Je, ni sahihi kumtambulisha Kassim Majaliwa kuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu?

Je, ni sahihi kumtambulisha Kassim Majaliwa kuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu?

Nawauliza watu wa itifaki kama ni halali kwa kipindi hiki cha mpito kumtambulisha Waziri mkuu wa awamu ya 5 Mh Kassim Majaliwa kama Waziri Mkuu Mstaafu.

Naomba majibu Tafadhali.

Maendeleo hayana vyama!
Soma hii sehemu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (kama ilivyofanyiwa marekebisho hadi 2005) inavyosema hasa kifungu kidogo cha 3(a). Huenda ukapata jibu.


SEHEMU YA TATUWAZIRI MKUU, BARAZA LA MAWAZIRI NA SERIKALI
Waziri Mkuu


51(1) Kutakuwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais kwa kufuata masharti ya ibara hii na ambaye kabla ya kushika madaraka yake ataapa mbele ya Rais kwa kiapo kinachohusika na kiti cha Waziri Mkuu kitakachowekwa na Bunge.
(2) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile ndani ya siku kumi na nne, baada ya kushika madaraka yake, Rais atamteua Mbunge wa kuchaguliwa kutoka katika Jimbo la Uchaguzi anayetokana na chama cha siasa chenye Wabunge wengi zaidi Bungeni au kama hakuna chama cha siasa chenye Wabunge wengi zaidi, anayeelekea kuungwa mkono na Wabunge walio wengi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, naye hatashika madaraka hayo mpaka kwanza uteuzi wake uwe umethibitishwa na Bunge kwa azimio litakaloungwa mkono na kura za Wabunge walio wengi.
(3) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, Waziri Mkuu atashika kiti cha Waziri Mkuu hadi- (a) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika kiti chake; au (b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka; au (c) siku atakapojiuzulu; au (d) siku Rais atakapomteua Mbunge mwingine kuwa Waziri Mkuu; au (e) atakapoacha kushika kiti cha Waziri Mkuu kwa mujibu wa masharti mengineyo ya Katiba hii.
 
Niko nje ya Mada kidogo, Shein amekuwa addressed kama Makamo wa Rais mstaafu na Rais mstaafu wa Zanzibar hilo sio shida

Je linapokuja swala la stahiki zake kama mstaafu atapewa zote kama ambavyo ametambulishwa ama kuna moja itaaachwa?
 
Niko nje ya Mada kidogo, Shein amekuwa addressed kama Makamo wa Raisi mstaafu na Raisi mstaafu wa Zanzibar hilo sio shida

Je linapokuja swala la stahiki zake kama mstaafu atapewa zote kama ambavyo ametambulishwa ama kuna moja itaaachwa?
Anapewa ile ya cheo alichostaafia.

Kwa mfano mzee Malecela aliwahi kuwa makamu wa Rais lakini anatambulika kama Waziri mkuu mstaafu tu!
 
Nawauliza watu wa itifaki kama ni halali kwa kipindi hiki cha mpito kumtambulisha Waziri mkuu wa awamu ya 5 Mh Kassim Majaliwa kama Waziri Mkuu Mstaafu.

Naomba majibu Tafadhali.

Maendeleo hayana vyama!
Nanukuu "SAA 72 zijazo Lissu atakuwa Rais na mimi Waziri mkuu" chandimu bwana hamnaga dogo!
 
Kwa ujumla hauna Waziri Mkuu mstaafu Tanzania. Hakuna Waziri yeyote aliyeondoka madarakani kwa kustaafu Bali waliondoka kwa muda wao kuisha. Kwa kingereza they are former Prime Minister and not Retired PMs.
Kwahiyo nini tofauti ya former President/Prime minister na retired President/Prime minister?

Naomba tafsiri ya kiswahili tafadhali.
 
Soma hii sehemu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (kama ilivyofanyiwa marekebisho hadi 2005) inavyosema hasa kifungu kidogo cha 3(a). Huenda ukapata jibu.


