Je, Rais Samia Suluhu ndo Deng Xiaoping wa Tanzania?

Je, Rais Samia Suluhu ndo Deng Xiaoping wa Tanzania?

Duniani ni wawili wawili! Wewe huamini ilo?
Wawili wawili ni mtu na mkewe. Sivyema MTU akifanya Jambo afrika mnatafuta wa huko nje wakumlinganishia, huo niutumwa wa kifikra...hatufanani nao kifikra,kitabia,kimazingira,kiimani,kihistoria,kijiografia hata kirangi.
 
K
Wawili wawili ni mtu na mkewe. Sivyema MTU akifanya Jambo afrika mnatafuta wa huko nje wakumlinganishia, huo niutumwa wa kifikra...hatufanani nao kifikra,kitabia,kimazingira,kiimani,kihistoria,kijiografia hata kirangi.
wa iyo kulinganisha watu ni utumwa? Huko shule ulisomea ujinga?
 
Amani iwe nanyi wadau

Leo ninakuja na Swali hili, Je, Rais Samia Suluhu Hassan ndo Deng Xiaoping wa Tanzania?

Kwa wale msiojua Deng Xiaoping ni Rais wa China aliyechukua usukani wa Uongozi wa China baada ya kifo cha Rais wa Kwanza wa China Mao Zedong. Mao Zedong alijulikana kwa wachina kama Rais mwenye msimamo mkali usioyumba ambaye hakupatana na Marekani na nchi za Magharibi. Aliiongoza China Kwa mkono wa Chuma ila katika kipindi chake China ilikuwa nchi yenye uchumi mbovu sana kutokana na Sera zake za kukataa uwekezaji kutoka nje na kugombana na nchi za magharibi.

Kwa wachina wengi pamoja na kumuheshimu sana Mao ila wanamchukulia Deng Xiaoping Kama Baba wa Mapinduzi ya Kiuchumi ya China. Hii ni Kwa sababu Deng Xiaoping ndo mtu aliyekuja kutengeneza China yenye siasa za kikomunist Ila yenye uchumi imara wa kibepari ulioongozwa na msemo wake “It doesn’t matter if a cat is white or black , as long as it catches a mice, it’s a good cat”

Kwa wasioelewa kimombo Deng Xiaoping alikuwa anamaanisha haijalishi paka ni mweupe au mweusi Ila ingawa anakamata panya basi huyo ni paka mzuri

Sera hii ya Deng Xiaoping ndo ilisababisha China kuanza kukaribisha uwekezaji mkubwa kutoka Magharibi ulioingiza fedha na mitaji mikubwa nchini China na hatimaye Leo hii China ni Taifa la pili kwa kuwa na uchumi mkubwa na maendeleo duniani na inasemekana ndani ya muda mchache atachukua nafasi ya kwanza na kuizidi Marekani.

Jana nimetoka kuongea na rafiki yangu ambaye ni mkurugenzi wa moja ya mabenki hapa nchini na ameniambia kweli sasa biashara imeanza kupaa. Wiki iliyo pita nilikuwa Mwanza na Arusha na kote wafanyabiashara wa ma hoteli wanasema biashara imeanza kuja juu sana saivi

Leo Hii ninapoandika huu uzi Kuna Rafiki yangu mwingine ameniambia Kuna wawekezaji wamekuja na wana mtaji wa pesa ndefu wameanza taratibu za kufanya uwekezaji wao hapa Tanzania.

Swali langu kwenu nyie wadau leo ni Je Rais Samia Suluhu Hassan ndo Deng Xiaoping wa Tanzania???

Uzi huu nitaufufua 2030 Inshallah tukiwepo Rais Samia akiwa anamaliza Urais wake( hapa naamini Chama chake kitampitisha kugombea tena 2025-2030

Muwe na jioni njema wanabodi!!
Of course kwenye uchumi mambo yatanoga ila kwenye siasa ataamua yeye afuate mambo ya kukandamiza upinzani au auende Katiba mpya.
 
Mungu atupe uzima. Kwa niliyoyasikia ikifika 2030 tutaufufua huu uzi.
Kwenye uchumi atafaulu Sana kwa sababu yeye pia ni mfanyabiashara kwa hiyo anaamini kwenye uchumi wa soko.

