Je, Scholarship ni mbinu ya kutengeneza Vibaraka hasa wa Kisiasa?

Je, Scholarship ni mbinu ya kutengeneza Vibaraka hasa wa Kisiasa?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
JE SCHOLARSHIP NI MBINU YA KUTENGENEZA VIBARAKA WA KISIASA?

Anaandika Robert Heriel.

Scholarship inaweza kuwa na maana nyingi, mojawapo ni kumsaidia mtu/mwanafunzi kirasilimali aweze kupata elimu Fulani; Rasilimali hiyo inaweza kuwa Fedha, au mahali pa kuishi(makazi), au chakula, au vitendea kazi vya kujifunzia.

Mara nyingi kama zote Scholarship hutolewa Kwa sababu kadhaa, zipo sababu za wazi na zile sababu za siri/nyeti ambazo mtoa scholarship hazitaji Mwanzoni.

Zipo scholarship zinazotolewa na Makundi Yafuatayo;
1. Mtu binafsi
2. Kampuni au shirika
3. SERIKALI

Mtu binafsi Kama Mimi na Wewe tunaweza kutoa scholarship Kwa wanafunzi wengine. Hata hivyo hatuwezi kukataa ukweli kuwa Scholarship haitolewi burebure.

Wapo watu waliopewa Scholarship wakasome ili waje kuoa/kuolewa na mtoto wa mtoa Scholarship. Wengine hutoa scholarship Kwa kusomesha watoto Yatima lakini katika hao Yatima wapo ambao baadaye hupewa majukumu Fulani huko mbeleni wakishafanikiwa kimasomo, huingizwa kwenye aidha mambo ya Siasa, au kuajiriwa katika sekta nyeti ili walinde maslahi ya waliowasomesha. Hata hivyo si lengo langu Kueleza scholarship za watu binfasi.

Pia makampuni, taasisi na mashirika makubwa hutoa scholarship Kwa watu wake Kwa lengo la kuimarisha future ya kundi husika.
Zipo taasisi za Kidini, hutoa scholarship na kuhakikisha zinapenyeza watu wao katika Sekta nyeti ndani ya serikali au katika makampuni na mashirika mengine. Vyama vya Kisiasa navyo hutoa Scholarship Kwa baadhi ya wanachama wake. Hata hivyo ni kawaida Kwa chama kimoja kinaweza kumsomesha mwanachama wa chama kingine pasipo chama husika kujua, kisha baadaye kumtumia mtu huyo katika kuangusha chama hasimu. Mfano, CCM inauwezo wa kumsomesha mwanachama wa CHADEMA bila CHADEMA kujua, mwanachama huyo akaenda mpaka Ulaya huku akiendelea kushiriki Kwa Hali na Mali na shughuli za CHADEMA mpaka kufikia kuaminika, alafu mwisho wa siku akipewa Madaraka makubwa au yanayokaribia ukubwa hukiteteresha Kama sio kukiangusha chama, hiyo ni kawaida kisiasa. Hata hivyo sina lengo pia la Kueleza Jambo hili.

Scholarship zitolewazo na serikali ndio lengo langu kuu katika andiko hili. Kila serikali inanamna yake ya kujiimarisha katika siku za usoni, moja ya mbinu za kufanya hivyo ni Kutoa Scholarship Kama sehemu ya kuwekeza Kwa watu Kwa maslahi ya siku zijazo.

Serikali nyingi za Afrika ikiwemo nch yetu mara nyingi huwapa Scholarship watoto wa viongozi bila kuangali na kufuata vigezo muhimu.
Scholarship Kwa maslahi ya Future ya nchi inapaswa ifuate na kutafuta watu wenye vigezo maalumu. Nitataja Kwa uchache;

1. Wenye Akili na Maarifa ya juu Kabisa
Sio akili za Darasani Bali hata akili za Mtaani, akili za kuongoza watu Kwa kutumia Akili. Zingatia ukiona nguvu kubwa inatumika sehemu ujue akili ndogo imetumika, na ukiona akili nyingi inatumika ujue nguvu ndogo itatumika.