SEHEMU YA TATUWAZIRI MKUU, BARAZA LA MAWAZIRI NA SERIKALI
Waziri Mkuu


51(1) Kutakuwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais kwa kufuata masharti ya ibara hii na ambaye kabla ya kushika madaraka yake ataapa mbele ya Rais kwa kiapo kinachohusika na kiti cha Waziri Mkuu kitakachowekwa na Bunge.
(2) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile ndani ya siku kumi na nne, baada ya kushika madaraka yake, Rais atamteua Mbunge wa kuchaguliwa kutoka katika Jimbo la Uchaguzi anayetokana na chama cha siasa chenye Wabunge wengi zaidi Bungeni au kama hakuna chama cha siasa chenye Wabunge wengi zaidi, anayeelekea kuungwa mkono na Wabunge walio wengi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, naye hatashika madaraka hayo mpaka kwanza uteuzi wake uwe umethibitishwa na Bunge kwa azimio litakaloungwa mkono na kura za Wabunge walio wengi.
(3) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, Waziri Mkuu atashika kiti cha Waziri Mkuu hadi- (a) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika kiti chake; au (b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka; au (c) siku atakapojiuzulu; au (d) siku Rais atakapomteua Mbunge mwingine kuwa Waziri Mkuu; au (e) atakapoacha kushika kiti cha Waziri Mkuu kwa mujibu wa masharti mengineyo ya Katiba hii.
Nadhani jibu lipo hapa ila je, anapewa stahiki zake kama waziri mkuu mstaafu?
 
Nawauliza watu wa itifaki kama ni halali kwa kipindi hiki cha mpito kumtambulisha Waziri mkuu wa awamu ya 5 Mh Kassim Majaliwa kama Waziri Mkuu Mstaafu.

Naomba majibu Tafadhali.

Maendeleo hayana vyama!
Kwakuwa bado haijulikani kama Rais Magufuli atampendekeza tena au ndiyo imetoka hiyo kuanza Kuitwa 'Mstaafu' si mbaya japo najua atarudi nae.
 
Waziri mkuu aliyemaliza muda wake.
Waziri mkuu wa awamu iliyomaliza muda wake
 
Lakini bado wanaitwa makamu wa Rais na naibu spika. Sijui kwanini katiba kuna mahali inakuwa kimya.
Nimeangalia tena ibara ya 50, kama Makamu wa Rais tofauti hajaapishwa, yule wa awali anaendelea kuwa Makamu wa Rais.

Yani hata kama Tundu Lissu angeshinda, Magufuli angekuwa Rais na Samia angekuwa Makamu wa Rais mpaka Lissu na Makamu wake wanapoapishwa.

Hii ni kuzuia "power vacuum".

Nchi haitakiwi kukaa hata siku moja bila Rais na Makamu wake.
 
Nimeangalia tena ibara ya 50, kama Makamu wa Rais tofauti hajaapishwa, yule wa awali anaendelea kuwa Makamu wa Rais.

Yani hata kama Tundu Lissu angeshinda, Magufuli angekuwa Rais na Samia angekuwa Makamu wa Rais mpaka Lissu na Makamu wake wanapoapishwa.

Hii ni kuzuia "power vacuum".

Nchi haitakiwi kukaa hata siku moja bila Rais na Makamu wake.
Umeiweka vizuri sana mkuu.
TL alijielekeza vibaya na kuwaamisha wafuasi wake tarehe 28 ndio mwisho wa Urais wa JPM.
Huo ulikuwa uwongo mweupe. Maana hata angeshinda na kutangazwa, Urais unaanza pale mtu anapokula kiapo.

JPM alithibitika kushinda Urais October 29, 2015.
Madaraka yake yalianza rasmi Nov 5, 2015.
JK aliendelea kuwa Rais mpaka Nov 5 2015 wakati anaingia uwanjani.

Hili ni jambo la kikatiba na kiutawala ambalo elimu ya uraia inabidi itolewe sana sana
 
Back
Top Bottom