Je, niolewe naye? Baba yake alizaa na Mama yangu

Sasa huyo dadako na mumeo wataitanaje? Shemeji au kaka na dada? Mie sikushauri uolewe nae manake ni kakako pia.
 
Mimi nafikiri kwa kuwa mama yako alishawahi kuzaa na baba yake huyo jamaa,hapo mnakuwa mmeunganishwa kama ndugu,kwani mdogo/dada yako aliyezaliwa toka kwa baba yake na huyo jamaa ni ndugu yake/half blood na yule jamaa na wewe pia una 1/2 blood na ndugu yako so ki-maadili si busara wewe kuoana na huyo jamaa labda kama mngekuwa hamjuani.
 
Yaani naona unataka kuolewa kwenye familia isiyo familia kamili.

Sasa wewe na yeye wote familia zenu zimejaa drama sana kwanini usitafute mwanaume anayetokea katika familia iliyotulia ili watoto wako nao wakue kitofauti nawe.

Duh embu achana nae huyo maana mtaishia kama wazazi wenu
 

Hapo kwenye red, baba B ni nani? umenichanganya! inakuwa kama vile baba B ni babu yao A na C! ndio hivyo au vipi?
 
Sasa huyo dadako na mumeo wataitanaje? Shemeji au kaka na dada? Mie sikushauri uolewe nae manake ni kakako pia.


Familia yangu na yake hazijuani kabisa na zina majina na malezi na historia tofauti. Kama nilivyoeleza A na C wamekutana hivi karibuni ukubwani tu.
 

Unaweza kunifafanulia Kimaadili ya namna gani?
 

Sasa jamani ni Drama zipi hizo tena? Kwani familia nyingine zilizotulia zikoje?

Kuhusu kutafuta, naamini ndoa inapangwa na Mungu. Nitatafutia wapi huyo Mwanaume na vipi?
 

Una visa wewe dada......!!

Hivi kwa maelezo hayo...ngoma bado nzito katika suala lipi tena??

Halafu hebu nisaidie...hivi moyo wako unapodunda unakueleza nini????....Yes, Yes, Yes ...au No, No, No.....????

Babu DC!!
 
Una visa wewe dada......!!

Hivi kwa maelezo hayo...ngoma bado nzito katika suala lipi tena??

Halafu hebu nisaidie...hivi moyo wako unapodunda unakueleza nini????....Yes, Yes, Yes ...au No, No, No.....????

Babu DC!!

Moyo unadunda YES mara kisha NO mara moja.

Babu kama hoja zinavyokingana hapa jamvini na mimi ndivyo ninavyochanganyikiwa.

Lakini nampenda sana Brother. Ni "Bonge la Bwana" haaaa haaaa
 
Moyo unadunda YES mara kisha NO mara moja.

Babu kama hoja zinavyokingana hapa jamvini na mimi ndivyo ninavyochanganyikiwa.

Lakini nampenda sana Brother. Ni "Bonge la Bwana" haaaa haaaa

Ngonja nikusaidie kidogo kuweka hitimisho.....

Lakini nampenda sana Brother. Ni "Bonge la Bwana" haaaa haaaa[

Kilichobaki muulize huyo bwana naye anasemaje...!!
 

OK. We have A, B, C, and let call u D, your mom E


so. B and E make C
A and C come from B
C and D come from E

So what is relation btn D, A, B
D, A, E

D = only to E
A = only to B

so: A is not equal to D

A and D are not equal Genetically
There is no any biological, social, culture or belief conflict if they marry


for christian read Genesis 28:2 you can read all story to chapter 30.
 
Dada kupenda ni ugonjwa ambao hauponi mpaka umetimia ni sawa na kuwa njuka, huponi mpaka umekuwa form two, chamsingi hapo washirikishe watu wazima kwani kwenye wakubwa hakuharibiki kitu, lkn NENO LA MUNUG lipewe nafasi kubwa sana kwani siku za usoni yakitokea mabaya utalaumiwa lkn kama humkosei Mungu wa kweli na Yesu kristo mwana wa mungu basi Rhuksa, kula kasa japo inaua wakati mwingine.
 
Akati mnaanza kupigana sound kwanini hamkujiuliza hayo maswali kwanza?
Acha unafiki we binti.
Ningekua nakujua ningekucharaza mboko kwanza!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…