Je, ni Morocco watakaovunja rekodi ya kufika Semi's?

Je, ni Morocco watakaovunja rekodi ya kufika Semi's?

Argentina wakati wanatetea taji mwaka 1990 hawakuwa wazuri na mechi ya ufunguzi walipigwa na Cameroon 1-0, Cameroon wakicheza na wachezaji 9 tu uwanjani.

Lakini ndio hivyo Argentina walicheza hadi fainali na kutolewa kwa bao la penalti feki waliyopewa Ujerumani.

Hata mwaka 1994 Italia hawakuwa wazuri baada ya kufungwa 1-0 na Ireland ktk mechi ya ufunguzi lkn walifika fainali na kutolewa kwa matuta na Brazil.

Hata mwaka 2002 Ujerumani ilikuwa na timu mbovu kabisa iliyochapwa 3-1 na Croatia kwenye makundi lakini walifika fainali na kufungwa na Brazil 2-0 kwa mabao ya Ronaldo de Lima.

Na hata Italia 2006 na Spain 2010 walianza vibaya kwa kupoteza mechi za mwanzo lakini mwisho wa mashindano waliibuka na kombe.

Kwenye kombe la dunia waga kuna maajabu sana kwa zile timu 8 zilizowahi kulitwaa hilo taji, yeyote anaweza akaibuka bingwa wakati kimpira hayuko kwenye form.

Tatizo la watanzania wengi wao hawapo kimpira, mahaba yamewazidi.
 
Kwani ufaransa ilikuwa na nini?

Asa kama senegal alimfunga ufaransa ile

Mbona morroco imekifunga kizazi cha dhahabu cha Beligimu?

Nakwambia morroco hakuna team ya kumtisha
[emoji1045] ina kizazi gan cha dhahabu? Hawa wazee au?
 
Na unaongelea Kimpira Morocco is the Best ? Statistically Senegal ndio Mabingwa wa Africa.... na kwenye ligi huenda Morocco asitoboe ila kwenye mituano Defense bora ni zaidi ya uwezo wa kufunga..., (Hapa hakuna point tatu ni unafungwa unaondoka).....
Kundi la morocco haliwezi kufanana na kundi la senegal, kumbuka belgium ni timu bora, na ipo nafasi ya pili katika ranking


FIFA ranking
Highest1 (November 2015 – March 2016, September 2018 – March 2022)
 
Kundi la morocco haliwezi kufanana na kundi la senegal, kumbuka belgium ni timu bora, na ipo nafasi ya pili katika ranking


FIFA ranking
Highest1 (November 2015 – March 2016, September 2018 – March 2022)
Hivi hapa tunaongelea nini na tunabishania nini ? Kama FIFA ranking ndio mambo yote kwanini Brazil asipewe Kombe kabisa na watu tuendelee na mengine ?

Na kwa Logic yako ya Fifa ranking timu Bora Africa ni ipi ?
 
Majibizano ni mazuri ila naomba mjibizane kwa hoja na Mimi nipate cha kusimulia banda umiza
Sasa kama hayana Hoja basi yatakuwa sio mazuri au ?

Au unamaanisha watu waweke stats na references ?, Mbona kama hizo zipo pia..., Lakini kuhusu nani atashinda ni utabiri tu ambao hata Pweza aliweza kutabiri mshindi wa 2010....
 
[emoji1045] ina kizazi gan cha dhahabu? Hawa wazee au?
Hlf kizazi chao cha dhahabu ndo kinaishia hivo, hawako bora kihivyo. Ufaransa alofungwa na senegal walikua kamili tena bingwa mtetezi.
 
Duh hivi tunaelewana lakini ?!!!

Jamaa kasema Morocco anaweza kumfunga mtu yoyote ndio nikamjibu kwenye karatasi hata Taifa Stars anaweza kufanya hivyo..., Ni kama ambavyo realistically kwa Saudi Arabia Kumfunga Argentina ni ni ngumu hata wakirudiana huenda mechi ikawa tofauti ila iliwezekana...

Au wenzangu hamjui maana ya kuwezekana ? (Mathematically hata wewe unaweza peke na familia yako unaweza kuwafunga Brazil) ingawa realistically its something else....