Kiongozi anayetumia nguvu kubwa ujue akili yake huwa kisoda.

2. VIPAJI NA KARAMA ZA JUU
Mtu mwenye kipaji iwe uimbaji, uchoraji, Machale na maono, Hesabu, kipaji cha lugha, kujua lugha ngeni Kwa wepesi, kuchezea computer na masuala yote ya IT, Ubunifu wa Teknolojia mpya au zilizopita kuziboresha, n.k.
Hawa ndio wanapaswa kupewa Scholarship Kwa maslahi ya nchi.

3. UZURI NA MVUTO WA MAUMBILE
Wanawake wazuri kupitiliza, na vijana wenye mvuto ni muhimu Sana kupewa scholarship hasa kwenye ishu za intelejensia ya nchi.

Kwa Wazungu wao Kwa kulijua hili ndio maana wakaanzisha MASHINDANO YA WALIMBWENDE ambayo hujulikana Kama MISS WORLD ambayo Kwa nje yanaonekana ni sehemu ya kukuza vipaji vya fasheni na uanamitindo lakini ajenda za ndani kabisa ni tofauti.

Hawa walimbwende wanaoshinda, wengi wao huzikimbia nchi zao, na kutokomea nchi za baridi huko Ulaya. Husomeshwa na Wale wasio na akili za darasani hupewa majukumu Fulani na kupewa mitaji ya pesa na connection kubwa kubwa.

Warembo hawa baadaye wengi wao hata hapa nchini tunajua wanashobokewa na kuolewa na vigogo Kama sio wafanyabiashara Wakubwa. Bado hujaelewa what next? 😀😀 Wakubwa mmeelewa.

Tusikubali wanawake Wazuri kupitiliza WA nchi hii watumike na watu wa nchi zingine.

Sitaki kuelezea baadhi Yao ambao huweza kuingizwa kwenye biashara hatari na nyeusi ambazo ni jinai kubwa hapa nchini. Biashara za madawa ya kulevya ambazo warembo wetu huweza kutumika Kama Punda kuzitoa upande mmoja wa nchi kwenda nchi zingine.

Hata hivyo ni lazima warembo hawa wajiingize katika mapenzi mazito na vigogo wa nchi husika, utashangaa Mrembo mkali Grade one wa nchi yetu akiingia katika penzi zito na Rais au kigogo wa nchi Fulani, nchi hiyo hata wamkamate huyu mrembo hawawezi kumfanya kitu sababu tayari ana-connection ya moja Kwa moja na vigogo wa nchi hiyo.

Tuachane na haya.

4. WATU WENYE KARAMA ZA UCHUNGAJI NA USHEIKHE NA UGANGA
Kundi hili ni nyeti Kwa sababu ni kimbilio na waovu na Wema.
Scholarship ni muhimu Kwa kundi hili kuliweka mahususi Kwa mipango ya siku zijazo.
Nani asiyejua hata hapa nchini wapo viongozi tena wa ngazi ya Urais kabisa walitoka hapa nchini kwenda mpaka Nigeria Kwa TB Joshua, unafikiri mtu Kama anashida akifika Kwa mganga au mchungaji au Sheikhe hatasema mambo yote kusudi asaidiwe?

Hapa nchini ni nadra Sana Kwa Kiongozi mkubwa wa Kisiasa au wakurugenzi WA makampuni au mashirika makubwa kutojihusisha na Uganga, ama wachungaji wakubwa au masheikhe wakubwa. Wengi WA watu au vigogo wakubwa lazima wawe na mganga wanayemtegemea au mchungaji au Sheikhe. Hilo pia Kwa Majambazi, wezi na wafanya dili HATARI.

Tukiachana na watu wenye sifa hizo.

Mataifa makubwa ya Ulaya, hutumia watu niliowataja hapo juu kuzitawala nchi ZETU.

Vijana wanasomeshwa, wanasoma na kufunzwa hasa namna ya kuwa kibaraka mtiifu. Kisha akihitimu shahada ya kwanza, huja nchini na kuanzisha viprogramu vyake vya hapa na pale.
Kisha huenda tena kusoma na kuchukua degree ya pili mpaka yatatu. Alafu anarudi.

