Je, Serikali ya Tanzania ni Mbia wa Kampuni ya Taifa Group?

Je, Serikali ya Tanzania ni Mbia wa Kampuni ya Taifa Group?

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Siku ya tarehe 23 Aprili, 2022 Rais Samia alishiriki utiaji saini wa makubaliano ya kibiashara baina ya kampuni ya Taifa Group na kampuni ya Northern feed co.

Mkataba huo wenye thamani ya Dola milioni 500 sawa na trilioni moja za kitanzania utakua katika uzalishaji wa soya, ngano , sukari etc.

Anayeonekana kusaini makubaliano hayo ni Bwn. Rostam Aziz ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni hiyo.

Bwn. Rostam Aziz ambaye ndiye mmiliki wa kampuni ya Taifa Gas alikuwepo pia katika delegation ya Rais iliyokwenda Kenya na kuingia makubaliano ya kuisambazia Kenya Gesi.

Kwakua Bwn. Aziz sio sehemu ya Serikali utiliwaji saini wa makubaliano hayo ni jambo binafsi zaidi kuliko la kisiasa.

Uwepo wa Rais ambaye ni nembo ya mamlaka ya Nchi katika jambo binafsi unaleta ukakasi kidogo kwani sisi wananchi hatuna taarifa zozote za umiliki wowote wa Serikali iwe kwa hisa au kwa namna yoyote katika kampuni hiyo.

Hivyo basi kama Tanzania ina shares katika kampuni ya Taifa Group ni vyema tukaambiwa ama la tueleweshwe kuhusiana na uwepo wa kampuni hii katika ziara za Rais na ulazima wa Taifa kuhusishwa katika mambo binafsi ya kampuni hii.





Screenshot_20220424-214113.png
 
Siku ya tarehe 23 Aprili, 2022 Rais samia alishiriki utiaji saini wa makubaliano ya kibiashara baina ya kampuni ya Taifa Group na kampuni ya Northern feed co...
Sio ajabu kwa Rais kushuhudia ubia wa biashara kati ya kampuni binafsi kutoka nchini kwake na kampuni nyingine ya nje.
Rais sio katibu mkuu kiongozi, sio katibu mkuu wa wizara, sio mkurugenzi wa shirika la umma. Ni Rais wa nchi.
 
Sio ajabu kwa Rais kushuhudia ubia wa biashara kati ya kampuni binafsi kutoka nchini kwake na kampuni nyingine ya nje.
Rais sio katibu mkuu kiongozi, sio katibu mkuu wa wizara, sio mkurugenzi wa shirika la umma. Ni Rais wa nchi.
Umejibu vyema kuwa ni Rais wa Nchi.

Sasa kiongozi wa Nchi anahusikaje katika mambo ya kampuni binafsi ambayo serikali sio mbia??
 
Umejibu vyema kuwa ni Rais wa Nchi.

Sasa kiongozi wa Nchi anahusikaje katika mambo ya kampuni binafsi ambayo serikali sio mbia??
Rais ni wa wote. Nimekupa mifano ya watu ambao kazi zao zinaishia ndani ya serikali tu au shughuli za umma tu ambao ni hao kama Katibu Mkuu Kiongozi.
Lakini Rais, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, kazi zao haziishii kwenye shughuli za umma tu. Zinaenda beyond.
Kuna zile kazi kuu 3 za Rais:
1. Mkuu wa nchi
2. Mkuu wa Serikali
3. Amiri Jeshi Mkuu.
Sasa hapo alikuwa akitekeleza kazi namba 1.
 
Rais ni wa wote. Nimekupa mifano ya watu ambao kazi zao zinaishia ndani ya serikali tu au shughuli za umma tu ambao ni hao kama Katibu Mkuu Kiongozi.
Lakini Rais, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, kazi zao haziishii kwenye shughuli za umma tu. Zinaenda beyond.
Kuna zile kazi kuu 3 za Rais:
1. Mkuu wa nchi
2. Mkuu wa Serikali
3. Amiri Jeshi Mkuu.
Sasa hapo alikuwa akitekeleza kazi namba 1.
Hayo makubaliano ni internal affairs za kampuni husika Rais wa nchi hana nafasi katika internal afairs za private company.
 
Hayo makubaliano ni internal affairs za kampuni husika Rais wa nchi hana nafasi katika internal afairs za private company.
Kwanza bweka usikike,

Uko upqnde gani?

Ni sahihi serikali kufanya biashara au ikuze sekta binafsi ibaki kukusanya Kodi?
 
Anaweza kusimama ceremonial tu katika hafla. Sio lazima asome mafaili.
Hilo tayari ni tatizo kubwa sana maana presence yake inamaanisha uwakilishi wa nchi katika hilo jambo.

Sasa mfano ikatokea kashfa ya Rushwa katika hiyo kampuni binafsi yeye anajiondoaje maana kuwepo hapo anamaanisha yeye ni part ya hiyo transaction.
 
Kwanza bweka usikike,

Uko upqnde gani?

Ni sahihi serikali kufanya biashara au ikuze sekta binafsi ibaki kukusanya Kodi?
Wewe tuambie ni nchi gani duniani imeachia kila kitu kwa sekta binafsi na kubaki kukusanya kodi?
Nyie ndio mnadanganywa na wajanja wa kizungu.
Za kuambiwa, changanya na zako.
 
Siku ya tarehe 23 Aprili, 2022 Rais samia alishiriki utiaji saini wa makubaliano ya kibiashara baina ya kampuni ya Taifa Group na kampuni ya Northern feed co...
Serikali ina hisa kwenye hiyo kampuni ndio chanzo cha kubadili jina kutoka mihan gas mpaka taifa gas na hisa hizo zilichukuliwa na kipindi cha magufuli kulikuwa na janja janja kama airtel napo serikali ilichukua hisa
 
Serikali ina hisa kwenye hiyo kampuni ndio chanzo cha kubadili jina kutoka mihan gas mpaka taifa gas na hisa hizo zilichukuliwa na kipindi cha magufuli kulikuwa na janja janja kama airtel napo serikali ilichukua hisa
Sio kweli serikali haina shares Taifa Gas.

Taifa Gas ilibadili tu jina toka Mihan Gas.

Mmiliki ni Bwn. Rostam.
 
Wewe una inside info, somebody told Me Taifa gas ni ya JPM na RA
Sio kweli. Taifa gas ni jina jipya lilibadilishwa kutoka kwa mihan gas ambayo ilikuwepo miaka na miaka.
Mihan gas ni ya rostam na yule mzee mwenye mvi. Baada ya mzee mwenye mvi kutoka ulingoni ndio baadae RA akaimiliki kwa 100% kupitia jina jipya la taifa
 
Umejibu vyema kuwa ni Rais wa Nchi.

Sasa kiongozi wa Nchi anahusikaje katika mambo ya kampuni binafsi ambayo serikali sio mbia??
Siku hizi una maswali fikirishi kwelikweli.

Tambua hili: wakati huu ni ujenzi wa 'Oligarchy' wa kiTanzania, kama wale wa Urusi.

Sasa anzia hapo kujibu maswali yako.

Huyu mama hana 'apologies' kabisa na msimamo wake huu, tena naona ni kama anachelewa sana kujenga tabaka hili la watu wake.
 
Sio kweli serikali haina shares Taifa Gas.

Taifa Gas ilibadili tu jina toka Mihan Gas.

Mmiliki ni Bwn. Rostam.
Sasa unauliza na unapewa jibu bado unapinga😂😂😂😂😂😂😂😂😂 Mkuu serikali inahisa nyingi tu taifa gas karibia asilimia 40
 
Back
Top Bottom