Je, ni sawa kwa Wanajeshi kurekodi video kama hizi na kuzisambaza mtandaoni?

Je, ni sawa kwa Wanajeshi kurekodi video kama hizi na kuzisambaza mtandaoni?

Huku ndiko tulikofikia mtu kurekodiwa anafanyishwa mazoezi ni kumdhalilisha ili akirekodiwa akikata mauno nusu uchi au vigodoro ni au akifanya ngono ni sifa
Mkuu hao wa nusu uchi huwa wanajirekodi wenyewe, au hata wakirekodiwa huwa ni kwa ridhaa yao, lazima ujue kutofautisha
 
Mkuu mbona umeandika hivi:
"Nimekutana na video hii mtandaoni, ambako huyu 'kuruta' (kama sijakosea) anapewa amri ya kugeuka kulia na kushoto, kijana huyo anafata maagizo aliyopewa huku anayetoa maagizo na wengine wakisikika wakicheka.

Nini dhumuni la kurekodi video hizi mpaka kufikia hatua ya kuzirusha mtandaoni?.........."

Kwa maana hiyo wewe umeamini hicho kitu ni kweli na ukachangia kukisambaza kutoka huko ulikokiona hadi ukakileta hapa kwa maGT - Jf.
Nimekuwekea visababu hivyo ili kukurudisha kwenye ukweli usiendelee kuhadaiwa.
Hapo hakuna kosa lolote kwani maigizo hufanywa na yeyote anayejisikia kufanya hivyo ( bure au kwa malipo)na wala sio lazima awe na official page.
Siwezi kusaidia jambo hewa. Wewe mwenyewe unajua jinsi ilivyo vigumu kuchukua picha ndani ya eneo la Jeshi lakini bado unaamini jambo hilo limerekodiwa Oljoro JKT.
Ni hayo tu.
Aaaah Mkuu, usiniambie hii ndiyo video ya kwanza ya mtindo kama huu kuiona mtandaoni, msema ukweli mpenzi wa Mungu
 
Aaaah Mkuu, usiniambie hii ndiyo video ya kwanza ya mtindo kama huu kuiona mtandaoni, msema ukweli mpenzi wa Mungu
Ni kweli sijaona video ya mtindo huu; lakini hilo halinizuii kuihoji Ukweli au Uhalali wake.
 
Jielimishe kidogo tu uache kutoa maoni kama haya, na wewe kama Dr. inabidi uwe muelewa zaidi kuhusu husu sababu unadeal na taarifa za watu pia. Haijalishi lengo lake wala sisi tunafikiria nini, kitendo cha kumrekodi bila ridaa yake na kurusha video hiyo mtandaoni ni kosa kwa Mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi na For Your Information imeanza kufanya kazi tokea May 2023.

Nakushauri ukaisome na uelewe vizuri, kwa comment hii ni dhahiri kuna uvunjifu mkubwa wa sheria upande wenu.
Tanzania uhuru umezidi ,Kisheria ni kosa kumchukua mtu video bila idhini yake
 
unashaangaa kupigwq picha jeshini watu wanapigwa hadi risasi kwa hizi fasi za kijeda unaleta masuala ya civil rights kwa makamanda
Una matatizo makubwa sana kichwani kwako.
Hivi mama yako mzazi angerekodiwa video wakati alipokuwa anajifungua ujauzito wako wewe huko hospitalini alikoenda kujifungua na Kisha video hiyo ingewekwa hadharani humu mitandaoni na kuonekana dunia nzima wewe ungejisikiaje??? Je, Ungefurahia kuiona video hiyo wakati huu ukiwa umekuwa mtu mzima??
 
Una matatizo makubwa sana kichwani kwako.
Hivi mama yako mzazi angerekodiwa video wakati alipokuwa anajifungua ujauzito wako wewe huko hospitalini alikoenda kujifungua na Kisha video hiyo ingewekwa hadharani humu mitandaoni na kuonekana dunia nzima wewe ungejisikiaje??? Je, Ungefurahia kuiona video hiyo wakati huu ukiwa umekuwa mtu mzima??
apo tunaongelea mafunzoni jeshini kiongozi ni kipi usichokielewa kwamba sheria zako zote unazozijua hazi apply jeshini wao wana martial laws kama unataka kufurah ingia YouTube wana chanel yao uone makuruta wanavyolia mpaka wanatoa kamas we utakua mgeni sana hapa duniani
 
apo tunaongelea mafunzoni jeshini kiongozi ni kipi usichokielewa kwamba sheria zako zote unazozijua hazi apply jeshini wao wana martial laws kama unataka kufurah ingia YouTube wana chanel yao uone makuruta wanavyolia mpaka wanatoa kamas we utakua mgeni sana hapa duniani
Maadili ya Kutunza Siri yapo kwenye taaluma zote, Sheria za kutunza Siri zipo na zina-apply kwa watu wote, uwe katika shughuli za kiraia au kwenye kazi za kijeshi
. Na kwa bahati mbaya zaidi, kwenye Majeshi kuna Sheria Kali zaidi za Kutunza Siri za Jeshi au Siri za Nchi, hili ni takwa la lazima kwa Majeshi yote hapa duniani. Na ndio maana Wanajeshi ni LAZIMA WAAPISHWE Viapo, ikiwamo na KIAPO CHA KUTUNZA SIRI.
 
Wakuu kwema?