Baadhi Yao hupewa majukumu ya kijamii Kwa kuanzisha vishirika visivyo vya kiserikali Kwa kulenga moja ya mambo Yafuatayo;
1. Kutetea haki za wanawake
2. Kutetea mashoga na wasagaji au mapenzi ya mtu na mnyama
3. Kutetea Demokrasia inayozua ghasia na kuchafua Amani ya nchi.
4. Kutafiti na kuwa consultant wa mambo ya kiuchumi na kupewa nyenzo zote. Hapa utaona vita katika tenda za serikali utashangaa nyingi zinashikiliwa na makampuni ya kigeni ingawaje makampuni mengine huwa na majina ya Watanzania Kama Geresha tuu. Yaani utashangaa Mimi Taikon namiliki Kampuni kubwa lakini kumbe nyuma yangu wapo mabeberu.
5. Kutetea maslahi ya Wazungu hasa kwenye mikataba inayopitishwa bungeni. Miongoni mwa mambo mengine.

Ukiachana na hayo;

Scholarship huweza kuathiri sekta nyeti Kama usalama wa taifa, Bunge na mahakama.

Siku zote hakuna kitu cha Bure.

Ushauri:
Serikali inapaswa iwe Makini Sana katika Jambo hili.

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
DAR ES SALAAM
 
1. Intellectual exploitation and modern slavery
2. Mercenarism
3. Political and social control
4. Economic deracination, evulsion & avulsion
5. Neo-colonialism
 
..lamsingi Africa ikitaka kuwa huru na kujitegemea inapaswa kutengeneza kila mfumo wake wa maisha kuanzia Elimu, Dini nk nje ya hapo WaAfrica wote ni watumwa bado..
Kutengeneza mfumo ni Jambo linalohitaji kujitoa na akili kubwa ambazo pengine Waafrika hatuna
 
Kutengeneza mfumo ni Jambo linalohitaji kujitoa na akili kubwa ambazo pengine Waafrika hatuna

ukiivuka hiyo stage....ndio chanzo cha matatizo yote inakuwa....na kuimplement hiyo stage watu lazima wakubali kufa na kuumia... hata hizo Dini Christian na Islam hazikuja kirahisi rahisi kuna mahala nguvu, utemi na kila umafia ulitumia kuziinstall na kuzifuata...
 
Sijui niseme nini hapa. Ila sio kila scholarship ina muelekeo huo, kuna wale ambao hutoka kama sadaka (Jaalia kwa waislam) nk.

Siwezi kukaidi andiko hili ila mimi ni mmoja wa watu ambao nilipata scholarship kusoma nchi za Scandnavia huko (DENMARK) ni kwenye Era ya JK. Nilisomea masuala ya fedha, lkn sikuweza hata pandikizwa kitu chochote kuhusu nchi yangu zaidi ya kujikwamua na umasikini kwa maana nilipata huo ufadhili kutokana na umasikini tu ambapo kuna shirika la KiDENISH nilikuwa napiga nalo kazi, so walinikubali mno ndio nikapelekwa huko.

2. Nilisoma na Watz wenzangu hiyo nchi kama 6 hivi, lkn nikiri wazi wale wenzangu wa3 wako kwenye Balozi za Tz mbali mbali, wawili wako makampuni makubwa ya simu haya. Na huyu mmoja yy yuko sehemu nyeti mno, ingawa nilijua alisomeshwa na Serikali kwa wakati huo.

3. Nchi ambazo hutumia hizo mbinu ni UFARANSA, USA kwa sana. Ukiona UFARANSA wanamsomesha mtu, ogopa sana, hao jamaa ndio chanzo cha mapinduzi mengi Afrika Magharibi.

4. Kuna fursa za masomo jmn ni za kawaida tu, wala hazina connection na ukoloni mamboleo.
 
..lamsingi Africa ikitaka kuwa huru na kujitegemea inapaswa kutengeneza kila mfumo wake wa maisha kuanzia Elimu, Dini nk nje ya hapo WaAfrica wote ni watumwa bado..
Suala la DINI is unmipakable---halina mipaka ya kijiografia wala kiakili. Kwa maneno mengine, DINI haina chama. This is why serikali haina DINI, but watumishi wa serikali na watawala wana DINI.

