Je, ni nini lengo la ziara ya Ghafla ya Paul Kagame hapa Tanzania 27-04-2023?

Je, ni nini lengo la ziara ya Ghafla ya Paul Kagame hapa Tanzania 27-04-2023?

Hakuna kitu ambacho ni cha moja kwa moja.Muda wakati ni mwamuzi wa mambo mengi.

Zile siasa za ubabe ubabe na uwekezaji mkubwa katika masuala ya ulinzi zinakwenda kubadilika kadri muda unavyosonga mbele.

Rwanda ina maadui wawili wakubwa ambao katika kipindi chote cha Utawala wa PAKA ameshindwa kuyadhibiti.

Adui Number moja yupo ndani.Ukabila ambao upo kwasababu za kihistoria.Bahati mbaya PAKA kaukuza na kuutukuza ukabila katika kipindi chote cha Utawala wake.Kabila lake la Tutsi ndio kila kitu huko Rwanda na kibaya zaidi anaamini sana katika himaya ya Bahima.

Tatizo la pili linazalishwa na tatizo la kwanza.PAKA ana amini makabila yote yenye asili ya Tutsi wana uhalali wa kutawala eneo lote la maziwa makuu.Alianzisha operation ya kuwatumia watutsi bila kujali wanatoka nchi gani,matokeo yake waangaza wa Tanzania au banyamulenge wa Congo wakaanza kukosa uhalali au kuaminika katika nchi zao za asili.

PAKA anajikuza sana kuliko uhalisia wa nchi yake ndogo ya Rwanda ambayo inazidiwa ukubwa wa eneo na hifadhi ya taifa ya Serengeti.Mkubwa wa hifadhi ya Serengeti ana tawala eneo kubwa kuliko nchi ya Rwanda.PAKA hawezi kuwa sawa na Rais wa Tanzania lakini hizo kelele mbwembwe utafikiri Rwanda labda ni Russia kila mahali penye ugomvi atapeleka wanajeshi wake wa kitutsi.Akienda Ulaya atasign mikataba ya kuchukua wakimbizi wakati Rwanda ni nchi ya tatu duniani kwa msongamano wa watu.


Wakati wa PAKA kuondoka unazidi kukaribia mbegu yake akiyoipanda ya ukabila ndio itakayomwondoa mapema zaidi.
Umemchambua vizuri kabisa.

Kujivimbisha kote alikokuwa akikufanya alitegemea 'sponsors'; sasa na wao wamegundua uchizi alionao na kumwambia wazi juu yake.

Yule mzee wa Hotel Rwanda kalazimishwa kumwachia huru.
 
Sasa kwanini tunakubali kuwa na watawala wasio na akili za kutosha? Makosa yale yale ya mababu zetu ya kuuza ardhi kwa kupewa ushanga na wakoloni bado tunayarudia!! Juzi juzi tu watawala wametiliana saini ya migodi mitatu na wawekezaji na kuahidiwa Fedha milioni kadhaa za kimarekani!! Je tumefanyika uchambuzi yakinifu wa thamani ya madini yatakayochimbwa na kujua kama hizo fedha na 51% shareholding kwenye hiyo migodi ni halali yetu?
Wataalam wa madini wanasema kuwa mgodi mmoja kati ya hilo mitatu kwa mwaka itatoa mara kumi ya hizo pesa walizowapa kwa hiyo migodi yote!
Zaidi ya yote maamuzi ya jinsi ya mgawanyo na kupata hiyo 51% baada ya uzalishaji hufanywa na Bodi ya hizo kampuni, je uwakilishii wa Watanzania kwenye hizo Bodi ukoje? Hayo dio mambo ya kufikiria tunapoingia kwenye mikataba na wageni!!
Kwa bahati mbaya hatujifunzi huko tulikotoka kwani tunatumia watu wale wale waliotuingiza mkenge na BARRICK GOLD kwenye Makinikia; wakina Kabudi kutengeneza mikataba mipya tukitegemea kuwa itakuwa bora kuliko ile ya BARRICK!! It is insane to use the same method as before and expect a different result!!
EeeenHeeee!
Hili tumelijadili hapa hivi juzi.

Tunahitaji viongozi "Wazalendo", siyo hawa wa uzalendo wa kuigiza. Tutaendelea kupigwa sana juu ya haya ya uhamishaji wa mali zetu kunakofanywa na hawa waliopo madarakani kutimiza matakwa yao binafsi.
 
Una taarifa za Ikulu kwamba hii ziara haijapangwa muda mrefu na imekua ghafla?
Unaweza kutuambia ughafla wake upoje? Aliamka asubuhi akasema kesho naja Tanzania?
Nahisi amesema Ni gafla kwa mantiki ya kwamba sis wananchi tumestukia tuu Pa,Ka yupo ikulu na mama. . Wakati... vice wa USA..tulijulishwa.. kila hatua za ujio wake.
 
Nahisi amesema Ni gafla kwa mantiki ya kwamba sis wananchi tumestukia tuu Pa,Ka yupo ikulu na mama. . Wakati... vice wa USA..tulijulishwa.. kila hatua za ujio wake.
Ziara nyingi tu za viongozi huwa tunajulishwa siku kadha wa kadha kabla ya ujio wao. But hii imekuwa ya haraka mno.
 
