Je, Serikali imeamua kugawana 50/50 tozo za simu na Wamiliki wa mitandao?

Si tulikua tunaambiwa mapato ya kodi yamepanda? Hiyo kodi ilikua haitoshi mpaka tuongezeane huu mzigo?
 
hii sasa ndio kampeni mpya ya chadema baada ya kuona katiba mpya imekuwa ndoto za mchana.
ila chadema inazidi kujichafua zaidi kisiasa kwa kuhamasisha mambo ambayo ni kinyume na uzalendo, hakuna anaye shawishika na uhuni huu .
 
Kwahio serikali imeshindwa kuwa na ubunifu wa kutengeneza namna ya kupata hizo 12 trillions mpaka ikopi Idea kwa wenye mitandao ya simu kwa kuimpose double taxation!
Of course wamekosa ubunifu, ndiyo maana miaka ya nyuma kodi ilikuwa kwenye Bia. Saivi ni Simu hadi tusema tawile, wangejaribu kusoma bajeti mbadala ya KUB wangepata maeneo mengine ya kodi na kupunguza mzigo kwenye simu 😂
 
Kwa namna nyingine, hii imekaa vizuri kwa sababu itawagusa karibia Watanzania wote.

Siku za nyuma, waliokuwa wakibambikiwa kodi za ajabu ajabu ilikuwa wafanyabiashara, wawekezaji na wenye magari. Sasa inagusa wote.

Halafu tutakiri au kukana kwa pamoja kwa hizi kodi dhulumati, kama Serikali ipo kwaajili ya kumgandamiza au kumwinua mwananchi.
 
Nisahihi Mkuu, ingawa binafsi ningependa kuona kodi kwenye gharama za vifaa vya ujenzi ikishuka. Mwaka wa fedha uliopita tumepata tabu sana kununua vifaa vya ujenzi kwa gaharama kubwa.
 
Huko ndio kabisa hapafai
Kuna haja Serikali kupitia Waziri wa fedha wakapunguza kodi kwenye vifaa vya Ujenzi, huku nilipo nimenunua Tiles ya 40 x 40 shilingi 25,000 boksi moja, Imagine kutoka shilingi 19,000 niliyonunua awali hadi 25,000 manake kuna increment ya 6,000 nzima
 
Kuna haja Serikali kupitia Waziri wa fedha wakapunguza kodi kwenye vifaa vya Ujenzi, huku nilipo nimenunua Tiles ya 40 x 40 shilingi 25,000 boksi moja, Imagine kutoka shilingi 19,000 niliyonunua awali hadi 25,000 manake kuna increment ya 6,000 nzima
Hizi gharama zikiwagusa wengi ndio sauti itasikikaa. Vinginevyo tunawapigia mbuzi gitaa.


Mzigo mkubwa wa kodi unawaangukia watu wachache wenye senti za kubangaiza.

Viongozi wetu wana dunia yao tofauti, nyumba na magari bure. Wengine Mishahara haina kodi, pesheni kedekede. Haya hayawagusi, hayawahusu na hivyo hawawezi kuyaona.

Pa kuwatikisa ni kwenye boksi la kura ambalo nalo lina matobo
 
Ni sahihi, ndiyo maana nyumba bora ni watu wachache wanaomudu kujenga. Waliowengi wana afford kujenga nyumba za tope za tembe
 
Mtamkumbuka Magufuli mwamba wa Africa tuh fangasi nyie
Umesahau yeye ndio alianzisha huu mchezo? Akatuwekea kodi ya gari kwenye mafuta, sasa hivi wamenogewa wameenda kwenye umeme na ela za kwenye simu
 
Mara nyingi baba hapendwi akiwa ndani ya nyumba ila atakumbukwa, majukumu ya ndani akiachiwa mama mwenye tamaa huwa yanavurugika.
"Nawaza kwa sauti"
Hii yote alianzisha magu msimlaumu mama kafuata nyayo zake
 
Mungu ametupatia akili hivi hakuna namna Bora ya kuepuka kufanya transaction kupitia mitandao hii? Hapa ndiyo muda wa kuwasikia vijana tuliowasomesha kwa Kodi zetu.
Bank zipo mkuu,
 
Ela niitabikie Mimi afu wale nchi nzima? Ni wizi tu huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…