Likewise, hakuna DINI ya Afrika wala DINI ya Mzungu. DINI, by definition, ni kumwamini Mungu.
 
ukiivuka hiyo stage....ndio chanzo cha matatizo yote inakuwa....na kuimplement hiyo stage watu lazima wakubali kufa na kuumia... hata hizo Dini Christian na Islam hazikuja kirahisi rahisi kuna mahala nguvu, utemi na kila umafia ulitumia kuziinstall na kuzifuata...


Na hapa ndipo pachungu kwani watakaomizwa na kufa ni watoto wa masikini
 
Sijui niseme nini hapa. Ila sio kila scholarship ina muelekeo huo, kuna wale ambao hutoka kama sadaka (Jaalia kwa waislam) nk.

Siwezi kukaidi andiko hili ila mimi ni mmoja wa watu ambao nilipata scholarship kusoma nchi za Scandnavia huko (DENMARK) ni kwenye Era ya JK. Nilisomea masuala ya fedha, lkn sikuweza hata pandikizwa...
Umenena vyema Kabisa.
 
Sijui niseme nini hapa. Ila sio kila scholarship ina muelekeo huo, kuna wale ambao hutoka kama sadaka (Jaalia kwa waislam) nk.

Siwezi kukaidi andiko hili ila mimi ni mmoja wa watu ambao nilipata scholarship kusoma nchi za Scandnavia huko (DENMARK) ni kwenye Era ya JK. Nilisomea masuala ya fedha...
Nilikua naongea na mwanaAfrika mashariki mmoja ambaye yuko ughaibuni kimasomo, akanambia watanzania ni waoga mno kuomba scholarships, ni wachache mno huko duniani ukilinganisha na wenzao wa Kenya.

Mtoa mada katuongezea UOGA mwingine hapa.
 
Nilikua naongea na mwanaAfrika mashariki mmoja ambaye yuko ughaibuni kimasomo, akanambia watanzania ni waoga mno kuomba scholarships, ni wachache mno huko duniani ukilinganisha na wenzao wa Kenya.
Mtoa mada katuongezea UOGA mwingine hapa.
Yaan sisi tunaaminishana hakuna maisha zaidi ya hapa TZ. Wengi ni waoga na tumezoea maisha ya changanyikeni hivyo maisha cool ya Ughaibuni ambayo hayana mazoea kama Manzese, Buza, Mbagala, Tandale nk.
 
Suala la DINI is unmipakable---halina mipaka ya kijiografia wala kiakili. Kwa maneno mengine, DINI haina chama. This is why serikali haina DINI, but watumishi wa serikali na watawala wana DINI.

Likewise, hakuna DINI ya Afrika wala DINI ya Mzungu. DINI, by definition, ni kumwamini Mungu.
Kumwamini "mungu" wa kwenye miti mikubwa na mapango nako si ni dini pia ?

Hoja ya jamaa hapo juu ni kwamba walikuja wazungu wakatuambia sisi kwamba sio "mungu huyo" ni "Mungu huyu" na kuabudu hakufanyiki "hivyo" (matambiko, n.k) bali kunafanyika "hivi" (misa, ibada, sala, n.k).

Hapa ndipo hoja yake kwamba hizo dini sisi tuliletewa na weupe kutoka Ulaya, Mashariki ya kati na Arabuni inapokua ina mashiko.
 
Kumwamini "mungu" wa kwenye miti mikubwa na mapango nako si ni dini pia ?

YES. But, hiyo ni imani potofu.

Hoja ya jamaa hapo juu ni kwamba walikuja wazungu wakatuambia sisi kwamba sio "mungu huyo" ni "Mungu huyu" na kuabudu hakufanyiki "hivyo" (matambiko, n.k) bali kunafanyika "hivi" (misa, ibada, sala, n.k).
FYI: Mzungu hakuleta DINI, literally; naye aliikuta kama mimi na wewe. Mzungu ALIENEZA DINI. Mwafrika naye ALIENEZA DINI. Ndicho kinachofanyika hadi leo.
 
