Je, shilingi milioni kumi inatosha kujenga nyumba nzuri kijijini?

Je, shilingi milioni kumi inatosha kujenga nyumba nzuri kijijini?

PAGAN

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2014
Posts
12,181
Reaction score
20,148
Asalaam wadau!

Nimenunua shamba mkoa wa Pwani, nje kidogo ya Mkuranga. Lengo kuu ni kumuweka Bi. Mkubwa wangu kwasababu maisha ya Dar es Salaam yamekuwa busy sana kwa mtu mzima kama yeye.

Sasa nataka kujenga nyumba yenye nafasi hata watoto wangu wakienda kumtembelea bibi wasibanane. Na yeye maisha yake yote ni ya mjini kwa hivyo ni lazima iwe yenye mazingira ya kuvutia kidogo.

Kwa sasa bajeti yangu ni shilingi milioni kumi tu. Swali, je hii pesa inatosha kujenga japo nyumba ndogo huko kijijini? Au ni nyumba ya aina gani inaweza kutosha kwa pesa hii?

Natanguliza shukrani.
 
Asalaam wadau!

Nimenunua shamba mkoa wa Pwani, nje kidogo ya Mkuranga. Lengo kuu ni kumuweka Bi. Mkubwa wangu kwasababu maisha ya Dar es Salaam yamekuwa busy sana kwa mtu mzima kama yeye.
Sasa nataka kujenga nyumba yenye nafasi hata watoto wangu wakienda kumtembelea bibi wasibanane. Na yeye maisha yake yote ni ya mjini kwa hivyo ni lazima iwe yenye mazingira ya kuvutia kidogo.
Kwa sasa bajeti yangu ni shilingi milioni kumi tu. Swali, je hii pesa inatosha kujenga japo nyumba ndogo huko kijijini? Au ni nyumba ya aina gani inaweza kutosha kwa pesa hii.

Natanguliza shukrani.
Kwa kiingereza kuna vitu vitatu residential shelter and house.....maisha ya Tz yalivo sasa hivi hiyo 10m unaweza kujenga shelter tena vyumba viwili tu na sebule bila finishing tu sio residetial
 
Bora ungeeleza unachokijua kuliko kusema ninadanganya
Nachojua huwezi kujenga nyumba ya kisasa kwa milioni kumi za kitanzania. Hilo shimo la choo tu linalamba theluthi nzima ya hiyo pesa... Hapo kilichobaki tofali, mabati, cement, nondo,kokoto na mbao... tayari hela ishaisha.
 
Assume nyumba yako itatumia bati 100 za gauge 30. 100@ 20000=2million
Misumari ya bati kilo 30@8000=240000/= kofia 20@10000=200000/= mbao 200@5500= 1100000/= na fisherboard 20@10000=200000/= na misumari ya nchi 4 kilo 45=130000/=

Jumla utapata = 3,840,000/= jumlisha hela ya fundi kama 800000/= kupaua jumla utapata 4,640,000/=

Chukua 10mil toa hiyo 4.6mil utabakiwa na kama 5.4 mil haya hiyo 5.4 ndo kwa ajili ya materials za kusimamisha boma na hela ya mafundi je unahisi itatosha?

Thus is why tunasema itakufikisha mahai ila haitamaliza
 
Nachojua huwezi kujenga nyumba ya kisasa kwa milioni kumi za kitanzania. Hilo shimo la choo tu linalamba theluthi nzima ya hiyo pesa... Hapo kilichobaki tofali, mabati, cement, nondo,kokoto na mbao... tayari hela ishaisha.
Hata gari zipo bei tofauti ndugu.
Unasema shimo?
Kuna mtu anachimba shimo moja.
Mwingine mawili, yaani kubwa na dogo. Had hapo kuna tofauti.
Kuna nyumba ya rum tatu, mwingine anajenga hekalu, mwingine godown.
Mwache kijana ajenge!
 
Hata gari zipo bei tofauti ndugu.
Unasema shimo?
Kuna mtu anachimba shimo moja.
Mwingine mawili, yaani kubwa na dogo. Had hapo kuna tofauti.
Kuna nyumba ya rum tatu, mwingine anajenga hekalu, mwingine godown.
Mwache kijana ajenge!
Haya mbe.

Mpe moyo tu. Lakini hata ajenge ndogo ya namna gani... 10m kumaliza nyumba ya kisasa ni ajabu jipya la dunia
 
Assume nyumba yako itatumia bati 100 za gauge 30. 100@ 20000=2million
Misumari ya bati kilo 30@8000=240000/= kofia 20@10000=200000/= mbao 200@5500= 1100000/= na fisherboard 20@10000=200000/= na misumari ya nchi 4 kilo 45=130000/=

Jumla utapata = 3,840,000/= jumlisha hela ya fundi kama 800000/= kupaua jumla utapata 4,640,000/=

Chukua 10mil toa hiyo 4.6mil utabakiwa na kama 5.4 mil haya hiyo 5.4 ndo kwa ajili ya materials za kusimamisha boma na hela ya mafundi je unahisi itatosha?

Thus is why tunasema itakufikisha mahai ila haitamaliza


Asante sana mkuu. Hii ni useful comment /suggestion. Kidogo napata picha kule ninakoelekea.
 
Assume nyumba yako itatumia bati 100 za gauge 30. 100@ 20000=2million
Misumari ya bati kilo 30@8000=240000/= kofia 20@10000=200000/= mbao 200@5500= 1100000/= na fisherboard 20@10000=200000/= na misumari ya nchi 4 kilo 45=130000/=

Jumla utapata = 3,840,000/= jumlisha hela ya fundi kama 800000/= kupaua jumla utapata 4,640,000/=

Chukua 10mil toa hiyo 4.6mil utabakiwa na kama 5.4 mil haya hiyo 5.4 ndo kwa ajili ya materials za kusimamisha boma na hela ya mafundi je unahisi itatosha?

Thus is why tunasema itakufikisha mahai ila haitamaliza
Jamaa umepiga hadi hela ya fundi unasahauje tofali na cementi?? Bila tofali na simenti na nondo hakuna boma
 
Jamaa umepiga hadi hela ya fundi unasahauje tofali na cementi?? Bila tofali na simenti na nondo hakuna boma


Amepiga mahesabu amebaki na milioni 5.4, hapo ndio utafute boma pamoja na fundi. Kwa mahesabu yangu ya haraka labda zinahitajika nyingine 5 ili mipango iende sawa.
 
Ooh, nlizani angeanza na boma hela ikiisha unajikusanya kufikiria kupaua[emoji848][emoji848][emoji848]
Amepiga mahesabu amebaki na milioni 5.4, hapo ndio utafute boma pamoja na fundi. Kwa mahesabu yangu ya haraka labda zinahitajika nyingine 5 ili mipango iende sawa.
 
Back
Top Bottom