Unadhani alipisema tv yake inakula hasara alipenda? Uchumi ukichanganya vyombo vya habari vinanufaika kwa matangazo.

Nakumbuka kabla ya 2015 taa za mijini zilikuwa zinapambwa na matangazo ya biashara na ilikuwa dili saizi ziko tupu hakuna wa kugusa maana uchumi umeanguka Sana.
 
Umesema vyema kuhusu Deng ku crack down Democracy. Ila huoni Samia ameendeleza katazo la mikutano ya hadhara ya kisiasa? Kuna tofauti gani hapo???

Juzi tu nimeona vikao vikirushwa tbc vya wadau wakianza kutoa maoni juu ya kubadili mtaala wa Elimu Tanzania. Je huoni Samia anatembea humo humo???

Umesikia mipango yake na alivyoanza kufanya juu ya uwekezaji ili kukuza ajira na kuleta maendeleo? Huoni nae anatembea mule mule kwa Deng The Great??
Mimi ukitaka nikuchukie uje na sera zako za kipumbavu za ujamaa na kutegemea serikali kila kitu ndio maana nilimchukia mwendazake nakuona ni mtu mjinga sana, Duniani kote ujamaa ulishafeli yeye akaanza kuleta uchumi ukaporomoka akaanza kupora pesa za watu.

Mama hana ule ujinga na ujuha,kwa mda mfupi wizara zote mama zimepata mafungu ya uhakika kilio cha Tarura kimepatiwa ufumbuzi,maji na sekta ya Elimu vyote ameviweza kwa mda mfupi.

Kitu kikubwa ambacho afanye mwaka ujao ni kupunguza VAT kutoka 18% hadi 10-12% hapa biashara nyingi zitafunguka,atapata kodi nyingi na demand itakuwa kubwa mwisho wa siku itastimulate uchumi Sana.
 
Mimi ukitaka nikuchukie uje na sera zako za kipumbavu za ujamaa na kutegemea serikali kila kitu ndio maana nilimchukia mwendazake nakuona ni mtu mjinga sana, Duniani kote ujamaa ulishafeli yeye akaanza kuleta uchumi ukaporomoka akaanza kupora pesa za watu.

Mama hana ule ujinga na ujuha,kwa mda mfupi wizara zote mama zimepata mafungu ya uhakika kilio cha Tarura kimepatiwa ufumbuzi,maji na sekta ya Elimu vyote ameviweza kwa mda mfupi.

Kitu kikubwa ambacho afanye mwaka ujao ni kupunguza VAT kutoka 18% hadi 10-12% hapa biashara nyingi zitafunguka,atapata kodi nyingi na demand itakuwa kubwa mwisho wa siku itastimulate uchumi Sana.
Msumari wa VAT ndo unaenda kumaliza kila kitu
 
Kuna wawekezaji wamekuja na wana mtaji wa pesa ndefu wameanza taratibu za kufanya uwekezaji wao hapa Tanzania.
Mama akiendelea kukaza shingo kuhusu katiba mpya hawa wawekezaji watakimbia ama watakimbizwa
 
Kwenye uchumi atafaulu Sana kwa sababu yeye pia ni mfanyabiashara kwa hiyo anaamini kwenye uchumi wa soko.

Unadhani alipisema tv yake inakula hasara alipenda? Uchumi ukichanganya vyombo vya habari vinanufaika kwa matangazo.

Nakumbuka kabla ya 2015 taa za mijini zilikuwa zinapambwa na matangazo ya biashara na ilikuwa dili saizi ziko tupu hakuna wa kugusa maana uchumi umeanguka Sana.
Mie hali ilianza kunishtua mwaka 2018. Mjini kampuni nyingi zilianza kupunguza wafanyakazi. Nyingine zikaanza kubana matumizi. Posta nikaanza kuona inakufa, Quality Centre na Quality Plaza ndo hadi zilinitoa machozi maana pale ni maelfu ya watu walipoteza ajira.
 
Mama akiendelea kukaza shingo kuhusu katiba mpya hawa wawekezaji watakimbia ama watakimbizwa
Fuatilia siasa za Singapore alafu Njoo tena urudi humu. Kwenye ubabe wa kisiasa kunaweza kuwa na wawekezaji wengi tu ili mradi ubabe wenu wa kisiasa hauathili uwekezaji wao
 
Back
Top Bottom