Yaan sisi tunaaminishana hakuna maisha zaidi ya hapa TZ. Wengi ni waoga na tumezoea maisha ya changanyikeni hivyo maisha cool ya Ughaibuni ambayo hayana mazoea kama Manzese, Buza, Mbagala, Tandale nk.
Unaonaje sisi tukupiga kazi kwa sana ili baadae tuje tutor ufadhili kwa wengine? au hauwezekani
 
Unaonaje sisi tukupiga kazi kwa sana ili baadae tuje tutor ufadhili kwa wengine? au hauwezekani
Inawezekana, binafsi nilichojifunza na ambacho ni kweli kabisa 80% watumishi wa serikali yetu ni vilaza, hivyo hata vision ya nchi huwa ngumu, wengi wa watumishi wetu hawana uwezo wa kuchambua mambo kikawaida tu.
 
YES. But, hiyo ni imani potofu.


FYI: Mzungu hakuleta DINI, literally; naye aliikuta kama mimi na wewe. Mzungu ALIENEZA DINI. Mwafrika naye ALIENEZA DINI. Ndicho kinachofanyika hadi leo.
"Dini" ni imani potofu over "dini" nyingine si ndio ?

Anyways nakuelewa maana hata dini ilikuja Afrika kutoka Arabuni inaona ile iliyotoka mashariki ya kati ni potofu, ya mashariki ya kati inaona ile iliyotokea Uchina ni potufu, ya uchina inaona ile India ni upotofu, ya bara Hindi inaona ile ya hapahapa Afrika ni upotofu na ushenzi mkubwa.

Maybe it is how they work.
 
Inawezekana hayo uliyo yatambulisha ndiyo sababu ya kuzaliwa bokoharam
 
JE SCHOLARSHIP NI MBINU YA KUTENGENEZA VIBARAKA WA KISIASA?

Anaandika Robert Heriel.

Scholarship inaweza kuwa na maana nyingi, mojawapo ni kumsaidia mtu/mwanafunzi kirasilimali aweze kupata elimu Fulani; Rasilimali hiyo inaweza kuwa Fedha, au mahali pa kuishi(makazi), au chakula, au vitendea kazi vya kujifunzia.

Mara nyingi kama zote Scholarship hutolewa Kwa sababu kadhaa, zipo sababu za wazi na zile sababu za siri/nyeti ambazo mtoa scholarship hazitaji Mwanzoni.

Zipo scholarship zinazotolewa na Makundi Yafuatayo;
1. Mtu binafsi
2. Kampuni au shirika
3. SERIKALI

Mtu binafsi Kama Mimi na Wewe tunaweza kutoa scholarship Kwa wanafunzi wengine. Hata hivyo hatuwezi kukataa ukweli kuwa Scholarship haitolewi burebure,
Wapo watu waliopewa Scholarship wakasome ili waje kuoa/kuolewa na mtoto wa mtoa Scholarship.
Wengine hutoa scholarship Kwa kusomesha watoto Yatima lakini katika hao Yatima wapo ambao baadaye hupewa majukumu Fulani huko mbeleni wakishafanikiwa kimasomo, huingizwa kwenye aidha mambo ya Siasa, au kuajiriwa katika sekta nyeti ili walinde maslahi ya waliowasomesha. Hata hivyo si lengo langu Kueleza scholarship za watu binfasi.