Na unaongelea Kimpira Morocco is the Best ? Statistically Senegal ndio Mabingwa wa Africa.... na kwenye ligi huenda Morocco asitoboe ila kwenye mituano Defense bora ni zaidi ya uwezo wa kufunga..., (Hapa hakuna point tatu ni unafungwa unaondoka).....
Hata wewe nae unakosea pia , kumbuka Morocco kwa sasa ipo chini ya kocha makini ambaye bila shaka ndiye kocha bora wa Africa kwa sasa toka kwenye vilabu yaani WALID REGRAGUI (Huyu ni master hasa kama unamchukulia easy rejea alichomfanya Al Ahly kwenye fainali.

Timu ilichoza mechi na Chile, Belgium , Canada na bado haijaruhusu bao itazame kwa umakini mkubwa , uzuri huyu jamaa ni mzoefu wa game za knock out stages so kuna kitu Morocco nahisi watafanya kikubwa sana

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Hata wewe nae unakosea pia , kumbuka Morocco kwa sasa ipo chini ya kocha makini ambaye bila shaka ndiye kocha bora wa Africa kwa sasa toka kwenye vilabu yaani WALID REGRAGUI (Huyu ni master hasa kama unamchukulia easy rejea alichomfanya Al Ahly kwenye fainali.

Timu ilichoza mechi na Chile, Belgium , Canada na bado haijaruhusu bao itazame kwa umakini mkubwa , uzuri huyu jamaa ni mzoefu wa game za knock out stages so kuna kitu Morocco nahisi watafanya kikubwa sana

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Duh !!!

Hivi aliyeleta huu Uzi ni nani na amesema nini kuhusu hili Jambo ?

Moja kutokana na Kocha mpya na kwamba alikuwa ana clean sheet tano tangia achukue hii timu ndio maana nikaleta uzi (nikimaanisha kushinda a Cup Competition hata ukiwa na Timu mbovu ukiwa na discipline na usipofungwa basi unaweza ukachukua Kombe)...

Jamaa akasema Morocco haogopi mtu na anaweza kumfunga mtu yoyote yule (jibu langu ni kwamba on paper hata Stars inaweza kumfunga mtu yoyote) hiyo ni happenstance ambayo kwenye cup competition inaweza ikatokea..., Can Morocco go all the way - Yes; Is Morocco the best team in the world - No....

Kumbuka World cup ni mechi nane tu....mtu anachukua ndoo
 
Hispania wamezidiwa leo, labda bahati tu iwabebe. Ila kimbinu wamezidiwa
 
Duh huenda Safari ikafikia Kikomo.....

Wakipenya ni either German au Spain....

Nadhani ni Bora iwe German sababu wakimfunga huyo ni either Portugal / Swiss alafu huenda ikawa France then Fainali

Ni mwendo wa discipline na Defense..., Matuta all the Way...
Like I said sio kazi kumfunga Portugal kama atapita ila huenda kwa Swiss ikawa tabu sababu na wao wapo good defensively na wana discipline....
 
What happened to Swiss defense ?!!!

Au Portugal without Ronaldo ni ngumu na haitakuwa rahisi kama Spain
 
Ah Morocco wanastahili kwa kweli heshima. Ngoja tuone Portugal kama atavunja hii rekodi. Ila jamaa back four zao wameng'ata senyenge sio kwa kukaza kule jamaa wako makini na wanajituma kwelikweli. Timu nzima inatisha.
 
Ah Morocco wanastahili kwa kweli heshima. Ngoja tuone Portugal kama atavunja hii rekodi. Ila jamaa back four zao wameng'ata senyenge sio kwa kukaza kule jamaa wako makini na wanajituma kwelikweli. Timu nzima inatisha.
Sifa zimuendee Kocha wao...., huyu atakuwa tactician mzuri...., kwa timu underdogs.... watakuwa wana discipline na wanafanya mazoezi kila mtu anajua kazi yake...

Ila sijui wakifanya kosa na kufungwa dakika ya kwanza inakuwaje sababu ukishapaki train / container mara nyingi kuliondoa inaweza ikawa tabu kidogo...

All in all huyu Kocha anajenga timu kwa kutumia strength za timu yake..., nampa sifa zote yeye...
 
Back
Top Bottom