwa mwaka tu inaweza kuendesha maisha vyema tu ukalipa ada na kila kitu ukafanya huku pengine una kazi yako maisha yanaenda tu!

Uwekezaji wa Real Estate ufanye ule wa kikweli kweli yani! Upangishe makampuni au staff wa makampuni ndio utainjoy uwekezaji wa nyumba ila ile style ya kukabana kila mwezi na wapangaji ni ngumu na inaboa.
Kabisa mkuu. Mimi nafanya biashara, lakini moja tu inanitosha. Nilijaribu kufungua nyingine usimamizi ukanishinda maana hata watoto nilikua nawaona jumapili tu. Sio maisha ninayotaka.
Nawaambia watu kila siku ukiwa na 100m ukanunua kiwanja na kujenga nyumba, huwezi kupata kodi zaidi ya laki 5 kwa mwezi, sawa na 6m kwa mwaka. UTT una uhakika wa 10m minimum bila jasho. Na wanaosema nyumba ni asset, well kwenye makaratasi sawa but in real life nyumba ya 100m mtaani haiuziki kirahisi, watu wana hela ya kujenga kidogo kidogo sio kununua nyumba yote. Halafu hata kama atapatikana mwenye hela lazima aipende nyumba yenyewe na location ilipo. So kwa mimi huo ni mzigo.
Kwa UTT ukiwa na shida labda ada imepungua kam 3m hivi, unaenda unapunguza investment yako kidogo unaenda malizia shida yako. Sasa ukishajenga nyumba unafanyaje kama sio kugombana na wapangaji wakupe kodi in advance 😂
Real estate sio biashara ya pesa ndogo. Ukiwa na mzigo wa kutosha ukawa na nyumba prime areas sawa, otherwise ni shida
 
Kwakweli ni sehem nzr na sahihi sana kuliko kuweka hela bank, huku unaona trend ya ongezeko la hela yako each day, the more the deposit, the more the profit.
Je unaweza kuweka kila mwezi au ukiweka mara moja basi
 
Back
Top Bottom