Pia makampuni, taasisi na mashirika makubwa hutoa scholarship Kwa watu wake Kwa lengo la kuimarisha future ya kundi husika.
Zipo taasisi za Kidini, hutoa scholarship na kuhakikisha zinapenyeza watu wao katika Sekta nyeti ndani ya serikali au katika makampuni na mashirika mengine. Vyama vya Kisiasa navyo hutoa Scholarship Kwa baadhi ya wanachama wake. Hata hivyo ni kawaida Kwa chama kimoja kinaweza kumsomesha mwanachama wa chama kingine pasipo chama husika kujua, kisha baadaye kumtumia mtu huyo katika kuangusha chama hasimu. Mfano, CCM inauwezo wa kumsomesha mwanachama wa CHADEMA bila CHADEMA kujua, mwanachama huyo akaenda mpaka Ulaya huku akiendelea kushiriki Kwa Hali na Mali na shughuli za CHADEMA mpaka kufikia kuaminika, alafu mwisho wa siku akipewa Madaraka makubwa au yanayokaribia ukubwa hukiteteresha Kama sio kukiangusha chama, hiyo ni kawaida kisiasa. Hata hivyo sina lengo pia la Kueleza Jambo hili.

Scholarship zitolewazo na serikali ndio lengo langu kuu katika andiko hili. Kila serikali inanamna yake ya kujiimarisha katika siku za usoni, moja ya mbinu za kufanya hivyo ni Kutoa Scholarship Kama sehemu ya kuwekeza Kwa watu Kwa maslahi ya siku zijazo.

Serikali nyingi za Afrika ikiwemo nch yetu mara nyingi huwapa Scholarship watoto wa viongozi bila kuangali na kufuata vigezo muhimu.
Scholarship Kwa maslahi ya Future ya nchi inapaswa ifuate na kutafuta watu wenye vigezo maalumu. Nitataja Kwa uchache;

1. Wenye Akili na Maarifa ya juu Kabisa.
Sio akili za Darasani Bali hata akili za Mtaani, akili za kuongoza watu Kwa kutumia Akili. Zingatia ukiona nguvu kubwa inatumika sehemu ujue akili ndogo imetumika, na ukiona akili nyingi inatumika ujue nguvu ndogo itatumika.

Kiongozi anayetumia nguvu kubwa ujue akili yake huwa kisoda.

2. VIPAJI NA KARAMA ZA JUU.
Mtu mwenye kipaji iwe uimbaji, uchoraji, Machale na maono, Hesabu, kipaji cha lugha, kujua lugha ngeni Kwa wepesi, kuchezea computer na masuala yote ya IT, Ubunifu wa Teknolojia mpya au zilizopita kuziboresha, n.k.
Hawa ndio wanapaswa kupewa Scholarship Kwa maslahi ya nchi.

3. UZURI NA MVUTO WA MAUMBILE.
Wanawake wazuri kupitiliza, na vijana wenye mvuto ni muhimu Sana kupewa scholarship hasa kwenye ishu za intelejensia ya nchi.

Kwa Wazungu wao Kwa kulijua hili ndio maana wakaanzisha MASHINDANO YA WALIMBWENDE ambayo hujulikana Kama MISS WORLD ambayo Kwa nje yanaonekana ni sehemu ya kukuza vipaji vya fasheni na uanamitindo lakini ajenda za ndani kabisa ni tofauti.

Hawa walimbwende wanaoshinda, wengi wao huzikimbia nchi zao, na kutokomea nchi za baridi huko Ulaya. Husomeshwa na Wale wasio na akili za darasani hupewa majukumu Fulani na kupewa mitaji ya pesa na connection kubwa kubwa.

Warembo hawa baadaye wengi wao hata hapa nchini tunajua wanashobokewa na kuolewa na vigogo Kama sio wafanyabiashara Wakubwa.
Bado hujaelewa what next? 😀😀 Wakubwa mmeelewa.

Tusikubali wanawake Wazuri kupitiliza WA nchi hii watumike na watu wa nchi zingine.

Sitaki kuelezea baadhi Yao ambao huweza kuingizwa kwenye biashara hatari na nyeusi ambazo ni jinai kubwa hapa nchini. Biashara za madawa ya kulevya ambazo warembo wetu huweza kutumika Kama Punda kuzitoa upande mmoja wa nchi kwenda nchi zingine.

Hata hivyo ni lazima warembo hawa wajiingize katika mapenzi mazito na vigogo wa nchi husika, utashangaa Mrembo mkali Grade one wa nchi yetu akiingia katika penzi zito na Rais au kigogo wa nchi Fulani, nchi hiyo hata wamkamate huyu mrembo hawawezi kumfanya kitu sababu tayari ana-connection ya moja Kwa moja na vigogo wa nchi hiyo.