Nimekutana na video hii mtandaoni, ambako huyu 'kuruta' (kama sijakosea) anapewa amri ya kugeuka kulia na kushoto, kijana huyo anafata maagizo aliyopewa huku anayetoa maagizo na wengine wakisikika wakicheka.

Nini dhumuni la kurekodi video hizi mpaka kufikia hatua ya kuzirusha mtandaoni? Anayerekodiwa ameridhia? Na hii sio mara ya kwanza kukutana na video kama hizi mtandaoni, za hawa wanafunzi wanaokwenda jeshi kwa mujibu wa sheria kurekodiwa katika matukio mbalimbali.

Huu ni udhalilishaji wa utu wake, tayari watu washaanza kutoa maoni mbalimbali juu ya muonekano wake, maumbile na kadhalika, kwa hali tu ya kawaida hakuna mtu angependa kurekodiwa katika hali hiyo na video hiyo irushwe kwa kila mtu kuona.

Hii sio sawa, kwanza ukipewa amri hapo lazima ufate, usipofata ni kukaidi na udhabu unapewa. Kwanini tunahalalisha udhalilishaji huu uendelee kutokea na kuonekana na kawaida? Wanajeshi wapo juu ya Sheria? Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi wao haiwahusu?

Aliyechukua video hii awajibishwe, Jeshi kama chombo cha ulinzi wanatakiwa kuwa mfano kwenye kufata sheria na sio kuwa wa kwanza kwenda kinyume na kudhalilisha utu wa watu.

Kutoka kwenye comments za video hiyo anayesikika akitoa amri ni Afande Sese, JKT Oljoro.

Sheria iwe msumeno, sio ikate kwetu tu halafu kwao kuwe butu.

Ipo siku tutaona wagonjwa wakipasuliwa thieta au kuzalishwa mtandaoni
 
Raia nawapenda sana , hapana kosa hapo acheni kukuza mambo jaribuni kusoma vifungu vya sheria za jeshi na za kiraia ila mathalani mjue kutofautisha neno muktadha na mazingira kwa minajiri ya jeshini au kikosini na uraiani bila kusahau , sheria ya mtandao hasa upande wa jeshini iko uchi kiasi chake hivyo ukija kichwa kichwa wewe raia hautaeleweka maana sheria zenu ni huko uraiani sio jeshini .

Sijaeleweka , jambo wakuu ?? Nisiulizwe chochote niko sawa .

Note : Shemeji yenu yuko hapa naomba mtu yeyote anijibu kwa staha na kwa logic kwenye komenti yangu ili asinione kilaza maana hatuna hata mwezi ni penzi jipya.
 
Raia nawapenda sana , hapana kosa hapo acheni kukuza mambo jaribuni kusoma vifungu vya sheria za jeshi na za kiraia ila mathalani mjue kutofautisha neno muktadha na mazingira kwa minajiri ya jeshini au kikosini na uraiani bila kusahau , sheria ya mtandao hasa upande wa jeshini iko uchi kiasi chake hivyo ukija kichwa kichwa wewe raia hautaeleweka maana sheria zenu ni huko uraiani sio jeshini .

Sijaeleweka , jambo wakuu ?? Nisiulizwe chochote niko sawa .

Note : Shemeji yenu yuko hapa naomba mtu yeyote anijibu kwa staha na kwa logic kwenye komenti yangu ili asinione kilaza maana hatuna hata mwezi ni penzi jipya.
Kwa hiyo hata huyo mkeo uliyenaye akienda kujifungua kwenye hospitali ya Jeshi akirekodiwa video huko wakati anajifungua mbele ya Madaktari/Wakunga Wanajeshi Wanaojifunza kazi na kisha video yake ikiwekwa mitandaoni ni sawa tu eti kwa sababu yuko katika Hospitali ya Jeshi inayozingatia Sheria za Jeshi????? Au unamaanisha nini??
 
Huku ndiko tulikofikia mtu kurekodiwa anafanyishwa mazoezi ni kumdhalilisha ili akirekodiwa akikata mauno nusu uchi au vigodoro ni au akifanya ngono ni sifa
Ebu soma ulichoandika na ukitafakari , upo timamu kwel ?
 
Hakuna Kosa hapo..
Hakuna Mtu anayejua Lengo la mchukuaji Video zaidi ya mchukuaji mwenyewe..

HIsia za Muonaji Sio hisia za mchukuaji..
Kwahyo Hakuna kosa hata kidogo..

Kisheria Na wala Ethically labda kama una Mada nyingine
halaf ww ndo unakuja kuwa kiongoz baadae , hahaa waafrika mpk tustaraabike ndo tutapata viongoz bora , yaan kwa akili yako unahisi hatokuja kuwa na familia baadae ? je watoto wake watajisikiaje ? Je aliridhia kurekodiwa ? unajuwa kosa la kuharibu privacy ya mtu ? je kuna umuhimu gan kumrekodi kwanza ? pili kuna umuhimu gan kusambaza video ulizorekodi ? TUJIFUNZE KUWAHESHIMU WENGINE BILA KUJALI UMRI , CHEO , KABILA , DINI AU JINSIA AU ELIMU , MAANA UPANDE MWINGINE ANAEZA KUWA MTU ANAEHESHIMIKA SANA , UNAEZA UKAONA NI KITU KDG ILA KIKAMUATHIRI KISAIKOLOJIA MAISHA YAKE YOTE
 
Back
Top Bottom