Haya hapa yanayomtisha kagame. Tuendelee tutaona mengi

 
Tumekwisha, huyu Kagame ni muuaji na dikiteita kuwahi kuwepo Africa, sasa kaja kupandikiza udikiteita. Twafa, omba tusirudi enzi za Jiwe.
Kuna nchi chini ya huo udikteta zimefanya mambo ambayo kwetu bado ni ndoto ila sie tusionufaika na udikteta wala demokrasia ndio kujifanya tunaupinga huo udikteta kama vile tumefaidika na hiyo demokrasia.
 
Ziara nyingi tu za viongozi huwa tunajulishwa siku kadha wa kadha kabla ya ujio wao. But hii imekuwa ya haraka mno.
Iko hivi: remote na spika haziendani. DJ kaamua kupita ya mkato na ku rap mwenyewe.

Angetoa taarifa, huenda wateja wasingelipa kiingilio.
 
humu hakuna wachangiaji wa mada naona wachangiaji waliotoka simba na yanga wamevamia mada hii wacha nitoke
 
Iko hivi: remote na spika haziendani. DJ kaamua kupita ya mkato na ku rap mwenyewe.

Angetoa taarifa, huenda wateja wasingelipa kiingilio.
Sijaelewa ulichoongea hapa. Mambo ya DJ yametoka wapi? Hapa DJ ni nani na anayetoa kiingilio ni nani?
Be open hatutaki mafumbo ambayo hayana ulazima wowote.
 
Wenye akili watakuwa wamenielewa.
Kwahiyo unaandika kwaajili ya watu hao unaowaita wenye akili? Inamaana gani sasa kuandika kwenye public? Sasa tukikuita wewe kuwa unaandika kama kichaa tutakuwa tumekosea?

Maana kuna njia ya kuwatumia watu wachache unaowalenga kwa kuandika PM. Sasa utajionaje kuwa unawaandikia wenye akili wakati wewe hizo akili hauna?
 
Kuna nchi chini ya huo udikteta zimefanya mambo ambayo kwetu bado ni ndoto ila sie tusionufaika na udikteta wala demokrasia ndio kujifanya tunaupinga huo udikteta kama vile tumefaidika na hiyo demokrasia.
UDIKTETA ni UHARAMIA tu. Kwa dunia iliyoendelea hauna nafasi. Unamsifu Kagame amefanya makubwa bila kuangalia namna alivyowafanya watu wake waishi kama MAZOMBIE tu. Yaani kuna mtu mmoja wa kuamua Rwanda iende vipi, ukidadisi unakufa.

Pili unatamani kusema Kagame kaijenga Rwanda kwa hiyo barabara moja Ķigali na vigorofa mnavyosema vinaifanya Kigali iwe jiji safi. Lakini unasahau kuwa amefanya yote hayo kupitia DESTABILISATION anayoifanya DRC kupitia M23 ambayo inamuwezesha kuiba madini ya Congo.

Namna ilivyotokea Sudan baada ya Omar Bashir, ndivyo itakavyotokea Rwanda atakapodondoka huyu mtu mrefu kama rula. Rwanda italipuka tena kama mwaka 1994

Sisi kwetu HATUKUTAKA hayo yatutokee tulimuomba Mungu akatuondolea DIKTETA Magufuli mwaka 2021 ambaye alipata mafunzo kwa Kagame mara baada ya kutawazwa kuwa Rais mwaka 2015
 
UDIKTETA ni UHARAMIA tu. Kwa dunia iliyoendelea hauna nafasi. Unamsifu Kagame amefanya makubwa bila kuangalia namna alivyowafanya watu wake waishi kama MAZOMBIE tu. Yaani kuna mtu mmoja wa kuamua Rwanda iende vipi, ukidadisi unakufa.

Pili unatamani kusema Kagame kaijenga Rwanda kwa hiyo barabara moja Ķigali na vigorofa mnavyosema vinaifanya Kigali iwe jiji safi. Lakini unasahau kuwa amefanya yote hayo kupitia DESTABILISATION anayoifanya DRC kupitia M23 ambayo inamuwezesha kuiba madini ya Congo.

Namna ilivyotokea Sudan baada ya Omar Bashir, ndivyo itakavyotokea Rwanda atakapodondoka huyu mtu mrefu kama rula. Rwanda italipuka tena kama mwaka 1994

Sisi kwetu HATUKUTAKA hayo yatutokee tulimuomba Mungu akatuondolea DIKTETA Magufuli mwaka 2021 ambaye alipata mafunzo kwa Kagame mara baada ya kutawazwa kuwa Rais mwaka 2015
Point yangu ni kwamba zipo nchi ambazo zimefanya makubwa zikiwa chini ya udikteta ila sie tumekazana kuupinga huo udikteta ila hadi sasa hakuna lolote tunaloweza kujivunia kwa hiyo demokrasia.
 
Mnapenda kumkuza na hizo consipiracy theories zenu. Kama kiongozi yoyote anatafuta fursa kwa ajili ya maendeleo ya taifa lake. Ana matatizo yake kama walivyo viongozi wengine wa kiafrika.

Mtu yupo bongo hajawahi hata kufika Rwanda au kuwa na jamaa wenye asili yao anakuja kutapika uharo hapa.

Wanyarwanda wanaishi vizuri na kwa amani, PK amezima upuuzi wa ukabila. Lile taifa lazima liende kwa mkono wa chuma bila hivyo migogoro itakua kama Burundi. Kama ni makosa anayo kama viongozi wengine wa kiafrika.
 
Back
Top Bottom