Tuachane na haya.

4. WATU WENYE KARAMA ZA UCHUNGAJI NA USHEIKHE NA UGANGA
Kundi hili ni nyeti Kwa sababu ni kimbilio na waovu na Wema.
Scholarship ni muhimu Kwa kundi hili kuliweka mahususi Kwa mipango ya siku zijazo.
Nani asiyejua hata hapa nchini wapo viongozi tena wa ngazi ya Urais kabisa walitoka hapa nchini kwenda mpaka Nigeria Kwa TB Joshua, unafikiri mtu Kama anashida akifika Kwa mganga au mchungaji au Sheikhe hatasema mambo yote kusudi asaidiwe?

Hapa nchini ni nadra Sana Kwa Kiongozi mkubwa wa Kisiasa au wakurugenzi WA makampuni au mashirika makubwa kutojihusisha na Uganga, ama wachungaji wakubwa au masheikhe wakubwa. Wengi WA watu au vigogo wakubwa lazima wawe na mganga wanayemtegemea au mchungaji au Sheikhe. Hilo pia Kwa Majambazi, wezi na wafanya dili HATARI.

Tukiachana na watu wenye sifa hizo.

Mataifa makubwa ya Ulaya, hutumia watu niliowataja hapo juu kuzitawala nchi ZETU.

Vijana wanasomeshwa, wanasoma na kufunzwa hasa namna ya kuwa kibaraka mtiifu. Kisha akihitimu shahada ya kwanza, huja nchini na kuanzisha viprogramu vyake vya hapa na pale.
Kisha huenda tena kusoma na kuchukua degree ya pili mpaka yatatu. Alafu anarudi.

Baadhi Yao hupewa majukumu ya kijamii Kwa kuanzisha vishirika visivyo vya kiserikali Kwa kulenga moja ya mambo Yafuatayo;
1. Kutetea haki za wanawake
2. Kutetea mashoga na wasagaji au mapenzi ya mtu na mnyama
3. Kutetea Demokrasia inayozua ghasia na kuchafua Amani ya nchi.
4. Kutafiti na kuwa consultant wa mambo ya kiuchumi na kupewa nyenzo zote. Hapa utaona vita katika tenda za serikali utashangaa nyingi zinashikiliwa na makampuni ya kigeni ingawaje makampuni mengine huwa na majina ya Watanzania Kama Geresha tuu. Yaani utashangaa Mimi Taikon namiliki Kampuni kubwa lakini kumbe nyuma yangu wapo mabeberu.
5. Kutetea maslahi ya Wazungu hasa kwenye mikataba inayopitishwa bungeni. Miongoni mwa mambo mengine.

Ukiachana na hayo;

Scholarship huweza kuathiri sekta nyeti Kama usalama wa taifa, Bunge na mahakama.

Siku zote hakuna kitu cha Bure.

Ushauri:
Serikali inapaswa iwe Makini Sana katika Jambo hili.

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
DAR ES SALAAM
Hiyo analysis siyo sahihi sana: Nyerere na Nkurmah walisoma kwa scholarship hizo hizo lakini hawakuwa vibaraka. wapo wengi sana nchini kwetu waliosoma kwa scholarships za Commonwealth, DAAD, British Council, Fullbright, Friendship (Urusi) na nyinginezo wakarudi nchini na na wanafanya kazi serikalini vizuri tu. Swala la uzalendo linatokana na mtu mwenyewe binafsi pamoja na system ya nchi yake. Wengine wanageuka na kuonekana wanatumiwa kama vibaraka iwapo mfumo wa nchi zao unawatenga. Kwa mfano, wasomi wengi wazuri Tanzania siku hizi wanatengwa na system mpaka waingie kwenye siasa. Sasa wale wasiopenda kuwa kwenye siasa wanaweza kujikuta wanajipatia riziki yao kwa kuwatumikia watu wa nje, na hivyo kuonekana vibaraka.
 
Back
Top Bottom